SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
- #101
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 17
Na Steve B.S.M
Brookhaven, New York.
Saa nne asubuhi
Bwana Lambert aliingia ndani ya ofisi akiwa analegeza tai shingoni.
Mkononi alikuwa ameshikilia mkoba mweusi wa ngozi.
Mkoba huo ulikuwa na kifungo cha chuma.
Aliushikilia mkoba huo vema, upo kifuani kwake ameukumbatia na mkono wake wa kuume.
Alipoingia tu ndani akaurejeshea mlango upesi na kwenda moja kwa moja kwenye kiti chake.
Akaketi na kuuweka mkoba wake ndani ya droo ya meza yake.
Kisha akatulia akiskizia.
Moyo wake ulikuwa unapiga kwa kasi.
Aliukua anausikia kabisa kwenye masikio yake makubwa.
Na pumzi yake haikuwa ya kawaida.
Alikuwa anahema kwa kasi japo si kwanguvu.
Alitulia hapo akifikiria.
Akifiria namna alivyotenda mpaka kufika hapo.
Alikumbuka nyendo zake zote alizopitia mpaka kufikia hapo alipoketi.
Akaona kila kitu kipo sawa.
Akashusha pumzi fupi kisha akatua koti lake sasa.
Koti kubwa jeupe
Akalipachika kwenye kiti kisha akawasha tarakilishi yake kwaajili ya kuandika baadhi ya taarifa ambazo zilipaswa kunakiliwa kwenye mafaili.
Akiwa anafanya hivyo, mara mlango ukafunguliwa.
Akarusha macho yake kutazama.
Mlangoni akawaona wanaume wawili waliovalia sare rangi ya bluu iliyokoza
Wamefunika vichwa vyao na kofia aina ya bareti zenye chapa ya ulinzi.
Wanaume hao, mmoja mweupe na mwingine mweusi, walikuwa wamebebelea bunduki mikononi mwao.
Bunduki kubwa mithili ya majangili wanaolenga kuangusha tembo nyikani.
Nyuso zao hazikuwa rafiki.
Macho yao makali yalimtazama Dr. Lambert kana kwamba mwalifu aliyetoka kufanya mauaji.
Naye Dr. Lambert akawatazama kwa kustaajabu.
Aliwatazama kwa macho yasiyoelewa chochote kinachoendelea hapa.
Aliwafahamu mabwana hawa kama wafanyakazi wa ulinzi wa kampuni mpya iliyopata tenda ya kuimarisha ulinzi eneo hili la maabara ya taifa.
Lakini pia aliwafahamu kama wana-ulinzi wa gredi ya pili, juu yao wakiwepo wanausalama.
Mabwana wale wanaovalia suti nyeusi.
Lakini kwanini hawa wako hapa wakiwa wamebebelea silaha?
Alikuwa anaenda kulijua hilo muda si mrefu.
Bwana mmoja kati ya hao walinzi wawili, yule mwanaume mweusi, akamfuata wakati mwingine akiwa amebakia pale mlangoni.
Akamwambia dokta,
"Tunataka kuona ulichokichukua kule maabara."
Dokta akastaajabu.
Alisema,
"Nini hiko? Sijachukua chochote mimi."
Bwana huyo mlinzi akamtazama kwa macho ya kina kirefu cha maji.
Hakuwa na masikhara.
Alitulia kwa kama sekunde tatu akimtazama dokta pasipo kutia neno.
Uso wake uliongea kila kitu.
Dokta akajifaragua akijitetea,
"Sijabeba kitu mimi. Naamini mtakuwa mmekosea au mmenifananisha."
Bwana yule mlinzi, akanyanyua silaha yake na kumwonyeshea.
Dokta akaogopa sana.
Kuona mdomo wa bunduki ukitazama uso wake kulimfanya atetemeke kwa hofu.
Bwana yule akasema,
"Sitarudia tena. Weka mezani kile ulichokichukua maabara."
Kisha akapayuka,
"Upesi!"
Dokta akaruka kwa woga.
Haraka, kwa mikono yake inayotetemeka, akafungua droo na kutoa mkoba mweusi.
Akauweka mezani.
Ulikuwa ni mkoba mweusi wa ngozi wenye kifundo cha chuma.
Punde tu alipouweka mezani, akanyoosha mikono yake juu na kusema huo ndo' mzigo wake alotoka nao maabara.
