Tuambiwe ukweli, Kassim Hanga, Abdulaziz Twala na wengine wote wamelala wapi? Halafu tusameheane

Tuambiwe ukweli, Kassim Hanga, Abdulaziz Twala na wengine wote wamelala wapi? Halafu tusameheane

Asante kwa majibu.

Kama nitakuwa sikubebeshi mzigo mzito, Naomba msaada wa hili.
Labda, kwa kunisaidia ili niwajue vizuri; naweza kupata wasifu wa kila mmoja mpaka muda wanatoweka? Yaani hasa shughuli walizokuwa wakizifanya na hata ukaaji wao kwa jamii na mahusiano yao na uongozi wa nchi kwa wakati huo.

Natanguliza shukrani.
Historia yao inasisimua Sana. Nenda YouTube tafuta Amani Thani alikuwa Katibu mkuu wa Hizbu nae ni mmoja wa wahanga wa Yale mapinduzi, hakika hutachoka kumsikiliza.
 
Asante sana, Mkuu. Kwa maelezo ya kina. Mkuu, Post yako ime'summarise' vizuri sana maelezo mengi niliyopitia jana juu ya K. Hanga (R.I.P).

Pia nashukuru, Umeniwezesha leo kumuona 'mtanzania' mwenzetu Elena. Nina imani, akiamua kurudi nyumbani tutamkaribisha.
Ingawaje inasemekana Hanga alifanya uhuni wa Kiafrika lakini bado Elena aliwahi kwenda Zanzibar ingawaje hakuwahi kumfahamu babake!

Inasemekana Hanga alikuwa very disappointed kusikia amezaliwa mtoto wa kike, kiasi kwamba akakata kabisa mawasiliano na familia yake iliyokuwa Russia.
 
Ila mimi sijaelewa lengo haswa la lisu kuhusu muungano. Lakini ikipendeza turudiwe na Tanganyika yetu.
Nchi mbli zilizppata uhuru zimeungana ikawa nchi moja... ila Kuna moja haipo kbs ndo tunaitaka Tanganyika
 
Ingawaje inasemekana Hanga alifanya uhuni wa Kiafrika lakini bado Elena aliwahi kwenda Zanzibar ingawaje hakuwahi kumfahamu babake!

Inasemekana Hanga alikuwa very disappointed kusikia amezaliwa mtoto wa kike, kiasi kwamba akakata kabisa mawasiliano na familia yake iliyokuwa Russia.

..binti wa Hanga atakuwa amepata shida sana ktk ukuaji wake.

..kwanza, kuwa mtu aliyechanganya damu ktk nchi yenye ubaguzi.

..pili, ni kukua bila kupata malezi na mapenzi ya baba yake.

..tatu, baba yake kupoteza maisha ktk mazingira yasiyoelezeka.
 
Historia yao inasisimua Sana. Nenda YouTube tafuta Amani Thani alikuwa Katibu mkuu wa Hizbu nae ni mmoja wa wahanga wa Yale mapinduzi, hakika hutachoka kumsikiliza.
Aisee...nemeenda kuzifatilia. Nimeangalia moja ya 3/5. Mzee anatoa maelezo yanayofikirisha sana.
 
Hili ni suala la kidini na wala si kisiasa kama linavyolitafsiriwa na wengi, this is the so called Islamophobia of that time.
 
Tafuta KUMBUKUMBU ZA MZEE AMAN THANI AKIELEZEA ALICHOKIONA NA YALIOMFIKA
Ni vizuri kufanya hivyo kwa kuanzia lakini ki ukweli Historia ya Zanzibar (including ya Tanzania yenyewe) imejaa sana biases, kwahiyo ukitaka upate kitu ambacho ni tangible kidogo lazima upitie sources nyingi sana kutoka kwa watu tofauti.

