Tukidhani ni Binadamu wenzetu, kumbe ni mashetani! Mtu unaombeaje mwenzako afe kwa Corona? Can't believe this wickedness! Huu sio utu, ni ushetani!

Tukidhani ni Binadamu wenzetu, kumbe ni mashetani! Mtu unaombeaje mwenzako afe kwa Corona? Can't believe this wickedness! Huu sio utu, ni ushetani!

Mimi siombei mtu kifo, ila namkumbusha tu huyo bwana kuwa kuna watu walisimama mstari wa mbele kuitetea Tanzania walirudi wakiwa vipofu wengine,
Nyuzi nyingi zinazohusu siasa mara nyingi umekuwa upande wa kutetea serikali na ni jambo zuri. Lakini mazuri kwa unayempenda ni kumuweka kwenye mstari wa sawa ikiwa kama anakosea. Mifumo inaongozwa na watu na asili ya sisi watu ni mapungufu.

Serikali yetu kwa miaka imekuwa ikifanya madhaifu mengi tena ya waziwazi ambayo ni yenye madhara kwa raia mmoja mmoja, mengine kwa wote na yana athiri nchi kwa ujumla. Suala la uchama liweke kando kwa sababu binafsi si mfuasi wa chama chochote bali mafungamano yangu ni kujitahidi kuishi kwa kadri niwezavyo kwa kuyaendea yale ambayo Mungu ametutaka tuyatende.

Nakuusia ndugu yangu pamoja na kuiusia nafsi yangu, ukiona heri limefanywa na yoyote lifurahie na lipongeze! Ukiona shari immefanywa na yoyote usione haya kukiri na kutafuta njia bora ya kulitengeneza liwe zuri, imma kwa kumwambia aliyekosea kuwa hapo umekosea! Akilifuata ni yeye na akiliacha ni yeye. Wewe hauna dhima tena kwani umeshfikisha kilichotakikana.

Kumbuka wa-Tanzania tupo takribani millioni 50. Ikiwa kama kiongozi akifanya dhulma kwa wa-Tz asifikiri kwamba amefanya dhulma kwa nchi! Bali amefanya dhulma kwa watu millioni 50. Na yeyote atakayeiunga mkono hiyo dhulma naye yumo kwa kuwadhulumu watu millioni 50. Sasa ndugu unamema kiasi gani cha kufidia idadi ya watu millioni 50? Ikiwa kama wamefanya dhulma x10 na wewe ukai support zidisha mill 50*10... Ila ni vipi hayo ikiwa unayafanya kwa heri? Tumuogope na tumukhofu Mungu! Mungu anatisha jamani! Haya mambo ya kidunia yasitupumbaze!

Mungu atuongoze kwenye kheri.
 
Vipi kuhusu yule aliyewafananisha watanzania wenzake na corona, yeye mbona ulikaa kimya
Ndiyo unafiki wenyewe Mkuu. Wanafikiri matatizo wameumbiwa wengine. Sasa kwanini watu wasifurahi pale Mungu wao anapowaadhibu maadui zao??

Kuna matatizo ya kutengenezwa na binadamu kwa mwenziye. Mf Yaliyomkuta Mh Lissu sote tunafahamu. Sasa inapotokea watesi wake wamepatwa na corona kisha wakadanja unategemea wafuasi wake watasikitika au watashangilia na kumtukuza Mungu wao kwa kujibu maombi yao??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mshahara za dhambi mauti bali karama la Mungu ni uzima wa milele!! Pasco nimewahi kuandika kwenye moja ya mabandiko yako kuwa utawala wa awamu ya tano umejenga chuki ya kiasi kisichomithirika miongoni mwa watanzania! watu wa Mungu tunatakiwa kuwatatkia watu mema hata wanaotuudhi lakini inahitaji moyo wa neema kuishi katika level hiyo!