Wakati huo wenzake wawili walikuwa wameshafika katika eneo la tukio.
Walisimama kule mlangoni wakitazama kwa kurusha macho yao ndani wapate kuona yanayoendelea humo.
Walizuiliwa kuingia ndani na yule mlinzi aloiyesimama hapo.
Mmoja wao alikuwa ni yule bwana mfupi kuliko wote, na mwingine ni yule kijana mwenye umri mdogo kuliko wote humu ofisini.
Mlinzi yule aliyesimama mkabala na dokta, akauchukua huo mkoba mweusi na kuufungua.
Akaupekua.
Kwa kama sekunde kumi hivi alifanya zoezi lake kisha akaurejesha mkoba huo mezani.
Akamtazama mwenzie aliyekuwepo mlangoni na kumpa ishara ya kutikisa kichwa.
Hamna alichopata.
Kumbe ndani ya mkoba kulikuwa na kiasi kidogo cha chakula kwenye kontena na matunda mawili, ndizi mbivu.
Dokta akauliza,
"Ni nini mmeona humo cha ajabu?"
Mabwana wale hawakujibu. Hapa akapata nguvu zaidi ya kuongea.
Aliunyakua mkoba wake akiwatuhumu walinzi wale kwa kuenenda kama wanyama wasiokuwa na akili.
Alisema ya kwamba yeye hubeba chakula chake hata anapokuwa akifanya kazi maabara kwasababu ya matatizo yake ya vidonda vya tumbo.
Hawezi kungoja mpaka muda wa chakula cha mchana ufike.
Anapaswa kufanya hivyo kwani hapa karibuni hali yake ilikuwa mbaya zaidi kiasi cha kutapika damu.
Aliposema hayo, walinzi wakamwomba radhi wakisema walikuwa katika majukumu yao.
Kisha wakaondoka zao na hali ya hapa ikapoa.
Mabwana wale wawili, wenza na dokta, wakaingia na kumpa pole mwenzao huku wakiwarushia tuhuma wanaulinzi hao kwa kutokuwa makini na kusababisha taharuki kali.
Bwana yule kijana alisema,
"Sasa kazi yetu imekuwa kama gereza. Bunduki na risasi zimegeuka kuwa sehemu ya maabara."
Baada ya muda kidogo, hali ikarudi kuwa shwari na shughuli zingine zikaendelea kama kawaida.
Dokta Lambert, akiwa amehakikisha kuwa kila mtu hapa anashughulika na yake, akafungua droo ya pili ya meza yake.
Macho yake yalikuwa na wangalifu mkubwa.
Alifungua droo hiyo kwa utaratibu mno kiasi kwamba hakutengeneza sauti yoyote.
Kisha akaitazama kwa kuibia.
Mkoba wake ulikuwa umekaa kwa kutulia.
Mkoba mweusi wenye fundo la chuma.
Mkoba huu ulikuwa ni wa pili wakati wa kwanza ukiwa kwenye ile droo ya kwanza ya meza..
Droo ambayo aliutoa mkoba ule aliowapatia walinzi kwaajili ya kuukagua.
Akatabasamu kwa mbali.
Mchezo wake ulienda vile alivyokuwa anatarajia.
Mikoba miwili inayofanana kwa kila kitu ilitosha kabisa kumvusha mto yordani.
Akahisi moyo wake umekuwa wa baridi na adhma yake inaenda kutimia.
Akatabasamu tena.
Baadae jioni, majira ya saa kumi, akiwa ameshamaliza kila jambo hapa kazini akaliendea gari lake akiwa na mkoba wake mkononi.
Alilenga kwenda nyumbani moja kwa moja.
Akauweka mkoba wake mahali salama ndani ya gari kisha akatekenya funguo kuwasha chombo.
Kabla hajaondoka, akasikia ngo-ngo-ngo.
Kuna mtu aligonga kioo cha dirisha la upande wake wa kulia.
Moyo ukamlipuka mithili ya guruneti.
Alishtuka kwa hofu kubwa aliyojitahidi kuizuia isionakane lakini uso wake ukafeli.
Macho yake yalijawa na woga.
Alitazama upesi akamwona mwanaume, kwa nje, akiwa anampungia kwa furaha.
Alikuwa ni bwana yule mfupi anayefanya naye kazi katika ofisi moja.
Bwana huyo alikuwa anatabasamu kwa upana akipeperusha kiganja chake.
Akashusha kioo apate kumsikia.
