Tujuzane maneno sahihi ya Kiswahili...

Tujuzane maneno sahihi ya Kiswahili...

Hivi decoder ni king'amuzi au kisimbuzi, zamani nilikuwa nasikia vinaitwa ving'amuzi, ila siku hizi neno linalotumika sana ni visimbuzi au yote sawa

Na password ni nywila, au nenofiche, au vyote kwa pamoja

Halafu kuna neno huwa nalisikia sana kwa hawa watangazaji wa soka, utasikia "anaubabatiza mpira", huku nako ndio kufanyeje tena
 
Hivi decoder ni king'amuzi au kisimbuzi, zamani nilikuwa nasikia vinaitwa ving'amuzi, ila siku hizi neno linalotumika sana ni visimbuzi au yote sawa

Na password ni nywila, au nenofiche, au vyote kwa pamoja

Halafu kuna neno huwa nalisikia sana kwa hawa watangazaji wa soka, utasikia "anaubabatiza mpira", huku nako ndio kufanyeje tena
Kuna maneno ambayo yanatumika kama msamiati mfano hilo neno nywila nadhani ni msamiati wenye maana ya nenofiche (Kwa uelewa wangu-Wataalamu wa lugha watatusaidia zaidi)

Kubabatiza mpira ama kitu chochote ni kutokupiga/Kutokushika ama kutokufanya kitendo kwa usahihi wake
 
Hivi decoder ni king'amuzi au kisimbuzi, zamani nilikuwa nasikia vinaitwa ving'amuzi, ila siku hizi neno linalotumika sana ni visimbuzi au yote sawa

Na password ni nywila, au nenofiche, au vyote kwa pamoja

Halafu kuna neno huwa nalisikia sana kwa hawa watangazaji wa soka, utasikia "anaubabatiza mpira", huku nako ndio kufanyeje tena
King'amuzi na kisimbuzi maneno haya namimi hunichanganya sana
 
Hivi decoder ni king'amuzi au kisimbuzi, zamani nilikuwa nasikia vinaitwa ving'amuzi, ila siku hizi neno linalotumika sana ni visimbuzi au yote sawa

Na password ni nywila, au nenofiche, au vyote kwa pamoja

Halafu kuna neno huwa nalisikia sana kwa hawa watangazaji wa soka, utasikia "anaubabatiza mpira", huku nako ndio kufanyeje tena
decoder ni kisimbuzi kwa maana kinasimbua mawimbi yani kinatafsiri king'amuzi ni kitu kinachong'amua hii maana yake yake kitu chenye ufahamu ndio hung'amua.. huo ni uelewa wangu.

kubabatiza ni kupigisha kwa makusudi yani mpira naupigisha kwenye mwili wako ili ihesabike aidha umeutoa au kwa chochote ambacho itakuwa nimeamua kitafsirike...
 
Afisi
Ofisi
Kipi ni kipi hapo?
Hiyo Afisi nimeona inatumika sana visiwani huku bara tunasema Ofisi, lakini wakati huo huo Officer tunamuita Afisa, kwahiyo hapo yawezekana wa visiwani wakawa sahihi
 
Mimi huwa naandika kiswahili sahii ila sio cha ndani ndani. Mpaka leo kuna vitu vinanitatiza.

Hivi ni kuloga au kuroga?

Anzeni hapa kwanza
 
Sema wazanzibari wana kiswahili cha tofauti kidogo ukikaa kule unaweza hisi huku bara hatuongei kiswahili, halafu baadhi ya maneno ya kule ni yale ambayo kwa huku kwetu tunayachukulia kama matusi, kwahiyo kama akili yako mbovu wakiongea unaweza jikuta unacheka mwanzo mwisho na unaweza hisi wanafanya makusudi
 
Sema wazanzibari wana kiswahili cha tofauti kidogo ukikaa kule unaweza hisi huku bara hatuongei kiswahili, halafu baadhi ya maneno ya kule ni yale ambayo kwa huku kwetu tunayachukulia kama matusi, kwahiyo kama akili yako mbovu wakiongea unaweza jikuta unacheka mwanzo mwisho na unaweza hisi wanafanya makusudi
Hiyo ni kawaida sana katika lugha ambazo huzungumzwa na watu wengi waliotawanyika kwenye eneo kubwa kimakazi.

Hiyo hali inaitwa lahaja.

Hata Kiswahili cha Mombasa kina tofauti na Kiswahili cha Nairobi na sehemu zingine za Kenya.

Hata Kisukuma nacho kina lahaja zake.

Kinyantuzu [Kisukuma cha Bariadi/ Simiyu] kina utofauti na Kisukuma cha Mwanza na Shinyanga. Hata Kisukuma cha Shinyanga kina tofauti zake na Kisukuma cha Mwanza.

Ila vyote ni Visukuma!

Kiingereza nacho ni hivyo hivyo.

Kiingereza cha Uingereza kina tofauti zake na Viingereza vya Marekani, Kanada, Australia, na New Zealand.

