Tujadili Demokrasia ndani ya CHADEMA. Je inashawishi ama kukatisha tamaa?

Tujadili Demokrasia ndani ya CHADEMA. Je inashawishi ama kukatisha tamaa?

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Matukio, mwenendo na mitazamo ya wengi kwa sasa yamejikita kwenye mchakato wa kupata Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA. Tunachokiona kwa sasa nimnyukano mkali ambao ulianza kama tetesi na hususan michakato mirefu ya chaguzi kuanzia ngazi za chini hadi sasa kwenye nafasi ya juu ya uongozi wa chama.

Nimeshawishika kuandaa uzi huu mahususi kujadili yanayojiri hususan mchakato wa kidemokrasia ndani ya chama hiko kikuu cha Upinzani nchini.

  1. Mchakato wa Uchanguzi ndani ya CHADEMA kuanzia ngazi ya chini hadi ngazi ya Kanda, umeshawishika kwamba demokrasia ndani ya CHADEMA inakua au inadumaa?
  2. Sisi wadau wa Demokrasia kwenye ngazi za chaguzi za Kitaifa, tumekosoa na kushauri sana namna bora ya kuboresha chaguzi za serikali, je ndani ya CHADEMA kuna mfanano au utofauti linapokuja suala la chaguzi ndani ya chama?
  3. CCM imetawala nchi hii kwa imla zaidi ya miaka 60 tangu uhuru, Watanzania walio wengi tunaona kwa facts hakuna maendeleo mtambuka yaliyoletwa na chama hiki, je Katiba ya CHADEMA inaweka viwango gani kwenye eneo la kung'ang'ania madarakani kama CCM inavyolifanyia Taifa letu?
  4. Tunajifunza nini kwenye hili la Uchaguzi wa ndani wa CHADEMA kulinganisha na michakato ya chaguzi za kiserikali?
Nawaalika JF Great Thinkers tujadili kwa pamoja, ndugu zangu hawa nawaalika kwa majina
Pascal Mayalla, Yericko Nyerere Retired johnthebaptist Chief TAJIRI MKUU WA MATAJIRI Lucas Mwashambwa MtuKwao figganigga
 
Mimi sioni tatizo lolote ndani ya CHADEMA ila ukiona hadi Lucas Mwashambwa anabubujika machozi kutokana na hotuba ya Mbowe basi ujue kuna jambo😏
 
Hakuna tatizo lolote la demokrasia ndani ya CHADEMA, ukomo wa madaraka sio kigezo muhimu cha demokrasia.

..ukomo wa madaraka sio jambo baya.

..sijui kwanini watu wa Mbowe wanatishika na ukomo wa madaraka.

..kipengele hicho kikirudishwa Mbowe atastaafu mwaka 2034, sasa tatizo liko wapi?

..kama Chadema inapigania ukomo wa madaraka ktk Katiba ya Jamhuri ni vizuri ikawa na kifungu hicho ktk Katiba ya Chama pia.
 
..ukomo wa madaraka sio jambo baya.

..sijui kwanini watu wa Mbowe wanatishika na ukomo wa madaraka.

..kipengele hicho kikirudishwa Mbowe atastaafu mwaka 2034, sasa tatizo liko wapi?

..kama Chadema inapigania ukomo wa madaraka ktk Katiba ya Jamhuri ni vizuri ikawa na kifungu hicho ktk Katiba ya Chama pia.
Ukomo wa madaraka sio jambo baya lakini sio jambo la msingi katika demokrasia, zipo nchi za kidemokrasia na vyama vya siasa vya kidemokrasia tele duniani ambako hakuna ukomo wa madaraka.

Umewahi kujiuliza kwa nini nchi nyingi duniani za kidemokrasia hata zenye ukomo wa madaraka kwa rais hazina ukomo wa madaraka kwa wabunge?
 
Msingi gani mmoja wa demokrasia uliokiukwa ndani ya CHADEMA?
Unajua Democracy sio Kupiga Kura tu au Liberalism tu!
Demokrasia ni Pia Kukubali watu kwa Muda Huo wamechoka aina ya Uongozi unayowaongoza Licha ya Kukuonea Aibu kukuambia..