Bwana yule akasema,
"Samahani sana, bwana. Nadhani unaelekea nyumbani. Unaweza ukaniacha hapo mbele kidogo?"
Bwana huyo alitaja mahali aelekeapo lakini Dr. Lambert akamruka kiunzi.
Alimwambia hapiti huko.
Hata na hivyo, bwana huyo akaendelea kusisitiza apewe lifti, atafahamu yeye mwenyewe pa kushukia huko mbele ya safari.
Dr. Lambert akafikiri kidogo.
Alikosa namna ya kumwepuka bwana huyu, hivyo basi, japo kishingo upande, akaridhia kwenda naye.
Akafungua mlango na kuingia ndani kwa furaha.
Akamweleza dokta namna gani anavyopata shida kwenye usafiri baada ya gari lake kupata hitilafu zinazochukua muda kuzitibu huko karakana.
Lakini maelezo yake, dokta hakuyajali. Badala yake alikuwa anawaza kero ya kumpakia bwana huyu kwenye gari yake akifahamu fika ni mtu wa maneno mengi.
Zaidi bwana huyo alikuwa akimpotezea mahesabu yake ya muda kwani alipanga kuongea na Mitchelle punde tu atakaposhika barabara akitoka maabara.
Aongee naye kuhusu mzigo wao kwasababu leo mwanamke huyo alikuwa akiungoja kwa hamu sana ikiwa ndo' siku ya mwisho kati ya zile alizompatia.
Basi aliendesha akiwa ametulia, mawazo mepesi yamemkaa kichwani.
Kuna muda alisahau kama ana mtu pembeni kwa namna alivyokuwa anafikiria mambo yake.
Muda aliomkumbuka akawa haachi kujiuliza bwana huyo atashukia wapi ili apate kuwa huru na shughuli zake.
Kuna muda alitamani kumshusha kwanguvu lakini ndo' hivyo, aliishia tu kutamani kwani asingeweza.
Jambo hilo lisingemjengea picha nzuri.
Gari likazidi kwenda huku mgeni wake haonyeshi dalili yoyote ya kushuka.
Hata alipobadili barabara akitegemea ataambiwa niache hapo, bado hakufanikiwa.
Mgeni alitulia tuli kana kwamba wanaelekea nyumba moja.
Swala hili likaanza kumjengea hofu taratibu.
Alijiuliza bwana huyu anataka nini?
Alianza kufikiria mienendo yake na hapa ndipo akakumbuka sakata lile la chooni.
Alikumbuka siku ile namna alivyotoka chooni kuongea na Mitchelle kisha akakuta mlango upo wazi.
Alipoenda kutazama ofisini hakumkuta bwana huyu mpaka kitambo kidogo aliporejea kutokea kusikojulikana.
Hapa hofu yake ikaongezeka zaidi.
Hajakaa vizuri, simu ikaita.
Hakuelewa ilikuaje, lakini alijikuta anatazamana uso kwa uso na bwana yule.
Akatoa simu mfukoni mwake na kutazama.
Ilikuwa ni namba isiyokuwa na jina lakini moja kwa moja aliishaitambua.
Alikuwa ni Mitchelle.
Akazima sauti kisha akaiweka simu juu ya dashboard ikiwa inatazama chini.
Kukawa na utulivu kidogo.
Lakini haikuchukua muda, simu ikaita tena.
Dokta akaitazama akiwaza. Mwendo wa gari kaupunguza.
Yule bwana wa pembeni akamwambia,
"Si upokee?"
Akamtazama.
Badala yake akaiminya tena simu hiyo na kuendelea na safari kidogo kabla hajaegesha gari pembeni na kumtama bwana yule ashuke.
Alimwambia,
"Nadhani hapa panakutosha. Naomba ushuke, nina safari zangu zingine."
Bwana yule akatabasamu.
Alikuwa ametulia kwenye siti yake kama mtu anayewaza jambo.
Kabla hajafanya kitu, simu ya dokta ikaita tena. Akamtazama dokta na kumwambia,
"Ni yule uliyekuwa unaongea naye chooni, sivyo? Sasa kwanini haupokei?"
Hapo dokta akayakodoa macho.
Akapokea simu ile iliyoita, akasema maneno machache,
"Tafadhali, nakupigia si muda mrefu."
Aliongea akiwa anamtazama mgeni wake. Alipokata, akiwa anatazama kwa walakini, akamuuliza bwana yule,
"Maongezi gani chooni?"
