Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Wanabodi,

Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.

Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.

Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na

  1. David Wakati
  2. Abdul Masudi (Jawewa)
  3. Eli Mbotto
  4. Stephen Mlatie
  5. Siwatu Luanda
  6. Salama Mfamao
  7. Salim Seif Nkamba (Mjomba)
  8. Michael Katembo
  9. Nelly Kidella
  10. Halima Mchuka,
  11. Omar Jongo
  12. Tumboi Tamimu Risasi
  13. Mohamed Ng'ombo
  14. Abisai Stephen (Uronu)
  15. Stephen Lymo.
  16. Nadhir Mayoka
  17. Juma Ngodae
  18. Rukia Machumu
  19. Karim Besta
  20. Henrick Michael Libuda
  21. Idrissa Sadalah
  22. Bati Kombwa
  23. Iddi Rashid Mchatta
  24. Dominic Chilambo

Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Pia sio vibaya kuwaulizia wale watangazaji wa siku nyingi ambao hatujui walipo, ili kama nao wametangulia tuyaingize majina yao.

RIP All the Fallen Heroes wa Tasnia ya Utangazaji Tanzania!,

Pascal.

Kuna mwingine nae umemsahau mungu alamlaze mahali pema. Huyo ni HASSAN NKUMBA. Nilikuwa napenda sana anavyosoma taarifa ya Habari.
 
Mkuu kwelitupu, kiukweli ukweli ni kitu kigumu, ila mimi ni mkweli!. Nilipojiunga, nilielezwa kuhusu uchawi!, bahati mbaya siamini kuwa uchawi upo!. Kiukweli uchawi upo, ila ni kwa wanaoamini tuu kuwa uchawi upo!, kwa sisi tusioamini, kwetu uchawi haupo!.

Wala siamini sababu ya vifo ni uchawi, ila pia naomba kuutoa ukweli mchungu kuhusu RTD ya enzi hizo!.

Ulikuwa unajua saa tuu ya kuingia kazini, ya kutoka huijui!. Mimi nakumbuka siku nikiingia asubuhi, unafuatwa saa 9 usiku, unapaswa kutoka saa 6 mchana, ila ukitoka ndipo ueanze kuandaa vipindi vyako!, kunawakati unaingia saa 9 usiku, unatoka saa 6 usiku siku inayofuata!.

Tulipoanza kazi Mjomba (SS Mkamba), akatuhusia mkitaka salama hapa, hawa akinadada waangalieni tuu!, msiwasogelee kwa sababu macho yote yako kwao!. Mimi na Abou tukamhakikishia Mjomba kuwa hilo kweli haliwezekani, kwa sababu, hao "wadada" wenyewe tuliwaona wachovu tuu!.

Baada ya kupita miezi 6, kumbe watu mnaokuwa nao kila siku, mara wa kwanza kuanza "kuona" ni Abou!, tukasema kumbe ful;ani ni mzuri hivi!, huku na kule, "akafika mahali!", kufumba kufumbua, Abou kahamidshiwa Nachingwea!.
Huko hata hoteli kuku ni mpaka ulipie kabla ndipo upikiwe!.

Ikaja zamu yangu!, ilikuwa ni balaa!, Mwanzoni tulianzia vile vi gesti Buguruni!, mambo yalipokolea, gesti mbali!, ni kila mahali, kuanzia "washroom!', studio!, juu ya meza ya ofisi!, kwenye ngazi!, hadi Telefon room!.

Mwanzo mwanzo tulitumia!, tulipozoeana, hatukukumbuka tena!. Wengi wa watumishi wa RTD wenye watoto, baba zao wako hapo hapo!. Kuna wengine wetu tumesurvive kwa kudra tuu ya Mwenyeezi Mungu!, tatizo kubwa la watangazaji wa zamani ni kuponzwa na umaarufu!, kujifungia studio kwa masaa mengi na watu wale wale hadi kujikuta kwenye Zero Grazing!, Ukisikia mtangazaji wa kike kaolewa, ujue aliyependa ni huyo mtangazaji wa kike!, yaani ili uoe mtangazaji, lazima kwanza mtangazaji huyo ndio akupende wewe!, vinginevyo! ukipenda wewe! jua.. ( japo nakiri sio wote).

Hii "zero graizing!" could be the main cause!.

