Tujielimishe: Ni Wakati gani polisi walibaini Kuna njama za Ugaidi kwenye kesi ya Mbowe? Ni mwaka 2020 au 2021?

Tujielimishe: Ni Wakati gani polisi walibaini Kuna njama za Ugaidi kwenye kesi ya Mbowe? Ni mwaka 2020 au 2021?

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2019
Posts
762
Reaction score
6,984
1. Watuhumiwa watatu kwenye hii walikamatwa mwaka 2020 na kuhojiwa Kisha kufunguliwa mashtaka yasiyo ya Ugaidi.

2. Watuhumiwa watatu baada ya kutoa maelezo Yao mwaka 2020 walipokamatwa awakuwahi kurejea uraiani walipelekwa mahakamani Kisha mahabusu,hivyo awajawahi kupata dhamana Wala kuhojiwa Tena.

3. Hadi watuhumiwa wanakamatwa Polisi walijua kwamba zipo Tuhuma za Ugaidi Kwa sababu Kwa mujibu wa Shahidi wa Jamhuri Denis Urio alishafikisha taarifa Polisi. Hivyo Polisi walikwenda kuwakamata watuhumiwa wa makosa ya Ugaidi Kwa mujibu wa Informer wao Be. Denis Urio

4. Polisi haohao ambao tayari walikuwa na taarifa zote awakumkamata mfadhili wa Ugaidi na kumweka mahabusu pamoja na watuhumiwa wengine,walimwacha.

5. Huku wakijua wazi wahusika wa uhalifu na uhalifu uliofanyika na madhara yake Kwa nchi hakuna hatua zozote zilizofanyika za kumamata mfadhili wa Ugaidi lakini pia Bado watuhumiwa waliendelea kukosa dhamana

6. Kwa kipindi Cha mwaka mzima hakuna popote kwenye maelezo ya mashahidi akiwemo mpelelezi wa shauri anaeleza kwamba alifanya upelelezi wa ziada uliopelekea watuhumiwa kuendelea kushikiliwa. Fact zilezile zilizoandikwa kwenye maelezo 2020 zilibaki zile zile ikiwemo, hakuna aliyekwenda hoteleni Aishi, hakuna aliyekwenda hoteli palipofanyika kikao Cha kwanza, hakuna aliyekwenda kufanya upekuzi Kwa mfadhili wa Ugaidi kuzuia asiwe na vilipuzi, hakuna aliyefanya chochote tofauti na kuandika maelezo ya watuhumiwa. Means upelelezi ulikamilika na kufungwa siku tu watuhumiwa watatu walipokamatwa na kuhojiwa.

7. Mfadhili aliendelea kufanya kampeni, akasafiri nje, akarudi akaendelea kufanya siasa na kukutana na makundi makubwa ya watu lakini hakuna aliyechukua taadhari mfadhili wa Ugaidi asitekeleze azma yake.

8. Kiongozi anayedaiwa kupata ya ugaidi ni mhalifu ambaye serikali hiyohiyo iliyosema alitegemewa kudhuriwa ndiyo hiyo imempeleka mahakamani kwamba alifanya uhalifu na kuendelea na uhalifu kabla Mbowe ajaajiri walinzi na baada ya kuajiri walinzi. Kwa maana nyingine Polisi waliaminishwa muhalifu anatarajia kufanyiwa uhalifu kipindi ambacho yeye Mwenyewe alikuwa anafanya uhalifu.

9. Kiongoz aliyepangwa kupata madhara akiwa DC ajawahi kuandikwa maelezo ya aina yoyote hata kuhusiana na uhusiano wake na shahidi aliyedai alikuwa anafanya kazi kwake. Hakuna ushahidi wowote unaoonyesha shahidi Kaaya alikuwa na mahusiano ya kikazi na DC Sabaya. Katika USO wa mahakama nivigumu kusema amewahi kuwa rafiki au hata mfanyakazi wa kiongoz mfungwa Sabaya

10. Hakuna chochote kilichokamatwa kinachothibitisha uwepo wa uhalifu. Si kwa mawasiliano Wala kwenye maelezo ya mashahidi.
 
Sabaya aliwaingiza chaka akina Kingai.
Ni wazi alishikwa na hofu alipobaini Mbowe anapanga kujiimarishia ulinzi kwa kuwatumia makomandoo.
Kwanza tukubaliane lengo la Sabaya lilikuwa kudhulumu afya na uhai wa Mbowe!

NB: Kinachodhihirika mahakamani ni levels za akili za Sabaya changanya na udhaifu wa polisi.
 
Ivi Urio anajisikiaje kuwa snitch wenzake, ambao aliwaambia wanaenda kufanya kazi ya ulinzi .
Urio hakuwa na nia yakuwauza....alitekwa issue nikujua nani alivujisha mpango wa Mbowe kuwa na walinzi kuna dhana tofauti huenda Urio anaurafiki na mapolisi so ktk ile kupiga story akasema Mbowe anataka walinzi na mapolisi yaikuwa yanataka vyeo kwa Jiwe so wakaanzia hapo nawaza tu
 
Pamoja na ukweli wote huu mshangao zaidi ni pale mahakama itakapowaona Mbowe et al. wana kesi ya kujibu.

