Tuamke, tuwaamshe mizimu wetu, katika nyakati za hatari watusaidie

Tuamke, tuwaamshe mizimu wetu, katika nyakati za hatari watusaidie

Kumbe unajua kuna mtu anaitwa YESU KRISTO?? Sishangai hilo jina unalomwita sababu anamajina mengi tu, JESUS, YESU, JEZUS, GESU, יֵשׁוּעַ ,يسوع, 耶稣, Ιησούς, EASHOA n.k.

Sasa kama unamjua YESU KRISTO iweje basi unang'ang'ania kuabudu "mizimu" ambayo ni "mapepo"???
Hatuabudu mizimu, bali tunatambua uwepo wao na nafasi yao katika ulimwengu wa Roho, Ibrahimu, isaka na yakobo, yote ni mizimu, na hata Yagashya aliwatambua na kuwaheshimu, ya kwenu nyie watakatifu, ya kwetu site ndio mashetani????? Tunatambua uwepo wa Mungu mmoja wa kweli, jina lake ni AMEN-RAA
AHAN AHASTA MAHAN HATEKET, ANU MENTUKEHET
 
wewe unauhakika " UPI kuwa hizo mbao ziliandikwa na Mungu "" kuna ambaye alimshuhudia " Musa akikabidhiwa hizo mbao na mungu "" kama hakuna " tukisema kuwa hicho ni kisa cha kutunga tutakuwa tunaongopa "".... kwanni mungu awape " mamlaka binaadamu "" wamtangazie dini yake " wakati yeye mwenyewe anakiri kuwa binaadamu hao ni wadhaifu "" ...neno dhaifu lina nyanja pana "" yaweza udhaifu wakutokuwa wakweli "" udhaifu wakutoelewa jambo wanapoambiwa au kufundishwa "" udhaifu wa afya bora " udhaifu wa kukosa upendo " na utu " etc ..... sasa aliwezaje kumpa mamlaka "" mwanadamu ya kumtangazia dini yake "" ilahli anajua fika miongoni mwao kuna wenye udhaifu wa sifa ya kutokuwa wakweli "" Hivi kweli alikuwa haoni kuwa kwa mantiki ya udhaifu huo "" kuna hatari ya maneno yake kufikishwa ndivyo sivyo kwa vizazi na vizazi " "tokana na sifa anayoielezea kuwa binaadamu ni wadhaifu ""...
Hebu ngoja nikuulize swali dogo tu ndugu yangu hearly hivi ni nani mbunifu wa MICROSOFT hapa duniani?

 
Hatuabudu mizimu, bali tunatambua uwepo wao na nafasi yao katika ulimwengu wa Roho, Ibrahimu, isaka na yakobo, yote ni mizimu, na hata Yagashya aliwatambua na kuwaheshimu, ya kwenu nyie watakatifu, ya kwetu site ndio mashetani????? Tunatambua uwepo wa Mungu mmoja wa kweli, jina lake ni AMEN-RAA
AHAN AHASTA MAHAN HATEKET, ANU MENTUKEHET
AMEN RAA ndiye Amun Ra mkuu nitaku PM kwa majadiliano zaidi
 
Unapoingia kwenye ulimwengu wa roho, hali ya mwafirika ni uchawi wa hali ya juu' kabisa, ni makufuli kabisa yametundikwa vichwani, huvunji ni laana kubwa, ni lazima ukutane na waalimu sahihi, makuhani nyabinghi, wakufanyie DUAT MAALUMU, NDIPO UTAFUNGULIWA
mkuu nakupm lakini inagoma
 
Hatuabudu mizimu, bali tunatambua uwepo wao na nafasi yao katika ulimwengu wa Roho, Ibrahimu, isaka na yakobo, yote ni mizimu, na hata Yagashya aliwatambua na kuwaheshimu, ya kwenu nyie watakatifu, ya kwetu site ndio mashetani????? Tunatambua uwepo wa Mungu mmoja wa kweli, jina lake ni AMEN-RAA
AHAN AHASTA MAHAN HATEKET, ANU MENTUKEHET
Imeandikwa hivi; "lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi Injili yoyote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri na alaaniwe". WAGALATIA 1:8

Wewe unatuhubiria injili mpya ambayo hatukukabidhiwa na Mitume wa BWANA YESU KRISTO, basi kutokana na maneno ya Mtume Paulo hapo juu, hakika na wewe ulaaniwe!
 
