SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
- #181
TUKIBAKI HAI, TUTASIMULIA - 25
Na Steve B.S.M
Baada ya siku moja ...
Katika sehemu ya siri, majira ya jioni.
Jennifer akiwa amebebelea kikombe kidogo cha udongo kinachofuka moshi, aliufungua mlango mkubwa kukutana na kibaraza cha nje.
Kibaraza hiko kilikuwa kikubwa kwa wastani, kinaning'inia kwenye ghorofa hili, refu la hadhi ya kati.
Ghorofa lenye sakafu kadha wa kadha.
Kwenye kiti kikubwa cha mtindo, katika kibaraza hicho, alikuwa ameketi mwanamke maridadi, Mitchelle.
Mwanamke huyo alikuwa kavalia bukta fupi sana rangi ya manjano na blauzi nyeusi kwa juu. Nywele zake kazibana vema kwa nyuma, uso wake unang'azwa na miale dhaifu ya jua la jioni.
Alikuwa anatazama namna jua linavyozama. Alikuwa anapenda sana jambo hili. Alitulia hapo huku akiwa anatafakari mambo kadhaa kichwani.
Alipenda utulivu huu maana kichwani mwake kulikuwa na vurugu sana.
Pembeni ya kiti hicho kulikuwa na kijistuli kidogo cha kioo. Juu ya stuli hiyo kulikuwa na kijidaftari kidogo kilichofungwa, pembeni kidogo kalamu ndani ya mfuniko wake.
Jennifer akasogeza kijidaftari hiko na kuweka kikombe alichokuja nacho kisha akamkaribisha Mitchelle.
Alimwambia kwa lugha yake ya ishara,
"Nimeona nikutengenezee kahawa yako unayoipenda. Pengine itakupa 'mood' nzuri leo."
Mitchelle akanyanyua kikombe na kukitia mdomoni. Akanywa fundo moja ...
Aaaaahhh ... akajiskia vema. Ni kana kwamba mwili wake ulikuwa unangoja kitu hiki muda wote huo.
Alikunywa tena fundo la pili kisha la tatu ndipo akarejesha kikombe kwenye stuli.
"Ahsante sana, Jenny. Ulijuaje hiki ndo' kitu nahitaji kwa sasa?"
Jennifer akatabasamu kisha akamwambia namna gani anavyomfahamu, na mara zote anapomwona akiwa yuko chini basi humwinua kwa kahawa yake pendwa.
Mitchelle akatabasamu.
Jennifer akamwambia akitumia mikono yake,
"Kwa leo siku nzima ndo' nakuona ukitabasamu kwa mara ya kwanza. Kuna jambo linakutatiza?"
Akatazama kijidaftari kwenye stuli kisha akaongezea,
"Ni mambo yako ya biashara, sio?"
Mitchelle akashusha pumzi fupi kisha akajibebea kikombe chake cha kahawa. Badala ya kujibu, akanywa fundo la kahawa.
"Jipe muda wa kupumzika," Jennifer akaendelea kumuhasa. "Naamini kila jambo litakuwa sawa. Jana na juzi hujalala vema, hakikisha unapata usingizi leo."
Mitchelle akampatia uso wa kumuashiria amemwelewa lakini hakusema jambo na kinywa chake.
Aliendelea kutazama anga jekundu, jua sasa likiwa halionekani.
Jennifer akamtazama kwa kitambo kidogo kisha akakata shauri kwenda zake. Kabla hajafika popote, Jennifer akamuuliza,
"Umeshaniandalia zile nguo zangu za mtoko wa jioni?"
Jennifer akampa ishara kuwa tayari ashafanya vivyo alafu akaenda zake. Akabaki Mitchelle peke yake.
Peke yake katika utulivu aupendao.
Akafungua daftari lake mara moja na kuandika mambo kadhaa kisha akalifunga na kuendelea kunywa kahawa yake.
Kahawa ambayo alizidi kuipatia hamu kadiri anavyoitumia.
