Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Du! mkuu, umenikumbusha mbali sana.

Mimi nilipenda sana usomaji wa taarifa za habari za watangazaji wafuatao.

Mzee mwenyewe nguli David Wakati RIP ( ambae hata kanisani Mtakatifu Albano) nasikia alikuwa akipenda kusoma somo la kwanza kwenye biblia)

Charles Hillary

Julius Nyaisanga

Salim Mbonde

Ahmed Jongo

Abisai Stephen

Peter Makorongo

Mikidadi Mahmud

Sekione Kitojo

Suleyman Kumchaya

Florian Kaiza

Jacob Tesha

Bujaga Izengo Kadago

Tumbo Tamim Risasi (alikuwa anapooza kidogo kwenye usomaji wake na ndio maana alikuwa hasomi taarifa kwenye "peek time" kama saa mbili usiku)

Sarah Dumba

Halima Kihemba

Betty Mkwasa

Chini ya marehemu David Wakati, RTD ilikuwa na heshima yake kwa wakati ule na kila msikilizaji aliweza kufahamu ni mtangazaji gani angesoma taarifa ya habari ya saa saba mchana, saa mbili jioni na saa nne ya usiku.Watangazaji walikuwa wakipangwa kusoma taarifa kulingana na uzito wa taarifa hizo na uwezo wao.

Kwa kweli RTD ilikuja kupoteza watangazaji hodari na wenye uwezo mkubwa wa utangazaji katika tasnia hiyo na ni masuala ya malipo ndio yaliyoanza kuwatawanya kwenye kutafuta maslahi sehemu zingine.
 
Nakumbuka kulikuwa na mzee Khalid Ponella na kipindi chake cha "Zilipendwa" kila Jumapili saa nne asubuhi na baadae jioni kipindi chake kingine cha "Klabu Raha Leo Show".
 
  • Thanks
Reactions: ram
Ulikuwa unaamshwa na kipindi cha Tumsifu Mungu, kipindi kilichokuwa kinatayarishwa na padre Athony Chilumba
 
Ulikuwa unaamshwa na kipindi cha Tumsifu Mungu, kipindi kilichokuwa kinatayarishwa na padre Antony Chilumba
 
Hivi ni kwel umemsahau beki wao mstaarabu, beki wa kupanda na kushuka mtaalam Ezekiel Mwalongo?
 
Sitawasahau CHILAMBO, HILLARY na JONGO. Kwanini? Nisikilize.....
Kwa kutambua umuhimu wa kila mmoja katika maendeleo ya soka au michezo kwa ujumla, leo nitawazungumzia watangazaji waliokuwa wakitangaza wakati huo ambao ufanisi wa kazi yao ulichangia kwa kiasi kikubwa msisimko wa soka.




Ninapokumbuka umahiri wa Chilambo, naishia kusema, Mungu amuweke mahali pema peponi! Amina.

Huku majina ya Khalfani Ngassa, Raphael Paul, Ali Bushiri, Hussein Marsha, Abdalah Bori, Kitwana Suleiman, David Mwakalebela, Rajabu Risasi, Rashidi Abdalah, Ibrahim Magongo, George Masatu, Nico Bambaga, Beya Simba na wengineo wa Pamba, yakipambwa vilivyo na Chilambo.

Chilambo, alikuwa na uwezo wa kumpatia picha kamili ya mchezaji kiumbo, kiuchezaji, kitabia, kitu ambacho ni watangazaji wachache wamejaliwa katika kutimiza wajibu na kazi zao.

Moja kwamoja kutoka uwanja wa CCM Kirumba mwanza, uwanja wa nyumbani wa wana Tupisa Lindanda;
Golkeeper yuko Paul Rwechungura, akisaidiwa na Fullback right David Mwakalebela na Fullback Left Saleh Muddy Saleh (Saleh Muhammad). Half back four yuko Goeerge Magere Masatu na Sentahafu yuko Abdallah Bori. Half Back six yuko Hussein Aman Marsha wakati right wing yuko Hamza Mponda. Inside right; nambari nane huyu, yuko Nico Bambaga wakati sentaforward yuko Kitwana Suleiman "Popat", Khalfan Ngassa yuko Inside left na Left wing yuko Beya simba/Nteze John Lungu.