Bwana yule hakujibu. Aliendelea kutabasamu kwa mbali akitazamana na dokta.
Macho yake yalikuwa yanaongea.
Dokta aliyatazama kwa umakini akauona ujumbe wake humo.
Bwana huyo alikuwa anajua JAMBO.
Kumbe siku ile hakukosea kabisa kuwa na mashaka naye pale alipotoka chooni.
Alimuuliza,
"Dr. Jean, niambie ni nini unafahamu?"
Bwana yule akatabasamu sasa akionyesha meno.
Kisha akamwambia Dokta kuwa aliskia kila jambo aliloliongea akiwa chooni.
Lakini pia kama haitoshi, alikuwa anajua kilichotokea leo hii kuhusu mkoba ule mweusi wa ngozi.
Alimwona Dokta akiwa maabara na kupakia baadhi ya vitu kwa siri. Na hata alitambua kuwa mkoba ule aliompa mlinzi kuukagua haukuwa wenyewe.
Mkoba halisi ulikuwepo kwenye droo ya pili. Na huo ndo' mkoba ambao anao hivi sasa kwenye gari.
Alisema,
"Kabla ya walinzi kuja, mimi nilishaona ulichokifanya nikiwa nimesimama dirishani punde baada ya wewe kuingia ofisini.
Niliujua mchezo wote uliokuwa umeupanga, Lambert."
Dokta akakosa cha kusema.
Kwa muda akatulia kitini akijaribu 'kurewind' mambo yote kichwani.
Mbona kila kitu alikiona kipo sawa?
Akajiuliza
Ilikuaje akawa mzembe kiasi hiko?
Maswali hayo yakamnyima fursa ya kumzingatia mgeni wake kwa muda.
Alikuja kurudishwa mchezoni na sauti ya dokta Jean ikisema,
"Sasa naweza nikashuka nikaondoka."
Upesi akamwahi bwana huyo kwa kumshika mkono.
Akamwambia,
"Ngoja kwanza."
Kisha akamuuliza,
"Kuna yeyote umemwambia haya?"
Dokta Jean akajibu,
"Kwa sasa hapana. Sijajua hapo mbeleni."
***
Na Steve B.S.M
Brookhaven, New York.
Saa nne asubuhi
Bwana Lambert aliingia ndani ya ofisi akiwa analegeza tai shingoni.
Mkononi alikuwa ameshikilia mkoba mweusi wa ngozi.
Mkoba huo ulikuwa na kifungo cha chuma.
Aliushikilia mkoba huo vema, upo kifuani kwake ameukumbatia na mkono wake wa kuume.
Alipoingia tu ndani akaurejeshea mlango upesi na kwenda moja kwa moja kwenye kiti chake.
Akaketi na kuuweka mkoba wake ndani ya droo ya meza yake.
Kisha akatulia akiskizia.
Moyo wake ulikuwa unapiga kwa kasi.
Aliukua anausikia kabisa kwenye masikio yake makubwa.
Na pumzi yake haikuwa ya kawaida.
Alikuwa anahema kwa kasi japo si kwanguvu.
Alitulia hapo akifikiria.
Akifiria namna alivyotenda mpaka kufika hapo.
Alikumbuka nyendo zake zote alizopitia mpaka kufikia hapo alipoketi.
Akaona kila kitu kipo sawa.
Akashusha pumzi fupi kisha akatua koti lake sasa.
Koti kubwa jeupe
Akalipachika kwenye kiti kisha akawasha tarakilishi yake kwaajili ya kuandika baadhi ya taarifa ambazo zilipaswa kunakiliwa kwenye mafaili.
Akiwa anafanya hivyo, mara mlango ukafunguliwa.
Akarusha macho yake kutazama.
Mlangoni akawaona wanaume wawili waliovalia sare rangi ya bluu iliyokoza
Wamefunika vichwa vyao na kofia aina ya bareti zenye chapa ya ulinzi.
Wanaume hao, mmoja mweupe na mwingine mweusi, walikuwa wamebebelea bunduki mikononi mwao.
Bunduki kubwa mithili ya majangili wanaolenga kuangusha tembo nyikani.
Nyuso zao hazikuwa rafiki.
Macho yao makali yalimtazama Dr. Lambert kana kwamba mwalifu aliyetoka kufanya mauaji.
Naye Dr. Lambert akawatazama kwa kustaajabu.
