think tank01
JF-Expert Member
- Aug 11, 2022
- 270
- 400
Haki hii ni movie
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Here I am.Tivuuu njoo basi
Kama umenifuatilia vema, mimi huwa naandika filamu sio riwaya.Haki hii ni movie
Niko hapa, mama.Tivu uko wapi eti
Kama kuna watu watano walio active muda huu basi nitapost.Tivu endelea jamaniii
Alikukosea nini? [emoji1][emoji1]Steve njoo tuendelee Bora huyu Dr afe tu sijui kwann sikumpenda kuanzia mwanzo
Tuendelee tuone yajayo.Dr Jean kaingilia mishe za watu kibabe sana! ni halali adedishwe chap otherwise mtchell aingilie kati...!
Teh! sikuzote mkuu SteveMollel mahudhurio ya Shunie kwenye simulizi zako huja na mibaraka tele kwetu sisi wafuatiliaji...!!Nawapatia bonus ... Kwa udhamini wa Shunie
Hatari [emoji91]TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 30
Na Steve B.S.M
Hilda alitazama nyuma yake, hakukuwa na mtu, alikuwa mpweke katika eneo hili, zaidi ni magari kadha wa kadha yaliyokuwa yemejiegesha kwa mstari mnyoofu, basi akafungua mlango na kuingia ndani ya jengo hili la ghorofa, alikuwa yupo hoi, macho yake ndani ya miwani yalikuwa yamelegea, mwili mchovu na mzito.
Alipandisha ngazi kivivu, akikanyaga kila hatua, mkono wake wa kuume ulikuwa umeshililia kingo ya ngazi hizo akijivuta kana kwamba mzigo.
Akiwa anapandisha ngazi hizo, alilaani kwanini jengo hili halina lifti, alitupa tuhuma zake ingali hakuna aliyemsi
Alipoingia sebuleni, akajitupa kwenye kochi na kushusha pumzi ndefu, pumzi ya uchovu, kisha akatulia hapo tuli kana kwamba anasinzia, muda kidogo simu yake ikaita kwa kunguruma, simu iliita kwa kama dakika moja ndipo akahisi jambo kwani alikuwa yu hoi sana, akaipokea na kuiweka sikioni akiwa amejilaza hapo kwenye kochi.
"Nimefika muda si mrefu ... ndio, niko salama kabisa." Simu ikakata, hakuitoa sikioni yeye akaendelea na usingizi wake hapohapo kochini muda si mrefu akawa amepitiwa na usingizi kabisa kiasi cha kukoroma. Aliuachama mdomo wake wazi akiwa yupo katika ulimwengu mwingine mbali na huu tunaoujua.
Baada ya dakika kadhaa, akiwa amelala hapahapa kochini, mlango ukateguliwa kitasa, hakusikia kitu, kitasa kikaguswa tena kama mara tatu hivi, mlango haukufunguka na Hilda hakugutuka kitu, alikuwa amezama kwenye usingizi mzito shauri ya pombe alizotoka kunywa huko kilabuni pamoja na Richie.
Baada ya majiribio hayo manne ya kufungua mlango kukawa kimya kidogo, ukimya wa sekunde kadhaa kisha ghafla kitasa kikaanza kutoa sauti ya kuchokonolewa na kitu mithili ya waya wa chuma hivi, kidogo tu, kitasa kikafunguka.
Aliyekuwa anachokonoa, akasogeza mlango taratibu, nao mlango ukaitikia amri yake, akatanguliza mguu wake wa kulia ndani, ulikuwa mguu mkubwa wenye kuvalia buti kubwa jeusi, kidogo akauingiza na mguu wake wa pili kisha akaufunga mlango, sasa mwili wake mzima ukawa ndani.
Kwa sekunde tano wana huyo aliyeingia ndani akatulia hapo, alikuwa anayasoma mazingira, kisha akanyanyua mguu wake kuzama ndani zaidi, alimpita Hilda akaenda zake chumbani.