Pia, hata Marekani kwenyewe kuna lahaja tofauti tofauti za Kiingereza chao.

Wazawa wa kusini mwa Marekani wana lahaja zao zilizo tofauti na za wazawa wa sehemu zingine za Marekani.

Tofauti hizo za lahaja huwa zipo kwenye tahajia, lafudhi, matamshi, na misamiati.

Zanzibar ‘biringanya’ huitwa ‘biringani’.

Kama hujui na kama mtu unayezungumza naye hajui, nyote mnaweza kudhani ‘yeye’ ndo anakosea, kumbe wote mko sawa ila hamjui tu uwepo wa hizo tofauti ndogo ndogo zilizopo chini na ndani ya lahaja.
 
Mimi huwa naandika kiswahili sahii ila sio cha ndani ndani. Mpaka leo kuna vitu vinanitatiza.

Hivi ni kuloga au kuroga?

Anzeni hapa kwanza
matumizi ya r na l tabu hata kwangu!
shida ya lugha muda mwengine haianaga kwanini!!
 
matumizi ya r na l tabu hata kwangu!
shida ya lugha muda mwengine haianaga kwanini!!
Binafsi sina tatizo la R na L ila naona hili neno watu wanachanganya sana. Kuna watu wanatamka "KUROGA" na inaonekana sawa tu... Neno sahii ni KULOGA lakini kuna watu ukisema hivyo wanasema umekosea.

Mlogaji ni Mlozi na sio MROZI.
 
Hiyo ni kawaida sana katika lugha ambazo huzungumzwa na watu wengi waliotawanyika kwenye eneo kubwa kimakazi.

Hiyo hali inaitwa lahaja.

Hata Kiswahili cha Mombasa kina tofauti na Kiswahili cha Nairobi na sehemu zingine za Kenya.

Hata Kisukuma nacho kina lahaja zake.

Kinyantuzu [Kisukuma cha Bariadi/ Simiyu] kina utofauti na Kisukuma cha Mwanza na Shinyanga. Hata Kisukuma cha Shinyanga kina tofauti zake na Kisukuma cha Mwanza.

Ila vyote ni Visukuma!

Kiingereza nacho ni hivyo hivyo.

Kiingereza cha Uingereza kina tofauti zake na Viingereza vya Marekani, Kanada, Australia, na New Zealand.

Pia, hata Marekani kwenyewe kuna lahaja tofauti tofauti za Kiingereza chao.

Wazawa wa kusini mwa Marekani wana lahaja zao zilizo tofauti na za wazawa wa sehemu zingine za Marekani.

Tofauti hizo za lahaja huwa zipo kwenye tahajia, lafudhi, matamshi, na misamiati.

Zanzibar ‘biringanya’ huitwa ‘biringani’.

Kama hujui na kama mtu unayezungumza naye hajui, nyote mnaweza kudhani ‘yeye’ ndo anakosea, kumbe wote mko sawa ila hamjui tu uwepo wa hizo tofauti ndogo ndogo zilizopo chini na ndani ya lahaja.
Yeah kuhusu lugha moja kuwa na tofauti kama hizo duniani nafahamu mkuu ila bila shaka wewe unasemea utofauti wa jambo moja kuwa na maneno zaidi ya moja katika lugha moja, mimi nasemea utofauti wa neno moja kuwa na maana zaidi ya moja tofauti katika lugha moja yani kuna maneno unakuta kule lina maana nyingine na huku lina maana nyingine, mfano kule kwao shamba ni kijijini ila huku kwetu shamba ni eneo zinakofanywa shughuli za kilimo au kule kwao tobo ni geti ila huku kwetu tobo ni uwazi kwenye kitu kilichoziba unaomfanya mtu aweze kuona ndani au upande wa pili
 
Mada hii itakuwa ni mada maalum ya kujulishana usahihi wa maneno yakiswahili,sanasana uandishi wa maneno hayo au maana n.k

Yapo maneno yanayotutatiza ama katika uandishi au matumizi yake,hapa pawe uwanja wakuchambua,kurekebisha nakuelimishana juu ya maneno hayo.
Nikianza namimi binafsi maneno haya yamekuwa yakinitatanisha...

1. Muziki au Mziki Kati ya hayo mawili lipi ni neno sahihi..??
itakuwa vyema jibu likitoka na sababu.

2. husda au husuda...??

orodha itaendelea kadri mjadala utakavyokuwa ukiendelea,lakini pia ningependa kugusia kitu hichi kidogo ni kutofurahishwa na baadhi ya maneno mapya ambayo yamekuwa yakitengenezwa ili kupanua lugha yetu!. Maneno hayo ni akili mnemba (artificial intelligence) na pia ndege nyuki yani (drone).
hili la ndege nyuki badala yakukaa kama jina limekaa kama sentensi!,ningeshauri kutunga majina badala ya kuunga sentensi!.
akili mnemba pendekezo langu ingeitwa akili sanifu!.

karibuni kwa mjadala.
'tujuzane' ni Kiswahili sahihi? Vipi 'tujulishane'?
 
Back
Top Bottom