Ezekiel Malongoooo..........Beki mstaarabu wa kupanda na kushuka.........!!!!!!Kwanza nakumbuka Ezekiel malongo akiwa studio. Mbwe mbwe kibao. Anatamka saa dakika hadi sekunde. Kweli. Mm huwa naburudika sana akiwa yeye hasa kipindi cha mchezo.
Mkuu umefanya nicheke! Wazee wa kukojoza hahhhhh! Social media imeteka akili za watu. Enzi hizo ulikuwa unasubiri kwa hamu kusikiliza taarifa ya habari, michezo n.k kuna kipindi nilikuwa nakipenda sana 'tuimbe sote'Siku hizi hawa Facebook wanasikiliza akina kibonde na wazee wa kukojoza basi
Kweli mkuu, social media imeharibu utaratibu wa mambo mengi sana.Mkuu umefanya nicheke! Wazee wa kukojoza hahhhhh! Social media imeteka akili za watu. Enzi hizo ulikuwa unasubiri kwa hamu kusikiliza taarifa ya habari, michezo n.k kuna kipindi nilikuwa nakipenda sana 'tuimbe sote'
Sawa alikuwa Cuban Marimba, je anaitwa Juma nani?Alikuwa Cuban Marimba
Bado sikuelewi anaitwa Juma nani?Juma ******
Je cha ngoma zetu na yule rafiki yake na Ben Kiko sikumbuki jina ngoja nilitafute.Alipenda kuwaweka wajaluo na ngoma zao halafu ataweka wahaya halafu wakurya. Alikuwa mchokozi wa watani. Ni mtu wa kusini alishatangulia mbele ya haki ila alikuwa na sauti nzuri saaana.duuuu jamani nimecheeeeeka kweli kweli yaani unayakumbuka yoooooote hayo aisee wee hatari mimi nilikuwa napenda kipindi cha Mama na Mwana cha Sara Dumba, kipindi cha salamu cha jioni njema... taarifa baada ya habari ilikuwa ikisimuliwa na SS Nkamba siku akisoma mtangazaji mwingine nilikuwa nazima radio au nabadilisha stesheni
Hadithi zake kama mfalme binti chura, ua jekundu.. Yaani ilikua as if unaangalia filamu
Yaani jamani utoto bwana. Mi nakumbuka nikiwa darasa la pili nikawa naenda saa nane shule wakati wengie woote ( broethers& sisters) wanaenda asubuhi. Sasa mimi naachwa na houseboy na housegirl. sasa housegirl anaenda sokoni ananichukua nakumbuka tunapitia nyumba Fulani ( hizi zilikuwa za serekali) na yetu ilikuwa ya serekali maeneo yanaitwa uzunguni, sitataja Mkoa isiwe identified. Basi sasa ndio najua huyo housegirl alikuwa anaenda kwa BF napewa fizzes ( sidhani kama sasa zipo) ileinawekwa kwenye maji unakunywa kama juice ( note: sio kuwa nyumbani havikuwepo basi tu utoto) napewa na buiscuit nakunywa wao wana- disappear. Jamani haya mambo unaweza andika kitabu!Mi nakumbuka nilikua ndo mtoto so kutumwa mara dukani mara kanunue mkaa mara nenda kwa flan.... Pia wakubwa walikua wananichukua natoka nao ili wapate gia ya kwenda kuonana na wapenzi wao [emoji28] [emoji28] [emoji28] eti mzazi asiwafikirie vibaya mi mdogo Naenda nao hahahaa hahahahahaah
Namakumbuka yaani kipindi akiwepo kinakuwa safi sana!Jamani wazee wenzngu munamkumbuka Ben Kiko?
Na Michael Katembo ( RIP) alikichangamsha kipindi!Kipindi cha ngoma za asili na Mkoa kwa Mkoa navikumbuka sana na natamani hata leo nipate fursa ya kuzisikiliza nyimbo za makabila mbali mbali
Nakumbuka mengi tu, jambooo, tuimbe sote, mwanamziki wetu, misakato, mkoa kwa mkoa, pole kwa kazi, mchana mwema, ombi lako, jioni njema, sukitaa, ATC hewani, mahokaa, mama na mwana, mchezo wa redio wa kina mzee jongo na jangala na vingine kibao. Watangazaji mahiri kama siwatu Luanda (RIP), abdallah ngalawa, Michael Katembo, David Wakati, Budyaga Izengo Kadago, somebody Aswile huyu alikuwa mke wa mchezaji wa Yanga Godwin Aswile bila kuwasahau wawakilishi wa mikoani Adisai Steven, Ben kiko, Dominic Chilambo, ilikuwa raha sana siku hizoWakuu hebu tukumbushane enzi zile za Radio Tanzania, enzi ambazo Radio ndio ilikuwa kila kitu katika suala zima la kupata habari. Tukumbushane watangazaji mahiri wa enzi zile, vipindi vizuri pamoja na vituko mbalimbali ambavyo huwezi kuvisahau enzi za RTD.
