Tubadilike siyo lazima Nahodha wa timu awe Mzawa

Tubadilike siyo lazima Nahodha wa timu awe Mzawa

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Kumekuwa na huu utaratibu wa muda mrefu wa timu za Simba na Yanga kuhakikisha nahodha na wakati mwingine nahodha msaidizi ni Watanzania. Sijajuaga dhana hii ilijengwa kwa sababu gani ila naona ilishapitwa na wakati.

Kuna vigezo inabidi tuvizingatie katika kuchagua nahodha wa timu, kikubwa kuliko vyote thamani yake katika timu (awe MVP wa timu). Hapa simaanishi mshahara bali mchango au utegemezi wa timu kwa mchezaji huyo. Hapa tunazungumzia wachezaji kama Diarra, Mayele, Inonga na Chama.

Pa ufahamu mzuri wa lugha mojawapo ya kimataifa inasaidia hasa katika mashindano ya kimataifa. Pale mchezaji anapokuwa na changamoto katika lugha ya kigeni kunampunguzia kujiamini na matokeo anashindwa kuitetea timu dhidi ya waamuzi au wachezaji wa timu pinzani.
 
Wachezaji wenyeji wana uhakika wa kuwepo muda mrefu kikosini... na pia wanajua vizuri mahitaji ya Simba na Yanga hasa wakati wa match ngumu na muhimu ndio wanatumika kubeba hirizi...
 
Hii hoja haikupewa sana kipaumbele ila naileta tena hadi muielewe. Kuna vitu naviona pale Simba haviko sawa ambavyo haviwezi kubadilika hadi mambo kama haya yabadilike.
 
Hii hoja haikupewa sana kipaumbele ila naileta tena hadi muielewe. Kuna vitu naviona pale Simba haviko sawa ambavyo haviwezi kubadilika hadi mambo kama haya yabadilike.

Nani ACHUKUE NAFASI ya Boko, au shabalala?????

Labda Simba wangemsajili Bangala
Lakini hakuna mchezaji wa maana wa kuvaa KITAMBAA.

NGOMA ni mzuri lakini Bado anahitaji zaidi nafasi.


Labda kwa Yanga.
Aucho amnyanga'anye mwamnyeto.
 
Labda kama imeanza kufuatilia mpira Jana.

1. Simba imewahi kuwa na Nahodha Method Mwanjali. Beki kutoka Zimbabwe.

2. Yanga Imewahi kuwa na Nahodha WA KIGENI.

C.... i Haruna NYONZIMA

C.....ii.Papy shishimbi.

.C.. iii. Kamusoko Nahodha msaidizi.

C .. iv Lamine Moro.
 
Kuwa nahodha wa timu ya mpira wa miguu kunahitaji sifa kadhaa kama

1. uongozi bora,

2. heshima kutoka kwa wenzake,

3. mawasiliano mazuri,

4.uwezo wa kuhamasisha timu

5. uzoefu katika uwanja wa mpira.

6 kujituma kwa timu na kuwa mfano bora kwa wachezaji wenzako.
 
Nani ACHUKUE NAFASI ya Boko, au shabalala?????

Labda Simba wangemsajili Bangala
Lakini hakuna mchezaji wa maana wa kuvaa KITAMBAA.

NGOMA ni mzuri lakini Bado anahitaji zaidi nafasi.


Labda kwa Yanga.
Aucho amnyanga'anye mwamnyeto.
Una maana gani unaposema "hakuna mchezaji wa maana"? Wewe unaangalia nini?

Nahodha unahitaji mtu aliye na nguvu ya kimamlaka ndani na nje ya uwanja na hii inachagizwa zaidi na uwezo wake na utegemezi wa timu kwa mchezaji huyo.

Boko hana nguvu hiyo maana hata namba tu hana na akiingia watu wanasonya. Zimbwe amekuwa uchochoro, naye anachezea jina tu. Mechi na Wydad, alimfuata refa kwa jazba, refa akamtuliza akatulia kama piritoni.

Che Malone ana utulivu sana ila unaona anacheza kimamlaka

Kapombe anapambana sana na bado anacheza kwa ufanisi

Ngoma pia hata kama bado anaingiwa taratibu kikosini ila experience yake inatosha kumpa heshima hiyo

Mzamiru ni senior player kwa wachezaji wazawa na bado ana namba

Isingekuwa figisu anazofanyiwa, Phiri pia angefaa maana ni mtu positive sana anacheka na kila mtu (pay attention jinsi Boko alivyojitenga na wenzake)

Hata Kanoute ingawa siyo muongeaji sana anaweza kabisa kuvaa kitambaa maana hapendi ujinga.
 
Back
Top Bottom