Hakuchukua muda mrefu, kahawa ikawa imeisha. Akamwita Jennifer amwongezee. Akiwa anangoja akapiga simu yake mara moja.
Jennifer akiwa anaandaa kahawa, akamsikia 'boss' wake akiwa anateta na simu. Sauti yake ilikuwa kali, anafoka kama mwehu.
Hata yeye akaogopa japo si mhusika.
Alipompeleka kahawa akamkuta akiwa amefura sana. Uso wake karibia wote umekuwa mwekundu.
Kwa hofu kubwa, akaweka chupa ya kahawa kwenye stuli, alafu akachoropoka upesi kwenda zake.
Hata Mitchelle hakumjali.
Alikuwa na mambo yake kichwani yanayomtinga. Mambo mengi kwelikweli.
Alikuwa anatazama daftari lake, akiandikaandika. Akikokotoa na kufunga hesabu.
Alisahau mpaka kahawa yake alomimina kwenye kikombe. Kahawa hiyo ikakaa mpaka ikapoa. Kahawa ilokuwepo kwenye chupa ndo' hakugusa kabisa.
Muda si mrefu alinyanyuka toka hapo akaenda kujiandaa. Baada ya muda mfupi akawa yumo ndani ya gari la kukodi, si 'Uber', akielekea kaskazini mwa eneo analoishi.
Alikuwa amevalia kawaida sana, si kama mtu mwenye mtoko mkubwa, hapa akiwa amejivesha blauzi na jeans tu.
Baada ya dakika kadhaa akawa amefika katika klabu moja ndogo, hapo akajiweka mahali palipotulia, muziki kwa mbali, akawa anakunywa taratibu wine kwa glasi.
Alimaliza glasi ya kwanza, ya pili ikiwa kati, bwana mmoja akaingia katika eneo hilo akiwa anaangazaangaza.
Bwana huyo alikuwa amevalia koti jeusi la ngozi, ndani tisheti nyepesi na chini jeans ikiambatana na raba nyeupe.
Bwana huyo alikuwa ni Bryson.
Alipoangaza upande wake wa kuume, Mitchelle akampungia mkono kumwita. Alisogea hapo na muda si mrefu akaja mhudumu kumsikiliza.
Akaagiza kinywaji laini ambacho hakikuchukua muda kufika. Glasi nyembamba yenye mrija mrefu wa kuvutia.
"Umekuja na kazi yangu?" Mitchelle akauliza.
"Ndio " Bryson akatoa flash kwenye koti lake na kumpatia Mitchelle.
"Ajabu," Mitchelle akasema akitazama flash hiyo, "kazi hii umeifanya kwa upesi sana. Ni kwasababu ya shida yako ama kuna kingine?"
Bryson akatabasamu. Tabasamu lake lilijieleza kuwa hiyo ndo' sababu ... Akanywa fundo moja la kinywaji chake kisha akaelezea ni namna gani alivyokuwa ana uhitaji wa kuonana naye.
Alisema,
"Unajua ni namna gani ilivyo ngumu kuonana na wewe. Niliamini nikifanya kazi hii nikaimaliza kwa haraka basi itakuwa rahisi kukushawishi."
Mitchelle akamtazama bwana huyo kwa macho ya udadisi. Akanywa fundo moja la wine yake alafu akamuuliza akiwa anaendelea kumtazama ... macho ya kupembua,
"Unataka nini, Bryson?"
Bryson kwanza akatulia. Alikuwa anayapanga mambo yake kichwani ... Alitafakari mambo yanayomkabili japo kwa muhtasari kisha akafunguka haja yake.
Alieleza namna gani alivyokuwa na uhitaji mkubwa wa pesa kwani watoto wake wanatakiwa kufanya upasuaji.
Akiwa anaeleza hayo, macho yake yalilenga kwa machozi. Na Mitchelle akajua namna gani bwana huyu alivyokuwa na shida haswa.
Asiseme kitu, akaagiza kinywaji kingine alafu akaulaza mgongo wake kitini.