hawa wanaoombea wengine wafe ni wale ambao wanajihisi kuwa helpless chini ya utawala huu wa mkono wa chuma lakini kwa upande mwingine kuna kundi ambalo kila siku wanasondeka watu ndani kwa kesi za ajabu ajabu, wanawapoteza watanzania wenzao au kuwaiga risasi kwamba yeyote mwenye mtazamo tofauti na wao huyo ni wa kufa kupotea au kuozea jela kwa kifupi chi yetu sasa ina hayo makundi mawili na kama hatutapa kiongozi mfariji wa kuturudisha pamoja kuna suala zima la ukabila pia linakuwa kwa kasi sana!
 
Ukweli ni kwamba taarifa zilizokuwa zinztolewa hazikuwa sahihi, (Ummy Mwalimu anajua), kwa hiyo kusema eti kuna award tunataraji ni uzwazwa wako tu, ilibashiriwa kwamba walikuwa wanajaribu kuficha ukweli ili kujidanganya kwamba maambukizi yako chini tanzania, ni ujinga kuficha jambo ambalo liko wazi, tunapima kizembe, tunaficha taarifa halafu watu wakisema wana hofu na taarifa hizo za kupikwa wanakamatwa na jeshi la polisi, endelea kuwapumbaza hao viongozi wenu uchwara muone mwisho wake
Kama zilikua ni za kupikwa jamii forums ni jukwaa huru na hata majina tunayotumia humu ni BANDIA hebu tupe takwimu za kweli zinasemaje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengine Hawa apa wamepewa kazi ya kuzka watu wanao kufa kwa Corona kina MBOWE utasema wanawazia matako Yan mtu et serekal inaficha ila wao wanajua sababu wao ndio wanazika IV mbowe mtaacha siasa Lin na kudanganya watu ao watanzania wanao kufa kwa ma mia wako wap? Na mliwazikia wap

Sent using Jamii Forums mobile app
Unataka kusema nini ndugu? Tuliza akili ndio uandike ujumbe wako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Paskali navyojua mimi wewe ni mhandishi huru,sio mfanyakazi wa serikali hii ya Magufuli. Kwa hiyo sio msemaji wa serikali hii.Wasemaji wapo.

Wacha serikali ijitetee yenyewe.Kwani ndio inawajibika kwa wananchi.sio wewe. Sana sana wewe ungedai transparency katika hilo swala la Corona.

As pressman ungedai press conference na vigogo wa serikali at least twice a day.
Unaona Free world jinsi press inavyo wahenyesha watawala na mabingwa wa tiba.
Hawa unaowatetea sio masultani,tumewaandika kazi WATUTUMIKIE si vinginevyo.

Wanaposhindwa kulitambua hilo wanapoteza sifa za uongozi.Sijui kwanini wasianzie kusotea uongozi Kivukoni ili wajue majukumu na miiko ya uongozi ni nini?
 
Ukiona hivyo utajiri wako ni wa mashaka na ni mla rushwa mkubwa hakuna mwenye kipato kizuri akalipa kodi ya halali na kujikomba kunifanya mdau wa serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiyo rushwa nimeanza kula lini,...Mimi bado kijana rika la kawaida tu..,sifanyi kazi hata huko serikalini...ni mdau wa serikali;namaanisha nina sapoti serikali iliyo madarakani,si chama..,ni tabia yangu toka utotoni...serikali yoyote ile hata chama gani kikiingia madarakani ntasapoti tu,japo maovu ntayakemea.
 
Si afadhali hata hao wanaoombea wengine wapate au wafe kwa covid19. Vipi wale ambao kwa kiburi chao cha madaraka, sasa watu wanapoteza maisha kwa hiyo hiyo corona? Tuwape jina gani?
 