Baada ya muda usiofahamika, Hilda akasikia kitu cha kumshtua, akafungua macho yake. Hakujua ni nini kimemwamsha ila usingizi wake mzito ulikata ghafla, akaangaza huku na kule.
Kuligeuka kuwa patulivu ajabu, hata huko nje hakukuwa na mtu anayekatiza ama kuongea koridoni.
Kidogo akasikia kitu tena, sauti mithili ya mtu anayetembea chumbani, moyo wake ukashtuka na kupasua, alidhani yupo peke yake humu ndani lakini sauti hiyo ikaanza kumfanya ahisi tofauti, pengine kuna mtu mwingine hapa.
Akanyanyuka, akapepesuka, mwili ulikuwa mzito anashindwa kuumudu. Alijitahidi kujikaza mpaka akasimama wima kisha akaelekea chumbani akijivuta.
Aliukuta mlango upo wazi, akausogeza na kuingia, akarusha macho yake huku na kule, hakuona kitu, hakukuwa na mtu wala chochote cha kumtia hofu, akaguna kwa kujishangaa.
"Hizi pombe hizi!" Alisema akitikisa kichwa chake na kuongezea, "kweli nimelewa."
Alikisogelea kitanda chake, akajitupia hapo kama mzigo wa tani mbili, muda si punde akawa anakoroma kama trekta bovu la shamba, hakufahamu chochote kinachoendelea kwani usingizi ulimmeza mzimamzima asibaki hata punje.
Lakini dirisha la mashariki mwa chumba hiki lilikuwa wazi kama vile mlango ulivyokuwa, Hilda hakulitambua hilo, kidogo tu moja ya gari lililokuwepo katika msururu ule wa magari yaliyojiegesha pale nje likatema moshi kwenye bomba lake kuashiria kuwaka kwa injini, punde gari hilo likanguruma na kupotea katika mazingira hayo.
Baada ya hapo mambo yakarudi katika kawaida yake.
***
"Nimewasiliana naye, na kama nilivyokuambia pesa ipo!" Jamal alisema kwa sauti yenye mkazo, macho yake yalikuwa yanamtazama kijana mweusi aliyeketi kwenye kiti, kwa jina Huncho.
Mwanaume huyo mwenye rasta alikuwa amevalia koti kubwa rangi ya manjano na suruali nyembamba rangi ya bluu liyobana miguu yake kisawasawa, chini amevalia raba kubwa rangi nyeupe.
Jamal yeye alikuwa amevalia kaushi nyeupe na pensi nyeusi ya michezo ya kikapu, chini yuko peku nyayo zake zikisabahi sakafu. Hapa walipo ni ndani ya sebule ndogo, pembeni ya meza yenye tarakilishi juu yake, tarakilishi hiyo ilikuwa 'on'.
"Jamal," Huncho akaita na kusema, "ndani ya mwezi huu nataka pesa yangu iwe imekamilika, sawa? Kama kukuvumilia nishavumilia vyakutosha, nadhani ni muda sasa wa kumalizana."
Aliposema hayo akasimama toka kisha akamsogelea Jamal kwa ukaribu usoni, akamwambia hatovumilia tena zaidi ya mwezi huo, kama fadhila ashazifanya kwa kumsaidia kumlipia ada ya chuo kwa semista kadhaa, sasa ni matanga ya kurejesha deni.
"Lakini Huncho, unajua kabisa lengo langu ni nini, sijadhamiria kukwepa deni lako, najua ulinisaidia kipindi cha shida lakini hiyo pesa kwa muda huo ulionipatia sitaweza kuipata, tazama sasa nishabakiwa na majuma mawili tu katika mwezi, majuma hayo nitafanya nini?" Jamal alilalamika, lakini hayo yote hayakuwa na maana kwenye masikio ya Huncho, yeye alichotaka ni pesa yake tu.
