Tuambiane ukweli kwa Mpira mbovu uliochezwa na Simba SC Kipindi cha Pili dhidi ya Mbeya City ikicheza na Azam na Yanga itafungwa

Tuambiane ukweli kwa Mpira mbovu uliochezwa na Simba SC Kipindi cha Pili dhidi ya Mbeya City ikicheza na Azam na Yanga itafungwa

Kwani Troisième Ceil anasemaje? 😂
Nilidhani 'Uzi' wangu huu kwa Umuhimu wake hasa 'Kiuchambuzi' Watu watakuja na 'Nondo' zaidi za 'Kiufundi' nashangaa kuona baadhi yetu tunakuja na 'posts' za Kuonyesha jinsi gani mlivyo na 'Vijitabia' vya 'Ushoga' kwa Kauli za 'Kike Kike' kama hii uliyoitoa ( uliyoiandika ) hapa. Kwa 'Upumbavu' wenu kuna Watu huwa mnanilazimisha GENTAMYCINE niwajibuni Kunya ( Shombo ) kama hivi. Mnakera..!!
 
Wachezaji wengi wa Simba umri ni mkubwa, sio vijana tena hivyo hawawezi kucheza kwa kasi ile ile mechi zote 34 za msimu mzima.

Zipo mechi inabidi watunze nguvu zao wakicheza mpira wa kasi ndogo. Kama Simba inataka msimu ujao ligi ya mabingwa afrika wavuke robo fainali basi kikosi cha kwanza kiwe na wachezaji kama watano au sita wenye damu changa.
 
Naunga mkono hoja - kuna tatizo katika back line hassa Kennrdy Juma allipoteza pasi nyingi na alickoka kipindi cha pili.
Kakolanya ni kipa wa kawaida kwa sasa hafai kwa mechi kubwa.
Erasto Nyoni alicheza eneo ambalo linahitaji pumzi na stamina na kwa umri wake alipwaya jana.
Kwa ujumla nilichoona jana ni uchovu wa wachezaji na kujiamini kupitiliza inaonyesha hawakuwa vizuri kambini ( kimaadili baadhi yao).
Illa tujue tu kocha kayaona na sidhani kabisa - Simba kwa level waliofikia watadharau mechi kubwa au zenye ubabe na kupania watacheza kama jana?
Tukumbuke tu mechi na Azam, Songea na changamoto ya uwanja haitabiriki.
Wachezaji wa Simba wakiamua hassa wanashinda mechi zote ni suala match fitness, stamina na maamuzi tu.
 
Cha ajabu zile Id za Mikia lialia mpaka hapa hazijaandika kitu. 😀😀😀

Ama kweli huu ni ukweli mchungu.
Umesema ukweli mtupu Mkuu japo wapo wana Simba SC wengine ambao siyo Wanafiki, wanajitambua nao wamekuja na 'wamechambua' hapa vile vile. au hujawaona katika 'Uzi' huu?

GENTAMYCINE nina tatizo moja Kubwa ambapo kwakuwa nimeshajiweka wazi kuwa Mimi katika Medani za Kisiasa ni mwana CCM na katika Medani za Michezo ni Simba SC hivyo Watu wanataka 24/7 niwe nasifia na kupamba tu CCM na Simba SC ila nikiwakosoa utasikia naambiwa Mimi ni CHADEMA na Yanga SC.

Na ukiona nakusema ( nakusiliba ) vilivyo hapa JamiiForums jua nakupenda na nataka kuona Mabadiliko na Ufanisi wa Kitija juu ya ama Mhusika au Taasisi. Sijazoea Unafiki, Uwoga, Upendeleo au Kujipendekeza na nipo radhi nichukiwe na Watu Milioni 50 ila Watu 1000 tu wanielewe na wanipende.
 