UKIONA HIVYO JUA KUNA CHANZO.
Bashite na pole pole walitoa matamko yasiyostahili kutolewa na kiongozi wa ngazi zao.Hukukemea wala kulalamika!
Wamesemwa hao "viongozi" tegemewa(kwa mtazamo wako) unaona tatizo. Hao si Mungu na hata wakiondoka (kwa corona au vifo vingine) maisha yataendelea na watasahaulika kama binadamu wengine! Hakuna mwenye roho ya thamani mara 2 au zaidi ya mwingine. Kila mmoja ashinde mechi zake.
Hata Levy Mwanawasa alikufa akiwa madarakani na Zambia ipo inaendelea. Wao sio Mungu kwamba wakifa na nchi inakufa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanabodi,

Mtu unachokiandika, ndicho unacho kiwaza!, kuna watu, tunaishi nao, tunakula nao, tunalala nao, tukidhani ni binaadamu wenzetu, kumbe ni machoni tuu ndio kama watu, lakini mioyoni ni mashetani wakubwa!. Mtu unaombeaje binaadamu mwenzako afe kwa Corona?!. Can't believe this wickedness imewakuta Watanzania wenzetu!. Huu sio utu, sio ubinaadamu, ni ushetani!

Unaweza usiamini hili ninaloandika hapa lakini ni kweli kabisa, wakati dunia ikihangaika na janga la ugonjwa wa Corona linaliitesa dunia nzima tukiwepo sisi Tanzania, kuna baadhi ya wenzetu humu mitandaoni utu na ubinaadamu umewatoka wamekuwa sio watu tena, sio binaadam bali ni mashetani kwa kuombea wenzao sio tuu wapate Corona, bali wapate Corona na wafe kwa vifo vya Corona!.

Hili nimelishuhudia humu jf na mitandao mingine baadhi ya wenzetu waki andika ku wish wenzao wapate Corona na wafe kwa Corona kwa wengine kuwataja kabisa kwa majina mimi nikiwa ni mmoja wao na wengine kuwataja kwa majina ya utani au hata bila kutaji jina ula unajua ni nani!.

Lengo la bandiko hili sio mimi kulalamika kuwa kuna watu wananitaka nipate Corona, kwasababu mimi ni nobody, hata nikichomoka na Corona, it's only my wife, my kids na my family ndio wata suffer, bali kuna watu very wicked wana wish viongozi wetu fulani fulani wafe kwa Corona, kutokana na positions za hao viongozi, ikitokea kweli wakachomoka kwa Corona, taifa tuta suffer kwa kupigwa na double tragedy!.

Mimi ni miongoni mwa Watanzania wenye uwezo wa kitu kinachoitwa graphology ni uwezo wa kusoma maandishi ya watu, kisha ukabaini mwandishi alimdhamiria nini, hata akiandika neno "bora tuu afe kwa Corona ", bila kumtaja ni nani, kupitia graphology unajua ni nani alidhamiriwa afe!, japo huyo mwandishi anaweza kuwa hakuandika kwa kumtaja jina expressly kuwa nataka fulani afe kwa Corona, lakini kupitia uwezo huo wa graphology, then unatambua impliedly aliyedhamiriwa ni nani!.

To wish someone specific afe kwa Corona ni highest stages of wickedness, Watanzania siku zote ni watu wenye upendo, tunapendana na tunawapenda viongozi wetu, na hata chama chetu japo tunakilalamikia sana humu mitandaoni kuwa ndicho chanzo cha umasikini na madhila yote yanayolikuta taifa letu, lakini in reality, tunakipenda sana na kila mwaka huwa tunakichagua tena na tena mwaka hadi mwaka, na kama janga la Corona halitadumu muda mrefu na kuleta madhara makubwa, then mwezi October, 2020, tunakichagua tena, sasa iweje binadamu wenzetu, Watanzania wenzetu kuingiwa na roho ya ushetani wa ajabu kwa kuwa na wishful thinking ya kuombea viongozi wetu fulani fulani tegemewa, wafe kwa Corona?!.