Unajua Kuwa Watu wengi walichoka Uongozi wa Mwalimu Nyerere ila hakuna Aliyemuambia Kwamba Anaongoza vbaya kwa kumuogopa..

Baadaye baada ya Kuona Athari (Nyerere) mwenyewe Aliamua kung'atuka..

Demokrasia sio kusubiri Mpaka Athari itokee Ila Demokrasia ni Kuepusha Mvunjiko au Athari ambayo unahisi Itatokea..

Na Hiyo ndo Maana halisi ya Kiongozi mwenye Maono na Mapinduzi ambayo kwa FAM ameikosa na Imeondoka na BoB nyanga makani
 
Unajua Democracy sio Kupiga Kura tu au Liberalism tu!
Demokrasia ni Pia Kukubali watu kwa Muda Huo wamechoka aina ya Uongozi unayowaongoza Licha ya Kukuonea Aibu kukuambia..

Unajua Kuwa Watu wengi walichoka Uongozi wa Mwalimu Nyerere ila hakuna Aliyemuambia Kwamba Anaongoza vbaya kwa kumuogopa..

Baadaye baada ya Kuona Athari (Nyerere) mwenyewe Aliamua kung'atuka..

Demokrasia sio kusubiri Mpaka Athari itokee Ila Demokrasia ni Kuepusha Mvunjiko au Athari ambayo unahisi Itatokea..

Na Hiyo ndo Maana halisi ya Kiongozi mwenye Maono na Mapinduzi ambayo kwa FAM ameikosa na Imeondoka na BoB nyanga makani
Maamuzi muhimu ya kidemokrasia yanatakiwa yaamuliwe kwa kura ya watu wengi kadri iwezekanavyo. Hamuwezi tu kukaa bar mlewe bia halafu mnasema fulani tumemchoka aondoke wakati mna fursa ya kupiga kura ukasema hiyo ni demokrasia.

Nyerere hakuwa anaongoza nchi ya kidemokrasia, hakuna nchi ya demokrasia ya chama kimoja.
 
Maamuzi muhimu ya kidemokrasia yanatakiwa yaamuliwe kwa kura ya watu wengi kadri iwezekanavyo. Hamuwezi tu kukaa bar mlewe bia halafu mnasema fulani tumemchoka aondoke wakati mna fursa ya kupiga kura ukasema hiyo ni demokrasia.

Nyerere hakuwa anaongoza nchi ya kidemokrasia, hakuna nchi ya demokrasia ya chama kimoja.
Umenena Vyema lakinj usisahau Wanaopiga kura Sio wananchi wa Kawaida..

Sisi Chadema wakimpitisha Mbowe Tunakutana kwenye Uchaguzi mkuu..
Na sasa Hivi hakuna Kuja Kulalamika eti sijui wameibiwa Kura ya Nyokwe Tutawaonyesha kwenye Box Mwak 2025 Na Chadema Itakuwa UDP "B" itapata Kura chini ya 0.01%
 
Matukio, mwenendo na mitazamo ya wengi kwa sasa yamejikita kwenye mchakato wa kupata Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA. Tunachokiona kwa sasa nimnyukano mkali ambao ulianza kama tetesi na hususan michakato mirefu ya chaguzi kuanzia ngazi za chini hadi sasa kwenye nafasi ya juu ya uongozi wa chama.

Nimeshawishika kuandaa uzi huu mahususi kujadili yanayojiri hususan mchakato wa kidemokrasia ndani ya chama hiko kikuu cha Upinzani nchini.