Hata ukiwa Na akili timamu, unaweza ukachukua tofali Na kumponda nalo mtoto mchanga kichwani, Ni maamuzi tu! Kwa hiyo wana nguvu wakitaka itumia kihuni Ni sawa
 
Urio hakuwa na nia yakuwauza....alitekwa issue nikujua nani alivujisha mpango wa Mbowe kuwa na walinzi kuna dhana tofauti huenda Urio anaurafiki na mapolisi so ktk ile kupiga story akasema Mbowe anataka walinzi na mapolisi yaikuwa yanataka vyeo kwa Jiwe so wakaanzia hapo nawaza tu
Wale makomandoo walionekana wakati wa kumpokea Tundu Lissu wakifanya ulinzi na pia walionekana wakati wa kampeni za uchaguzi wakifanya ulinzi.

Sasa watu wenye vichwa vya panzi wakaanza kujiuliza kwanini chadema wanawatumia wanajeshi wastaafu kama walinzi wa viongozi wao. Issue ikawafikia mapolisi amboa akili zao hazijahi hata kwenye kisoda.

Wakakulupuka kwenda kuwakamata na kuwahoji kwa mateso makali wakitaka kujua wamefikaje chadema. Wakaambiwa Urio ndio amewaunganisha kwa kazi ya ulinzi ya viongozi wa chadema. Polisi walifahama hapa hakuna kesi na ndio maana hao makomandoo mwanzo kabisa hawakufunguliwa kesi ya ugaidi na ndio maana hata Mbowe hawakumgusa

Mbowe alipoanza mambo ya katiba mpya na mama kusema hiyo ni chokochoko na kuonekana hataki kabisa mambo ya katiba mpya. Mbowe alikahidi kauli ya mama na kuendelea na kampeni ya katiba mpya. Baada ya hapo ndipo walipoanza mikakati ya kumtia adabu Mbowe na kwa bahatia mbaya wakakulupuka na kumfungulia kesi ya ugaidi bila ya kujipanga vizuri.
 
Hapo namba mbili umesema watuhumiwa watatu baada ya kukamatwa na kutoa maelezo walifikishwa mahakamani, ni mahakama gani hiyo walifikishwa?

Navyojua hao jamaa waliwekwa jela muda wote huo na wangeendelea kukaa huko zaidi kama Mbowe asingelazimisha kwenda Mwanza kwaajili ya kongamano la kudai Katiba Mpya.

Hao watuhumiwa hawakuwa na tofauti na watuhumiwa wengine waliojazwa kwenye magereza mbalimbali nchini wakituhumiwa ugaidi bila kufikishwa mahakamani.
 
Wale makomandoo walionekana wakati wa kumpokea Tundu Lissu wakifanya ulinzi na pia walionekana wakati wa kampeni za uchaguzi wakifanya ulinzi.

Sasa watu wenye vichwa vya panzi wakaanza kujiuliza kwanini chadema wanawatumia wanajeshi wastaafu kama walinzi wa viongozi wao. Issue ikawafikia mapolisi amboa akili zao hazijahi hata kwenye kisoda.

Wakakulupuka kwenda kuwakamata na kuwahoji kwa mateso makali wakitaka kujua wamefikaje chadema. Wakaambiwa Urio ndio amewaunganisha kwa kazi ya ulinzi ya viongozi wa chadema. Polisi walifahama hapa hakuna kesi na ndio maana hao makomandoo mwanzo kabisa hawakufunguliwa kesi ya ugaidi na ndio maana hata Mbowe hawakumgusa

Mbowe alipoanza mambo ya katiba mpya na mama kusema hiyo ni chokochoko na kuonekana hataki kabisa mambo ya katiba mpya. Mbowe alikahidi kauli ya mama na kuendelea na kampeni ya katiba mpya. Baada ya hapo ndipo walipoanza mikakati ya kumtia adabu Mbowe na kwa bahatia mbaya wakakulupuka na kumfungulia kesi ya ugaidi bila ya kujipanga vizuri.
Sasa hapa nimeelewa mkuu shukrani sana
 
Hapo namba mbili umesema watuhumiwa watatu baada ya kukamatwa na kutoa maelezo walifikishwa mahakamani, ni mahakama gani hiyo walifikishwa?

Navyojua hao jamaa waliwekwa jela muda wote huo na wangeendelea kukaa huko zaidi kama Mbowe asingelazimisha kwenda Mwanza kwaajili ya kongamano la kudai Katiba Mpya.

Hao watuhumiwa hawakuwa na tofauti na watuhumiwa wengine waliojazwa kwenye magereza mbalimbali nchini wakituhumiwa ugaidi bila kufikishwa mahakamani.
Kosa lao kubwa ni wao kuwa walinzi wa Tundu Lissu.
 
Back
Top Bottom