Ajabu kubwa zaidi ni idadi ya members watakao toa likes kwa huyo mtu, inaonyesha jinsi tulivyo na kundi kubwa Watanzania wenzetu ambao ni wicked kwa kusupport hizo wicked ideas!, na kipimo rahisi kwa mashetani hawa, utakiona kwenye uchangiaji kwenye hili bandiko.

Swali la kujiuliza hivi ni kweli Watanzania watu tuliiokuwa na upendo wa ajabu zaidi hata ya upendo wa mshumaa, wa kumulikia wengine huku kwako unateketea, sasa tumefika hapa kuombeana vifo vya Corona?. Huu ni utu, ni Ubinaadamu au ni ushetani wa ajabu?.

Hivi kweli sisi Watanzania tumefikia stage ya kuishi na binadamu wenzetu wenye mawazo ya kishetani kama haya halafu tunaishi nao tukiendelea kula nao, kunywa nao na kulala nao na wengine hadi tunawapongeza!, hivi ushetani huu unatofauti yoyote na ule ushetani wa Sodoma na Gomorrah?!.

Ingekuwa kila kitu mtu anachokiwaza kinaandikwa kwenye paji la uso wake, hivyo nikikuambia ufunge macho na kuwish ulitaka mtu gani afe kwa Corona, amini usiamini, watu tungekuwa surprised kukuta mke ana wish mume ndio afe, mume ana wish mke ndio afe na nikiuliza ungewish kiongozi gani afe kwa Corona, majibu yangekuwa yanaandikwa usoni!, watu mngeshanga na ungeweza usiamini!.

Tiba Nambari One Duniani ni Imani, yaani faith, kwa janga kama la Corona ili liishe na lisilete madhara makubwa na maafa kwa Tanzania na duniani kwa ujumla, ni kama Watanzania na watu wote, ikiwa wote tuta wish kwa dhati ya mioyo yetu kumuomba Mungu kwa dhati, alipishie mbali, hili janga la Corona, lakini kitendo cha wengine tunasali, na kumuomba Mungu atuepushe na janga la Corona, huku kuna wenzetu wengine wao waki wish fulani apate Corona afe, kunapunguza nguvu ya sala zetu, huu sio Ubinaadamu, sio utu, ni ushetani!.

Hala hala kwa mashetani hawa, ingekuwa dua ls kuku linampata mwewe, saa hizi siku nyingi kuna watu tungekuwa ni historia, lakini Mungu sio Athumani, kila mtu atakufa siku yake Mungu aliyompangia tena kwa kifo kile kile mtu ulichopangiwa, kama mtu umepangiwa kufa kwa Corona, utakufa tuu kwa Corona and no one can do anything kuzuia, ili kitendo cha mtu kumwish mtu fulani afe kwa Corona, sheria ya karma my act kwa kanuni ya what goes around, comes around, wakati uki wish fulani afe kwa Corona, karma may act upon you na ku reverse your wishes on opposite directions, hiyo wish ikakurudia wewe na familia yako!.
Tupendane wandugu, na tuwishiane mema!.

Mungu Ibariki Tanzania
Mungu wasamehe Watanzania wenzetu waliomkaribisha shetani ndani yao na umtume Roho Mtakatifu wako, awasafishe na kuwatakasa with their evil thoughts and wickedness na kuliepusha taifa letu na janga la Corona.

Amen.

Paskali
Jiulize nini kimetufikisha hapo?? Kwakweli hata mimi natamani watu fulani ianze nao kwanza. Sema ni vile tu haichagui.
 
Hili jambo nimeliona sana humu...Achana na hilo, kuna wengine hata nyuzi za tanzia wanaonekana kufurahia....limenistaajabisha sana hili.
Wameumizwa mioyo na kujeruhiwa miili na nafsi ko watesi wao wakitembea mbele kwa covid nao watapumua na kupata ahueni maana haingii akilini mtu anakutesa afu uache kumuombea mabaya ili atoweke na wewe upate nafuu
 
Back
Top Bottom