Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Je cha ngoma zetu na yule rafiki yake na Ben Kiko sikumbuki jina ngoja nilitafute.Alipenda kuwaweka wajaluo na ngoma zao halafu ataweka wahaya halafu wakurya. Alikuwa mchokozi wa watani. Ni mtu wa kusini alishatangulia mbele ya haki ila alikuwa na sauti nzuri saaana.
Michael Katembo
 
Nilipenda External Service sana nikiwa likizo nilikuwa namsikiliza Eda Sanga akituma salam na miziki ya akina Michael Jackson, Cool and the Gang, Bonny M halafu habari toka wapigania uhuru waliokuwa wanatumia External kwenye propaganda zao. Hapo uzalendo ulitujaa tunataja kanuni, imani bila kukosea nukta. We baba wee. Yako wapi sasa. Radio nyingi lakini hakuna chochote watoto watajua.
Elimu ya watu wazima, Kilimo chetu, umoja wa mataifa week hiii.
Malenga wetu bana
 
Tumbuizo asilia zilikuwa zinapigwa nyimbo za makabila yote tz

Wooh.... good memories kwakweli, yaani it can't happen again
Tulikuwa tunawajua watangazaji wote kwa sauti zao tu, kabala hata hajataja jina, unajua huyu ni Aleicia Maneno au christine chokunogela, au Siwatu Luanda (she was cute kwa sura na sauti yake pia) na wengine wengi....
 
Mkuu umefanya nicheke! Wazee wa kukojoza hahhhhh! Social media imeteka akili za watu. Enzi hizo ulikuwa unasubiri kwa hamu kusikiliza taarifa ya habari, michezo n.k kuna kipindi nilikuwa nakipenda sana 'tuimbe sote'

Kwenye hiki kipindi kwaya za jeshi na mashirika mbali mbali ndio utazisikia humu, Marehemu Komba nae alianzia mbali tangu "Tuimbe Sote"
 
Wakuu hebu tukumbushane enzi zile za Radio Tanzania, enzi ambazo Radio ndio ilikuwa kila kitu katika suala zima la kupata habari. Tukumbushane watangazaji mahiri wa enzi zile, vipindi vizuri pamoja na vituko mbalimbali ambavyo huwezi kuvisahau enzi za RTD.

Karibuni...

Kuna kipindi likuwa lazima tusikilize shuleni, kile cha masomo sikumbuki kinaitwaje ila mnasikiliza mwanzo mwisho baadae mwalimu anaanza kuuliza maswali kutokana na kilichofundishwa.
Kipindi cha wakati wa kazi, kilikuwa marvelous hiki kilikuwa kinawahoji wafanyakazi wa mashirika mbali mbali jinsi wanavyofanya kazi, so ilikuwa ni rahisi kujua mashirika yanafanya kazi gani, changamoto wanazokutana nazo n.k
 
Dah Mengi
Usomaji wa taarifa wa habari ulikuwa wa makini. Sisi tukiwa wadogo tulikuwa tunabashiri wasomaji.
Na hii ndio Taarifa ya Habari isomwayo na ...... David Wakati, SS. Nkamba/ Juma nGondae/ jamani we
Kipindi cha klabu raha leo Shooooooow!
Salamu kwa wagonjwa!
Mchana mwema
Kipindi cha wafanyakazi jamani- Wimbo wa Msondo-n Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio.......( mwenye clip hiyo aiweke)
Pwagu na Pwaguzi
Mchezo wa Redio jamani wanaact kama vile unawaona!! Wasanii hao wangekuwepo leo wangepata hela sana!
Wazungu wanasema "Old is Gold" tulikua pembeni ya babu zetu tukifatisha wasoma habari.

Na kuna kale kamwimbo ukikasikia tu unajua mida wa kuamka kwenda shule...daah kalikia kanakata stim zooote.
 
Kipindi cha Pwagu na Pwaguzi

Matangazo ya vifo

Maneno hayoooo

Mazungumzo baada ya Habari

Ile jingle ya habari za michezo tulikuwa tunaimba hivi " baba yake juma ana mavilaka..anamavilaka.
.anamavilakaaaaaaa!'...