Aliwatazama kwa macho yasiyoelewa chochote kinachoendelea hapa.
Aliwafahamu mabwana hawa kama wafanyakazi wa ulinzi wa kampuni mpya iliyopata tenda ya kuimarisha ulinzi eneo hili la maabara ya taifa.
Lakini pia aliwafahamu kama wana-ulinzi wa gredi ya pili, juu yao wakiwepo wanausalama.
Mabwana wale wanaovalia suti nyeusi.
Lakini kwanini hawa wako hapa wakiwa wamebebelea silaha?
Alikuwa anaenda kulijua hilo muda si mrefu.
Bwana mmoja kati ya hao walinzi wawili, yule mwanaume mweusi, akamfuata wakati mwingine akiwa amebakia pale mlangoni.
Akamwambia dokta,
"Tunataka kuona ulichokichukua kule maabara."
Dokta akastaajabu.
Alisema,
"Nini hiko? Sijachukua chochote mimi."
Bwana huyo mlinzi akamtazama kwa macho ya kina kirefu cha maji.
Hakuwa na masikhara.
Alitulia kwa kama sekunde tatu akimtazama dokta pasipo kutia neno.
Uso wake uliongea kila kitu.
Dokta akajifaragua akijitetea,
"Sijabeba kitu mimi. Naamini mtakuwa mmekosea au mmenifananisha."
Bwana yule mlinzi, akanyanyua silaha yake na kumwonyeshea.
Dokta akaogopa sana.
Kuona mdomo wa bunduki ukitazama uso wake kulimfanya atetemeke kwa hofu.
Bwana yule akasema,
"Sitarudia tena. Weka mezani kile ulichokichukua maabara."
Kisha akapayuka,
"Upesi!"
Dokta akaruka kwa woga.
Haraka, kwa mikono yake inayotetemeka, akafungua droo na kutoa mkoba mweusi.
Akauweka mezani.
Ulikuwa ni mkoba mweusi wa ngozi wenye kifundo cha chuma.
Punde tu alipouweka mezani, akanyoosha mikono yake juu na kusema huo ndo' mzigo wake alotoka nao maabara.
Wakati huo wenzake wawili walikuwa wameshafika katika eneo la tukio.
Walisimama kule mlangoni wakitazama kwa kurusha macho yao ndani wapate kuona yanayoendelea humo.
Walizuiliwa kuingia ndani na yule mlinzi aloiyesimama hapo.
Mmoja wao alikuwa ni yule bwana mfupi kuliko wote, na mwingine ni yule kijana mwenye umri mdogo kuliko wote humu ofisini.
Mlinzi yule aliyesimama mkabala na dokta, akauchukua huo mkoba mweusi na kuufungua.
Akaupekua.
Kwa kama sekunde kumi hivi alifanya zoezi lake kisha akaurejesha mkoba huo mezani.
Akamtazama mwenzie aliyekuwepo mlangoni na kumpa ishara ya kutikisa kichwa.
Hamna alichopata.
Kumbe ndani ya mkoba kulikuwa na kiasi kidogo cha chakula kwenye kontena na matunda mawili, ndizi mbivu.
Dokta akauliza,
"Ni nini mmeona humo cha ajabu?"
Mabwana wale hawakujibu. Hapa akapata nguvu zaidi ya kuongea.
Aliunyakua mkoba wake akiwatuhumu walinzi wale kwa kuenenda kama wanyama wasiokuwa na akili.
Alisema ya kwamba yeye hubeba chakula chake hata anapokuwa akifanya kazi maabara kwasababu ya matatizo yake ya vidonda vya tumbo.
Hawezi kungoja mpaka muda wa chakula cha mchana ufike.
Anapaswa kufanya hivyo kwani hapa karibuni hali yake ilikuwa mbaya zaidi kiasi cha kutapika damu.
Aliposema hayo, walinzi wakamwomba radhi wakisema walikuwa katika majukumu yao.
Kisha wakaondoka zao na hali ya hapa ikapoa.
Mabwana wale wawili, wenza na dokta, wakaingia na kumpa pole mwenzao huku wakiwarushia tuhuma wanaulinzi hao kwa kutokuwa makini na kusababisha taharuki kali.
Bwana yule kijana alisema,
"Sasa kazi yetu imekuwa kama gereza. Bunduki na risasi zimegeuka kuwa sehemu ya maabara."