Kwa ukimya huu wa sekunde chache, muziki laini uliokuwa unapiga hapa ukatawala.
Wimbo wa 'Stuck on You' wa Lionel Richie ulishika hatamu watu wakijifurahisha na vinywaji vyao, wengine wakiimba na wengine wakitikisa miili yao taratibu kuitikia wimbo huo mwanana.
Kwa muda huo Mitchelle, kama kobe aliyejificha ndani ya gamba lake, alikuwa anatunga sheria kichwani.
Kinywaji kilipowasili, akanywa kwanza mafundo mawili alafu ndo' akarejea katika mjadala huu.
Alisema,
"Bryson, pesa kubwa kama hiyo lazima iambatane na makubaliano. Nadhani utakubaliana na mimi katika hilo."
Bryson akasema,
"Bila shaka. Nipo tayari kwa makubaliano yoyote yale alimradi nisaidie watoto wangu."
Mitchelle akatabasamu.
Tabasamu dogo.
Kisha akasema,
"Ok, lakini huenda kuna jambo natakiwa kukusisitizia zaidi, Bryson. Mimi ni mtu 'strict' sana kwenye maagano ninayoyaweka.
Huwa sipindishi wala kupunguza kile ambacho ninaweka nacho maagano, na huo ndo' udhaifu wangu mkubwa. Hivyo nakusihi sana, kuwa makini unapofunga makubaliano na mimi."
Alipofikia hapo, akamkumbusha Bryson makubaliano waliyoyaweka hapo kabla. Alimuuliza kama bado anayaishi makubaliano hayo, naye Bryson akaapa kuwa kila kitu kipo kama vile walivyokubaliana.
"Usiwe na hofu kabisa," alimtoa shaka. "Nasimamia kila tulichokubaliana."
Akiwa anasema haya, akajikuta moyo wake unaenda kasi.
Aliyakumbuka yale mazingira aloyakuta kule kwa Hilda akajikuta anajikaza tu. Alijipa matumaini huenda hamna cha ajabu cha kuhofia kiasi hiko, lakini ... Vipi kama ... Basi tu ...
Aliomba kila jambo liwe kama vile anavyotaraji. Aliupiga moyo wake konde.
Asingeweza kuacha pesa hizi kwani alikuwa ana uhitaji mno.
"Sawa," akasema Mitchelle, "sasa nikuambie maagano yangu kama utayaridhia."
Bryson akasema,
"Niko tayari."
Basi Mitchelle akamweleza yake anayoyataka. Alichukua kama dakika nne kueleza kila agano. Alipomaliza akamwambia Bryson kuwa pesa itaingizwa kesho yake majira ya asubuhi katika akaunti ya benki.
Bryson akafurahi kweli. Hakuamini macho yake.
Alijiona mshindi wa kila vita.
Hakujali makubaliano aliyoyaweka ni makubwa kiasi gani bali ukubwa wa furaha ya kuokoa uhai wa wanae.
Aliondoka hapo akiwa na tabasamu usoni, na alipofika tu nje akampigia simu mkewe kumpatia habari hizi njema.
Naye mkewe akafurahi sana kwani sasa tumaini lilishuka.
Upesi wakatoa taarifa kwenye uongozi wa hospitali na maandalizi ya upasuaji ya watoto wote wawili yakaanza mara moja.
Mama akajawa na tabasamu.
Lakini hakumuuliza mumewe ni maagano gani aliweka kupata pesa hiyo kubwa ... Pengine hilo halikuwa na umuhimu kwake kwa wakati huo.
Cha muhimu ni kuokoa watoto.
Ndani ya klabu Mitchelle, akiwa sasa peke yake, akaagiza tena kinywaji, akaendelea kunywa taratibu akikoshwa na muziki kwa mbali.
Alitazama saa yake, ilikuwa ni saa mbili ya usiku, akaona aendelee kuuvuta muda hapo akingojea saa tatu ifike.