Naunga mkono hoja - kuna tatizo katika back line hassa Kennrdy Juma allipoteza pasi nyingi na alickoka kipindi cha pili.
Kakolanya ni kipa wa kawaida kwa sasa hafai kwa mechi kubwa.
Erasto Nyoni alicheza eneo ambalo linahitaji pumzi na stamina na kwa umri wake alipwaya jana.
Kwa ujumla nilichoona jana ni uchovu wa wachezaji na kujiamini kupitiliza inaonyesha hawakuwa vizuri kambini ( kimaadili baadhi yao).
Illa tujue tu kocha kayaona na sidhani kabisa - Simba kwa level waliofikia watadharau mechi kubwa au zenye ubabe na kupania watacheza kama jana?
Tukumbuke tu mechi na Azam, Songea na changamoto ya uwanja haitabiriki.
Wachezaji wa Simba wakiamua hassa wanashinda mechi zote ni suala match fitness, stamina na maamuzi tu.
Mkuu umechambua vizuri sana na Kuelezea Mambo ya Kimsingi na ya 'Kiufundi' zaidi. Heko mno Kwako na naamini Watu wa Simba SC ( Uongozi na hata wa Benchi la Ufundi ) huu 'Uzi' wanaupitia na haya Mawazo ( Maoni ) yetu wanayasoma ili wakayafanyie Kazi kwa Mafanikio zaidi ya Klabu ( Timu ) yetu pendwa na tukuka ya Simba Sports Club.
 
Unaona mashabiki wa Simba? Wapo buzy kuongea mapungufu ya timu yao ili yarekebishwe na sio kuilaumu TFF au marefa
Umesema ukweli mtupu Mkuu na Siku zote Mashabiki wa Simba SC ni Watu 'very smart upstairs' kulinganisha na wa Yanga SC ambao ni 'Fools naturally' na hili Wala halihitaji Akili Kubwa kulijua ( kulibaini ) iwe ni hapa JamiiForums au huku Mitaani Kwetu.
 
Mkuu niamini maneno yangu kama Wachezaji wa Simba SC watacheza 'Kipuuzi' kama walivyocheza Kipindi cha Pili jana pale tukicheza na Azam FC Kombe la ASFC Jumamosi ile 'Derby' yetu na Yanga SC tarehe 3 July, 2021 tunaenda Kufungwa Mechi zote hizo Mbili ambazo ni Muhimu mno Kwetu...
Nadhani goli za haraka ziliwafanya wabweteke, na kuanza kuwaza mechi zijazo, wakiamini ile ilisha isha ndiyo maana 2nd half mpira ukawa mbovu usishangae haya yaliyo onekana jana yakawa tofauti kwa next fixtures!
 
Kwa kweli GENTA umemaliza kila kitu na kama kuna mtu yupo karibu na benchi la ufundi la Simba au uongozi awafikishie haraka sana. Vinginevyo wakipuuza hayo madini yako adimu wasije kulaumu kuwa hawakuelezwa huko mbele watakapokutana na Azam na Yanga.

Wachezaji walikuwa wanapiga pasi za kipuuzi sana tena kwenye "zone" yao wakati wanafahamu kabisa mpira akiupata adui ni hatari kwa sababu ni karibu na goli lao na walipokuwa wanaamua kupeleka mipira mbele walikuwa wameshachelewa kwani Mbeya City walikuwa tayari wameshajipanga. Boko na Morison muda mwingi walikuwa wanachoka wanakimbia bure wanafungua pembeni lakini mipira ilikuwa haiendi kwa wakati.

Kosa lingine kubwa ni kukosa mechi walau mbili za kirafiki na hata timu za daraja la kwanza kwa kipindi chote cha mapumziko ya wiki mbili ya mechi za kimataifa amabazo zingewapa utimamu wa mwili.

Mechi kama ya jana ilitakiwa Simba itafute goli zisizopungua 4 za haraka haraka halafu unawatoa "key players" mapema wanaenda benchi kusubiri mechi ngumu na pia inatoa nafasi kwa wakaa benchi kujiamini. Lakini hebu tazama Kakolanya alivyopoteza kujiamini japo ni kipa mzuri. Inatakiwa walau Kakolanya awe anacheza walau hata dakika kumi za mwisho kwenye zile mechi ambazo hazina ushindani sana na Simba wanaongoza goli nyingi.
 
Simba kucheza show game nakuunga mkono kabisa ,kuna wakati mchezaji anaamua tu kufanya show game halafu mpira unachukulia na kuleta madhara
 
Jambo lingine la hatari sana kwenye "back line" ya Simba ni mipira ya juu krosi na kona. Wanakaba mipira ya juu kwa macho sana badala ya kuwabughudhi wachezaji wa timu pinzani. Benchi la ufundi lisipofanyia kazi hayo mapungufu haraka sana basi wajiandae na kipigo kama sio vipigo siku za karibuni.
 
