Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Mchezo wa mzee Jangala ikidhaminiwa na pombe aina ya chibuku, nakumbuka nyimbo, idara yetu ya uhamiaji nalo jukumu kubwa saanaaaa kuwakaribishaa kuwasafirishaa na kulinda mipaka yetu[emoji441][emoji443][emoji443][emoji445][emoji445]

Watoto wasafi moyonii ni nyoota za macho ya wazaziiiiii[emoji445][emoji445][emoji445][emoji443][emoji443][emoji441]

Shamba aaanii shambaani shambaani mazaoo boora shambaani, haya twendenii shaambanii wananchi tukaalimeee [emoji443] [emoji444] [emoji446] [emoji447]

Wanawakee wa Tanzania wazuuuriii saaaanaaa, wanawakeeee tanzaniaa maendeleo tanzaniaaaa[emoji445][emoji443][emoji441][emoji443][emoji445]

Kuleni chakula boora cha kuujenga muili naku.... Pa kulala pawe boraa[emoji443][emoji445][emoji441]

Wakati umewadia wa salam za wagonjwa hosipitalinii leo tunawapa poleee, ajuaye bwana Mungu kwa mfu kuwa mzima mgonjwa kuwa salamaa leo tunawapa polee[emoji445][emoji445][emoji443][emoji445][emoji445][emoji441]

Wananchiiiii tujifunzeni ushirikaaaaa wananchi tujifunzeni ushirikaaaaa [emoji441][emoji445][emoji445][emoji445][emoji445]

Jamani vitaa imetangazwaa jamaaa wananchi wote tuwe imara, vijijini na mjini msisite kuwasema walanguzi[emoji445][emoji445][emoji445]


Matangazo sasa
1. Tumaa vifurushiii barua na pesa vitu mbalimbali vifike harakaaa tena kwa uhakikaaa, itumie sasaa shirika la posta na simu tanzaaaaniaaa ndio tegemeo letuu.

2. Hebu jitokezeee jioneshe simamaa mbelee za watuuu

3. Tairi general kutoka arushaaa tanzaaaaniaaa

4. Revolaaa revolaaaaa revolaaaaaa revolaaaaaaaa

5. Wee acha kula mali ya umma wee acha kujitafuna tafuna weeeee, wachaaaaaaaaa

6. Tumia chibuku ndio pombe bora, radha ya chibuku hujulikana, sifa moja na nyinginezo ni kulinda hadhi ya mnywaji

7. Komoooooaaaaa aaa komooooaaaa komoaaaa

8. Benki ya akiba ya posta ndio yako, benki ya akiba ya posta ni kwa watanzaniaaa woooote wakubwa kwa wadogo... Wananchi unaweza kufungua akaunti ya kawaaida, akaunti ya muda na akaunti ya muda maaalum.. Usingoje kesho ooo fungua akaunti yako leooo

Watangazaji hahaha Mama Deborah, Dominic Chilambo
Nimejikuta napata sweet memories tu

Mkuu ongeza tangazo bima ....Bima yako,..kwa ajali..bima yako kwa majanga... na kulikuwa na promo ya mshikamanooo mshikamanoo...kumekuchaaa
 
Namkumbuka pia Edda Sanga wa kipindi cha mama na mwana pia alikuwa mmahiri sana wa kusoma habari pamoja na mtangazaji Mwafisi kwa habari walikuwa vizuri
....viashiria vyote kilikuwa kinanikonga kile cha Majira...na jingle ya uzazi wa mpango...wameiona nyota ya kijani ya uzazi wa mpango..zindukaa🙂
 
Mimi siyo wa zamani saana ila nakumbuka tuu haya machache:
-twende na wakati
-pilika pilika
-Michezo ba ezekiel marongo
-Mpira wachaa wee
 
Mazungumzo baada ya habari pamoja na maneno hayoooooo
Ivi yule jamaa wa mazungumzo baada ya habari na maneno hayo alikuwaga nani maana alikuwa na maneno kuntu sana yule jamaa! Yuko wapi na anajishughulisha na nini?
 
Pia kulikuwa na kipindi cha muziki wa mwambao. Taarab laini zina jumbe nzitinzito ndani yake ila wameweka mafumbo mpk unaumia kichwa siku hizi mambo hadharani
Pendoooo linauaa lasumbuaa walimwenguuu walimwenguuu walimwengu pendooo
 
Na katika kipindi cha majira hakuna aliemzidi Nsuma Ernest kusign out...alikuwa anavuta jina lake mimi ni Nsuuma Err... those were days aisee! 🙂
 
Back
Top Bottom