Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Mkuu,umenitoa machozi.

Kulikuwa na watangazaji mahiri kama kina Bujaga Izengo Kadago,Omar Jongo,Ahmed Jongo,Nadhir Mayoka,Rashid Idd Mchata,Edda Sanga,Salah Dumba,Bett Chalamila,Sunday Shomari,Omar Liongo,Abdalah Majura na wengine wengi tu
 
ALIYEKUWA mkuu wa wilaya ya Njombe na mwanahabari mkongwe Bi Sarah Dumba amefariki dunia ghafla akiwa wilayani Njombe mkoa wa Njombe.

Mkuu huyu wa Wilaya amefariki usiku huu kwa Presha na mwili wake umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya ya Njombe, Kibena
RIP Dada Sarah Dumba.

Paskali
 
Ilikua mpira ukitangazwa na Ahmed jongo na Charles hilary utapenda uusikilize tu! Utamsikia Charles hilary kabla ya mpambano anakwambia;

"Eeeh! Refalee wa leo ni Meja gwaza Mapunda wa Morogoro" Dominic chilambo alikua akipenda kusema;

"Uwanja umenona,watu ni wengi kwelikweli,Polisi ni wengi pia!!

RTD ilikua ni radio ya wote aiseeee! Kitambo sana!
 
Hivi kile kipindi cha MAZUNGUMZO BAADA YA HABARI kilikua kikiletwa na mtangazaji gani? Kwa mwenye kujua atujuze please!
 
Nimemkumbuka Malima Ndelema, huyu alikuwa bingwa wa kipindi cha ngoma za asili za makabila mbalimbali, sijui yu hai bado au sijui yu wapi sasa huyu mtu.

Ni watu waliokuwa wanakupa sababu na kukulazimisha kusikiliza radio tofauti kabisa na sasa!
Sasa hivi ni u know what n'm sayin..kubana pua na kulamba lamba midomo.Hawa watoto wa kiume,shida saana.Niliacha siku nyingi kusikiliza radio.
 
Vipindi:
1.0 Kutoka Umoja wa mataifa (UN)
2.0 Mbiu ya Mikoa
3.0 Wakati wa kazi
4.0 Mgeni wetu
5.0 Kipindi cha wagonjwa/salaam za wagonjwa
6.0. Bendi zetu
7.0 matangazo ya vifo
8.0 Club raha leo
9.0 Tumwabudu Mungu
10.0 Ana kwa Ana
11.0 Majira
12.0 ''kipindi cha nyerere' (ilikuwa baada ya taarifa ya habari ya saa 2 usiku)
 
Vipindi:
1.0 Kutoka Umoja wa mataifa (UN)
2.0 Mbiu ya Mikoa
3.0 Wakati wa kazi
4.0 Mgeni wetu
5.0 Kipindi cha wagonjwa/salaam za wagonjwa
6.0. Bendi zetu
7.0 matangazo ya vifo
8.0 Club raha leo
9.0 Tumwabudu Mungu
10.0 Ana kwa Ana
11.0 Majira
12.0 ''kipindi cha nyerere' (ilikuwa baada ya taarifa ya habari ya saa 2 usiku)
Huyu alikuwa sister wangu sana, wimbo wake wa mwisho kabla hajaanza kuumwa uliitwa "Ousmane Bakayoko", siku ya kifo chake nilimpigia wimbo "Salama" wa Marijani Rajab

Nkizisikia nyimbo hizi, namkumbuka sana Salama!.

Nawe Mkumbuke.

Marijani Raajab - Salama - YouTube

Pascal
Daaah!! Heshima kwako mkuu,asante sana kwa huo wimbo,nimejikuta nausikiliza huku nimejaa majonzi telee!! Kitambo sana Mkuu.
 
Wanabodi,

Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.

Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.

Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na

  1. David Wakati
  2. Abdul Masudi (Jawewa)
  3. Eli Mbotto
  4. Stephen Mlatie
  5. Siwatu Luanda
  6. Salama Mfamao
  7. Salim Seif Nkamba (Mjomba)
  8. Michael Katembo
  9. Nelly Kidella
  10. Halima Mchuka,
  11. Omar Jongo
  12. Tumboi Tamimu Risasi
  13. Mohamed Ng'ombo
  14. Abisai Stephen (Uronu)
  15. Stephen Lymo.
  16. Nadhir Mayoka
  17. Juma Ngodae
  18. Rukia Machumu
  19. Karim Besta
  20. Henrick Michael Libuda
  21. Idrissa Sadalah
  22. Bati Kombwa
  23. Iddi Rashid Mchatta
  24. Dominic Chilambo
  25. Hassan Mkumba
  26. Khadija Said
  27. Ally Saleh
  28. Kwegier Munthali
  29. Leonard Mtawa
  30. Khalid Ponera
  31. Ben Kiko
  32. Restuta Bukholi
  33. Sarah Dumba

Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Pia sio vibaya kuwaulizia wale watangazaji wa siku nyingi ambao hatujui walipo, ili kama nao wametangulia tuyaingize majina yao.

RIP All the Fallen Heroes wa Tasnia ya Utangazaji Tanzania!,

Pascal.

NB. Pia unaweza Kupata Taarifa za Baadhi ya Watangazi waliotutoka hapa.

Tribute to David Wakati, Kikwete, Mengi, Nchimbi na ...

Tribute to David Wakati: His Legacy Will Live On!
Mzee David Wakati Katutoka Leo Translate this page



Tribute To Uncle J. Nyaisanga: Jee Unamkumbuka kwa Lipi?!. Kuagwa ...

TBC haikumtendea haki marehemu David Wakati - Jamii Forums


  1. Tribute to Halima Mchuka: Alikuwa Mtu wa Watu!
    Halima Mchuka hatunae duniani - Page 2 - JamiiForums
    Hii RTD unaikumbuka? - JamiiForums
    Msiba wa halima mchuka hauna nafasi tbc - JamiiForums
    Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa RTD - Jamii Forums
    Topic: Nimewakumbuka hawa pia..................zamani... - Jamii ...


    Mtangazaji Maarufu wa RTD Amefariki Dunia Asubuhi Hii ..
Mh hii post ya mwaka 2013. Lkn ina jina la aliyefariki jana. Hii ikoje?
 
upload_2016-6-14_18-36-13.jpeg
upload_2016-6-14_18-36-28.jpeg

Wakuu hebu tukumbushane enzi zile za Radio Tanzania, enzi ambazo Radio ndio ilikuwa kila kitu katika suala zima la kupata habari. Tukumbushane watangazaji mahiri wa enzi zile, vipindi vizuri pamoja na vituko mbalimbali ambavyo huwezi kuvisahau enzi za RTD.

Karibuni...
 
Nakumbuka usomaji wa taarifa ya habari wa Christi e Chakunegela saa nne usiku alisoma bila kukosea hata neno moja na taarifa ya habari ilikuwa kama vile inasomwa na software

Namkumbuka Mahokaaaaaaaa!!!!

Mikingamo mwendo wa kuchomeana utambi
 
Back
Top Bottom