Tuamke, tuwaamshe mizimu wetu, katika nyakati za hatari watusaidie

And why should I trust what u have just said??
 
Ujinga ndio dhambi kubwa kuliko zote, ukifuatiwa na uongo, mawili haya yanakupa dhambi ya tatu, uuaji, hii ni matokeo
 
Bado hatujakupata faraghani pm
 
Wewe hujitambui.
Wewe hujitambui zaidi, kwa sababu umeshindwa kujibu maswali yangu.

Umeshindwa kuthibitisha Mungu yupo. Umeshindwa kuondoa contradictions katika dhana ya kuwepo huyo Mungu.

Unaamini katika vitu ambavyo huwzi kuvielezea vikaeleweka.

Sasa kati yako unayeamini katika vitu ambavyo huwezi kuvielezea, na mimi ninayekuuliza maswali ambayo hujaweza kuyajibu, nani hajitambui hapo?
 
Kiranga haamini ana taka kujua. Kwa Maelezo yake ukishajua hupaswi kuamini
Tatizo ninaojibizana nao wengi hata tofauti kati ya kuamini na kujua hawafahamu.

Wanafikiri kuamini ni kujua.

Hata hawajiulizi, kama kuamini ni kujua ukweli, inakuwaje sasa tuna dini tofauti zinaamini miungu tofauti, zote zina mamia ya mamilioni ya watu wanaamini vitu tofauti.

Kama kuamini ni kujua kweli, mbona hawa watu tofauti wanaamini vitu tofauti? Ina maana vitu vyote tofauti wanavyoamini ni kweli kwa mpigo?

Haiwezekani, maana vingine vinapingana, haviwezi kuwa kweli vyote.

Sasa mtu atajuaje anachoamini kwenye dini yake ni kweli na si upotovu?
 
Hivyo ni wajibu wa kwanza kwa kila binadamu, kuutafuta ukweli kwa gharama yoyote ile
Na kweli ni nini????..............KWELI ni NENO la MUNGU, na neno la MUNGU ni YESU KRISTO, hivyo basi YESU KRISTO ndiyo njia, kweli na uzima, mtu hataenda kwa MUNGU pasipo kupita kwa njia ya YESU KRISTO; hiyo ndiyo KWELI!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…