Huko ndio usiseme sasa, nimecheza sana.
Nimecheza rede(nilikuwa napenda kuingia kama mtu wa kotekote), mchezo mmoja sisi tunauita IKHALU( upo kwenye picha hapo juu watoto wanarusha kajiwe juu huku wakiingiza vijiwe vingine kwenye kashimo kadogo chini), mwingine tulikuwa tunauiya CHAILETI (tunachora madrafti chini makubwa halafu unachukua kajiwe unaanza kukasukuma kiruke hayo madrafti kwa mguu mmoja huku mwingine ukiwa umeukunja usiguse chini), mchezo wa kushika kamba watu wawili halafu mmoja akiwa katikati anarukaruka.
Hiyo ni baadhi tu ambayo tulikuwa tunacheza tukiwa mix na wasichana