Tukichana na keyboard warriors, Watanganyika tuna mtu yupi wa uhakika anaeweza kutupigania tuwe na Tanganyika yetu?

Tukichana na keyboard warriors, Watanganyika tuna mtu yupi wa uhakika anaeweza kutupigania tuwe na Tanganyika yetu?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Niite utakavyo lakini nachokiona kwa mwacho yangu kwa sasa huu muungano gia zimebadilika angani, Alieuanzisha na kuusimamia kwa kiasi kikubwa kashatutoka na kwa sasa gia zimebdailika na kibao kimewageukia Tanganyika, Tanganyika inakamuliwa vibaya mno aisee japo kwa wazanzibari malalamiko yao ni sawa na mtu alie na maji mengi ila kikombe kimemkinai anataka mrija.

Kwa sasa hivi mambo mengi yamebadilika sana, Mashuti tunayofumuliwa ndani ya box kwa kisingizo cha muungano ni mazito mno, gloves za kudakia zimefuaa na maumivu yameanza kuwa makali,

Zanzibar inaingia zaidi ya mara 350 ili iwe na ukubwa wa Tanganyika lakini uwiano wake wa manufaa anayopata unaona wazi kabisa Tanganyika inabinuliwa.
 
Achana na mawazo mgando..!! Dhambi ya Ubaguzi ni mbaya Sana..mkashakua watanganyika mataanza tena wakusini na wakanda ya ziwa etc
 
Achana na mawazo mgando..!! Dhambi ya Ubaguzi ni mbaya Sana..mkashakua watanganyika mataanza tena wakusini na wakanda ya ziwa etc
Mbona wewe umewabagua wakenya Na Wakanda?? Kwanini hujalazimisha yote iwe Tanzania?
 
Kwa sasa hivi hakuna hata mmoja iwe mtanganyika au mwingine yoyote anaweza kulizungumzia hilo kinagaubaga.

Kiti pekee kitakacho wezesha kurudi kwa tanganyika ni nyakati, hakuna yoyote aliweza kuushinda wakati, so wakati ukifika hilo litatokea, na haupo mbali sana japo sio karibu, itagharimu walao kizazi kimoja.
 
Ni kweli tunahitaji sana tanganyika ipi siku wazanzibar wataiteta tanganyika

Tukumbuke wazanzibar toka muungano huu usio kuwa na faida uanze wanakiongozi ikulu anayeitwa makamu wa Rais
 
Watazania bara wanawawikilishi wao ambao ni wabunge kazi yao kubwa ni kulinda masalhi mapana ya Tanzania bara siyo kupinga usingizi.....ila Muungano ni jambo jema kuuimarisha na kuudumisha
 
Achana na mawazo mgando..!! Dhambi ya Ubaguzi ni mbaya Sana..mkashakua watanganyika mataanza tena wakusini na wakanda ya ziwa etc
Mbona alijaribu Mch. Mtikila akakosa wa kumuunga mkono?
Wenye uwezo huo wapo sana tu, tatizo ni sisi wanachi, wakijaribu wanabaki peke yao.

Tundu Lisu kapambana wee akaishia kumiminiwa risasi,akabaki peke yake anaugulia maumivu na familia yake.

Wananchi wakijitambua ni rahisi sana. Hata Hayati Seif Shariff alipata ujasiri kwa sababu alikuwa na watu nyuma yake.

Raila wa Kenya leo anagombea urais kwa kupigiwa debe na Rais aliyeko madarakani,unafikiri Uhuru alikuwa anampenda Raila? No!! Raila ana watu nyuma yake,chochote akiwaambia wafanye watafanya.

Aliwaambia anataka kuapishwa kuwa Rais wa wananchi,kitu ambacho ni uhaini na Mwanasheria mkuu wa wakati Profesa Muigae,alionya kwamba Raila anachofanya ni highest treason. Raila hakujali sababu alikuwa na watu.

Ukipata watu umepata uthubutu wa kufanya chochote.
 
Viongozi wetu wamefanikiwa kututisha kuwa wao ni Miungu watu jambo ambalo halina ukweli wowote.

Yaani Ubunge,uwaziri, na vyeo vingine wote hao ni watumishi wa wananchi lakini kilichopo ni kinyume chake.

Watu wanataka kuabudiwa na kusifiwa kwa nafasi zao.
 
Back
Top Bottom