Alirudia kauli yake kisha akaenda zake akimwacha Jamal na maswali mengi asiyojua namna ya kuyatatua.
Jamal, mwanafunzi wa mwaka wa nne sasa chuoni akisomea Genomics, ni mwanaume ambaye amezoea kukumbana na changamoto katika maisha yake ya taaluma tangu 'High School' baada ya kuwapoteza wazazi wake wawili kwa ajali mbaya ya ndege, tangu hapo, haswa baada ya kukosa haki kamili za baba yake, amekuwa akitangatanga na kushika hili na lile ili kupata elimu anayoiwazia, elimu anayoitamani tangu enzi na enzi, elimu ya vinasaba, almaarufu The Genomics.
Kwasababu kozi hiyo ni gharama kubwa, amekuwa akihangaika kupata ufadhili kumudu gharama zote, na kwasababu hiyo ilikuwa inampasa kutafuta kazi za hapa na pale kwaajili ya kufidia ada yake lakini pia kumudu maisha ya kila siku, lakini kama ilivyokuwa kwa ndege kuwa sio kila atakapowahi kuamka basi atapata wadudu ndivyo ikawa kwa Jamal pia, si kila mara alipata kazi za kumpatia pesa za kujikidhi hivyo kumpasa akope ili ajisogeze, na mmoja wa watu aliowakopa kiasi kingi cha pesa ni Huncho.
Huncho hakuwa mtu wa kukaukiwa na pesa abadani, biashara yake haramu anayoifanya katika mazingira ya chuo imemfanya kuwa na pesa chafu, pesa za haramu, angeweza kukupatia pesa yoyote unayoihitaji alimradi akuamini, lakini shida huja pale wanaomkopa wanapogeuka kuwa wakaidi, hapo bwana huyu hasiti kutumia njia zake kwenye kukusanya madeni yake, mara nyingi akifanya hivyo huku akiacha mikono yake kuwa safi.
Jamal alikuwa analifahamu hili, yeye si wa kwanza kupewa pesa na bila shaka hatokuwa wa mwisho, anatambua fika ni kadhia gani itamkumba endapo hatopata pesa ya kumlipa bwana huyu na hakutaka kabisa jambo hilo, lakino ataipatia wapi pesa ndani ya muda huo mfupi?
Aliketi akatazama tarakilishi yake, macho yake yakagotea kwenye kazi alokuwa anaifanya, kazi alopewa na bwana Richie pamoja na Hilda, kazi hiyo ilikuwa imebakia nusu kwisha, akimaliza atapata pesa, lakini pesa hiyo atakula kiasi gani, alipie ada kiasi gani? Ni wazi haikuwa inatosha kabisa, pesa ilishaisha kabla hajaishika mkononi.
Akashika kichwa chake akitafakari, lazima apate njia, alisema na nafsi yake, na alipofikiria zaidi akaishia kwenye kazi hii, hakukuwa na mlango wowote wa pesa isipokuwa kazi hii, lakini ataipataje?
Baada ya shauri fulani, akanyanyua simu yake na kupiga. Simu ikaita na kidogo ikapokelewa, akasema,
"Hello, Richie!" Kisha akaongezea, "Naomba tuonane ndugu yangu .... Hata kesho sawa ... Hautapata nafasi siku nzima? ... Ndio, ndugu yangu nina shida sana ... Ni pesa lakini tutafanya makubaliano .... Sio hivyo, ndugu yangu ni ..."
Simu ikakata, akaitazama kama vile haamini kuwa imekatwa, akasema 'hello' mara mbili lakink hakukuwa na kitu, simu ilikatwa, akajaribu kupiga mwenyewe lakini haikuita wala haikusema kitu, zaidi ilipiga beep-beep na kukata yenyewe, hapa bwana huyu akaamini huenda amepigwa kufuli.
