Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nshatuma mama.Tivu tunalala au tusubiri
Asnt sn[emoji123]TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 19
Na Steve B.S.M
Jamal akampatia Richie muhtasari wa data ile aliyompatia akaifanyie kazi.
Akamweleza ya kuwa yale yote yaliyomo katika taarifa hiyo yanamhusu binadamu na vijenzi vyake.
Data za muunganiko wa damu ya binadamu, mate ya binadamu na karibia kila kitu kuhusu kemikali zote zilizomo katika mwili hai wa binadamu.
'Chemical composition' za vyakula karibia vyote ambavyo hutumika na binadamu, na pia composition ya karibia kemikali zote ambazo ni sumu kwa matumizi ya binadamu..
'Chemical reactions' karibia zote zinazofanya mwili wa binadamu kufanya kazi kwa ufanisi wake, na athari ya kukosekana kwa kila kemikali ndani ya mwili huo.
Kemikali ambazo zipo tumboni. Kwenye mifupa. Kwenye ubongo.
Kemikali zote zinazozalishwa na ini la binadamu na kazi takribani mia tano za kikemikali zinazofanywa na 'organ' hiyo ndani ya mwili.
Alimwambia Richie,
"Kwa mujibu wa tafiti ya wanasayansi wa chuo cha California waliyoifanya katika mwili wa mwanamke mjamzito, walibaini kuna kemikali takribani mia moja na tisa katika mwili wa binadamu.
Ikiwemo kemikali hamsini na tano ambazo hazikuwahi kuripotiwa popote pale hapo nyuma.
Pia kemikali arobaini na mbili ambazo vyanzo vyake na matumizi yake katika mwili wa binadamu hayafahamiki mpaka leo hii kwa wanasayansi.
Kemikali hizo huitwa 'mystery chemicals'.
Huenda kila mmoja anazo.
Kazi yake mwilini, hakuna anayejua. Chanzo chake mwilini, hakuna anayejua pia.
Lakini ajabu ni kwamba, katika chapisho ulilonipa, zimeanishwa kemikali mia mbili ambazo ni 'mystery'.
Kemikali mpya kabisa, sijapata kuziona wala kujifunza popote pale. Haswa katika mwili wa binadamu.
Kemikali hizo sijajua kazi yake ni nini katika mwili uliotajwa. Na nilishindwa kutafuta majibu zaidi sababu ya masharti uliyonipatia."
Richie akasafisha koo lake kisha akayabandua macho yake kwenye karatasi alilokuwa anasoma.
Akamtazama Jamal usoni.
Mwanaume huyo mweusi alikuwa na macho mekundu. Ni wazi hakupata wasaa wa kutosha wa kulala usiku wa kuamkia siku hii.
Kazi hii ilikuwa kubwa mno.
Wingi wa makaratasi aliyoyashika Richie, ulithibitisha hilo.
Richie akauliza,
"Una uhakika hakuna mtu anayejua kuhusu taarifa hii?"
Jamal akaapa.
Alisema hata mwenzake anayelala naye hakupata kujua ni nini anafanya, hivyo kila kitu kipo salama.
Lakini akamwambia Richie kwamba kemikali hizo ambazo bado hawajazifahamu, huenda angepata taarifa zake kama angemshirikisha profesa wa chuoni kwao.
Alisema,
"Pengine hiko ndo' kinafanya taarifa hii kuwa siri. Huoni hilo?"
Richie akatikisa kichwa.
"Hapana, Jamal. Ni hatari. Naamini kuna taarifa nyingi zijazo, tutakapozipata kwa ukamilifu wake basi tutajua mengi. Acha kwanza nikapitie hizi."
Simu ya Jamal ikaita.
Aliichomoa mfukoni akaitazama. Jina Huncho.
Akaminya sauti kisha akaendelea na maongezi.
Alimtaka Richie ampate pesa yake aondoke kwani yuko nyuma ya muda.