Ila pia naomba kuwahakikishieni, pamoja na yote hayo, chanzo cha vifo sio UKIMWI!, kwa sababu Ukimwi ni "ukosefu tuu wa kinga mwilini!, yaani mtu hawezi kufa kwa "ukimwi" kwa kasabu ukimwi sio ugonjwa!, ila ukishakosa hiyo kinga mwilini, mwili wako unakuwa dhaifu na kuwa rahisi kushikwa na ugonjwa ambao ndio hupelekea kifo!.

Pasco.

Asante sana kaka Paschal Mayalla kwa kuutoa ukweli wenyewe. Wengine tulikuwa tunasikia juu ya suala hilo la kuzungukiana hapo hapo RTD, sasa wewe umetupa first hand information. Anyway hali hiyo ipo katika taasisi nyingi tu labda tofauti tu ni kuwa mlikuwa mnafanya kazi muda wote hadi usiku kucha.
 
Kuna wengine walipata ajali na kufariki (nafikiri gari iligongwa na treni hapo dsm miaka ya 70's) mmoja wapo alijulikana kwa jina la Ally Saheh. Kipindi hicho ilisemekana Bandarini na TBC kulikuwa na ushirikina wa kupitiliza!

Mkuu TBC haikuwepo kipindi hicho.
Acha kupotosha...
 
Pius Nyamko, alikuwa kocha wa Pamba, nilisoma na binti yake Prisca Pius Nyamko, sijui yuko wapi nw dayz


Mimi na marehemu baba yangu tulikuwa washabiki kisawasawa wa Pamba ya Mwanza TP Lindanda wanakawekamo!
Kupitia Pamba FC nilikuwa shabiki mkubwa sana wa Dominic Chilambo!!! RIP my father , RIP Dominic Chilambo , RIP Pius Nyamko (mnamjua?)
 
Mkuu TBC haikuwepo kipindi hicho.
Acha kupotosha...
Mkuu Bramo, sio wengi wanaofahamu kuwa RTD iliitwa TBC kabla haijawa RTD na sasa hilo jina la TBC ni imelirudia tuu, sio jipya, tofauti ni mwanzo ilikuwa Tanganyika, sasa Tanzania!. Kwa watu wa miaka ile, licha ya kubadilishwa jina kuitwa RTD, paper work zote ziliendelea kuwa TBC!. Tena baadhi ya stationaries mpaka mimi naondoka zilikuwa za Government of Tanganyika!.
 
Jamani mmenikumbusha mbali sana mbona kama vile ninaona maisha huko tulikotoka ndiko kuzuri?
Nitafieni na PASKAL MAYALA original na kipindi chake cha kitimoto ndani ya itv miaka hiyo yuko wapi huyu bwana?
 
Jamani mmenikumbusha mbali sana mbona kama vile ninaona maisha huko tulikotoka ndiko kuzuri?
Nitafieni na PASKAL MAYALA original na kipindi chake cha kitimoto ndani ya itv miaka hiyo yuko wapi huyu bwana?

Pascal Mayalla yupo. Tunamsubiri aje kuiongoza Kurugenzi ya Mawasiliano kwa weledi.
 
Last edited by a moderator:
Nimemkumbuka Malima Ndelema, huyu alikuwa bingwa wa kipindi cha ngoma za asili za makabila mbalimbali, sijui yu hai bado au sijui yu wapi sasa huyu mtu.

Ni watu waliokuwa wanakupa sababu na kukulazimisha kusikiliza radio tofauti kabisa na sasa!

Malima Ndelema yuko TBC Taifa anaendelea kuchapa kazi. May Day kitaifa ya mwaka huu tulikuwa naye Mbeya.Pascal Mayala amenikumbusha mengi ikiwa ni pamoja na swali tulilokuwa tukijiuliza tangu miaka ya 80
 
Pascal Mayalla yupo. Tunamsubiri aje kuiongoza Kurugenzi ya Mawasiliano kwa weledi.
Mkuu Mzito Kabwela, ni kweli bado nipo, ila kiukweli hapa nilipofika, sio kuwa najidai, bali niliishaivuka hiyo stage!, yaani niko over and above hiyo posti unayoitaja!, niliacha kutumwa tangu mwaka 2002!, mimi sasa ni kuku wa kienyeji, with 10+ years ya kuchakura, I don't see my self kama naweza kufugika na kusubiri kuletewa chakula kwa kutumwa tena na yeyote no matter who s/he is!.
Pascal.
 