Muda huo alikuwa na ahadi nyingine, hivyo hapa alikuwa na kama lisaa limoja la kukaa. Akautumia muda huo kunywa na huku akitafakari mambo yake ya pesa.
Alinyanyua simu yake akampigia Taiwan, simu ikaita na kupokelewa ndani ya muda mfupi.
Akasema,
"Nitakuja mwenyewe kwenye mnada."
Taiwan akaita,
"Naam!"
Mitchelle akarudia taarifa yake kwamba atahudhuria mwenyewe kwenye mnada.
Taiwan akauliza,
"Ma'am, kuna haja ya wewe kuja huku? Au ni kwasababu ya kudorora kwa biashara hapa karibuni? ... Usijali, nitasimamia kila jambo na kila kitu kitakuwa poa si muda mrefu."
Mitchelle akamwambia kuwa hili jambo atalisimamia yeye. Anataka iwe hivyo.
Aliposema hayo akakata simu.
----
Ni jambo gani Mitchelle amejadiliana na kukubaliana na Bryson?
Shaka la Bryson kwenye usiri wa Hilda litaishia wapi?
Ni mnada gani Mitchelle anataraji kuhudhuria?
Na miadi yake ya saa tatu usiku ni kukutana na nani?
***
Saa nane usiku ...
Mitchelle alipotoka bafuni alikuta kila kitu kikiwa kimeandaliwa mezani, pamoja pia na tarakilishi yake.
Ulikuwa ni usiku mkubwa lakini tayari Jennifer alishafanya kazi yake.
Punde tu Mitchelle aliporejea, aliamka akatimiza wajibu wake huo na sasa alikuwa pembeni akingoja kupakua na kuanua vyombo.
Macho yake yalikuwa mekundu, ameelemewa na usingizi. Japo Mitchelle alimsihi akapumzike lakini bado aliona ni kheri kuwapo hapa.
Alimpakulia Mitchelle chakula chepesi alichokiandaa, supu na 'bites', kisha akaketi kungoja. Mitchelle akawa anakula huku akipapasa tarakilishi yake.
Alichomeka 'flash drive' alopewa na Bryson akawa anatazama kazi yake humo.
Alichokuwa anafanya ni kuwianisha kati ya kazi hiyo na ile aliyoipokea toka kwa Dr. Lambert kuona kama zinarandana.
Taratibu alikula na taratibu akawa anapekua kazi.
Muda si mrefu, akabaini kazi ile haikuwa imetimia.
Takribani karatasi kama kumi na mbili hivi hazikuwapo!
Mapungufu hayo yalikuwa ni makubwa sana kiasi kwamba yalionekana kwa wepesi mno kwenye macho ya Mitchelle.
Akajiuliza, ina maana aliyezichapa hakufahamu upungufu huo?
Akaamini huenda alizichapa kwa haraka ili amletee upesi na amweleze shida yake, hapo akampigia simu Bryson kuhakiki wazo lake.
Akamuuliza kama kuna tatizo lilijiri katika uchapaji wa kazi, bwana huyo akamtoa shaka kuwa kila kitu kilienda sawa.
Alihakikisha hilo kabla hajaweka kazi hiyo kwenye flash drive.
Aliuliza,
"Kwani kuna tatizo?"
Mitchelle akamuuliza idadi ya karatasi zilizoandikwa, hapo Bryson akapatwa na kigugumizi. Alijitetea kuwa alizichapa kwa haraka hivyo hakupata wasaa wa kutazama idadi.
Mitchelle akakata simu.
Maelezo aliyoyapata yakamzalishia mashaka zaidi.
Aliwaza ...
Ina maana Bryson hakufanya kazi ile kwa mikono yake?
Alimpatia nani?
Mbona aliahidi hapo awali kuwa anafuata makubaliano waliyoyaweka?
Hamu ya chakula ikamwisha.
Alisikia damu ikimkimbia kwa kasi mwilini mwake.
"Uko sawa?" Jennifer akamuuliza akitumia mikono yake.
