Tujikumbushe vya zamani kidogo, vimepotelea wapi hivi?

Art

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2015
Posts
611
Reaction score
88
Vya enzi vizuri wakuu...siku hizoo zilizopita michezo ya watoto ilikuwa ikiwavuta na kuwaweka watoto pamoja sana na ilidumisha umoja na mshikamano hata kwa wazazi.

Cha kushangaza watoto wale wa enzi hizo pamoja na michezo yao ya mchana na usiku bado walikuwa na ADABU,HESHIMA na UTII na zaidi wengi walifanya vizuri madarasani.

Hata hivyo nimekumbuka vifuatavyo:-

*Bites

-Kashata
-Ngubiti
-lawalawa
-ubuyu wa unga
-Mabumunda

*Mavazi

-Mwisho saa sita (viatu)
-Pima juu...chini mwaga (suruali)
-Pensi nyanya.
-Saspenda
-Shumizi (Nliskia mabinti wakiita)

*Syle ya kunyoa

-Panki
-Fidodido
-Kiparangoto
-kukata way

*Michezo

-Gololi (Mpusa)
-Manati (kuwinda Vitorondoo)
-Kombolela
-Tiari bado.
-Esta esta (mabinti)
-Rede (Mabinti)
-One touch (Boys)

Ilikuwa zaidi kwa watoto wabishi na si kwa watoto wa kotaz na magetini.
 
kuna hili songi nimekumbuka

Mungu mkubwa, bwa bwabwa na samaki, ki king majuto, to tone la maji, ji jitu la kale, le lenye midevu, vu vumbua dhahabu........Nimesahau linaendeleaje
 
kuna hili songi nimekumbuka

Mungu mkubwa, bwa bwabwa na samaki, ki king majuto, to tone la maji, ji jitu la kale, le lenye midevu, vu vumbua dhahabu........Nimesahau linaendeleaje

Hahaha...hiyo iliimbwa na watoto krb TZ nzima.
 
kuna hili songi nimekumbuka

Mungu mkubwa, bwa bwabwa na samaki, ki king majuto, to tone la maji, ji jitu la kale, le lenye midevu, vu vumbua dhahabu........Nimesahau linaendeleaje

Bu bubu wa semii....mi mimi mdogo.......go gogo la mti ti tina na mjuba..ba...


Nmekumbuka enzi zile kitu ya kombolelaaaa...

Banda umizaaa.....dj afro...
Pale moro, mafiga..real miss
 
Bu bubu wa semii....mi mimi mdogo.......go gogo la mti ti tina na mjuba..ba...


Nmekumbuka enzi zile kitu ya kombolelaaaa...

Banda umizaaa.....dj afro...
Pale moro, mafiga..real miss
Daah..Umenikumbusha Tina na Mjuba..Kipindi hicho Tausi iko hot mbaya...wakina Dama,Siti bin Kasri,Kalumanzira,Rhoda,Lindi, Balaza n.k ....Kitambo sana aisee
 
Hakuna mchezo wa mpira mtamu kama one touch

Hii ilileta kina Masatu, Masha, Mogella, chumilla, Abeid mziba, lunyamila, Malota soma na wengi mahiri kwenye mpira.
 
Mkuu ongeza na "makida makida" sana mabinti walipenda sn huu mchezo na ulivuma sn kitambo iko...walikuwa wakiruka kwa kutumia mpira mwembamba wa manati km sikoseiBila kusahau 'bilingeba yoyo bilingeba yo..tunamuomba talentboy atuoneshe maringo yke bingilibingili mpaka chini"...,...aisee!Ila mkuu hii si ilibidi uipelleke kule 'chit chat' hii.
 
kuna hili songi nimekumbuka

Mungu mkubwa, bwa bwabwa na samaki, ki king majuto, to tone la maji, ji jitu la kale, le lenye midevu, vu vumbua dhahabu........Nimesahau linaendeleaje
Bu bubu hasemi mi mimi mdogoo go gogo la mti ti tina na mjuba baba mkali lindi ina vita ta ta hahahaha long time
 
Bu bubu wa semii....mi mimi mdogo.......go gogo la mti ti tina na mjuba..ba...


Nmekumbuka enzi zile kitu ya kombolelaaaa...

Banda umizaaa.....dj afro...
Pale moro, mafiga..real miss

Hii kombolela umenikumbusha ya kubadilishana nguo..aisee siku hizi watoto hawafaidi kabisa.
 
Hii kombolela umenikumbusha ya kubadilishana nguo..aisee siku hizi watoto hawafaidi kabisa.

We ulikuwa unabadilishana na mkaka au mdada nguo?

Mitoto ya siku hizi iulize kuhusu series za kikorea tuuu,
 
kuna hili songi nimekumbuka

Mungu mkubwa, bwa bwabwa na samaki, ki king majuto, to tone la maji, ji jitu la kale, le lenye midevu, vu vumbua dhahabu........Nimesahau linaendeleaje

Mganga wa mchezo wa tausi aliitwa nani Kalumanzila lala salama mama wa kambo mbona wanitesa sasa naondoka ka kaa peke yako koma kunipiga gari la baba ba baba mzazi zi zizi la ng'ombe mbe mbele ya nyumba mba mbali na mungu Mungu mkubwa bwawa la samaki ki king majuto to tone la maji jitu la kale le lenye midevu vu vumbua dhahabu bu bubu hasemi mi mi mdogo gogo la mti ti tina mjuba ba bahari ya hindi ndi hindi la kuchoma ma macho yanaona mbali li mbali na upeoo o ondoka upesi........utaendelea

Nakumbuka nilipokua naimba huu wimbo leo palivyo noma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…