Lakini akasihi chapisho lingine litakapopatikana basi apatiwe maramoja kwani kuna jambo amelihisi na nafsi yake.
Alisema,
"Yawezekana huu ukawa ni mradi wa kutengeneza watu. Sina uhakika lakini ... Sijui ... Nahisi tu."
Richie akamuuliza akiwa ameyakodoa macho yake,
"Kwanini unahisi hivyo?"
Akapandisha mabega yake na kuupinda mdomo.
Akasema,
"Kwa namna taarifa zilivyopangiliwa humo. Taarifa zenyewe zilizowasilishwa. Na usiri wake. Auhisi jambo? ... Ni hisia tu, nilishawahi kusikiasikia haya mambo ... kama nilivyosema hapo mwanzo ... Nahisi tu. Kama si hivyo basi yawezekana ni kuhusu Pharmaceuticals.
Tutapata dira baada ya kupitia kazi zijazo.
Lakini ..."
Hapa akarudi kwenye swali lake la kwanza kabisa alilouliza
"Richie, umetoa wapi hizi data?"
Richie hakuwa tayari na swali hilo. Akasema hayo ni yake na aachiwe mwenyewe.
Kama ilivyo ahadi, akatoa pesa ndani ya begi na kumpatia Jamal.
Jamal akahesabu na kuona ni timilifu. Akashukuru na kuaga.
Muda wote huo simu ya Jamal ilikuwa inaita kwa kutetemeka mfukoni.
Richie akamtazama mwanaume huyo akienda zake.
Alipotoka tu mgahawani, akatoa simu yake na kumpigia Hilda.
Akamweleza yale yote aliyopata kuambiwa na Jamal.
Alisema,
"Kama utapata muda, naomba tuonane."
Hilda akamjibu,
"Sidhani kama itawezekana leo. Kuna kazi kubwa ya boss Bryson nafanya hapa."
Richie akahamaki,
"Kazi nyingine?"
Hilda akamweleza ya kazi hiyo kuwa amepatiwa asubuhi ya siku hii pale alipokutana na Bryson mahali fulani.
Richie akapendekeza wakutane sehemu ili amsaidie kuifanya.
Pendekezo hilo likamfurahisha Hilda.
Alicheka mtu wa pembeni angesikia.
Kwa upande wa Jamal, bwana yule, kijana barobaro, aliyetoka kuongea na Richie muda si mrefu ulopita, aliingia ndani ya basi akaketi pembeni ya dirisha.
Alipoketi tu, akatoa simu yake iliyokuwa inaita mfukoni na kuipokea.
Alikunja sura akisema,
"Huncho, ukipiga mara mbili inatosha kwani nyumba inaungua moto?"
Sauti ya upande wa pili ikazozana naye. Ilikuwa ni sauti ya mwanaume ikikwaruza.
Sauti hiyo ilisema,
"Jamal, ulisema mpaka muda huu utakuwa ushantumia pesa yangu. Naona kimya, vipi?"
Jamal akamwambia yu kwenye basi. Pesa anayo mfukoni.
Punde atakaposhuka basi atamrushia kwenye simu.
Swala hilo likawa gumu kwa Huncho. Hakupenda wazo hilo.
Alitaka pesa yake cash.
Akamwelekeza Jamal mahali alipo kisha akasema anangoja hapo.
Jamal akakata simu.
Akairudisha mfukoni huku akiongea mwenyewe kwa kulalama.
Alisema,
"Madawa yatakuja kumuua huyu mjinga. Yeye anawaza unga tu, hamna kingine."
Baada ya robo saa akashuka toka kwenye basi.
Akaitoa pesa yake na kuitenganisha mfuko kisha akaendelea na safari.
Muda kidogo akawa amekutana na Huncho mahali palipojificha kiasi.
Mwanaume huyo alikuwa mrefu, mweusi, mwenye kuvalia nguo za rangi rangi nyingi.
Nywele zake amezisokota rasta zilizofika mabegani.