Kwa kweli GENTA umemaliza kila kitu na kama kuna mtu yupo karibu na benchi la ufundi la Simba au uongozi awafikishie haraka sana. Vinginevyo wakipuuza hayo madini yako adimu wasije kulaumu kuwa hawakuelezwa huko mbele watakapokutana na Azam na Yanga...
Umechambua vizuri sana Mkuu na Heko.
 
Mabeki kushindwa kuruka kuzuia mipira ya juu ya Krosi au Kona ni tatizo sugu sana kwa Beki ya timu ya Simba.
Ni Onyango tu kidogo anajitahidi kuruka.
Na ndilo tatizo lililo iondoa Simba katika michuano ya Club Bingwa Afrika.
Kaizer Chief waliusoma udhaifu huu, wakautumia ukawaletea matokeo.

Na bado hawajirekebishi.
 
Hivi wewe dogo Simba wamekuajiri au kwa hiyo hapa mbayuwayuni umepanga et!! We endelea tu Kuna siku utarudia getoni😂😂😂😂
 
Kwanza nianze kwa Kupongeza Ushindi mzuri wa Goli 4 kwa 1 ambayo Simba SC imeshinda leo ( Usiku huu ) dhidi ya Mbeya City.

Pia nikiri kuwa Klabu ya Simba si tu kwamba inaishia kuwa na Kikosi kizuri (Timu nzuri) ila pia ina Wachezaji wenye Vipaji Asilia Binafsi kuliko wa Timu nyinginezo nchini Tanzania.

Hata hivyo pamoja na Kongole (Pongezi) zote hizi kuna baadhi ya Mapungufu ya Kimsingi niliyoyaona na kama Benchi la Ufundi pamoja na Wachezaji wenyewe wasipoyafanyia Kazi kuna uwezekano mkubwa mno Azam FC wakatufunga katika ASFC tarehe 26 June, 2021 na Yanga SC nao wakatufunga tarehe 3 June, 2021.

1. UKABAJI MBOVU
Bado Simba SC ina tatizo katika Ukabaji japo kidogo kidogo wanalifanyia Kazi, ila bado naliona hivyo lisipofanyiwa Kazi Mechi zote za Smba SC ilizobakiza dhidi ya Yanga SC, KMC FC, Coastal Union FC, Azam FC na Namungo FC.

2. WACHEZAJI WANAJIAMINI KUNAKOPITILIZA
Sema tu Mbeya City walishindwa kuja na Plan B ambayo wangekuwanayo na wangeshinda ( wangetufunga ) sana tu na Simba SC Kuumbuka.

3. MIPIRA YA JUU (VICHWA )
Bado tatizo la Wachezaji wa Simba SC hasa Mabeki kutokujua Kuruka Miipira huku 'Wakitegeana' lipo na Benchi la Ufundi wasipolifanyia Kazi mechi zetu Muhimu za Azam FC na Yanga SC 'tutafungwa' Goli nyingi na kuanza Kutafutana kwa Mkapa Temeke.

4. PUMZI KUKATA MAPEMA
Timu inaanza Kucheza vyema Kipindi cha Kwanza ila cha Pili Wacheza wanapoteana sana huku wakionyesha dhahiri kuwa hawana 'Match Fitness' na huenda pia huko kukaa Wiki Mbili Ligi Kuu ya VPL Kusimama Kumechangia Mpira mbovu walionao Simba SC sasa na ule walioucheza leo Kipindi cha Pili.

5. MTIBIENI VYEMA MUGALU NA MMWAMBIE LWANGA KADI ZA NJANO ZISIMZOEE
Leo tumeona kabisa Pengo la Chris Mugalu katika Ushambuliaji akiwa kama Pacha wa John Boko Magoli na la Thadeo Lwanga katika Kiungo cha Ukabaji kiasi kwamba ilimlazimu Kocha abadili Mfumo na Kucheza na 'Double Pivot' katika Nafasi ya Kiungo cha Kukaba.

Tafadhali Chris Mugalu atibiwe upesi Majeraha yake ili kstika Mechi na Azam FC katika ASFC awepo lakini pia Thadeo Lwanga nae aambiwe aepuke mno hizi Kadi xa Njano na Nyekundu anazozipata mara kwa mara kwani huwa zinaigharimu Timu katika sehemu hiyo Muhimu ya Kiungo cha Ukabaji.

