Tuiachie Serikali itoe majibu ya nani anahusika na shambulio la Lissu, msituchanganye wananchi

u nailed it mkuu tatizo wanadhani sis watanzania wote ni wajinga
 
fuatilia msimamo wake kwenye tume ya katiba ulikuwaje sio unaongea tu .nji huijui kijana
 
Nilitarajia katika hiyo orodha usema pia alikuwa nani muhusika...Maana nyingi tu zimebaki ni watu wasiojulikana.
 
hili bandiko la HOVYO heri ungelibakisha kulekule instagram kwenye followers wako ambao wanakukubalia kila kitu kuliko humu ambako kuna watu wanaojielewa na wenye mawazo huru ambao huwezi kuwapangia maoni maana kule unawablock wenye uelewa mkubwa unabaki na mbulula wanaokuitikia kila unachowaandikia FACT FACT FACT.

kwanza ulichoandika kinakiingiza chama chako na serikali ya CCM kwenye UTATA kwamba ni kweli hayo mambo uliyoyaorodhesha yamefanyika katika vipindi tofauti vya serikali ya CCM ila mnachotaka kufanya ni kuitoa awamu hii kwenye UTATA huo kitu ambacho HAKIWEZEKANI,RAIS mwenyewe kwa kauli zake anasema maneno kama SIJARIBIWI,UKIWATOA BUNGENI WAKIWA URAIANI HAWANA KINGA TUTAWASHUGHULIKIA,anawaambia wana usalama kwamba NI HERI MVUNJE SHERIA MKILINDA RASILIMALI ZETU kweli?

FACT ni kwamba matukio yoote mabaya yaliyofanyika hakuna suluhisho lolote lililopatikana so far,amepotea ben saanane serikali haina majibu,mtu kavamia studio usiku ameambiwa kwa jeuri apige kazi,NAPE katishiwa BASTOLA na ingekuwa ni uchochoroni wangemshuti hakuna chochote kilichofanyika,wametekwa watu wameteswa mpaka leo hakuna majibu na kikawaida haya matukio mtu tu mtu akurupuke alikotoka akafanye matukio kama haya anakamatwa mchana kweupe.Niwakumbushe tu hizi ni ZAMA zingine sio ZAMA mlizopitia nyie ujanani enzi za mwalimu uelewa wa mambo umeongezeka na mnayoyafanya yanazidi kuwafumbua macho watu na tutafika mnapopataka tufike.
 
fuatilia msimamo wake kwenye tume ya katiba ulikuwaje sio unaongea tu .nji huijui kijana
Hakuna unachokijua we mzee! Msimamo wake ulikuwa upi?! We unataka kusema Senkondo ambae tangia hapo hakuwa mwanasiasa mwenye msimamo mkali ndo aligeuka kuwa mwenye msimamo mkali kwenye mkutano wa wajumbe ambao ndani yake kulikuwa na wajumbe wenye itikadi za CUF ambao ulikuwa huwaambii chochote kuhusu muungano? Nini kwenye katiba ile ambacho kilikuwa hot kama sio suala la Muungano?! Ni wajumbee kutoka upande upi wa muungano ambao ulikuwa huwezi kuwaambia chochote linapokuja suala lla Muungano?

Kawadanganyeni maju'ha ya Lumumba.
 
Lini hiyo serekali ilitoa majibu mbona kwa shekh ponda haikutoa sanasana utasikia watu wasio julikana basis kwisha
 
Ni kweli Rais hakuwa magufuli lakini alikuwa member wa baraza la mawaziri! Watch it!
 
- Nimesema hivi Mwangosi aliuawa nikiwa nimerudi Bongo, na haikuwa MWaka 2002 so relax tafuta hoja ya msingi na infact Rais hakuwa Magufuli

le Mutuz
Yaani nilikuwa nakuheshumu Sana.
Unataka Kujustify nini?
So kama mambo hayo uliyotaja hayakutokea kipindi chake so INA thibitisha kipindi hiki haiwezekani kwake?
Sikulaumu sana .
Maisha yalivyo magumu Na Wewe huna kazi ya Maana mjini umepata pa kula Hata viatu utawasafishiaaaa.
Jamani tusimlaumu hiyo Ndo kula yake
Njaa isikieni hivi hivi ukiangalia kwenye URITHI hayumo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Polisi wamesema wanataka taarifa toka kwa wananchi
Waambieni wasome JF taarifa zipo nyingiii tu mbona. Au mnataka tuweke 'crime stoppers hiyo unapiga tuu hakuna anayetaka kujua wewe nani wanachohitaji taarifa'
 
Let the people speak it cures many hidden sorrows... Let them speak to lessen the bite inside them! Let them speak so that you can know their thoughts n the TRENDING!
protect them! Protect their speech even if it sores you... AND THEN ACT ACCORDINGLY... because you are not perfect

Jr[emoji769]
 
Ninamkumbuka mzee kingunge alisema huyu alistahili kuwa mnyampala wa Barabara na si vinginevyo sasa yametimia
 
Magufuli amejaa damu mikononi ya Lissu na wananchi wa Kimara wanaobomolewa makazi yao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…