Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Wanabodi,
Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.

Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.

...............Huyu Mungu TUNAMSINGIZIAGA SANA. Nadhani muda mwingi huwa anacheka tu! We Paschal shukuru umeondoka pale bado mdogo. Ungemkuta alieanzisha haya maafa labda na wewe usingekuwepo leo. Mtoto wa kizaramo kaifyeka RTD si mchezo. Na hii mifano imo maofisi mengi ya serikali, mashirika ya umma na hata binafsi. Kitendo cha kuzungukana na kung'ang'ania mtu mmoja. Kinatekeza sana watu hapa Tanzania.
 
namkumbuka Ben Kiko (Benedict Kikoti) na kipindi chake cha mambo hayo kutoka kanda ya kati dodoma. bila kumsahau Abdallah Mlawa.

kwa ujumla RTD haikuwa na mchovu hata mmoja. Ndio maana watangazaji wengi wapo ktika radio za mashirika ya nje.

nikikumbuka watangazaji wa mpira akina:
1. Charles Hillary..... Namna gani pale
2. Dominic Chilambo
3. Omary Jongo
3. Ahmed Jongo .... Inakuwa Obstruction pale
4. Na wengineo
5. Wa sasa hovyoooooo...
 
We Pascal ina maana sie mafundi uwa hatukubukwi. Au unataka nife kwanza ndo mtatukumbuka. Umewasahau mafudi kama vile Domitla Urassa, Juma Bungara. Bundala, Mzee Juma Sereka, Konsalva Mwereke nk. Ndio hao waliokufanya usikike na upate umaarufu kwa kukuandalia lineup ya mziki na kurekebisha sauti yako wakati wako pale studio Red na Studio Blue. Bila hao ngoma za ZIPOMPAPOMBA husingetamba nazo wewe
 
Dah! nilikuwa nimemsahau huyu ndugu, aisee RTD ilikuwa kiboko. Uliyeuliza kuhusu malima ndelema, bado yuko hai, mara ya mwisho nilimsikia alikuwa anatangaza matangazo ya moja kwa moja kutoka mbeya, sikumbuki ilikuwa ni sherehe gani
Bujaga Izengo Kadago alikuwa bonge la mtu mwenyeji wa Tinde Shinyanga.
 
Kweli aise, mtangazaji alikuwa hawezi kuanza kipindi hadi amtambulishe fundi mitambo na anapomaliza kipindi lzm amshukuru.... wapi Lando Mabula
We Pascal ina maana sie
mafundi uwa hatukubukwi. Au unataka nife kwanza ndo mtatukumbuka.
Umewasahau mafudi kama vile Domitla Urassa, Juma Bungara. Bundala, Mzee
Juma Sereka, Konsalva Mwereke nk. Ndio hao waliokufanya usikike na upate
umaarufu kwa kukuandalia lineup ya mziki na kurekebisha sauti yako
wakati wako pale studio Red na Studio Blue. Bila hao ngoma za
ZIPOMPAPOMBA husingetamba nazo wewe
 
Ben Kiko, sijui yuko wapi huyu jamani
Alesia maneno na Alesia Isabula nadhani bado wapo TBC taifa
Watangazaji wa zamani walikuwa watangazaji kweli
Chezea Michael Katembo na Kipindi cha mkoa kwa mkoa
Nilikuwa nampenda Siwatu Luanda(RIP)nakumbuka alifariki nikiwa drs la tano miaka hiyo

ben kiko bado yu hai,na mwanae ni swaiba wangu sana,na ben kiko mwenyewe yupo tabora
 
Hii ni taarifa ya habari kutoka Redio Tanzania Dar Es Salaam msomaji Sango Kipozi. Kwanza habari kwa ufupi.
Rais wa jamhuri ya muugano wa Tanzania Mwalimu Julius Nyerere leo amemfukuza kazi Waziri wa Elimu kwa utendaji dhaifu katika wizara hiyo uliosababisha matokeo mabaya sana kwa Wanafunzi waliomaliza kidatu cha nne mwaka jana.
 
Wanabodi,

Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.

Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.

Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na

  1. David Wakati
  2. Abdul Masudi (Jawewa)
  3. Eli Mbotto
  4. Stephen Mlatie
  5. Siwatu Luanda
  6. Salama Mfamao
  7. Salim Seif Nkamba (Mjomba)
  8. Michael Katembo
  9. Nelly Kidella
  10. Halima Mchuka,
  11. Omar Jongo
  12. Tumboi Tamimu Risasi
  13. Mohamed Mombo
  14. Abisai Stephen (Uronu)
  15. Stephen Lymo.
  16. Nadhir Mayoka
  17. Juma Ngodae
  18. Rukia Machumu
  19. Karim Besta
  20. Henrick Michael Libuda
  21. Idrissa Sadalah
  22. Bati Kombwa

Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Pia sio vibaya kuwaulizia wale watangazaji wa siku nyingi ambao hatujui walipo, ili kama nao wametangulia tuyaingize majina yao.

RIP All the Fallen Heroes wa Tasnia ya Utangazaji Tanzania!,

Pascal.
NAMJUA ABDU MASUDI na David wakati TUU KWA SURA LAKINI WENGINE SIWAJUI HATA MMOJA KWA SURA hata nikikutana nao new York au Tel Aviv. halafu miaka ya mwanzononi ya 70's, kulikuwa na kipindi cha mbiu za mikoa na mazungumzo baada ya habari. Vipindi hivi vilijaa maneno ya kudanganya umma kuliko kitu chochote duniani. Vilijaa matusi kwa mabepari na uongo wa maendeleo vijijini. Utasikia wakulima wa pamba geita wamepata bilion nane za mauzo ya pamba! au wakulima wa miwato kwimba wamepata milion arobaini ! au wakulima wa pareto njombe wamepata bilion tisini! ukigawana pesa hizo kwa idadi ya kila mmoja utakuta kila mkulima kapata shilingi alfu nane tuu!

nakumbuka mazungumzo baada ya habari yaliyokuwa yanasema,: "weweee, mitaji haramu ya kujijengea mali umeipata wapi weweeee!" au yale ya " baba baba, unafanya nini hapo ulipo"

hawa watangazaji wa iliyokuwa RTD nawapa hongera ya kupotosha umma kuliko kuelimisha watu! Ujamaa ulikuwa ni sumu kwa umma kuliko hata ukimwi!
 
Hapa mimi nimewatambua Charles Hilali na Na maskini marehemu Nyaisanga R.I.P
Kaka Pascal Mayalla naomba ututambulishe wengine kupitia picha hizi:

Watangazaji-wa-Zamani-RTD.jpg
 
Back
Top Bottom