Tujikumbushe penzi la Juma Nature na Sinta

Tujikumbushe penzi la Juma Nature na Sinta

The only

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2011
Posts
10,805
Reaction score
14,181
Wahenga salaam,

Nakumbuka zama hizo Sinta aliibukia kwenye uigizaji enzi hizo na ray Kigosi , ghafla Shigongo naye akadondoka na magazeti ya udaku, miaka hiyo penzi la P Didy na j lo linatamba USA, mwanadada Sinta ndo ilikuwa habari ya jiji yaani hakuna gazeti lililokua halimtaji na kiki kumbe hazijaanza jana mtoto akadeclare yeye ni bikra kwa kweli niadmit nilikuwa A level huyu chama cha CHAPUTA veterans tuna mengi ya kumshukuru.


FRONTPAGEJ52.jpg

Katika mpangilio wa kiki binti akaliteka soko kwa kukamata moyo wa huyu bwana (Juma Nature) ambae by then na pini zake kali kama kighetogheto, jinsi kijana e.tc alikuwa gumzo Diamond na Alikiba watasubiri maana alikuwa anawakilisha maisha halisi ya watanzania halisi wa uswahilini na vijijini.

Sasa jamaa anaonekana alizoea wasichana wa kwao Mbagala Kiburugwa na Wazaramo, ghafla akauvagaa mtiti wa watoto wa mjini mapenzi A kuloga A kwa mwana Sinta (J lo wa Bongo) na hili ndo kosa alilolifanya kijana Diamond kwa Wema sepenga. Sasa msichana chati ikapanda wenye mihela yao wakaanza mwaga dau nakumbuka kuna tajiri wa unga alikuwa Iringa mjini ana magari ni mchaga aliwahi mhonga mil 2 ili alale naye usiku mmoja by then ilikuwa inatosha kununua gari, Nature masikini akawa anaambiwa haamini.

Kasheshe mtoto wa Dandu akadondoka na midola kufika Bongo anaambiwa demu mkali na wa kiki ni Jlo(Sinta) akamuomba awe video qeen kwenye wimbo wake wa mpenzi, Nature akamaindi msichana akamtuliza kuwa ni kazi, cha ajabu shoot imeenda hewani msichana bado yuko beach za Mwanza ndo kwa hasira akapiga chini na kutoa nyimbo za ''sitaki demu'' na ''inaniuma sana''.
 
Mara nyingi Nilipokuwa napita njia ya Victoria kipindi kile nilikuwa nakumbuka ajli ya Dandu. Halafu watu wakasema Juma alimroga...
Alikuwa na haki aseee maana alimuotea sana jamaa alikuwa anajipatia toke likapigwa teke
 
Kasheshe mtoto wa Dandu akadondoka na midola kufika Bongo anaambiwa demu mkali na wa kiki ni Jlo(Sinta) akamuomba awe video qeen kwenye wimbo wake wa mpenzi, Nature akamaindi msichana akamtuliza kuwa ni kazi, cha ajabu shoot imeenda hewani msichana bado yuko beach za Mwanza ndo kwa hasira akapiga chini na kutoa nyimbo za ''sitaki demu'' na ''inaniuma sana

 
Back
Top Bottom