Tujenge utamaduni wa kuwapa thamani wachezaji wazawa

Tujenge utamaduni wa kuwapa thamani wachezaji wazawa

Labda utoe mfano mwingine siyo Feitoto huyu hana body language nzuri,(how do you support him),
Halafu unakuta mbongo kama wewe eti unachukizwa na drama za Feitoto lakini hauchukizwi hata kidogo na zile dramas za morison na si ajabu hata ulikuwa unamtetea kisa tu huyobMorison anatoka huko West Africa wakati Fei ni mbongo mwenzio.... najua sana akili zenu wabongo
 
Umenikumbusha zamani tulivyokuwa wadogo, mgeni akitutembelea nyumbani siku hiyo lazima achinjiwe kuku hata kama nyumbani hamfugi kuku basi mzazi ataenda hata kukopa pesa amnunue huyo kuku, kikubwa tu mgeni ale vizuri na aondoke huku amefurahi...

Unachosema ni kweli kabisa hii kasumba imeanzia kwenye malezi... na sasa imeshakomaa mpaka imetufanya tumekuwa wapuuzi na watu wakujipendekeza pendekeza ovyoo.

Leo hii wewe na muhindi mkienda pale Kurasini kushughulikia suala la passport, huyo muhundi anaweza asichukue hata siku tatu akawa akapewa passport yake, ila wewe mbongo halisi unaweza ukazungushwa hata miezi mitatu... inaudhi kwakweli hii kasumba.

Ukienda taifa kam Misri au Morocco huko kwenye ligi hata ufunge goli 100 kama wewe sio mzawa hakuna media yoyote itakayokuimba.. Mayele huyo hapa huwa analalamika pamoja na kuwa yeye ni striker tegemeo wa Pyramid na anafunga sana, lakin hapewi ile King treatment aliyokuwa anapewa hapa Bongo. Kiufupi huko wanamuona ni mtu wa kawaida sana.

Binafsi huwa kuna muda nachukia hata kuzaliwa kwenye hili taifa, maana huwa naona ni kama aina fulani ya laana yaani kuzaliwa Tanzania ni moja wapo ya adhabu ambayo Mungu amekupa... Mungu kama anakupenda basi ungezaliwa kwenye mataifa yanayoeleweka na sio hili
Ni kuendelea kuelimishana, kidogo kidogo watu watabadilika.

Unajua kasumba na mazoea ni kitu kibaya sana. Mtu kwa kuwa amezoea na ameishi akiona jambo fulani linafanyika hivi au jamii ina mtazamo fulani kuhusu jambo fulani, basi yeye akili yake itafungwa akiamini hivyo ndivyo inavyotakiwa kuwa hata kama jambo hilo lina kasoro. Inachukua muda mrefu na mpaka labda muhusika apate exposure fulani kidogo ndiyo akili yake inafunguka.

Huwa sichoki kuleta mada kama hizi mara kwa mara kwa vitu ambavyo nimeona vimeota mizizi katika jamii pamoja na kwamba vina kasoro, ukimgusa mtu mmoja ukabadilisha mtazamo wake inatosha.
 
Wachezaji wazawa hawajipi thamani wenyewe,mfano ukilinganisha uwezo wa maamuzi na usahihi wa matendo kiwanjani unaona kabisa wageni wametuacha mbali hivyo thamani yetu lazima iwe ya kawaida,wazaawa wanaripuka msimu mmoja kisha wanapotea mazima mfano George mpole,Mbaraka yusuph,Malimi busungu,Abrahman Mussa,Eliud Ambokile na wengine wengi. japokuwa sikatai swala la media na wadanganyika kuwashobokea wageni.

Tumekuwa tunasikia majina ya kina Sande Manara,Mohamed mwameja,Nteze John,Peter Manyika,Peter Tino,Lunyamila n.k hawa ni wazawa ambao walitamba na kutawala soka na kupewa thamani.....wahezaji wazawa wajitathmini wanafeli wapi.......kingine hizi timu mbili kubwa ndio wanaoshusha thamani za wahezaji mhezaji akitakiwa na timu hizi haangalii thamani yake.
 
Halafu unakuta mbongo kama wewe eti unachukizwa na drama za Feitoto lakini hauchukizwi hata kidogo na zile dramas za morison na si ajabu hata ulikuwa unamtetea kisa tu huyobMorison anatoka huko West Africa wakati Fei ni mbongo mwenzio.... najua sana akili zenu wabongo
Soma uzi unasemaje hata hivyo mimi siyo mashabiki kwa wanaojiitoa ufahamu , (am not in favor of unbecoming behavior). I call a spade a spade not a big spoon
 
Back
Top Bottom