Tuhuma nzito kama hii ilipotolewa Bungeni, Bunge lilichukua hatua gani kulingana na sheria, taratibu na kanuni za Bunge?

Tuhuma nzito kama hii ilipotolewa Bungeni, Bunge lilichukua hatua gani kulingana na sheria, taratibu na kanuni za Bunge?

Mag3

Platinum Member
Joined
May 31, 2008
Posts
13,413
Reaction score
23,592



















Fikiria tuhuma nzito kama hii inatolewa ndani ya Bunge na Mheshimiwa Mbunge halafu ukimya unatanda. Bunge kimya, vyombo vya usalama kimya, chama husika kimya na wananchi wanaowakilishwa na huyo Mbunge kimya! Je ni woga, ujinga au ukondoo.

Watanzania hebu tutulie, tujitafakari na tujiulize kama kweli sisi ni binadamu kama binadamu wenzetu hapa duniani! Je huyo anayetoa vitisho hadi kwa Mbunge wa kuchaguliwa akiwakilisha maelfu ya wananchi, hiyo jeuri yake inatokana na nini?

Kwanini tuwe na Bunge kama chombo hicho kiko dhaifu kiasi hicho? Katika kipindi kifupi tumeshuhudia madaraka ya Bunge yakiporwa taratibu lakini Bunge kimya. Tumeshuhudia Bunge likiogopa kutumia mamlaka yake ya kuisimamia serikali na badala yake likitumika kama chombo cha propaganda cha serikali.

Tumeshuhudia jinsi chombo hicho cha kutunga sheria kilivyoshindwa kutekeleza majukumu yake hadi kufikia kushindwa kuwalinda na kuwatetea wabunge huku likiendeshwa kama tawi la chama tawala.

Kweli Watanzania wenzangu tumefikia hali ya Mbunge kumiminiwa risasi za kuweza kumuua tembo na Bunge lisiunde hata tume kuchunguza kulikoni? Hapana, si bure, kuna tatizo pahala na tatizo lenyewe ni kubwa zaidi ya tunavyofikiria, ni tatizo linalohitaji ufumbuzi wa haraka kama tunataka kubaki salama kama taifa.

Kama Mbunge kutoka chama tawala anatishwa kama hiyo video inavyoonesha akilalamika ndani ya Bunge na hakuna hatua inayochukuliwa wala taarifa kutolewa, basi huko mbele tunakoelekea kunatisha zaidi.
 
Ukimya ni sababu Mwenyekiti wao wa CCM hakutoa tamko..Magu ndiyo dira yao
Akisifu hata kama ni la kijinga Watasifu,
Akikosoa Watakosoa,
Akinyamaza nao Wananyamaza .
(Ndugai, Magufuli, Makonda) wote hao lao moja nadhani umenielewa (Unholy alliance)
The unholy trinity
Kwa mbali nakumbuka ile kauli, "watoe bungeni tuwashughulikie." Kumbe jukumu la kuwashughulikia wanaotolewa bungeni kapewa Bashite!
 
Kweli Watanzania wenzangu tumefikia hali ya Mbunge kumiminiwa risasi za kuweza kumuua tembo na Bunge lisiunde hata tume kuchunguza kulikoni? Hapana, si bure, kuna tatizo pahala na tatizo lenyewe ni kubwa zaidi ya tunavyofikiria, ni tatizo linalohitaji ufumbuzi wa haraka kama tunataka kubaki salama kama taifa. Kama Mbunge kutoka chama tawala anatishwa kama hiyo video inavyoonesha akilalamika ndani ya Bunge na hakuna hatua inayochukuliwa wala taarifa kutolewa, basi huko mbele tunakoelekea kunatisha zaidi.
Mimi nadhani mwanzo wa kutorudi nyuma ni uchaguzi huu wa Oktoba.

Taifa likishindwa kurekebisha hii hali iliyopo sasa, basi ndio tutakuwa tumetumbukia kabisa kwenye majanga.

Mapendekezo ya marekebisho aliyoyatangaza Mbowe kwenye taarifa yake na waandishi wa habari, hiyo ndio iwe 'bottomline' ya mwanzo huu wa kukataa taifa letu kuvurugwa.

Kama hapatakuwepo marekebisho ya kuzibadili sheria mbovu zinazosimamia uchaguzi na tume isiyokuwa huru, mbadala wa kuyakataa mapendekezo hayo kiubabe ni kuazimia kuwa hapatakuwepo na uchaguzi mkuu hiyo Oktoba.

Itakuwa ni jukumu la viongozi wa vyama vya siasa na asasi mbalimbali za kijamii kuwaelimisha na kuwaongoza watu wauzuie uchaguzi huo kwa kila njia zinazowezekana.

Nchi haiwezi kuendelea kuburuzwa na mtu mmoja kana kwamba ni mali yake binafsi.
 
