Tujikumbushe MV Bukoba enzi za uhai wake

Mkuu mawakili wa serikali ni tatizo....
Yani makosa 159 lakini wakashindwa kuwapata na hatia...

Too bad, huyo Feleshi aliyekua anaendesha iyo kesi ndo akaja kua DPP!
Sasa hivi ni Jaji Kiongozi...so unaweza kuona system ilivooza
Ile meli pamoja na mistake iliyofanyika ya kujaza watu judgement ilionyesha hakuna ushahidi wa wazi ulioonyesha kwamba kulikuwa na uzembe pia hata shirika la reli enzi hizo halikuwa na orodha kamili ya abiria waliopanda meli hiyo. Pia kwa upande mwingine hiyo meli ilikuwa ina shida ya balance ikiwa inaelea na ndio maana iliweza kusafiri kutoka Bukoba mpaka inakaribia Mwanza ndio ikazama kutokana na watu wameamka na kuanza movement ikapelekea kuegemea upande mmoja (mara nyingi wasafiri hupenda kukaa upande mmoja na kuwa wanaangalia jiji la Mwanza wakati inakaribia kufika.

Kupitia ajali hii ilipelekea kuifanyia marekebisho meli nyingine inafanana na Mv Bukoba ambayo ipo Lake Tanganyika inaitwa Mv Mwongozo ambayo nayo ilikuwa ina shida ya balance na zote zilitengenezwa na kampuni moja
 
Walipigiwa simu tokea wapi mkuu!???na kampuni gani!??ilikua 1996,21 May Kumbuka!!
Enzi hizo ilikuwepo Mobitel ilibadilika ikawa Buzz kabla ya kuwa Tigo sasa hivi, enzi ilikuwa inachuana na Tritel (ambapo baadae Tritel alifulia akaondoka baada ya miaka 4 baadae ikaja Vodacom). TIGO ndo wahenga katika kutoa huduma za simu za mkononi Tanzania.

Hii ni story nadhani inasemekana aliepiga simu alikuwa mhindi flani hivi na walipotoboa tu nadhani walifanikiwa kutoa watu kama wawili tu na kitu kizama (ilienea sana hii issue ya kupiga simu those days)
 
Mkuu upo sahihi kabisa, ulichokiandika ndicho kilicho kwenye Ripoti ya ajali ya Mv Bukoba. Tatizo kubwa lilikuwa stability, utaratibu wa kutojua idadi ya sahihi na hakukuwa na rejesta ya abiria.
 
Sasa hii inakuaje,maana ki uhalisia wahusika wa meli walipaswa kujua idadi ya waliongia ndani ya meli na kama hawakuwa na idadi basi huo ni uzembe na ni kosa la kumfunga mtu sijajua wahusika walichomokaje!!!! Anyway ishatokea mimi nani nipinge ni mawazo tu kuonesha urasimu uliopo kwa watoa haki.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kabla ya meli kuondoka siku hiyo watu wengi walikuwa wamekata tiketi na wengine walilazimisha kwenda Kemondo.

Ukifatilia Marine Casualty Investigation na mpaka hukumu kutolewa wale wahusika wa meli walikuwa hawana hatia.
 
Ingekuwa tupo ana kwa ana ningekupa point ambazo ungekubali kuwa ni hukumu sahihi.

Mimi ripoti hiyo ya ajali nimeisoma kuna sehemu niliikuta yote, nimefika Bandari zote za Bukoba,Kemondo na kukutana na wahusika waliokuwepo.
Pia Marine Casualty Investigation nailewa kwa kiasi chake na nilichukua muda binafsi kujifunza kuhusu ajali ya Mv Bukoba.
 
Ni kweli upo sahihi lilishapita hilo, of course kwa kutokosekana regester ya abiria hapo ilikuwa ni system yote Shirika la Reli kitengo cha meli maana sio hiyo tu hata sehemu nyingine hali ilikuwa hivyo, from there ndio wakaanza kuandika majina. Hii iliwahi pia kutokea hata kwenye train baada ya ajali nao utaratibu ukabadilika
 
Ndugu inasikitisha sana ajali zingine zinazuilika ila uzembe wa watu wachache umegharimu maisha ya watanzania wengi na mwisho wa siku wazembe hao wanaachwa eti hakuna ushahidi wa kuwatia hatiani!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu inasikitisha sana ajali zingine zinazuilika ila uzembe wa watu wachache umegharimu maisha ya watanzania wengi na mwisho wa siku wazembe hao wanaachwa eti hakuna ushahidi wa kuwatia hatiani!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Fanya kosa wewe hata kama kosa halina kifungu cha sheria cha kukutia hatiani, utatafutiwa kifungu mbadala
 
Ulisoma wapi taarifa za hiyo hukumu Tempus Fugit ?? Tafadhali share link kama unaikimbuka.🙏🏾🙏🏾🙏🏾
 
Inatisha
 
Aaah..kumbe jana ilikuwa kumbukizi ya kuwakumbuka wapendwa wetu waliozama ..jana nlipita makaburin miti ya Nyerere nikaona watu wengi wakiwa na camera kumbe ndo tarehe yenyew meli ilipozama?
 

Ilinunuliwa mwaka gani? Nani walihusika kununua?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…