Tubadlike: Tunapoteza asili yetu kwa kuwaiga vitu vingi wazungu na waarabu kwa kujidanganya ni dini

Tubadlike: Tunapoteza asili yetu kwa kuwaiga vitu vingi wazungu na waarabu kwa kujidanganya ni dini

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Haijalishi ni Ukristo au uislamu, hizi dini sio kwajili ya wazungu na waarabu kama watu wengi wanavyodhani, hizi dini ni kwajili ya mtu yoyote sehemu yoyote duniani.

kumekuwa na mazoea mabovu tangu zamani ya wanaoabudu hizi dini kwa kudhani kwamba ili kuabudu dini ya kiisalamu inabidi uige ige vya waarabu na ili kuabudu ukristo inabidi ufanye vile wanavyofanya wakristo wazungu.

MAJINA - Mnyakyusa wa Mbeya unamkuta anaitwa Steven, kaacha majina yake ya kinyakyusa kama Atupele, Atuganile, n.k.

Mnyamwezi kapata binti anampa jina la Ashura, kaacha jina zuri la asili kama Minza, tena mbaya zaidi hata jina la ukoo limebadilishwa kuwa la kiarabu Mohammed, hapo mtoto ataitwa Ashura Mohammed.

NDOA - Mkristo atavaa suti kama wazungu, mke atavaa shela, viapo ni vile vile ila vimetafsiriwa, honey moon, n.k. yani ni copy paste. hakuna chembe yoyote ya kutamaduni kwa asili labda kuweka mziki wa kikabila kwajili ya burudani ukumbini.

Muislamu wa bongo kwenye kuoa nako ni hivyo hivyo, ili ndoa ifane atakifuga jambia kiunoni kama muarabu, atavaa kama muarabu, n.k.

MISIBA - hapa napo ni yale yale tu.
 
Tatizo jamii imeshakariri hivyo, wakikuona unaitwa Banzi, Mkude,au Kobelo wanakuona umepotea...hakika tunahitaji kuwa wazalendo kama wenzetu wa uchina
 
Inasikitisha sana..tumeacha kuenzi majina ya mamabu zetu ndio mana tunalaana kila kona.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Si ufate wewe hizo din za asili au tamaduni zako kwani tatizo nini??!!waacheni wenye kufata din tufate mi huwa siwaelewagi kabisa yaani mnafosi kabisa eti mila za kiafrica vaeni ngozi na majani tuone matako na matiti yenu basi
 
inasikitisha sana kwakweli. Yaani tumepoteza identity kwa spidi ya 5G. Sisi wenyewe ndo wakupinga huu upuuzi. Si mzungu wala mwarabu atakuja kututoa kwenye ushenzi huu
 
Tatizo jamii imeshakariri hivyo, wakikuona unaitwa Banzi, Mkude,au Kobelo wanakuona umepotea...hakika tunahitaji kuwa wazalendo kama wenzetu wa uchina
Ni unafiki mtupu anza wewe basi kuvaa ngozi na majani tujue kweli ni muafrica hao wachina wenyewe wanaiga kila kitu kwa wazungu , mfano mavazi suti, ndoa nk mpaka teknolojia 🤣🤣🤣😂😂😂 tafuta ujue mavazi ya wachina yalivyo uone😂😂😂
 
Na ishu hii imeibuka eti birthday. Ukimuuliza Kama baba yake ama babu yake aliyafanya hawezi kukujibu
 
Wewe ulishawahi kuvaa zile nguo za asili yako kabisa?
La kuvaa zile nguo tuliweke pembeni maana hiki kizazi ni cha hovyo kwenye matamanio. Majina ya asili na zile ngoma au nyimbo zina radha yake, hakuna kubana pua wala kukausha koo...
 
Ni kweli ulichoandika ila naona tunaweza ku combine vyote pamoja. Vyakula wape watoto ma burger, wafundishe pia kula ugali na kisamvu cha karanga na kwa mikono. Harusi vaeni shela na suti baadae badiisheni vaeni nguo za tamaduni zenu. Kweye party chezeni Michael Jackson na pigeni mdumange pia. Hii itatufanya tusipoteze identity yetu.
 
