Tuhuma za Askofu Josephat Mwingira zimehanikiza umuhimu wa kuundwa haraka kwa Tume ya Ukweli na Maridhiano ya Taifa

Wengine wamefika mbali na kuiomba serikali ichukue hatua za kisheria dhidi ya vyombo vya habari i.e redio, TV, magazeti, YouTube channels zilizosaidia kurusha matangazo hayo ikibidi vinyang'anywe leseni, vifungiwe au vionywe
Na kama angeamua kuyasemea hayo kwenye stand ya mabasi pale Mbezi kituo kile kingefungwa
 
Hili ni swali zuri sana. Uthibitisho wa madai ya mwingira uko wapi?
Umetaka akakuambia hana?

Amesema mashamba yake na trekta zake ziliharibiwa, hilo linahitaji uthibitisho wa macho tu...

Kuna akina Freeman Mbowe nao mashamba yao na mali zao ziliharibiwa chini ya usimamizi wa kiongozi mteule wa Rais Magufuli (Mkuu wa wilaya - Hai - Kilimanjaro) mchana kweupe huku kesi ikiwa mahakamani....

Kuna uthibitisho gani unataka kama hata macho yenu hayaoni...??
 
Bado hawa hawajaibuka na kusema waliyotendewa
Mo Dewji
Askofu Kakobe
Roma Mkatoliki
Zakaria Tarime
Endeleza.......
 
Kama hukuathirika na utawala wa Magufuli, huwezi kuelewa maana na mantiki ya hoja hii...

Lakini kudhulumu haki na uhai wa watu ni kosa ambalo halikosi kuwa na hukumu ya adhabu kubwa sana kwa kiongozi yeyote mwenye mamlaka toka kwa Yehova Mungu mwenyewe....

Wenye akili hutubu (hukukiri au hukubali) makosa, wakatengeneza na kujenga mahusiano mapya...

Wasio na akili hushapaza shingo na mwisho z8kavunjika...!
 
Kwa Tabia alokuwanazo Magufuli, kuna uwezekano mkubwa Mwingira anasema ukweli. Kama Tundu lissu alipigwa na mgambo wa wahuni then Magu ndo alikuwa kiongozi wa wahuni mwenyewe.
Mimi naamini ni kweli tupu kwa sababu ya circumstantial evidence ya aina ya uongozi na utawala wake...!
 
Halafu kukatokea nini...?

Kwa lugha nyingine ni kuwa kila ulichopost hapa kwa madai ya kutendwa na Mwingira, ni makosa ya jinai...

Kama ni kweli alifanya hivi, alishtakiwa? Na mwisho hukumu ilikuwaje..?

Kumbuka jinai hushughulikiwa na serikali...
 
Nadhani tusitishane na Sheria...Zilikuwepo sheria na watu walizitumia kwa kujilinda wao, lakini leo hawapo Duniani na Dunia inaendelea. Watuhumiwa wa masuala haya nao waje hadharani kujibu hoja moja baada ya nyingine. Atakaye shindwa na mjadala wa hoja hizo akae kimya.
 
Unakurupuka tu kusema ni awamu ya tano, unajua hizo mali zake ziliharibiwa mwaka gani?

Mkiwa waongo muwe na kumbukumbu nzuri...Maana naona kila muovu anatamani uovu wake utumike kuisulubu awamu ya tano iliyowaweka hafharani waovu wengi....

Kumbe kwa usahihi wako wewe, hizo mali ziliharibiwa mwaka na awamu gani eti...?

Na unapojibu kumbuka, tangu Uhuru hadi sasa TANU/CCM ndiyo wenye awamu zote...

So whatever "awamu is", it doesn't make any difference kwa sababu CCM ni CCM tu na serikali ni ileile...
 
Nakubaliqna na wewe...

Na hii ndiyo mantiki ya hoja yangu kuu ktk andiko langu...

Kwamba, suluhu hapa ni kukaa chini wote wanaolalamika/tuhumu na wanaolalamikiwa/tuhumiwa na kila mtu ajibu tuhuma zake na kisha kama ni kusameheana, tunasameheana...

Na kama kuna wa kuwajibika kwa mujibu wa sheria watawajibishwa na kama kuna wa kufidiwa, wafidiwe...

Huu ndiyo utaratibu wa ki Mungu kumaliza matatizo...
 
Kungekuwa na uovu kama huo mnao jisemesha wabunge na viongozi wenu wangeunga mkono juhudi??.