Pata maelezo ya watu wa Umma, ASP, ZNP na ikibidi tafuta hadi declassified intelligence sources kama vile za CIA ambazo zilifichua uhusika wa moja wa moja wa CIA kumshawishi Mwalimu kuleta muungano na ZNZ kwa sababu tu CIA na Western Countries kwa ujumla waliyaogopa sana Mapinduzi ya Zanzibar na kuiona ZNZ kama the Next Cuba in Africa!

Tena vile walivyoona mtu kama Abdulrahman Babu alikuwa na watu wake China, huku akipeleka vijana wake Cuba kuchukua mafunzo ya kijeshi na kwa upande mwingine akina Hanga nao wakiwa na watu wao Soviet Union, CIA wakaona ZNZ ni Shipa, na dawa yake ni kuwaunganisha na Tanganyika ili hatimae kui-dissolve!
 
..Vyombo vya dola, na CCM, wamekuwa kimya kuhusu suala hili kwa muda wote.

..Hawaelezi kwanini walikamatwa. Na haielezwi nini kiliwakuta. Na haielezwi miili yao iko wapi.

cc Mohamed Said
Msimamo wa tasnifu ya kiwanuka ni kuwa hya ilibidi yafanywe ili kulinda umoja wa kitaifa, ni kama tu mauaji ya kina sheikh Aboud Rogo kule Kenya.
 
Hapa Hanga (R.I.P) alituangusha waafrika. Hata hivyo, ni mapungufu ya kibinadamu yanaweza kusameheka.
Of course, tena ukizingatia kwa nyakati zile bado Waafrika tulikuwa na ujinga ujinga mwingi kichwani! No wonder hata Elena hakujali na hatimae kwenda kutafuta asili yake!

And I'm very certain kama Hanga angekuwepo hai, lazima tu angemtafuta binti yake, sema ndo hivyo tena alitangulia mbele za haki mapema sana, tena akiwa bado kijana!
 
Msimamo wa tasnifu ya kiwanuka ni kuwa hya ilibidi yafanywe ili kulinda umoja wa kitaifa, ni kama tu mauaji ya kina sheikh Aboud Rogo kule Kenya.

..tangu auwawe mpaka leo hii huo umoja wa kitaifa umepatikana?

..na walioketi na kubuni huo mpango wa kulinda umoja wa kitaifa na kumtoa roho mwenzao ni kina nani?
 
..binti wa Hanga atakuwa amepata shida sana ktk ukuaji wake.

..kwanza, kuwa mtu aliyechanganya damu ktk nchi yenye ubaguzi.

..pili, ni kukua bila kupata malezi na mapenzi ya baba yake.

..tatu, baba yake kupoteza maisha ktk mazingira yasiyoelezeka.
Tena sana... back in the days niliwahi kuangalia show moja ambayo iliwakutanisha Elena, binti wa Muhammad Ali (US Boxer) na mama mmoja wa mwandishi wa Loss Angeles Times.

Hapa walikuwa wanaelezea historia zao as blacks in Russia.
 
..tangu auwawe mpaka leo hii huo umoja wa kitaifa umepatikana?

..na walioketi na kubuni huo mpango wa kulinda umoja wa kitaifa na kumtoa roho mwenzao ni kina nani?
Ukitaka kufahamu ukweli juu ya vita dhidi ya uislamu isome historia ya Tanganyika kabla, wakati na baada ya ukoloni. Moja ya mifano hai ni kutekwa na kuuawa kwa watu hao.
 
Msimamo wa tasnifu ya kiwanuka ni kuwa hya ilibidi yafanywe ili kulinda umoja wa kitaifa, ni kama tu mauaji ya kina sheikh Aboud Rogo kule Kenya.
Ulikuwa unajaribu kusema nini hasa?! Kwamba mauaji ya akina Abdallah Kassim Hanga ilikuwa lazima yafanyike ili kulinda umoja wa kitaifa?! Kama jibu lako ni NDIYO, unaweza kutueleza hapa ni kwa namna gani na taifa lipi ambalo umoja wake ulikuwa mashakani kutokana na uwepo wa akina Hanga?!
 
Napigilia msumari hapo.