Usoni amevalia miwani nyeusi ya jua.
Jamal alimpatia pesa akazihesabu na kukiri zipo sawa kisha akasema,
"Tuonane tena siku nyingine."
Akaondoka zake akimwacha Jamal hapo.
***
New York Police Department, New York.
Saa sita mchana
Mpelelezi alitoka kwenye ofisi ya mkuu wake wa kazi akiwa ameshika kiuno.
Alikuwa amevalia shati jeupe na 'suspender' nyeusi. Suruali ya kitambaa na kiatu kinachong'aa.
Macho yake yalikuwa yamelegea kama mtu aliye na usingizi, kuchoka au vyote kwa pamoja.
Sauti kali iliyotoka kwenye ofisi ya mkuu wake ilifoka,
"Nakwambia unacheza na sharubu za simba. Sitakustahimili tena, afisa. Sitakustahimili tena!"
Mpelelezi akaufunga mlango na kwenda zake.
Uso wake umeparara.
Akiwa anajongea, akasikia mtu anamwita.
Aligeuka akamwona Babyface kwa mbali.
Bwana huyo alikuwa amevalia suti nyeusi nadhifu.
Nywele zake zinang'aa na kulala kama zimelambwa na paka.
Usoni mwake amevaa tabasamu pana linaloonyesha meno yake yote.
Alimpungia mpelelezi mkono, akamwonyesha ishara kuwa anakuja kisha akaenda zake mwelekeo wa ofisi ya mkuu wa upelelezi.
Mpelelezi akamtazama bwana huyo akiwa anatafakari yake kichwani.
Hakukaa hapo, akaelekea kwenye ofisi yake alipojibwaga katika kiti na kushusha pumzi ndefu puani.
Taratibu akiwa anazungusha kiti chake kwenda huku na kule, akawa anatafakari.
Alikuwa na mambo mengi kichwani.
Ni kama vile ujenzi wa ghorofa ulikuwa unaendelea katika ubongo wake.
Alitafakari mambo yanavyokwenda.
Moja baada ya jingine.
Akili yake ikampeleka mbali ...
Siku za nyuma: Majira ya saa nne asubuhi.
Kule San Fransisco, California. Majira ya saa nne asubuhi.
Aliamka kichwa kikiwa kinamuuma.
Alihisi mtu yumo ndani ya fuvu lake akibondabonda na nyundo.
Akiwa ameshika kichwa chake kuugulia maumivu, akakagua mazingira ya hapa alipo.
Palikuwa ni pageni machoni mwake.
Hayakuwa mazingira ya 'lodge' ile aloilipia.
Akaketi kitako akiwaza na kuwazua.
Palikuwa kimya sana hapa.
Hakujua amefikaje.
Aliwaza kama ni hoteli ama nyumbani mwa mtu.
Akatoka kitandani na kuufuata mlango.
Kifua chake kilikuwa wazi, akiwa amevalia suruali pekee.
Chini yuko peku, anauhisi ubaridi wa sakafu.
Kabla hajaufungua mlango, akasikia sauti ya mwanamke ikiwa inaongea huko upande wa pili.
Akatulia tuli, asikie mwanamke huyo anaongea nini.
Kwa dakika moja za kuskiliza, hakuambulia kitu.
Sauti haikusikika vema.
Ni kana kwamba mtu alikuwa anaongea akiwa ndani ya chungu.
Akaufungua mlango na kushika korido.
Alinyookea sebuleni akamkuta mwanamke akiwa ameketi kwenye kochi kubwa, mezani kuna sahani nyeupe yenye bites.
Sebule hii ilikuwa pana lakini yenye uhaba wa samani.
Makochi mawili tu yalikuwapo hapa pamoja na meza ndogo.
Ni bayana mkazi wa hapa alikuwa akipendelea zaidi nafasi kuliko mrundikano wa vitu.
Mwanamke huyo alikuwa anaongea na simu, na punde alipomwona Mpelelezi akakatisha maongezi yake ili apate kumlaki.