Hawa jamaa acha kabisa, Pamba ilikuwa na hazina ya wachezaji ambao rekodi yao haijawahi fikiwa na timu yoyote hapa Tanzania. Wengine ni akina Madada Lubigisa, Rajab Msoma, Alphonce Modest(Beki mtulivu/mstaarabu), Mao Mkamy "Ball Dancer", Goerge Gole "Double G" Fumo Felician, Pascal mayala, Hamisi Nyembo, Pamba mko wapi jamani.
 
Jangala pia unamkumbuka? Kipindi Chao cha maigizo kilikuwa kinarushwa hewani saa tatu usiku kikifadhiliwa na kibuku kila jumapili usiku. Kuna siku mshamu alimvamia Baba yake jangala na wenzake wakampiga na kumwacha akimbie wenzake mshamu wakasema acha masiala bwana dingi lake mshamu linayeya kama pajero kesho take ikawa gumzo kitaa. Je na hili tangazo la bp pia una unalikumbuka? Mazungumzo baaada ya habari mmeletewa kutoka radio Tanzania dar es salaam. Enzi hizo tunaishi kota za Wazo hili tukicheza na watoto wa nizar karamagi wanakaa magorofani. Am 33 years now.
Dah, kitambo sana enzi za kina Hendrick Maiko Libuda, lakini nasahau jina la yule
Mtangazaji alitangaza mechi ya simba na Atletico sports Aviacao ya Angola ambayo
ilikuwa na wachezaji wakali kama Kanka wemba, Abilio Amanali, Gito, Libenge, Bravo
Yanda, Nero sijui nelo n.k


Wakati huo simba ilikuwa ni kina Abdul Mashine, Mohammed Mwameja, Hussein Masha, Yamadhani Leny
Damian Kimti, Mteze John Rungu, Malota Soma, Edward Chumila n.k


Umenifanya nivikumbuke vipindi maarufu kama HISIA NA MUZIKI, MAHOKA, PWAGU NA PWAGUZI
PITIO LA KITABU NA SAIF D KIANGO N.K

Debora mwenda sitamsahau kamwe kwa kukifanya kipindi cha mama na Mwana
kipendwe hata na watu wazima......... acha Bwana hadithi tamu kama Ua Jekundu,
Binti chura, Kibibi jitu n.k Enzi zimepita sasa watoto wanacheza viduku.

Pia ninawakumbuka waigizaji kama Mzee MUNDU, Mshamu, Matuga n.k
 
Kwa vijana wa zamani. Unakumbuka nini unapopitia majina haya? Je, yuko wapi kwa sasa? Unamkumbuka katika kipindi kipi kilichokufurahisha?

1. Bujaga Izengo Kadago
2. Debora Mwenda
3. Sarah Dumba
4. Julius Nyaisanga
5. Charles Hillary
6. Eshe Mhidini
7. Frolian Kaiza
8. Tumbo Risasi
9. David Wakati
10. Halima Kihemba
11. Betty Mkwasa
12. January Costantine
13. Lando Mabula
14. Ben kiko
15. Abubakary Lyongo
16. Sued Mwinyi
17. Abisai Stevin
18. Nswima Ernest
19. Malima Ndelema
20. Richard Leo
21. Ahmed Jongo
22. Christina Chokunogela
23. Shaban Kissu
24. Jacob Tesha
25. Sallim Mbonde
26. Sekion

27. Omary
28. Abdalla Majura
CRDB ni benki ya wakulima kama..... Vijijini unalikumbuka hili tangazo? Tegemea bp ni nini...trekta meli ndege na vyombo vinginevyo...bp Tanzania limited ni zaidiiii! Je unakumbuka? Vikoromboso vinavyoendelea sasa iv kwenye radio ni aibu tupu. Damn I miss my childhood!!!
 