Mlivyo na akili fupi utasema walinunuliwa.
Ukiulizwa unaushahidi utakodoa mimacho tu.
Yani mtuakitoka chadema kwenda ccm amenunuliwa, yani mnaamini mtuhawezi kwenda chama kingine kwa maamuziyake binafsi bila kununiliwa.

Hebu nikuulize!.

Lowasa na sumaye walivyo hamia chadema kutoka ccm mliwanunua sh, ngapi????.
 
Anza wewe sema ulizulumiwa nini, pengine hapo ulipo unafuata mkumbotu hata hujui wanao lalamika malalamikoyao msingi wake ni nini,we unaunga telatu bilakujua unakokwenda mbaka ukitumbukia bondeni ndio akili inakukaa.
 

Lowassa alihamia CDM akalipa ili apewe nafasi ya kugombea urais maana aliikosa CCM. Sumaye alizira na akaona pa kujifichia ni CDM. Ila zaidi ya 90% ya walioenda kuunga juhudi walinunuliwa ama kutishwa, japo waliahidiwa nafasi hizo hizo iwapo watahamia CCM. Pale ndio tuliona chaguzi za kishenzi na kihayawani kupata kutokea hapa nchini. Ukweli huu hata mtumie nguvu kiasi gani hamuwezi kuuondoa.
 
Hii tabia itaendelea kujitokeza ,watu kutoa shutuma dhidi ya serikali iliyopita .
Kwa ajili ya kujipatia umaarufu .
Ni siasa zisizokuwa na mantiki Kwa taifa..
Tunatakiwa tuwe na siasa za kusema kwel.
Na sio umalaya wa kisiasa

Kwa taarifa yako ikitokea tume huru kudhibitisha uovu uliofanywa na awamu ya tano, kila kitu kitawekwa peupe. Usidhani vitisho ndio vitazuia huo ukweli wa uovu uliofanywa na Magufuli. Mnaweza kutishia watu leo au kesho maana serikali hii imepatikana kwa uovu wa utawala wa Magufuli, lakini ukweli huo utakaa wazi tu taka msitake. Namna pekee ni kuunda tume ya maridhiano, na tufunge ukurasa wa uovu ule kisha tusonge mbele. Uzuri uovu ule tumeshuhudia kwa macho yetu na kuusikia.
 
Hili ni swali zuri sana. Uthibitisho wa madai ya mwingira uko wapi?

Hivi mnadhani uovu ule ilikuwa siri sana, ama kwakuwa watu waliingia hofu ya kusema ukweli kwa kuogopa kutekwa na kuuwawa, hivyo mnadhani hakuna udhibitisho?
 
Kwahiyo Lowasa alikuja na pesa akalipia hiyo nafasi ya uraisi ndio akaruhusiwa kugombea urais??.
Nawewe ndio aina ya wapigakelele humu mnaetaka kupewa nchi muogoze watu???
Ndio aina ya watukama wewe mnataka serikali iache kazizake isikilize maombi uchwara haya ya maridhiano yasiyo eleweka??.
Ngoja mwenyekiti wenu na miga aionehii comments yako.
 

Naona unafikiri mimi ni wa kubahatisha, pitia nyuzi zangu zote kuhusu ujio wa Lowassa ndani ya CDM. Nilisema kabisa kuwa Lowassa alitoa pesa kwa viongozi wa CDM chini ya Mbowe, wakafanya maamuzi ya kipuuzi kabisa kumpa nafasi ya kugombea kupitia CDM, wakati hakuwa na imani, wala hatakuwa na imani au mapenzi na CDM. Na kama ni pesa viongozi wote hutoa kwa makundi ya wapambe wao ili kuwasadia kwenye propaganda na kampeni. Ukimtoa Nyerere, ni kiongozi gani aliwahi kuwa muadilifu, kiasi kwamba ushangae Lowassa kupewa nchi?

Inaonekana ukiongea kwa kupanick utafanikiwa kututoa kwenye hoja yetu ya maridhiano. Ukweli mchungu ni kuwa Magufuli alikuwa rais muovu, na hakustahili kukalia kiti cha urais, bali alipaswa kuishia kwenye uwaziri mkuu, kwani hakuwa na busara ya kiti cha urais. Kwahiyo usitake kuongea kwa jazba na kuchanganya changanya sijui Lowassa, sijui serekali iache kazi zake as if serikali ina watu special sana, kiasi kwamba hawana muda na kushughulikia ukweli wa uovu ule.

Kinachowafanya muuongee kwa jazba ni ukweli wa uovu wa Magufuli kuwekwa hadharani, hivyo muushughukie ili tupate maridhiano au muache hilo mtajua nyie, lakini hamuwezi kuzuia sisi kusema ukweli wa uovu ule.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…