Tuijue Katiba: Rais akifia madarakani, basi makamu wake aliyegombea naye akapigiwa kura anarithi. Je, vipi kama makamu hakupigiwa kura?

Tuijue Katiba: Rais akifia madarakani, basi makamu wake aliyegombea naye akapigiwa kura anarithi. Je, vipi kama makamu hakupigiwa kura?

Soma Ibara ya 50 (1) & (2)(d).

-Kaveli
50.-(1) Isipokuwa kama atajiuzulu au atafariki mapema zaidi,
mtu aliyechaguliwa, au kuteuliwa kwa mujibu wa ibara ya 37(5),
kuwa Makamu wa Rais, bila ya kuathiri masharti mengine ya
ibara hii, atashika kiti cha Makamu wa Rais kwa muda wa miaka

mitano tangu alipochaguliwa kuwa Makamu wa Rais.

(2) Makamu wa Rais atashika kiti hicho hadi-
(a)muda wake utakapokwisha;
(b)akifariki dunia akiwa katika madaraka;
(c)atakapojiuzulu;

(d)atakapoapishwa kuwa Rais baada ya kiti cha Rais
kuwa wazi;


(e)atakapotiwa hatiani kwa kosa lolote la jinai
linaloonyesha utovu wake wa uaminifu;
(f)atakapoapishwa Rais mwingine kushika nafasi ya
Rais pamoja na Makamu wake;
(g)atakapoondolewa madarakani baada ya kushtakiwa
Bungeni kwa mujibu wa masharti ya ibara ndogo ya
(3) ya ibara hii;
(h)atakapoacha kushika kiti cha Makamu wa Rais
vinginevyo kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.

=========================================

SWALI LA MTOA HOJA NI: Ataapishwa kuwa Rais ktk mazingira gani?

Mathalani kwa huyu aliyepo sasa Dr Philip Isidory Mpango ha - fit kwenye sifa inayotajwa na ibara ya 37 (5) maana hakuwahi kupigiwa kura na Rais huyu aliyepo..?

Hauoni kuwa, katiba haina jibu sahihi kwa scenario hii iwapo itatokea...?
 
Back
Top Bottom