Karibuni...
Bi Sara Dumba, Amefariki miezi michache iliyopita akiwa mkuu wa wilaya ya njombeNiliwahi kusoma kitabu cha binti chura nikiwa darasa la 3, ilikuwa bonge la stori yule mama sijui yuko wapi....
Unamkumbuka mtoto wa mzee jangala! Mshamu... Zilikuwa haziivi kabisa na Baba yake.1 Taarifa ya habari na ile ngoma ya yule mzee asiyeona na ngoma kumi
2. Wakati wa kazi. "ujuzi niliupata hapa hapa kazini"
3. Hii ni kwaresimaa.
4. Lala salama.
5. Vipindi vya masomo ya shule za msingi tukikaa darasa zima watoto 40 na kusikiliza mwalimu wa redio. Wengine hata hiyo redio ilikuwa haisikiki vizuri lakini ilikuwa lazima mhu!
6. Kipindi cha wagonjwa. (Ajuaye bwana Mungu kwa mzima kuwa mfu, mgonjwa kuwa salaaaama leo tunatoa pole).
7. Mchezo wa Redio (Mkataa pema pabaya panamwita) Sikosi hapo. watu mnakaa kana kwamba mnawaona akina Jangala na wenzie na yule mwenye sauti kubwa na yule mama aliyekuwa na roho mbaya. Mtu unamchukia mtu hata bila kuona sura yake.
8. Mpiraa. Nakumbuka Yanga ilikuwa inacheza na Simba 74 tulipiga teke redio ya baba mimi na kaka yangu. Tulikula mkong'oto.
9. Hotuba za Mwalimu. Kila wakisema anaongea na wazee wa Dar ujue kuna kitu. Hapo hatutoki kama tupo likizo, wazee wote wa jirani wanakuja kwetu ili wasililize hotuba. Shuleni boarding kulikuwa na redio moja inazunguka kila bweni kila week.
10. Mchana na usiku mwema na miziki yake!! We acha akina Mbaraka Mwinshehe, Juma ******, Marijani Rajab, Western Jazz, Ndala Kasheba, Polisi Jazz, JKT, Tankat Almasi, Taarab nk. Samahani nimeandika mengi lakini ni kama therapy kutoa haya ya sasa kichwani. Big up mtoa mada.
Kweli kabisa, huko KBC unakutana na harambeeeeHeri yako wewe ulikuwa na option ya cassette, sisi ilikuwa only Radio basi, nakumbuka kitu kikubwa brand ya "National Panasonic". Iwapo hupendi kipindi/ program fulani option ilikuwa ni kuchagua KBC Nairobi, na huko KBC ulikuwa unaombea usikutane na ile miziki yao ya "kanindo"
you made my evening.Unamkumbuka mtoto wa mzee jangala! Mshamu... Zilikuwa haziivi kabisa na Baba yake.
Tutumie kibuku uuuu ni pombe bora, tumia kibuku ni pombe bora, ngoja nirudi nije nighani kama yule dada[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Huyu alikua antangaza kutokea (Kama sijakosea) kanda ya katiNamakumbuka yaani kipindi akiwepo kinakuwa safi sana!
Ua jekundu ilikiwa sikosi.. unasimuliwa mpaka inahisi unaangalia video ya kinachosimuliwaNakumbuka mengi tu, jambooo, tuimbe sote, mwanamziki wetu, misakato, mkoa kwa mkoa, pole kwa kazi, mchana mwema, ombi lako, jioni njema, sukitaa, ATC hewani, mahokaa, mama na mwana, mchezo wa redio wa kina mzee jongo na jangala na vingine kibao. Watangazaji mahiri kama siwatu Luanda (RIP), abdallah ngalawa, Michael Katembo, David Wakati, Budyaga Izengo Kadago, somebody Aswile huyu alikuwa mke wa mchezaji wa Yanga Godwin Aswile bila kuwasahau wawakilishi wa mikoani Adisai Steven, Ben kiko, Dominic Chilambo, ilikuwa raha sana siku hizo