Alimsogelea karibu akimtazama kwa macho ya mashaka.
****
Na Steve B.S.M
Baada ya siku moja ...
Katika sehemu ya siri, majira ya jioni.
Jennifer akiwa amebebelea kikombe kidogo cha udongo kinachofuka moshi, aliufungua mlango mkubwa kukutana na kibaraza cha nje.
Kibaraza hiko kilikuwa kikubwa kwa wastani, kinaning'inia kwenye ghorofa hili, refu la hadhi ya kati.
Ghorofa lenye sakafu kadha wa kadha.
Kwenye kiti kikubwa cha mtindo, katika kibaraza hicho, alikuwa ameketi mwanamke maridadi, Mitchelle.
Mwanamke huyo alikuwa kavalia bukta fupi sana rangi ya manjano na blauzi nyeusi kwa juu. Nywele zake kazibana vema kwa nyuma, uso wake unang'azwa na miale dhaifu ya jua la jioni.
Alikuwa anatazama namna jua linavyozama. Alikuwa anapenda sana jambo hili. Alitulia hapo huku akiwa anatafakari mambo kadhaa kichwani.
Alipenda utulivu huu maana kichwani mwake kulikuwa na vurugu sana.
Pembeni ya kiti hicho kulikuwa na kijistuli kidogo cha kioo. Juu ya stuli hiyo kulikuwa na kijidaftari kidogo kilichofungwa, pembeni kidogo kalamu ndani ya mfuniko wake.
Jennifer akasogeza kijidaftari hiko na kuweka kikombe alichokuja nacho kisha akamkaribisha Mitchelle.
Alimwambia kwa lugha yake ya ishara,
"Nimeona nikutengenezee kahawa yako unayoipenda. Pengine itakupa 'mood' nzuri leo."
Mitchelle akanyanyua kikombe na kukitia mdomoni. Akanywa fundo moja ...
Aaaaahhh ... akajiskia vema. Ni kana kwamba mwili wake ulikuwa unangoja kitu hiki muda wote huo.
Alikunywa tena fundo la pili kisha la tatu ndipo akarejesha kikombe kwenye stuli.
"Ahsante sana, Jenny. Ulijuaje hiki ndo' kitu nahitaji kwa sasa?"
Jennifer akatabasamu kisha akamwambia namna gani anavyomfahamu, na mara zote anapomwona akiwa yuko chini basi humwinua kwa kahawa yake pendwa.
Mitchelle akatabasamu.
Jennifer akamwambia akitumia mikono yake,
"Kwa leo siku nzima ndo' nakuona ukitabasamu kwa mara ya kwanza. Kuna jambo linakutatiza?"
Akatazama kijidaftari kwenye stuli kisha akaongezea,
"Ni mambo yako ya biashara, sio?"
Mitchelle akashusha pumzi fupi kisha akajibebea kikombe chake cha kahawa. Badala ya kujibu, akanywa fundo la kahawa.
"Jipe muda wa kupumzika," Jennifer akaendelea kumuhasa. "Naamini kila jambo litakuwa sawa. Jana na juzi hujalala vema, hakikisha unapata usingizi leo."
Mitchelle akampatia uso wa kumuashiria amemwelewa lakini hakusema jambo na kinywa chake.
Aliendelea kutazama anga jekundu, jua sasa likiwa halionekani.
Jennifer akamtazama kwa kitambo kidogo kisha akakata shauri kwenda zake. Kabla hajafika popote, Jennifer akamuuliza,
"Umeshaniandalia zile nguo zangu za mtoko wa jioni?"
Jennifer akampa ishara kuwa tayari ashafanya vivyo alafu akaenda zake. Akabaki Mitchelle peke yake.
Peke yake katika utulivu aupendao.
Akafungua daftari lake mara moja na kuandika mambo kadhaa kisha akalifunga na kuendelea kunywa kahawa yake.
Kahawa ambayo alizidi kuipatia hamu kadiri anavyoitumia.