Sikiliza bwana umeme..

tingtingtingtingtingtingtingiiiiiiiiiiiiiiiii

HIVI SASA NI SAA KUMI KAMILI....
Duuh wazee hadi matangazo ya vifo mlikua hamyakosi
 
Wazungu wanasema "Old is Gold" tulikua pembeni ya babu zetu tukifatisha wasoma habari.

Na kuna kale kamwimbo ukikasikia tu unajua mida wa kuamka kwenda shule...daah kalikia kanakata stim zooote.
Unadhani 42_0007, Old is Gold indeed!
 
Lakini yoote Tisa ukisikia sauti ya David WAKATI wacha kabisa. alijua anatangaza nini!!
halafu lugha waliijua barabara. kiswahili sanifu. sio cha mtaani.
ukija kwemya mpira - raha tupu
mkute ahmed Jongo
Salim Mbonde
mikidadi mahamood
dominic Chilambo
baadaye abubakar Lyongo

taarifa za majira- Ben Kiko- mnakumbuka wakati wa vita vya kagera alitoa live mpaka wakamrudisha nyuma
( WAKAJA WAKAMUOWA....... endelea...)

Yapo mengi.
 
Zile ngoma zilizokuwa zikipigwa kama kiashiria cha kuanza kwa taarifa ya habari, kilikuwa kiashirio cha watoto kukaa kimya vinginevyo tulikula bakora toka kwa wakubwa.
Kwakweli zamani kila kitu kilikua kwenye mpangilio..
 
Kipindi cha Lugha Ya Kiswahili nilipenda sana wimbo(jingle) yake
"Tanzania Bara na Visiwani....ya Taifa hili lugha...." Nimesahau unavyoendelea.

Pia kipindi cha rushwa. Wimbo wake
"Wito nautoa kwa taifa zima, tuchukie rushwa kwani ni adui...."

Pia Mahoka na Pwagu na Pwaguzi.

Mchezo Wa redio nilikuwa nampenda mwigizaji mmoja akiitwa Matuga.
.
 
Mchezo wa mzee Jangala ikidhaminiwa na pombe aina ya chibuku, nakumbuka nyimbo, idara yetu ya uhamiaji nalo jukumu kubwa saanaaaa kuwakaribishaa kuwasafirishaa na kulinda mipaka yetu[emoji441][emoji443][emoji443][emoji445][emoji445]

Watoto wasafi moyonii ni nyoota za macho ya wazaziiiiii[emoji445][emoji445][emoji445][emoji443][emoji443][emoji441]

Shamba aaanii shambaani shambaani mazaoo boora shambaani, haya twendenii shaambanii wananchi tukaalimeee [emoji443] [emoji444] [emoji446] [emoji447]

Wanawakee wa Tanzania wazuuuriii saaaanaaa, wanawakeeee tanzaniaa maendeleo tanzaniaaaa[emoji445][emoji443][emoji441][emoji443][emoji445]

Kuleni chakula boora cha kuujenga muili naku.... Pa kulala pawe boraa[emoji443][emoji445][emoji441]

Wakati umewadia wa salam za wagonjwa hosipitalinii leo tunawapa poleee, ajuaye bwana Mungu kwa mfu kuwa mzima mgonjwa kuwa salamaa leo tunawapa polee[emoji445][emoji445][emoji443][emoji445][emoji445][emoji441]

Wananchiiiii tujifunzeni ushirikaaaaa wananchi tujifunzeni ushirikaaaaa [emoji441][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445]

Jamani vitaa imetangazwaa jamaaa wananchi wote tuwe imara, vijijini na mjini msisite kuwasema walanguzi[emoji445][emoji445][emoji445]


Matangazo sasa
1. Tumaa vifurushiii barua na pesa vitu mbalimbali vifike harakaaa tena kwa uhakikaaa, itumie sasaa shirika la posta na simu tanzaaaaniaaa ndio tegemeo letuu.