Baada ya muda kidogo, hali ikarudi kuwa shwari na shughuli zingine zikaendelea kama kawaida.
Dokta Lambert, akiwa amehakikisha kuwa kila mtu hapa anashughulika na yake, akafungua droo ya pili ya meza yake.
Macho yake yalikuwa na wangalifu mkubwa.
Alifungua droo hiyo kwa utaratibu mno kiasi kwamba hakutengeneza sauti yoyote.
Kisha akaitazama kwa kuibia.
Mkoba wake ulikuwa umekaa kwa kutulia.
Mkoba mweusi wenye fundo la chuma.
Mkoba huu ulikuwa ni wa pili wakati wa kwanza ukiwa kwenye ile droo ya kwanza ya meza..
Droo ambayo aliutoa mkoba ule aliowapatia walinzi kwaajili ya kuukagua.
Akatabasamu kwa mbali.
Mchezo wake ulienda vile alivyokuwa anatarajia.
Mikoba miwili inayofanana kwa kila kitu ilitosha kabisa kumvusha mto yordani.
Akahisi moyo wake umekuwa wa baridi na adhma yake inaenda kutimia.
Akatabasamu tena.
Baadae jioni, majira ya saa kumi, akiwa ameshamaliza kila jambo hapa kazini akaliendea gari lake akiwa na mkoba wake mkononi.
Alilenga kwenda nyumbani moja kwa moja.
Akauweka mkoba wake mahali salama ndani ya gari kisha akatekenya funguo kuwasha chombo.
Kabla hajaondoka, akasikia ngo-ngo-ngo.
Kuna mtu aligonga kioo cha dirisha la upande wake wa kulia.
Moyo ukamlipuka mithili ya guruneti.
Alishtuka kwa hofu kubwa aliyojitahidi kuizuia isionakane lakini uso wake ukafeli.
Macho yake yalijawa na woga.
Alitazama upesi akamwona mwanaume, kwa nje, akiwa anampungia kwa furaha.
Alikuwa ni bwana yule mfupi anayefanya naye kazi katika ofisi moja.
Bwana huyo alikuwa anatabasamu kwa upana akipeperusha kiganja chake.
Akashusha kioo apate kumsikia.
Bwana yule akasema,
"Samahani sana, bwana. Nadhani unaelekea nyumbani. Unaweza ukaniacha hapo mbele kidogo?"
Bwana huyo alitaja mahali aelekeapo lakini Dr. Lambert akamruka kiunzi.
Alimwambia hapiti huko.
Hata na hivyo, bwana huyo akaendelea kusisitiza apewe lifti, atafahamu yeye mwenyewe pa kushukia huko mbele ya safari.
Dr. Lambert akafikiri kidogo.
Alikosa namna ya kumwepuka bwana huyu, hivyo basi, japo kishingo upande, akaridhia kwenda naye.
Akafungua mlango na kuingia ndani kwa furaha.
Akamweleza dokta namna gani anavyopata shida kwenye usafiri baada ya gari lake kupata hitilafu zinazochukua muda kuzitibu huko karakana.
Lakini maelezo yake, dokta hakuyajali. Badala yake alikuwa anawaza kero ya kumpakia bwana huyu kwenye gari yake akifahamu fika ni mtu wa maneno mengi.
Zaidi bwana huyo alikuwa akimpotezea mahesabu yake ya muda kwani alipanga kuongea na Mitchelle punde tu atakaposhika barabara akitoka maabara.
Aongee naye kuhusu mzigo wao kwasababu leo mwanamke huyo alikuwa akiungoja kwa hamu sana ikiwa ndo' siku ya mwisho kati ya zile alizompatia.
Basi aliendesha akiwa ametulia, mawazo mepesi yamemkaa kichwani.
Kuna muda alisahau kama ana mtu pembeni kwa namna alivyokuwa anafikiria mambo yake.
Muda aliomkumbuka akawa haachi kujiuliza bwana huyo atashukia wapi ili apate kuwa huru na shughuli zake.
Kuna muda alitamani kumshusha kwanguvu lakini ndo' hivyo, aliishia tu kutamani kwani asingeweza.
Jambo hilo lisingemjengea picha nzuri.
Gari likazidi kwenda huku mgeni wake haonyeshi dalili yoyote ya kushuka.
Hata alipobadili barabara akitegemea ataambiwa niache hapo, bado hakufanikiwa.