Kwa mujibu wa maandiko wewe unayoamini Watu wote ni wana Mungu sasa kipi spesho hapo Yesu mpka umwite yeye pekee ndio mwana wa Mungu
YESU KRISTO ni spesho sababu yeye hakutokana na wanadamu bali alikuja duniani kutoka kwa MUNGU na kabla MUNGU hajaiumba dunia au ulimwengu YESU KRISTO alikuwa pamoja na BWANA MUNGU.

Wanadamu ni wana wa MUNGU ndiyo, lakini mwanadamu anakuwa mwana wa MUNGU pale tu anapotenda na kufanya yale yote aliyoagizwa na MUNGU. Ikiwa mwanadamu hatendi wala haishi kwa mujibu wa Amri za MUNGU, mwanadamu huyo anakuwa siyo mwana wa MUNGU bali ni mwana wa shetani.

Wana wa MUNGU ni wale tu wanaozishika Amri za MUNGU na KUITII sauti yake. Na ndiyo maana wale wanaoitii sauti ya MUNGU, atawahifadhi hai na kuwapa uzima wa milele lakini wale wote wanaotenda maovu na kuitii sauti ya shetani watachomwa moto pamoja na shetani wao.
 
bill gate "" haya leta hoja yako ""
Hebu ngoja nikuulize swali dogo tu, Bill Gates ndiye mbunifu wa MICROSOFT, sasa hebu niambie wakati anaibuni na kuitengeneza hii program wewe hukuwepo wala hukumwona, umesoma tu kwenye vitabu kuwa Bill Gates ndiyo mwanzilishi wa MICROSOFT na unaamini hivyo na kukubali. Sasa iweje unaamini sana kazi za Wanadamu kwa kusoma tu, lakini hutaki kuamini kazi za MUNGU kwa kusoma pia???

Kwanini unahoji uwepo wa MUNGU wakati kazi alizozifanya zinaonekana ikiwamo wewe mwenyewe ni kazi ya mikono yake, kila kitu unachokula ni kazi ya mikono yake, hewa unayovuta ni kazi ya mikono yake, kila kitu ni kazi ya mikono yake??

Habari za MUNGU umesoma kwenye vitabu, lakini unapinga na kuhoji uwepo wake na kazi za mikono yake unazikataa, mbona umesomo uwepo wa akina Bill Gates na kazi za mikono yao unazitumia lakini haupingi uhalali wao?? Kwanini unapinga uhalali MUNGU?
 
Pepo maana yake ni Roho, Yagashya(Yesu) hakuacha ukiristo, mliutengeneza wenyewe, aliacha Imani, na mambo mengi aliyosema hayakuandikwa yote, ukiristo ni politics za utawala, nyinyi mnaabudu, pepo jeupe tengenezo la wanadamu, na Yagashya aliyaona yote haya na kukemea, aliwajua wayahudi ni kizazi Cha ibilisi, kweli tunayo sisi, pole sana ndugu
Mkuu hebu tufafanulie kidogo,sawa yesu hata kama ni black au mweusi haiondoi utakatifu wake.

Huyo yesu unayemzungumzia wewe ndo Yule aliyezaliwa na bikira,akateswa,akafa na kufufuka??
 
Mkuu hebu tufafanulie kidogo,sawa yesu hata kama ni black au mweusi haiondoi utakatifu wake.

Huyo yesu unayemzungumzia wewe ndo Yule aliyezaliwa na bikira,akateswa,akafa na kufufuka??
Hiyo tutazungumza kwenye uzi wake
 
Back
Top Bottom