Alphonce modest beki mstaarabu wa kupanda na kushuka hafanyi kosa ndani ya kumi na nane. Je wachezaji wengine John bosco juma pondamali Mohamed Hussein Fred Felix minziro mwamba kizota na Huyu amenitoka kidogo Kuna wakati Edo kumwembe alikuwa anawaomba watanzaniawamchangia alikiwa mlinzi kilombero. Da jamani Enzi hizo.
 
Umenikumbusha mbali sana kaka wakati huo sh. mia inaitwa nyanga. Anyways mnayakumbuka na matangazo ya biashara na vipindi yaliyokuwa yanarushwa RTD kipindi hicho?

1. TANGAZO LA PEDI ZA JESI:
Wanawake kuweni na furahaaa, furahaaa, wakati wote popote na jesi,
Jesi, pedi mpya za kike za njano, ni nyororo raha kuvaa wakati wote......

2. TANGAZO LA DAWANOL
Mgongo wangu waniuma maumivu teleee, dawa ya maumivu dawa yenye nguvu dawa ni dawanol

3. TANGAZO LA SABUNI YA MSHINDI. n.k

MATANGAZO YA VIPINDI:

1. MASHIRIKA YA TAIFA: Mashirika ya taifa Tanzania yapo Mengi... na matangazo mengine mengi. Huwa natamani sana siku moja niende pale RTD nikaombe nipewe hayo matangazo niwe nayasikiliza tu mwenyewe ili niwe nakumbuka utotoni...DA INANIKUMBUSHA MBALI SANA

Singing; posta na simu kweliiii,kweli
Barua na posta, zifike haraka,tena kwa uhakika,litumie sasa,shirika la posta na simu tanzaniaaaaa.......

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Ulikuwa unaamshwa na kipindi cha Tumsifu Mungu, kipindi kilichokuwa kinatayarishwa na padre Antony Chilumba

au Sheikh Amrani Kilemile, mmoja wa wanazuoni mahiri. Akitoa tafsiri ya Qur'an kwa kasi na ufasaha mkubwa, huku akizingatia muda mfupi wa kipindi !
 
Nakumbuka kulikuwa na mzee Khalid Ponella na kipindi chake cha "Zilipendwa" kila Jumapili saa nne asubuhi na baadae jioni kipindi chake kingine cha "Klabu Raha Leo Show".

Du! umenikumbusha hilo jina nilikuwa nalitafuta sana, maana kipindi cha zilipendwa kwa kweli huyu mtu alikuwa nankipatia sana. Anakuwekea mziki wa zilipendwa na ukiisha anaanza kumwaga sifa kemkem kwa mwanamuziki au bendi hiyo.

Asante kwa kutukumbusha.
 
kuna tangazo la sabuni ya kodrai, kondraiiiiiiiiiii,....... lilikuwalinapigwa baada ya kipindi cha majira asbh.likinikuta nyumbani hili tangazo nilikuwa najua hapo tayari nimeshachelewa no skonga,maana kwa dk 4 au 5 zilizobaki nisingeweza kuwahi skonga.
Tangazo la kodrai nilikuwa nalipenda jinsi sauti walivyozipangilia.
 
Mwingine mkongwe naona wengi mnamsahau ni Mohammed Kisengo,​ kwa sasa yupo radio one, maranyingi taarifa ya habari ya saa moja asubuhi, huwa anaisoma kwa utulivu sana.
 
Loo jamani RTD enzi hizo ilitimia.Lakini leo hii mnaionaje hawa wenzetu wa TBCCM? Kuweni wakweli ni wangapi leo mmefungulia tbc!iwe radio au tv?Au ni wangapi walio soma gazeti la uhuru au mzalendo?Enzi zile ktk mzalendo kulikuwa na katuni za CHAKUBANGA,POLO,BUSHIRI..leo hii hakuna kitu
 
singing; posta na simu kweliiii,kweli
barua na posta, zifike haraka,tena kwa uhakika,litumie sasa,shirika la posta na simu tanzaniaaaaa.......

Sent from my blackberry 9780 using jamiiforums

dah hiyo mwaka 92 kaka.
 
Back
Top Bottom