Kichwa kikamuwaka moto, sasa akawaza wazo ambalo hakutaka kuliwaza, maamuzi ambayo hakutaka kuyafikia, na akaweka nadhiri endapo njia zingine zikifeli basi hatokuwa na namna isipokuwa kuenenda na hii.
Hii njia ya hatari.
Sasa afanyaje?
***
Maabara, Brookhaven, New York.
Yalikuwa ni majira ya jioni, watu wanatoka kwenye shughuli zao kwaajili ya kwenda majumbani kwa mapumziko, miongoni mwao alikuwa ni Dr. Jean, alikuwa anashuka ngazi akitazama saa yake ndogo ya mkononi. Si kwamba lifti haikuwapo katika jengo hili, la hasha, alipendelea tu kutumia ngazi kwaajili ya mazoezi binafsi.
Basi akiwa anashuka, mara simu yake ikaita, aliitoa mfukoni na kuitazama, namba ngeni, akapokea na kuiweka sikioni.
"Ndio ... Nimeshakamilisha zote, ndio ... Sawa, saa nne usiku."
Simu ikakata, akaiweka mfukoni na kunyookea gari yake, gari mithili ya Ford Ranger rangi yake nyeusi, gari alokuwa anasema ipo kwa fundi ikipata matengenezo sasa ilikuwa isharudi barabarani, akaingia humo na kukanyaga mafuta.
Aliendesha akiwa anaskiza muziki taratibu na huku kichwani kwake akiwa anayapanga mambo makubwa makubwa, mambo ya pesa ndefu, akajikuta anatabasamutabasamu mwenyewe, muda mwingine bila hata ya sababu.
Alipofika kwenye foleni akapata wasaa mdogo, basi akatoa simu yake mfukoni mwake na kutazama akaunti yake ya benki, hakika ilikuwa inapendeza, 'six digits' zilikuwa zinasoma, basi akajiongelesha mwenyewe,
"Mazuri bado yanakuja."
Kisha akatabasamu tena, kidogo mataa yakaruhusu lakini hakuwa na ufahamu, akapigiwa honi lukuki zilizomshtua na kumrejesha kwenye usukani wake, akatimua chombo.
Alipofika nyumbani, hakupoteza muda bali akaanza kujiandaa kwaajili ya miadi yake ya saa nne za usiku, maandalizi haya hayakuwa ya nguo, lah, bali ya mzigo wa kwenda kuukabidhi.
Alichukua lisaa limoja kujiweka sawa kwa kila kitu ndipo sasa akatulia apate kuoga na kuangalia mengine kwani alibakiwa na lisaa limoja mkononi, lakini muda haugandi, si punde muda wa miadi ukafika, ni kama vile muda ulirushwana rimoti, bwana huyu akajiandaa na kuingia ndani ya gari lake kisha akaanza safari akielekea kaskazini.
Alipotembea kwa muda mchache, simu ikaita, kutazama ilikuwa ni namba ngeni lakini alikumbuka ndo' namba ileile aliyoongea nayo hapo kabla, basi akapokea upesi.
"Ndio nipo njiani .... Kama dakika sita tu n'takuwa hapo."
Akairejesha simu mfukoni na safari ikaendelea, kweli baada ya dakika chache akawa amewasili eneo aliloitwa, akatoa simu mfukoni na kupiga.
"Tayari n'shafika."
Alipotoa taarifa hiyo akakaa hapo akitulia, kidogo tu, kama baada ya dakika mbili hivi, akasikia kioo cha dirisha kinagongwa ngo ngo ngo, kabla hajafungua akatabasamu.
Hakujua kuwa hilo ndo' lilikuwa tabasamu lake la mwisho hapa duniani.
****
****
Hahaha huyu dada anajua kuomba sana alafu anatia huruma.Teh! sikuzote mkuu SteveMollel mahudhurio ya Shunie kwenye simulizi zako huja na mibaraka tele kwetu sisi wafuatiliaji...!!