Hakuchukua muda mrefu, kahawa ikawa imeisha. Akamwita Jennifer amwongezee. Akiwa anangoja akapiga simu yake mara moja.
Jennifer akiwa anaandaa kahawa, akamsikia 'boss' wake akiwa anateta na simu. Sauti yake ilikuwa kali, anafoka kama mwehu.
Hata yeye akaogopa japo si mhusika.
Alipompeleka kahawa akamkuta akiwa amefura sana. Uso wake karibia wote umekuwa mwekundu.
Kwa hofu kubwa, akaweka chupa ya kahawa kwenye stuli, alafu akachoropoka upesi kwenda zake.
Hata Mitchelle hakumjali.
Alikuwa na mambo yake kichwani yanayomtinga. Mambo mengi kwelikweli.
Alikuwa anatazama daftari lake, akiandikaandika. Akikokotoa na kufunga hesabu.
Alisahau mpaka kahawa yake alomimina kwenye kikombe. Kahawa hiyo ikakaa mpaka ikapoa. Kahawa ilokuwepo kwenye chupa ndo' hakugusa kabisa.
Muda si mrefu alinyanyuka toka hapo akaenda kujiandaa. Baada ya muda mfupi akawa yumo ndani ya gari la kukodi, si 'Uber', akielekea kaskazini mwa eneo analoishi.
Alikuwa amevalia kawaida sana, si kama mtu mwenye mtoko mkubwa, hapa akiwa amejivesha blauzi na jeans tu.
Baada ya dakika kadhaa akawa amefika katika klabu moja ndogo, hapo akajiweka mahali palipotulia, muziki kwa mbali, akawa anakunywa taratibu wine kwa glasi.
Alimaliza glasi ya kwanza, ya pili ikiwa kati, bwana mmoja akaingia katika eneo hilo akiwa anaangazaangaza.
Bwana huyo alikuwa amevalia koti jeusi la ngozi, ndani tisheti nyepesi na chini jeans ikiambatana na raba nyeupe.
Bwana huyo alikuwa ni Bryson.
Alipoangaza upande wake wa kuume, Mitchelle akampungia mkono kumwita. Alisogea hapo na muda si mrefu akaja mhudumu kumsikiliza.
Akaagiza kinywaji laini ambacho hakikuchukua muda kufika. Glasi nyembamba yenye mrija mrefu wa kuvutia.
"Umekuja na kazi yangu?" Mitchelle akauliza.
"Ndio " Bryson akatoa flash kwenye koti lake na kumpatia Mitchelle.
"Ajabu," Mitchelle akasema akitazama flash hiyo, "kazi hii umeifanya kwa upesi sana. Ni kwasababu ya shida yako ama kuna kingine?"
Bryson akatabasamu. Tabasamu lake lilijieleza kuwa hiyo ndo' sababu ... Akanywa fundo moja la kinywaji chake kisha akaelezea ni namna gani alivyokuwa ana uhitaji wa kuonana naye.
Alisema,
"Unajua ni namna gani ilivyo ngumu kuonana na wewe. Niliamini nikifanya kazi hii nikaimaliza kwa haraka basi itakuwa rahisi kukushawishi."
Mitchelle akamtazama bwana huyo kwa macho ya udadisi. Akanywa fundo moja la wine yake alafu akamuuliza akiwa anaendelea kumtazama ... macho ya kupembua,
"Unataka nini, Bryson?"
Bryson kwanza akatulia. Alikuwa anayapanga mambo yake kichwani ... Alitafakari mambo yanayomkabili japo kwa muhtasari kisha akafunguka haja yake.
Alieleza namna gani alivyokuwa na uhitaji mkubwa wa pesa kwani watoto wake wanatakiwa kufanya upasuaji.
Akiwa anaeleza hayo, macho yake yalilenga kwa machozi. Na Mitchelle akajua namna gani bwana huyu alivyokuwa na shida haswa.
Asiseme kitu, akaagiza kinywaji kingine alafu akaulaza mgongo wake kitini.
