Tuijue Katiba: Rais akifia madarakani, basi makamu wake aliyegombea naye akapigiwa kura anarithi. Je, vipi kama makamu hakupigiwa kura?

Hapa inabidi uwe specific, akichagua mbunge aliyepigiwa kura kama mbunge? Vipi hapo?
 
Ibara ya 50 (2)(d) inampa mamlaka Makamu wa Rais aliyeteuliwa (ambaye hakuchaguliwa) kushika madaraka ya rais endapo rais atafariki.

Soma hapa.

50.-(1) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi, mtu aliyechaguliwa, au kuteuliwa kwa mujibu wa ibara ya 37(5), kuwa Makamu wa Rais, bila ya kuathiri masharti mengine ya ibara hii, atashika kiti cha Makamu wa Rais kwa muda wa miaka mitano tangu alipochaguliwa kuwa Makamu wa Rais.

(2) Makamu wa Rais atashika kiti hicho hadi-
(a) muda wake utakapokwisha;
(b) akifariki dunia akiwa katika madaraka;
(c) atakapojiuzulu;
(d) atakapoapishwa kuwa Rais baada ya kiti cha Rais kuwa wazi;
 
Ibara ya 37 (5)
"Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais
kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu
kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa
kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais
ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi
cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya
40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka
Rais atapendekeza jina la mtu atakae kuwa Makamu wa Rais na
uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua
asilimia hamsini ya Wabunge wote."

Katiba inamtaja Makamu wa Rais kama mrithi wa kiti cha Rais.

Katiba haijaweka masharti kwamba huyo Makamu awe amechaguliwa kwenye kura za uchaguzi Mkuu.
 
KATIBA IBARA 37(5)
"Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais
kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu
kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa
kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makami wa Raia ataapishwa na atakuwa Raisi kwa muda uliobaki katika kipindi
cha miaka mitano na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya
40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka
Rais atapendekeza jina la mtu atakae kuwa Makamu wa Rais na
uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua
asilimia hamsini ya Wabunge wote"

Tanzania Raisi anapatikana kwa njia mbili.

1) Kwa uchaguzi Mkuu, ambapo Yeye na Makamu wake watateuliwa pamoja toka kwa chama Chao Cha siasa

2) Kwa Makamu kum-succeed Raisi aliyekuwa madarakani na akakoma kuwa Raisi kwa sababu za kikatiba. Huyu Makamu wake atapatikana kwa uteuzi toka katika chama chake Cha siasa utakathibitishwa kwa zaidi ya nusu ya wabunge.
 
Pa Pascall mayala aje na ufanunuzi ni muhimu sana kujua sheria
 
Vipi kuna nini huko Dasilam sisi huku mkoani tunalima maana mvua za mwanzo ndiyo za kupandia.
Kuna kitu sijaelewa

--- Kila ukipita kwenye post za watu ( hata mimi nimeuliza ) wanaouliza kuhusu Samia yuko wapi, unakutana na Team ya Waziri Rajabu inatoa matusi ya nguoni kwa wanaouliza Rais wa Nchi Yuko wapi

--- Kwa kipi rahisi? Kuajili Team kutukana watu mtandaoni au Samia kujitokeza tu na kupoza hii hali ambayo imeendelea kwa wiki mbili sasa?

-- Watu wanahoji sababu wanajua sheria za nchi zinasemaje, Lakini pia haiwezekana Rais wa Nchi akaondoka na kwenda nchi kama Marekani kisha akapotea tu kama upepo na kusiwe na Mswali

-- Kwa nini Gharama kubwa inatumika kutuma watu kutukana badala ya kuja na HOJA

Hii inaacha maswali makubwa zaidi, sababu haiwezekana serikali ikatumia gharama kubwa kulipa wahuni badala badala ya ku address suala muhimu la Samia yuko wapi

Mwisho serikali inatakiwa kujifunza wakati wa Magufuli alipopotea serikali ilikuja kwa namna inavyokuja sasa na kuna baadhi ya watu walikamatwa mwisho wa siku tukamzika Magufuli, Mpaka leo serikali imekaa kimya awakuomba radhi

Samia YUKO wapi, hii ndio hoja ijibiwe
 
KUNA WATU WATAAIBIKA VIBAYA SANA SIKU SI NYINGI.
ANYWAY MUNGU IKIKUPENDEZA TUPE OMBOLEZO LA KITAIFA TUMEMISS SANA ZILE NYIMBO ZA AKINA MSECHU NA MJOMBA MPEKU PEKU.
 
Tatizo la nchi ya Tanzania ni mifumo iliyokosewa tangu mwanzo.

Kinachotokea sasa na kitazidi kutokea ni watu kutafuta wa kumlaumu na kumbebesha lawama mtu mmoja. One person cannot be a sole cause for our problems.

Tatizo la hii nchi ni kila mwananchi kutokuona umuhimu wa kuungana kupigania haki zake.

Tumebakiza kupiga ramli tu na kuombea viongozi vifo. Pathetic
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…