Alikuwa ni mwanamke yule wa Casino.
Alikuwa amevalia blauzi fupi rangi ya pink iliyoacha tumbo lake bapa kuwa wazi.
Chini amevalia kibukta kifupi rangi nyeusi chenye michirizi meupe pembeni.
Nywele zake amezibana kwa ustadi mkubwa usidhanie kabisa kama ni ndefu kiasi tunachojua.
Alitabasamu akasema,
"Karibu sana bwana. Naona umeamka."
Mpelelezi akamuuliza imekuaje akafika hapo. Alitaka kujua ni nini kilitokea jana yake usiku.
Mwanamke yule akampoza.
Akamsihi atulie kwanza, atafahamu kila kitu.
Alimuuliza,
"Unajiskiaje?"
Mpelelezi akajibu yuko sawa, lakini mwonekano wake ukiwa kinyume na anachosema.
Kila saa alikuwa anakunja uso wake kwa maumivu ya kichwa na mwenyeji wake akalibaini hilo.
Akamwambia,
"Nilikuandalia supu kwaajili ya hangover. Ni vema ukaipata sasa."
Mwanamke huyo akaenda jikoni na punde akaja na bakuli zuri lenye supu ndani yake.
Akampatia Mpelelezi akimkaribisha.
Lakini kabla Mpelelezi hajatia kitu mdomoni, akauliza,
"Nini kilitokea jana? ... Nataka kujua."
Mwanamke yule akamjibu,
"Nadhani ulikunywa kupita kiasi."
Mpelelezi akapata mashaka.
Hakuwahi kunywa kiasi cha kupoteza kabisa fahamu zake.
Hiyo jana kulitokea nini kiasi cha kushindwa kujimudu?
Ghafla akajipapasa mfukoni mwake.
Hakuhisi kitu.
Mwanamke yule akamwambia,
"Simu zako nilizihifadhi kwaajili ya usalama. Ngoja nikupatie."
Akaenda zake chumbani.
Mpelelezi akiwa hapo sebuleni peke yake, akarusha macho yake huku na kule kufanya ukaguzi wa mazingira ya hapa.
Kichwa bado kilikuwa kinamgonga.
Kuna muda alishindwa kuhimili akakishika kwanguvu.
Punde Mwanamke yule akarejea akiwa na simu mbili mkononi pamoja pia na dawa ya kutuliza maumivu.
Akampatia Mpelelezi.
Mpelelezi akanywa dawa hizo maramoja akisindikizia na maji mengi alopewa.
Akiwa anafanya hivyo, mwanamke yule akawa anamtazama kwa udadisi.
Alimwambia,
"Kunywa sasa supu yako kabla haijapoa."
Mpelelezi akafanya vivyo, lakini kiu yake ya kutaka kujua yanayoendelea hapa ikambana.
Alitaka kuuliza.
Upesi mwanamke yule akamsihi,
"Kula kwanza. Najua una maswali mengi. Nami ninayo pia."
Kisha akatabasamu.
Mpelelezi akazidi kuamini.
Mwanamke huyu alikuwa ni wa ajabu.
***
Kidogo tu? Haya njoo tuendelee.Tivuuu kidogo tu
Kaka naomba unicheki PMAsnt sn[emoji123]
AhsanteeeeeeeeeKidogo tu? Haya njoo tuendelee.
Natuma moja ya ziada. Au unasemaje?Mbona tamu hivi inasisimua hautamani iishe daah
Hata mbili sio mbaya tivuNatuma moja ya ziada. Au unasemaje?
Shukrani, mkuu. Nakuomba pm.MWENYEZI MUNGU aendelee kubariki kipaji chako Mr[emoji123]
Asante sana tivu ila namuonea huruma sana mpelelezi masikini
Karibu sana. Hutojutia.Nime kuja kutoa maoni ili kuweka alama uzi huu nikiwa na utulivu niupitie wote kwa ufasaha