Tujikumbushe maneno ya zamani ya Kiswahili cha mtaani ambayo yamepotea hayatumiki tena

Tujikumbushe maneno ya zamani ya Kiswahili cha mtaani ambayo yamepotea hayatumiki tena

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Lugha yoyote hunakshiwa kwa maneno ya kudumu na yale ya muda mfupi. Lugha ya Kiswahili imekuwa na bahati ya kupata maneno mengi ya misimu na baada ya muda hutokomea kusiko julikana.

Kupitia uzi huu tukumbushane maneno mbalimbali ambayo yanapotea kwa kasi hivi sasa.

  • Kula jiwe- kukaa kimya
  • Kujikata kisilesi- kuondoka
  • Kishtobe- mlimbwende myange
  • Lofa- masikini
  • Lodi- tajiri
  • Wakuja- mshamba
  • Njenge- nyumba
  • Njelii- Mwanjelwa
  • Mkoko- gari
  • Kala kidato- msomi
Orodha itaendelea
 
Back
Top Bottom