Uchaguzi 2020 Tuikomboe Tanzania kupitia Lissu, hakuna nchi Duniani ina mifumo miwili ya lugha za kufundishia

Ni sawa mimi nimezungumzia kuhusu performance itapungua kwa shule za serikali.
 
Mkuu ilo ni zao la kuchanganya lugha za kufundishia , sidhani kama mwalimu kasoma kwa kiingereza toka nursery hadi chuo hatashindwa kufundisha kwa kiingereza, wanaosumbuliwa na kufundisha kwa kiingereza ukifanya tafiti utagundua ni zao la shule za serikali walizosoma primary.
 
Nami naunga mkonyo ooh! mkono hoja.
 
Watanzania hawapangiwi cha kufanya.Pambana na Hali yako, Sisi tutachagua tunachoona sahihi na tulichokizoea hatutakuwa wanaotaka kujifunza
 
Mh Tundu Lissu ameongea ukweli ila mfumo kama huu uweze kufanikiwa inabidi waalimu wa shule ya msingi wapewe mafunzo ya lugha ya kiingereza. Nchi nyingi wanasoma lugha zaidi ya moja kuanzia primary. Mfumo mzima inabidi ubadilishwe lakini sidhani hiyo itakuwa agenda ya Rais Magufuli maana yeye alishasema ni kiswahili tu!
 
basi si angeandika kwa kiswahili ili tumuunge mkono kweri nimeamini sisi ambao hatujuwi kujieleze kwa English kichaka chetu kinakuwa kizingu sio akiri lakini tunaumia kiundani tukikimuona ZZK ,Membe au TAL wanakitwanga fresh tuu roho inauma lakini.
 
Kama umekaa Ulaya kizazi kipya wote wanajifunza kiingereza..cc Christiano Ronaldo
 

Ukitaka mtoto wako awe mtumwa, mpeleke akasome shule za kufundishwa kwa kiswahili. Katika vitu nimesema siwezi kufanya ni huo ujinga.
 
Wewe mwanasaccos hapo Afrika ya Kusini tu wameamua Kiswahili kuingizwa kwenye mtaala wao wakufundishia kwenye shule zao!! Wewe unadharau kiswahili!!

Kuingizwa kwenye mtaala huo uchafu? Taja jimbo ambalo huo uchafu unatumika kufundishia huko Afrika kusini.
 
Mfumo wa kutumia lugha moja tu ya kiingereza kufundishia katika elimu yetu hauwezi kuwork katika shule zetu.

Kumbuka unavyokuja na mambo haya tambua tupo over 50 million. Tatizo la wanasiasa kama Lissu mnapoona mnameneji peleka watoto wenu international school basi mnafikiri ni rahisi kiasi hicho. Hamfikirii hata pato la nchi yetu kuweza kuaccomodate mipango hiyo.

Kwa mfano tukianza na elimu ya msingi, tuna wastani wa wanafunzi million 10, kuaccomodate mpango huo kwa mtoto mmoja si chini ya sh. 500,000 kwa mwaka, ukizidisha kwa watoto million 10 unapata trillion 5.

Hapo bado hujawekeza kwa watoto wa sekondari bado hujatoa mikopo kwa wanafunzi wote wa chuo kama sera yenu ilivyo.
Bado hujajenga miundo mbinu na kuendesha nchi.

Kwa sera hizi hebu mtuache tu na CCM yetu. Hamna jipya.
 
Ila kitumike kiswahili.

Au kuwe na shule aina 3.

Za english medium na kiswahili medium.

Pia Na kama zilizopo sasa.

Alafu tupime ufanisi wa kila medium.

English medium zote watajaa watoto wa wapinzani, huko kiswahili medium watajaa watoto wa wanaccm maana huo ccm ni nguvu bila akili.
 
Njooni ni mpango mkakati wa kuongeza pato la taifa kwanza na sio kujitungia tu sera ambazo hazitekelezeki.
 
English medium zote watajaa watoto wa wapinzani, huko kiswahili medium watajaa watoto wa wanaccm maana huo ccm ni nguvu bila akili.
Ongelea reality. Sio uongee ukitanguliza mahaba.

Kwani sahvi hakuna watoto ambao wazazi wao wako CCM wanasoma private.
 
Ongelea reality. Sio uongee ukitanguliza mahaba.

Kwani sahvi hakuna watoto ambao wazazi wao wako CCM wanasoma private.

Umesema ziwekwe za English & Swahili medium, nikakuambia mgawanyo wa idadi.
 
Ndo ulichoelewa?
 
mweongo,

Mi nafikiri jitihada zizingawe kukikuza kiswahili zaidi siku moja kiswahili kitumike kufundishia pia. Tunakipa ukuu wa bure tu icho kiingereza, kuna nchi zna lugha zao wenyewe na zimeendelea pakubwa tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…