Kwa ukimya huu wa sekunde chache, muziki laini uliokuwa unapiga hapa ukatawala.
Wimbo wa 'Stuck on You' wa Lionel Richie ulishika hatamu watu wakijifurahisha na vinywaji vyao, wengine wakiimba na wengine wakitikisa miili yao taratibu kuitikia wimbo huo mwanana.
Kwa muda huo Mitchelle, kama kobe aliyejificha ndani ya gamba lake, alikuwa anatunga sheria kichwani.
Kinywaji kilipowasili, akanywa kwanza mafundo mawili alafu ndo' akarejea katika mjadala huu.
Alisema,
"Bryson, pesa kubwa kama hiyo lazima iambatane na makubaliano. Nadhani utakubaliana na mimi katika hilo."
Bryson akasema,
"Bila shaka. Nipo tayari kwa makubaliano yoyote yale alimradi nisaidie watoto wangu."
Mitchelle akatabasamu.
Tabasamu dogo.
Kisha akasema,
"Ok, lakini huenda kuna jambo natakiwa kukusisitizia zaidi, Bryson. Mimi ni mtu 'strict' sana kwenye maagano ninayoyaweka.
Huwa sipindishi wala kupunguza kile ambacho ninaweka nacho maagano, na huo ndo' udhaifu wangu mkubwa. Hivyo nakusihi sana, kuwa makini unapofunga makubaliano na mimi."
Alipofikia hapo, akamkumbusha Bryson makubaliano waliyoyaweka hapo kabla. Alimuuliza kama bado anayaishi makubaliano hayo, naye Bryson akaapa kuwa kila kitu kipo kama vile walivyokubaliana.
"Usiwe na hofu kabisa," alimtoa shaka. "Nasimamia kila tulichokubaliana."
Akiwa anasema haya, akajikuta moyo wake unaenda kasi.
Aliyakumbuka yale mazingira aloyakuta kule kwa Hilda akajikuta anajikaza tu. Alijipa matumaini huenda hamna cha ajabu cha kuhofia kiasi hiko, lakini ... Vipi kama ... Basi tu ...
Aliomba kila jambo liwe kama vile anavyotaraji. Aliupiga moyo wake konde.
Asingeweza kuacha pesa hizi kwani alikuwa ana uhitaji mno.
"Sawa," akasema Mitchelle, "sasa nikuambie maagano yangu kama utayaridhia."
Bryson akasema,
"Niko tayari."
Basi Mitchelle akamweleza yake anayoyataka. Alichukua kama dakika nne kueleza kila agano. Alipomaliza akamwambia Bryson kuwa pesa itaingizwa kesho yake majira ya asubuhi katika akaunti ya benki.
Bryson akafurahi kweli. Hakuamini macho yake.
Alijiona mshindi wa kila vita.
Hakujali makubaliano aliyoyaweka ni makubwa kiasi gani bali ukubwa wa furaha ya kuokoa uhai wa wanae.
Aliondoka hapo akiwa na tabasamu usoni, na alipofika tu nje akampigia simu mkewe kumpatia habari hizi njema.
Naye mkewe akafurahi sana kwani sasa tumaini lilishuka.
Upesi wakatoa taarifa kwenye uongozi wa hospitali na maandalizi ya upasuaji ya watoto wote wawili yakaanza mara moja.
Mama akajawa na tabasamu.
Lakini hakumuuliza mumewe ni maagano gani aliweka kupata pesa hiyo kubwa ... Pengine hilo halikuwa na umuhimu kwake kwa wakati huo.
Cha muhimu ni kuokoa watoto.
Ndani ya klabu Mitchelle, akiwa sasa peke yake, akaagiza tena kinywaji, akaendelea kunywa taratibu akikoshwa na muziki kwa mbali.
Alitazama saa yake, ilikuwa ni saa mbili ya usiku, akaona aendelee kuuvuta muda hapo akingojea saa tatu ifike.