Mgeni alitulia tuli kana kwamba wanaelekea nyumba moja.
Swala hili likaanza kumjengea hofu taratibu.
Alijiuliza bwana huyu anataka nini?
Alianza kufikiria mienendo yake na hapa ndipo akakumbuka sakata lile la chooni.
Alikumbuka siku ile namna alivyotoka chooni kuongea na Mitchelle kisha akakuta mlango upo wazi.
Alipoenda kutazama ofisini hakumkuta bwana huyu mpaka kitambo kidogo aliporejea kutokea kusikojulikana.
Hapa hofu yake ikaongezeka zaidi.
Hajakaa vizuri, simu ikaita.
Hakuelewa ilikuaje, lakini alijikuta anatazamana uso kwa uso na bwana yule.
Akatoa simu mfukoni mwake na kutazama.
Ilikuwa ni namba isiyokuwa na jina lakini moja kwa moja aliishaitambua.
Alikuwa ni Mitchelle.
Akazima sauti kisha akaiweka simu juu ya dashboard ikiwa inatazama chini.
Kukawa na utulivu kidogo.
Lakini haikuchukua muda, simu ikaita tena.
Dokta akaitazama akiwaza. Mwendo wa gari kaupunguza.
Yule bwana wa pembeni akamwambia,
"Si upokee?"
Akamtazama.
Badala yake akaiminya tena simu hiyo na kuendelea na safari kidogo kabla hajaegesha gari pembeni na kumtama bwana yule ashuke.
Alimwambia,
"Nadhani hapa panakutosha. Naomba ushuke, nina safari zangu zingine."
Bwana yule akatabasamu.
Alikuwa ametulia kwenye siti yake kama mtu anayewaza jambo.
Kabla hajafanya kitu, simu ya dokta ikaita tena. Akamtazama dokta na kumwambia,
"Ni yule uliyekuwa unaongea naye chooni, sivyo? Sasa kwanini haupokei?"
Hapo dokta akayakodoa macho.
Akapokea simu ile iliyoita, akasema maneno machache,
"Tafadhali, nakupigia si muda mrefu."
Aliongea akiwa anamtazama mgeni wake. Alipokata, akiwa anatazama kwa walakini, akamuuliza bwana yule,
"Maongezi gani chooni?"
Bwana yule hakujibu. Aliendelea kutabasamu kwa mbali akitazamana na dokta.
Macho yake yalikuwa yanaongea.
Dokta aliyatazama kwa umakini akauona ujumbe wake humo.
Bwana huyo alikuwa anajua JAMBO.
Kumbe siku ile hakukosea kabisa kuwa na mashaka naye pale alipotoka chooni.
Alimuuliza,
"Dr. Jean, niambie ni nini unafahamu?"
Bwana yule akatabasamu sasa akionyesha meno.
Kisha akamwambia Dokta kuwa aliskia kila jambo aliloliongea akiwa chooni.
Lakini pia kama haitoshi, alikuwa anajua kilichotokea leo hii kuhusu mkoba ule mweusi wa ngozi.
Alimwona Dokta akiwa maabara na kupakia baadhi ya vitu kwa siri. Na hata alitambua kuwa mkoba ule aliompa mlinzi kuukagua haukuwa wenyewe.
Mkoba halisi ulikuwepo kwenye droo ya pili. Na huo ndo' mkoba ambao anao hivi sasa kwenye gari.
Alisema,
"Kabla ya walinzi kuja, mimi nilishaona ulichokifanya nikiwa nimesimama dirishani punde baada ya wewe kuingia ofisini.
Niliujua mchezo wote uliokuwa umeupanga, Lambert."
Dokta akakosa cha kusema.
Kwa muda akatulia kitini akijaribu 'kurewind' mambo yote kichwani.
Mbona kila kitu alikiona kipo sawa?
Akajiuliza
Ilikuaje akawa mzembe kiasi hiko?
Maswali hayo yakamnyima fursa ya kumzingatia mgeni wake kwa muda.
Alikuja kurudishwa mchezoni na sauti ya dokta Jean ikisema,
"Sasa naweza nikashuka nikaondoka."
Upesi akamwahi bwana huyo kwa kumshika mkono.
Akamwambia,
"Ngoja kwanza."
Kisha akamuuliza,
"Kuna yeyote umemwambia haya?"
Dokta Jean akajibu,
"Kwa sasa hapana. Sijajua hapo mbeleni."
***