6. KIPA BENO KAKOLANYA KAPOTEZA KABISA KUJIAMINI NASHAURI ATAFUTWE KIPA MKUBWA WA KUMPA CHANGAMOTO KIPA AISHI MANULA
Kama isingekuwa Bahati tu leo Kipa Beno Kakolanya 'angeigharimu' Simba SC kutokana na Udakaji wake mbovu, usio wa Kimakini huku akiwa amepoteza Kabisa 'Kujiamini' ili atufungishe 'Kizembe' Magoli karibu matatu.

Sijui ni kwanini Kocha Mkuu Gomez hataki kumpa nae ( Kipa Kakolanya ) game time ili 'Kujiamini' Kwake kurejee kwani 'technically' imeonyesha kuwa Matukio ya Kizembe aliyoyafanya leo ni kwakuwa amelizoea mno Benchi.

Nashauri kama Kocha Gomez hamuamini Kipa Kakolanya basi auombe Uongozi wa Simba SC utafute Kipa bora kumzidi Aishi Manula (tena awe ni wa Kigeni) ili Simba SC iwe na hazina ya Uhakika ya Makipa Wawili au Watatu ambao watakuwa na Msaada mkubwa kwa Timu katika Michuano ya ndani na ile ya nje (Kimataifa)

7. WACHEZAJI WAPUNGUZE SANA ANAO ANAO ( SHOW GAME ) KWANI WANAKARIBISHA KUCHEZEWA RAFU ZA KUWAWEKA NJE KWA MAUMIVU
Haoa nieleweke vyema tafadhali sisemi kuwa Simba SC iachane na 'Culture' yake ya 'passing and flowing game' wenyewe mnaita Pira Biriani, Pira Sambusa na Pira Sharma bali ichezwe kwa uangalifu mkubwa ili Wachezaji wetu wasiwe wanaumizwa 'Kimakusudi' na Wachezaji wa Timu Pinzani na wasije 'Kuigharimu' Timu kwa Kutokuwepo ( Kutokucheza ) Kwao.

Tafadhali namalizia kwa Kusisitiza kuwa Simba SC isirudie tena Kucheza Mpira mbovu ilioucheza leo Kipindi cha Pill dhidi ya Mbeya City pale ikicheza na Azam FC Kombe la (ASFC) tarehe 26 June, 2021 na ikicheza na Yanga SC (VPL) tarehe 3 July, 2021 kwani kuna hatari Simba SC ikafungwa na Azam FC na 'Kulitema' Kombe la ASFC na pia ikafungwa na Yanga SC katika VPL na tukachukua Ubingwa ila tukiwa na Jeraha Kubwa la Kufungwa nao.

Huu ni Uchambuzi wangu tu wa Kimtazamo Mimi GENTAMYCINE na sikulazimishi uukubali japo umalazimika Kuuheshimu kama ambavyo nami pia nitaenda Kuiheshimu yenu.
Mjasiri haachi asili!! Harufu ya uto haikuachi salama!
 
Hao jamaa jana sijui walikula maharage ya wapi?! Kuna muda hadi matola alisimama na kusema mambo gani hayo mnafanya ilikuwa kati ya Kennedy na Nyoni hapa na hapa walipeana pasi za hovyo kabisaa! Kuhusu kakolanya alichagizwa pia na ubovu wa safu ya ulinzi mbeya city walifika sana kwenye box la simba hii ni hatari sana kwa timu zenye washambuliaji hatari
Timu ipi ina washambulizi wazuri? Nitajie pia timu nzuri duniani ambayo huwa haifungwi! Kufungwa kwa simba jana ni matokeo ya kawaida ya mpira wa miguu. Huwezi ukahukumu uzuri au ubovu wa timu kwa kigezo cha mechi moja au mbili. Kitaalam hutumika mechi tano mfululizo kuamua form ya timu kwa wakati husika.
Portugal kafungwa 4 juzi na Ujerumani, na mabeki kisiki walijifunga magoli 2!! Je Portugal ni timu mbovu? Hao ndik mabi gwa watetezi!! Bale juzi kakosa penati!! Je Bale ni mchezaji mbovu? Ndio maana makocha makini hawamnyimi mchezaji kupiga penati eti kwa sababu penati iliyopita alishindwa kufunga!! Ni kweli jana Simba walijichanganya kipindi fulani cha pili, wakasababisha goli! Lakini walijirekebisha na mambo yakamalizika vizuri! Ronaldo ni mpigaji mzuri sanà wa penati lakini kuna penati zingine hushindwa kufunga! Huo ndio utamu wa mpira!!
 
Back
Top Bottom