Mkuu Mzito Kabwela, ni kweli bado nipo, ila kiukweli hapa nilipofika, sio kuwa najidai, bali niliishaivuka hiyo stage!, yaani niko over and above hiyo posti unayoitaja!, niliacha kutumwa tangu mwaka 2002!, mimi sasa ni kuku wa kienyeji, with 10+ years ya kuchakura, I don't see my self kama naweza kufugika na kusubiri kuletewa chakula kwa kutumwa tena na yeyote no matter who s/he is!.
Pascal.

ina maana huyu ndie pasco mayalla ninaye mfahamu mie? He jamani
 
daddy hizi picha umezitoa wapi maana nami nilitumwa kule chuoni niende nazo kwa ajil ya research ulikataa kunipa ulizficha wapi naziomba nipeleke japo moja
Kumbu-kumbu-01.jpg
 
Deborah Mwenda,kipindi hicho nilikuwa sikosi mama na mwana
 
ina maana huyu ndie pasco mayalla ninaye mfahamu mie? He jamani
Pascal Mayalla ni jina tuu, lakini wako Pascal Mayalla wengi.
Mimi ni yule Pascal Mayalla aliyekuwa RTD, pia namfahamu Pascal Mayalla fulani alikuwa JWTZ, yupo mwingine alisoma Urusi, kuna mwingine alisoma India, kuna mmoja aliishi US pale Maryland na mpaka leo mke wake yuko kule, kuna Pascal Mayalla aliyekuwa mtangazaji wa Kitimoto, yuko yule aliyekuwa TBC akifanya program za CCM, yuko Pascal Mayalla fulani ni mshauri wa siasa wa ubalozi wa Uingereza nchini, kuna Pascal Mayalla fulani ni mwandishi wa habari wa kujitegemea, kuna Pascal Mayalla fulani alisoma sheria kwa miaka 4 pale UDSM, hadi kuna Pasco wa jf, naye nasikia pia sometimes akichanganywa na Pascal Mayalla, hivyo inategemea huyo unayemfahamu wewe ni yupi!, unaweza ukawa unamfahamu yule Pasco wa jf, ukifikiri ndiye Pascal Mayalla Mtangazaji, kumbe ni watu wawili tofauti!.
Pasco.
 
Mkuu Mzito Kabwela, ni kweli bado nipo, ila kiukweli hapa nilipofika, sio kuwa najidai, bali niliishaivuka hiyo stage!, yaani niko over and above hiyo posti unayoitaja!, niliacha kutumwa tangu mwaka 2002!, mimi sasa ni kuku wa kienyeji, with 10+ years ya kuchakura, I don't see my self kama naweza kufugika na kusubiri kuletewa chakula kwa kutumwa tena na yeyote no matter who s/he is!.
Pascal.

Paschal....

Habari yako mkuu wangu....

Mkuu naomba pia kujua walipo watangazaji mahiri wa RTD na STZ enzi hizo....

Rosemary Mkangara...

Nathan Rwehabura-Mara ya mwisho alikuwa Sahara comm....

Othman Matata....

Kassim Mikongoro...

Daniel Msangya....

Wilson Malosha....

Geoffrey Erneo....

Abdallah Mlawa.....

Yusuph Omar Chunda (mzee wa methali na nahau huyu)....STZ

Makame Abdallah...STZ

Nkwabi Ng'wanakilala - Alikuwa Director wa RTD huyu....Nadhani hata wewe ulikuwa chini yake....

Nikutakie siku njema mkuu....

Bala.
 
Hiki ni kikosi cha first 11 ya Radio One.
Waliokaa kutoka Kushoto ni Charles Hilary kwa sasa yuko BBC-London
Mikidadi Mahamod (Brother) sasa ni Mkurugenzi wa Radio Uhuru, Mzungu Mike Ross, na Uncle J. Nyaisangah.

Waliosimama toka kushoto, Deo Mshigeni yuko US, Monica Mfumia yuko UK, Florah Nducha ni Mkuu wa UN Radio New York, Vicky Msina, ni PRO wa BOT, Aboubakar Liongo yuko DW-Radio ya Ujerumani, Lilian Mbaga sasa ni Mkurugenzi wa TGNP, Sunday Shomari yuko VOA na Taji Liundi sasa ni Meneja wa PRT ya TBC.

Mkuu Mayala sahihisho. Taji hayupo tena TBC. Wakat akiwa pale alikuwa ni mkuu wa idhaa ya kiingereza (TBC international) sio TBC FM
 
Back
Top Bottom