Muda huo alikuwa na ahadi nyingine, hivyo hapa alikuwa na kama lisaa limoja la kukaa. Akautumia muda huo kunywa na huku akitafakari mambo yake ya pesa.
Alinyanyua simu yake akampigia Taiwan, simu ikaita na kupokelewa ndani ya muda mfupi.
Akasema,
"Nitakuja mwenyewe kwenye mnada."
Taiwan akaita,
"Naam!"
Mitchelle akarudia taarifa yake kwamba atahudhuria mwenyewe kwenye mnada.
Taiwan akauliza,
"Ma'am, kuna haja ya wewe kuja huku? Au ni kwasababu ya kudorora kwa biashara hapa karibuni? ... Usijali, nitasimamia kila jambo na kila kitu kitakuwa poa si muda mrefu."
Mitchelle akamwambia kuwa hili jambo atalisimamia yeye. Anataka iwe hivyo.
Aliposema hayo akakata simu.
----
Ni jambo gani Mitchelle amejadiliana na kukubaliana na Bryson?
Shaka la Bryson kwenye usiri wa Hilda litaishia wapi?
Ni mnada gani Mitchelle anataraji kuhudhuria?
Na miadi yake ya saa tatu usiku ni kukutana na nani?
***
Saa nane usiku ...
Mitchelle alipotoka bafuni alikuta kila kitu kikiwa kimeandaliwa mezani, pamoja pia na tarakilishi yake.
Ulikuwa ni usiku mkubwa lakini tayari Jennifer alishafanya kazi yake.
Punde tu Mitchelle aliporejea, aliamka akatimiza wajibu wake huo na sasa alikuwa pembeni akingoja kupakua na kuanua vyombo.
Macho yake yalikuwa mekundu, ameelemewa na usingizi. Japo Mitchelle alimsihi akapumzike lakini bado aliona ni kheri kuwapo hapa.
Alimpakulia Mitchelle chakula chepesi alichokiandaa, supu na 'bites', kisha akaketi kungoja. Mitchelle akawa anakula huku akipapasa tarakilishi yake.
Alichomeka 'flash drive' alopewa na Bryson akawa anatazama kazi yake humo.
Alichokuwa anafanya ni kuwianisha kati ya kazi hiyo na ile aliyoipokea toka kwa Dr. Lambert kuona kama zinarandana.
Taratibu alikula na taratibu akawa anapekua kazi.
Muda si mrefu, akabaini kazi ile haikuwa imetimia.
Takribani karatasi kama kumi na mbili hivi hazikuwapo!
Mapungufu hayo yalikuwa ni makubwa sana kiasi kwamba yalionekana kwa wepesi mno kwenye macho ya Mitchelle.
Akajiuliza, ina maana aliyezichapa hakufahamu upungufu huo?
Akaamini huenda alizichapa kwa haraka ili amletee upesi na amweleze shida yake, hapo akampigia simu Bryson kuhakiki wazo lake.
Akamuuliza kama kuna tatizo lilijiri katika uchapaji wa kazi, bwana huyo akamtoa shaka kuwa kila kitu kilienda sawa.
Alihakikisha hilo kabla hajaweka kazi hiyo kwenye flash drive.
Aliuliza,
"Kwani kuna tatizo?"
Mitchelle akamuuliza idadi ya karatasi zilizoandikwa, hapo Bryson akapatwa na kigugumizi. Alijitetea kuwa alizichapa kwa haraka hivyo hakupata wasaa wa kutazama idadi.
Mitchelle akakata simu.
Maelezo aliyoyapata yakamzalishia mashaka zaidi.
Aliwaza ...
Ina maana Bryson hakufanya kazi ile kwa mikono yake?
Alimpatia nani?
Mbona aliahidi hapo awali kuwa anafuata makubaliano waliyoyaweka?
Hamu ya chakula ikamwisha.
Alisikia damu ikimkimbia kwa kasi mwilini mwake.
"Uko sawa?" Jennifer akamuuliza akitumia mikono yake.
Alimsogelea karibu akimtazama kwa macho ya mashaka.
****