Kwa nini tuwe na Bunge kama chombo hicho kiko dhaifu kiasi hicho? Katika kipindi kifupi tumeshuhudia madaraka ya Bunge yakiporwa taratibu lakini Bunge kimya. Tumeshuhudia Bunge likiogopa kutumia mamlaka yake ya kuisimamia serikali na badala yake likitumika kama chombo cha propaganda cha serikali.
Samahani sana mkuu Mag3, kwa kufuatilia mada yako hii na kuikatakata vipande kama hivi ninavyofanya hapa.

Maana yake ni kwamba nimerudi mwanzo kukusoma tena na yaliyomo niyaelewe. Nimenukuu kipande hiki hapo juu kutaka kueleza mwanzo wa yote haya.

Juhudi za kunyamazisha na kutia watu wote woga, na wabunge wakiwemo, mahabusi zilipoanza kutumika kwa yeyote aliyeonekana kumsema mkuu kwa lolote litakaloonekana kama baya juu yake.

Kwa mfano, kuna mtu aliwekwa gerezani miezi sita kwa kuropoka tu na kusikika akisema "Rais kitu gani bwana!"
Na kabla ya huyo wapo wengi tu waliosweka ndani kwa maneno yao tu, kama akina Lema kwa ndoto zao.

Juhudi hizi ziliendelea, lengo likiwa ni hilo hilo moja tu la kutia watu woga na kuwatisha wasihoji. Haya hayakufanyika nje kwa raia pekee, bali yaliingizwa Bungeni. Wabunge wa upinzani walionja joto ya jiwe kweli kweli, na hatimae tunaweza kusema matokeo yalipatikana. Siku hizi kama sio Zitto, unamsikia nani tena huko Bungeni akihoji baada ya Lissu kuondolewa!

Kwa hiyo, katika hali ya kwaida tungeweza kuhitimisha kwamba lengo la huyo aliyetaka aogopwe, asihojiwe kwa lolote lilikaribia kutimia; kasoro tu uwepo wa wakorofi sugu kama Zitto, na ndio maana juhudi zile zile za kuendelea kutishia zinaendelea na wala husikii mtu yeyote akikemea mambo haya ambayo hatujawahi kuyashuhudia katika taifa letu.

Mtu ambaye anapaswa kutoa sauti na kukemea, hata kwa gheresha tu, humsikii akisema lolote. Kwa sababu yanayofanyika ndilo lengo la mipango yake.
 
Mag3,
Heri kunyamaza hadi pale "moshi unaofuka utapozaa moto mkubwa" ndipo wahusika na wale washangiliaji watakapojua kwamba wanaiteketeza nyumba kwa kulea vibaya wana watukutu...
 
Sio Bunge tu hata Taasisi nyingine za.serikali zimekuwa Dhaifu hasa kwa aina hii ya Utawala tulio nao Nchi kwetu kwa sasa ,Vyombo vya Usalama vipo kimya kama vile havioni au kusikia yanayo endelea lazima ipo Sababu.

Binafsi nnaona tatizo ni Mfumo mzima wa Nchi yetu kuanzia Katiba na Sheria nyinginezo ,zinatoa mwanya kwa Wanasiasa wabovu kutawala na kupelekea matokeo mabovu kama haya.Tumeona C.A.G. alie ondoka na alie teuliwa namna walivyo tishwa/Sheria zinavyo kanyangwa na Watawala.
 
daah.. aiseee.. tena anasema mengine mabaya siyasemi, ina maana ana mengi ya kusema lakini anaogopa asije kuuwawa
 
Bashite ni mbuzi jike alikuwa kwenye joto sasa USA imeishamwambia nyanyua mkia tukushughulikie
 
Kwalugha rahisi ni kua Makonda alimwambia bosi wake kua mimi nitawashughulikia wote wanaokupinga wewe nilinde tu; Boss akamwambia endelea na kazi upo salama kabisa.
Sikujua kua kuna siku tutakua na kikundi kidogo hatari namna hii ndani ya muda mfupi hivi; je akiendelea kukaa miaka mitano zaidi hicho kikundi nani atakibomoa?
 
Sio Bunge tu hata Taasisi nyingine za.serikali zimekuwa Dhaifu hasa kwa aina hii ya Utawala tulio nao Nchi kwetu kwa sasa ,Vyombo vya Usalama vipo kimya kama vile havioni au kusikia yanayo endelea lazima ipo Sababu.

udikteta1.jpg
 
Ingekua Kenya wangekua washaandamana, ila kwa Tanzania hii wanaounga mkono matendo haya ni wengi kuliko wanaoyapinga.
 
Duh...!, sijui haya yalisemwa lini, ila kama ni zamani, Makonda aliishaitwa kuhojiwa na
Bunge, ila pia Spika ni mwelewa anatambua kuwa...


P
 
Back
Top Bottom