Ni unafiki mtupu anza wewe basi kuvaa ngozi na majani tujue kweli ni muafrica hao wachina wenyewe wanaiga kila kitu kwa wazungu , mfano mavazi suti, ndoa nk mpaka teknolojia 🤣🤣🤣😂😂😂 tafuta ujue mavazi ya wachina yalivyo uone😂😂😂
Ila wa Africa tumezidi unakuja kafika kundi la watu idadi nyingi wana majina kama waarabu au wazungu
 
Ni unafiki mtupu anza wewe basi kuvaa ngozi na majani tujue kweli ni muafrica hao wachina wenyewe wanaiga kila kitu kwa wazungu , mfano mavazi suti, ndoa nk mpaka teknolojia [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23][emoji23] tafuta ujue mavazi ya wachina yalivyo uone[emoji23][emoji23][emoji23]
Mbona umekomalia kwenye mavazi tu? Kumbuka ufumaji wa nguo ulianzia Afrika ikiwa ni kazi ya mikono, Wazungu wakaboresha vitendea kazi.
 
➡️ **MAVAZI**Kanzu ni mavazi ya asili ya jamii ya Asia mpaka far east, kusnzia wahindi, wachina, waarabu, wayahudi hayo ni mavazi ya kitamaduni kabisa yanatofautiana tu mashono na mfumo kutokana na jamii moja na nyingine. Wale manabii walioishi kwenye jamii hizo wslivaa kuendana na jamii hayana uhusiano na maelekezo ya Mungu. Kama wangeanzia umassini wangevaa rubega

➡️UKAAJI suala la ukaaji chini ni mila za waasia wote, kuanzia wachina, wajapani , wahindi na waharabu halina uhusiano na imani. Manabii nao walikaa hivyo kutokana na jamii ssliyoikuta. Africa tamaduni zetu za asili sii kukaa chini mgeni akija hata kama huna uwezo wa kigoda utamtafutia gogo ili akae

➡️SUALA LA CHAKULA Mikate, divai, tende nk ni vyakula vya asili ya huko middle and far east havihusiani na imani. Manabii walivitumia kwa sababu walivikuta katika mazingira hayo, haiingii akilini kuacha vyakula vya asili yetu na kuiga vya wageni waliotuletea dini eti tuwe karibu na Mungu.
Mitume wangeshukia mfano Kilimacharo basi kwenye maandiko tungekuta vyakula vya ndizi , ugali na vinywaji kama mbege

➡️SUALA LA LUGHA Mungu aliumba kila jamii na lugha yake. Alifanya hivyo ili muweze kuwasiliana ninyi kwa ninyi na muwasilishe maombi kwake kupitia lugha aliyowapa maana Mungu anajua lugha zote na saa zote yupo miongoni mwa kila jamii. Kitendo cha kutumia lugha za kigeni kumuomba Mungu kwanza anatushangaa na kuona tuna mdharau kwa kutupa lugha ya Mama. Yawezekana hata baraka tunazipeleka kwenye hizo nchi tunazotumia lugha zao kusali
 
Simu, mitandao ya kijamii kama JF pia achana nayo, ni mambo ya magharibi tumeiga sio asili yetu wala ubunifu wetu.
 
La kuvaa zile nguo tuliweke pembeni maana hiki kizazi ni cha hovyo kwenye matamanio. Majina ya asili na zile ngoma au nyimbo zina radha yake, hakuna kubana pua wala kukausha koo...
Ha ha ha nilizani tuanzie hapo [emoji3][emoji3]
Vipi na simu unayotumia ku type hapa?
 
Mkuu athari za ukoloni ni zaidi ya zile zenye kuonekana kimaumbile bali ni za kiakili zaidi. We jaribu tu kuangalia hata majina yetu hapa jukwaani, avatar pamoja na lugha tunazotumia sisi wenyewe hapa jukwaani. Vyote vinaakisi athari hizo.
 
Back
Top Bottom