2. Hebu jitokezeee jioneshe simamaa mbelee za watuuu

3. Tairi general kutoka arushaaa tanzaaaaniaaa

4. Revolaaa revolaaaaa revolaaaaaa revolaaaaaaaa

5. Wee acha kula mali ya umma wee acha kujitafuna tafuna weeeee, wachaaaaaaaaa

6. Tumia chibuku ndio pombe bora, radha ya chibuku hujulikana, sifa moja na nyinginezo ni kulinda hadhi ya mnywaji

7. Komoooooaaaaa aaa komooooaaaa komoaaaa

8. Benki ya akiba ya posta ndio yako, benki ya akiba ya posta ni kwa watanzaniaaa woooote wakubwa kwa wadogo... Wananchi unaweza kufungua akaunti ya kawaaida, akaunti ya muda na akaunti ya muda maaalum.. Usingoje kesho ooo fungua akaunti yako leooo

Watangazaji hahaha Mama Deborah, Dominic Chilambo
Nimejikuta napata sweet memories tu
Dah! Huo wimbo wa salam za wagonjwa hospitalini ulikuwa unanikosha sana!
 
Kulikuwa na igizzo moja na mtu mmoja alikiwa anaitwa sande aliye kuwa dereva wa magari ya mzigo akapata ukimwi. Aisee then kulikuwa na kina jangala anzi hizo,mzee pwagu etc
1 Taarifa ya habari na ile ngoma ya yule mzee asiyeona na ngoma kumi
2. Wakati wa kazi. "ujuzi niliupata hapa hapa kazini"
3. Hii ni kwaresimaa.
4. Lala salama.
5. Vipindi vya masomo ya shule za msingi tukikaa darasa zima watoto 40 na kusikiliza mwalimu wa redio. Wengine hata hiyo redio ilikuwa haisikiki vizuri lakini ilikuwa lazima mhu!
6. Kipindi cha wagonjwa. (Ajuaye bwana Mungu kwa mzima kuwa mfu, mgonjwa kuwa salaaaama leo tunatoa pole).
7. Mchezo wa Redio (Mkataa pema pabaya panamwita) Sikosi hapo. watu mnakaa kana kwamba mnawaona akina Jangala na wenzie na yule mwenye sauti kubwa na yule mama aliyekuwa na roho mbaya. Mtu unamchukia mtu hata bila kuona sura yake.
8. Mpiraa. Nakumbuka Yanga ilikuwa inacheza na Simba 74 tulipiga teke redio ya baba mimi na kaka yangu. Tulikula mkong'oto.
9. Hotuba za Mwalimu. Kila wakisema anaongea na wazee wa Dar ujue kuna kitu. Hapo hatutoki kama tupo likizo, wazee wote wa jirani wanakuja kwetu ili wasililize hotuba. Shuleni boarding kulikuwa na redio moja inazunguka kila bweni kila week.
10. Mchana na usiku mwema na miziki yake!! We acha akina Mbaraka Mwinshehe, Juma ******, Marijani Rajab, Western Jazz, Ndala Kasheba, Polisi Jazz, JKT, Tankat Almasi, Taarab nk. Samahani nimeandika mengi lakini ni kama therapy kutoa haya ya sasa kichwani. Big up mtoa mada.
 
1. Nakukumbuka kile kipindi cha ATC hewani .... basi mie nikisikia ule mngurumo wa ndege mie roho kwatu kama nimepanda vile.
2. Kahawa ni mali, yule mama sijui anaitwa Bernadeta Kulaya alikuwa mtangazaji...lafudhi ya kichaga
3. Mama na Mwana.... hasa ikiwepo hadithi za binti chura mie raha.
4. Kile kipindi cha mchana mwema, salamu ...nikisika tu najua niwakati wa uji kunyeka
5. Sikiliza Bwana Umeme....
6. Kipindi cha Jambo
7. Halafu Zilipendwa
8. Kile pindi cha dini Jumapili hasa mida ya Jion, ilikuwa simanzi kwangu
9. Ila nilikuwa sipendi kipindi cha salam...wakianza hapo watatajana weee mpaka inakera
10. Majira
 
Back
Top Bottom