Tukiachilia mbali umasikini /ufukara wa wazazi wetu ilishawahi kujiuliza unakwama wapi?

Tukiachilia mbali umasikini /ufukara wa wazazi wetu ilishawahi kujiuliza unakwama wapi?

Mhafidhina07

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2014
Posts
3,340
Reaction score
4,659
Umasikini si ukilema ila ni hali ya kukosa mambo muhimu ambayo mtu unayahitaji katika maisha yako ya kila siku ,japo wapo watu wanajaribu kusema masikini ni kilema ila anaekosa hayo mambo muhimu anaitwa fukara,siwezi kubisha ila mtazamo wangu umependa kuamini nivyoamini.

Nimeona kwa asilimia kubwa watu wengi tukilalamikia umasikini wetu ambao umerithishwa kutoka kwa mababu na mabibi zetu kufika mpaka kwa watoto zao na bado wajukuu umeendelea kutushika,zipo nadharia ambazo zinasema umasikini ni circle hua na kawaida ya kujirudia(kuzunguka),wengine husema umasikini ni uvivu,matumizi mabaya ya rasilimali mfano watu wa pwani kwao muhimu sherehe kuliko kula yao na maendeleo yao na mwisho kabisa serikali ndiye anayebeba lawama ya wananchi wake.

Najua tupo wengi katika daraja umasikini la katikati hivi unazani tatizo lipo wapi,huenda kuna tabia zinatusumbua na ukizitaja tunaweza kujiokoa nazo.

Shukrani.
 
Wengi tunasumbuliwa na tatizo ambalo hata umasikini wa nchi yetu unatokana na tatizo hilo.
1. Uvivu (uvivu wa fikra na vitendo)
2. Kukosa malengo/dira ya maisha (vision).
3. Uhujumu uchumi (watanzania wengi ni design ya ponda mali kufa kwaja)
4. Majungu
5. Ujuaji mwingi
 
Malengo kila mtu anayo ila miezi hyo namba moja nahisi wengi tunalo.
 
Back
Top Bottom