Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Nikitangaza kutoka tabora Mimi no Ben kikowa rrrrrrrrrrrrrrrrrredio tanzzzzaniaaaa.

Dah tulikuwa tunapenda sana kusikiliza RTD, kipindi cha Majira cha saa 3 usiku na 12 asubuhi.Tena cha saa 12 asubuhi ndo ulikuwa muda wa kujiandaa kwenda shuleni.
 
Ladha kumi za bongo na abd ilikuwa nzuri sana radio one
 
Bro mick,Ben kiko,Charles hilal,rwegasira,rose chitala,abubakar lyongo,Samadu hasan,Steven kabuye(kiss FM)
 
Dominic Chilambo, Ahmed Jongo, Omar Jongo, Mikidadi Mahamoud, Charles Hilily N.k Hasa Sisi Wapenzi Wa Kandanda, Ilikuwa Raha Tupu!!!
 
Iwe ni kwenye Radio au TV. Me naanza na hawa;

Misanya Dismas Bingi
Julius Nyaisanga "Anko Jay"
Halima Mchuka

Karibu uendelee...
Julius Nyaisanga "Anko Jay"
Halima Mchuka '' stoe lady hawa Mungu awaweke mahala pema.
 
Dah! Nilikua ctaki kupitwa na reporter toka TBR Ben kiko, Tumbo Risasi KGM, Restuta Bukoli SHY na watangazaji kama dkt. Roy Hilaric Maganga kwenye sintosahau na usiku wa mahaba RFA na mapresenter wengine kibao kama Halima mchuka Ahmed jongo pia walikua the best kwangu
 
Enzi hizo za kuchaguzi mkuu kulikuwa na jamaa anaitwa SPENCER LAMECK alikuwa anareport vizuri sana asee
 
Julias Nyaisanga KWA taarifa ya habari alukuwa balaa, Mungu amlaze pema
 

Mkuu,umenitoa machozi.
 
Mkuu umenikumbusha huyo jamaa ilikuwa nikufungua kiss fm nikimsikiliza sichoki.. yupo vizuri sana.

Mkuu,kuna mwingine alikuwa anaitwa Silyverter Bahati,alikuwa mwenyeji wa programu ya Kiss late night show,nakumbuka rafiki zangu walikuwa wanafananisha lafudhi na sauti yangu kama yake.Yuko wapi siku hizi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…