Huwezi ukamsikiliza LISSU kisha ukamchoka.
 
Ukitaka kufahamu ukweli juu ya vita dhidi ya uislamu isome historia ya Tanganyika kabla, wakati na baada ya ukoloni. Moja ya mifano hai ni kutekwa na kuuawa kwa watu hao.

..mimi nadhani suala hili linachoma bila kujali imani za victims.

..Na ninapenda HAKI sawa kwa watu wote.
 
Ulikuwa unajaribu kusema nini hasa?! Kwamba mauaji ya akina Abdallah Kassim Hanga ilikuwa lazima yafanyike ili kulinda umoja wa kitaifa?! Kama jibu lako ni NDIYO, unaweza kutueleza hapa ni kwa namna gani na taifa lipi ambalo umoja wake ulikuwa mashakani kutokana na uwepo wa akina Hanga?!
Hiyo ni kwa mujibu wa tasnifu ya kiwanuka si Mimi, hembu rejea tena uthibitishe. Na lengo langu katika hilo ni kuonesha kuwa wapo watuwanaounga mkono matukio kama haya.
 
Hiyo ni kwa mujibu wa tasnifu ya kiwanuka si Mimi, hembu rejea tena uthibitishe. Na lengo langu katika hilo ni kuonesha kuwa wapo watuwanaounga mkono matukio kama haya.
Na ndio maana katika moja ya posts zangu hapo juu nikasema kuielewa historia ya Zanzibar (in fact ya Tanzania kwa ujumla) ni lazima mtu atumie multiple sources kwa sababu imejaa biases nyingi sana!!

Mfano mzuri, hadi kesho Wanazi wa CCM kutoka ASP bado wanamuita SAS kama Mwarabu kwa sababu alikuwa ZNP! Wakati huo huo wanasahau au hawataki kuisema kweli kwamba SAS huyo huyo pamoja na kuwa ZNP ("Chama Waarabu"/Hizbu), ni yeye na wenzake "Waarabu" walijitoa ZNP na kuunda Umma Party kwa ajili ya kupambana na serikali iliyokuwa chini ya Sultan!!

Ni "Waarabu" hao hao kutoka kundi la SAS/Umma ndio miongoni mwao walienda Cuba kuchukua mafunzo ya kijeshi ili kuja kupambana na serikali ya Sultan:-
Umma Party.png
Na wala hawataki kusema jinsi mmoja wa hao "Waarabu" anayeenda kwa jina la Abdulrahman Babu jinsi ambavyo ofisi yake ilivamiwa na polisi wa Sultan na kisha Babu kutupwa jela baada ya kukutwa documents zilizo-highlight namna ya kufanya mapinduzi ya Serikali ya Shamte iliyokuwa chini ya Sultan!!

Hawa akina Hanga na akina Babu, mwanzoni ingawaje walikuwa vyama tofauti (Babu na wenzake Umma Party, Hanga na wenzake ASP) lakini wote walikuwa na nia moja ya kuondoa kwa nguvu Utawala wa Kisultani!!

Ukweli ni kwamba, Mzee Karume alikuwa anawaogopa sana Wasomi wa ASP na wale waliokuwa Umma Party na ndio maana mwanzoni kabisa mwa utawala wake, karibu wote aliwaweka mbali na SMZ kama vile wengine kuwapeleka ubalozi kama vile akina SAS na Omari Sharrif, na wengine kuwapeleka Bara kwenye Serikali ya Muungano kama ilivyokuwa kwa Babu na Hanga!

Kwa upande mwingine, mtu kama Babu alikuwa haaminiki hata na Nyerere na bila shaka kutokana na misimamo yake ya kimapinduzi/kikomunist!

Ukaribu wa Hanga na Oscar Kambona na wenyewe ulishakuwa red alert kwa Mwalimu hasa baada ya Kambona kuanza kupinga sera za Mwalimu na hatimae kukimbilia UK!

Kwahiyo madai kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya usalama wa taifa ni porojo tu za Team Karume!!!
 
Back
Top Bottom