  1. Mchakato wa Uchanguzi ndani ya CHADEMA kuanzia ngazi ya chini hadi ngazi ya Kanda, umeshawishika kwamba demokrasia ndani ya CHADEMA inakua au inadumaa?
  2. Sisi wadau wa Demokrasia kwenye ngazi za chaguzi za Kitaifa, tumekosoa na kushauri sana namna bora ya kuboresha chaguzi za serikali, je ndani ya CHADEMA kuna mfanano au utofauti linapokuja suala la chaguzi ndani ya chama?
  3. CCM imetawala nchi hii kwa imla zaidi ya miaka 60 tangu uhuru, Watanzania walio wengi tunaona kwa facts hakuna maendeleo mtambuka yaliyoletwa na chama hiki, je Katiba ya CHADEMA inaweka viwango gani kwenye eneo la kung'ang'ania madarakani kama CCM inavyolifanyia Taifa letu?
  4. Tunajifunza nini kwenye hili la Uchaguzi wa ndani wa CHADEMA kulinganisha na michakato ya chaguzi za kiserikali?
Nawaalika JF Great Thinkers tujadili kwa pamoja, ndugu zangu hawa nawaalika kwa majina
Pascal Mayalla, Yericko Nyerere Retired johnthebaptist Chief TAJIRI MKUU WA MATAJIRI Lucas Mwashambwa MtuKwao figganigga
kibaraka wa mabwenyenye ya magharibi alipojitokeza kugombea uenyekiti wa chadema Taifa, na ushawishi wa chadema kwa umma wa waTanzania ukapotea kabisa na kuwakatisha tamaa wanachama, wajumbe na mashabiki wote wa chadema, dah,

migawanyiko na mpasuko ukajitokeza ghafla sana dah!

aise,
sasa hivi uhasama ni mkubwa na ni hatari kwa afya na maisha ya kila mjumbe wa mkutano mkuu Taifa :pulpTRAVOLTA:
 
Umenena Vyema lakinj usisahau Wanaopiga kura Sio wananchi wa Kawaida..

Sisi Chadema wakimpitisha Mbowe Tunakutana kwenye Uchaguzi mkuu..
Na sasa Hivi hakuna Kuja Kulalamika eti sijui wameibiwa Kura ya Nyokwe Tutawaonyesha kwenye Box Mwak 2025 Na Chadema Itakuwa UDP "B" itapata Kura chini ya 0.01%
Sijui unamaanisha nini unaposema wanaopiga kura sio wananchi wa kawaida.

Hizo tambo za kuwanyoosha CHADEMA katika box la kura ni tambo za hovyo tu, kama mnaweza kuwanyoosha kwa nini sasa mnaengua wagombea wao??
Kwa nini mawakala wao wa kusimamia kura hawapewi haki sawa na wa CCM? Kwa nini hamtaki walinde kura zao?
Kwa nini hamtaki watu huru tofauti na wa serikali wasimamie uchaguzi?
Kwa nini hamruhusu matoke yahojiwe maakamani?
 
Ukomo wa madara sio jambo baya lakini sio jambo la msingi katika demokrasia, zipo nchi za kidemokrasia na vyama vya siasa vya kidemokrasia tele duniani ambako hakuna ukomo wa madaraka.

Umewahi kujiuliza kwa nini nchi nyingi duniani za kidemokrasia hata zenye ukomo wa madaraka kwa rais hazina ukomo wa madaraka kwa wabunge?

..tuangalie manufaa na madhara yake kwa Chadema, lakini sio kupinga, au kuunga mkono moja kwa moja.

..kwa upande wa manufaa inaweza kuwa fursa kwa viongozi kujituma zaidi kukitumikia chama, na kuongeza hamasa na kutoa nafasi kwa wanachama wengi zaidi kuonyesha vipaji vyao.
 
..tuangalie manufaa na madhara yake kwa Chadema, lakini sio kupinga, au kuunga mkono moja kwa moja.

..kwa upande wa manufaa inaweza kuwa fursa kwa viongozi kujituma zaidi kukitumikia chama, na kuongeza hamasa na kutoa nafasi kwa wanachama wengi zaidi kuonyesha vipaji vyao.
Mbowe amesema sio rahisi kupata viongozi weledi wa chama cha upinzani Tanzania kwa sababu hakuna fursa kama ilivyo chama tawala, fikiria Cecil Mwambe, Zitto Kabwe au Kitila Mkumbo wangepewa uenyekiti wa CHADEMA leo hii ingekuwa wapi.

Lissu alisema waliondoa ukomo wa madaraka kwa sababu ya ugumu wa kupata viongozi kwa hiyo haikuwa na mashiko unapata kwa shida viongozi bora halafu bado unawaondoa kwa ukomo wa madaraka.

Sioni maana yoyote ya ukomo wa madaraka kwa chama cha siasa, sina mfano wa chama cha siasa bora duniani katika nchi yoyote ya kidemokrasia ambacho kimewahi kuweka ukomo wa madaraka kwa viongozi wake.
 
Back
Top Bottom