Tukifanya haya tunaweza tusihangaike na tozo za benki

Tukifanya haya tunaweza tusihangaike na tozo za benki

bulabo

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2015
Posts
628
Reaction score
780
NAWAZA kivingine. Haya ni mawazo tu namna tunaweza kutoka hapa tulipo kama nchi na mama hii kitu inamharibia sana wananchi walianza kumpenda sasa wanalia na tozo.
  1. Boresha Bandari yako, Punguza ushuru wa Magari ya kuanzia mwaka 2013-2018 watu wataagiza wengi na serikali itapata hela nyingi.
  2. Jenga Viwanda vingi kwa kutafuta wawekezaji wengi kwa sbb tayari raw material nchi hii tunayo ya kutosha utapata kodi nyingi
  3. Punguza misafara isiyo ya lazima. Ukiwa na ziara nenda na watu wachache tu
  4. Badilisha mfumo wa kununua magari. Magari kama V8 yawe kwa Waziri Mkuu tu Mawaziri Wakuu wa Mikoa na Viongozi wote Serikalini wanunulie VANGUARD zinawatosha
  5. Punguza Safari za Nje, Tumia Mabalozi, Safari za nje safiri zile tu mnaenda kuweka Mikataba. Mikutano Mtume Waziri mkuu hana msafara mkubwa
  6. Punguza Warsha Serikalini ambazo sio za Lazima
  7. Wekeza kwenye tehama kila kazi serikali ziwe kwenye mfumo
  8. Punguza baraza la mawaziri liwe dogo. Naibu Waziri na Naibu katibu hawana kazi
  9. Punguza Idadi ya Wabunge bungeni
  10. Ongeza UShuru kwenye Bia ni starehe watu hawanywi kila siku
  11. Safirisha Mizigo kupitia reli badala ya barabara
  12. Tutengeneze PikPiki na Bajaji tuuze kwa nchi majirani ni technolojia rahisi
  13. Uza Nyama Nje ya Nchi
  14. Uza Maziwa Nje ya Nchi
  15. Ondoa Mikutano ya chama peleke pesa vuta mabomba ya maji kutoka Ziwa Tanganyika kuja miko yenye shida ya maji na ziwa Victoria.
  16. Jenga Kutumia FORCE ACCOUNT tumia JKT
Mama sio kwamba ana nia mbaya na sisi ila yawezekana washauri wake japo na yeye anatakiwa kuchuja.

Tanzania Naipenda.
 
Hakuna linalotekelezeka hapo kwa hawa wanasiasa wetu waliolewa madaraka mpaka kupitiza.
 
Tusisahau hawa tunaowashauri ama muda mwingine kuwalaumu hatuishi nao Tanzania moja, unaweza ukamuuliza hata nauli ya daladala kutoka tegeta hadi posta akakujibu amesahau.
 
Tulia mama aifungue nchi,Magufuli alikuwa dikteta sana na alituchelewesha sana kupata maendeleo.Alisikika chawa mmoja mpumbavu hivi.
 
Tuweke msisitizo kwenye kilimo,ni aibu nchi yetu kuagiza ngano na mafuta kutoka nje...wakati maeneo makubwa ya nchi yetu ni mapori.
 
Mama sio kwamba ana nia mbaya na sisi ila yawezekana washauri wake japo na yeye anatakiwa kuchuja.
Tatizo 'walamba asali".

Hangaya alipowaruhusu wale kwa urefu wa kamba hapo ndipo tatizo lilipoanzia.
Na wameshamjulia kwa udhaifu wake uko kwenye kutaka kusifiwa....kila siku sifa sifa sifa
Na yeye akisifiwa anajisahau kabisa na kushindwa kusimamia kama raisi wa nchi kwenye mambo ya msingi.
 
Haya yanaweza kufikiriwa na hata kutekelezwa kwa kiasi fulani na watawala wanaojua kuwepo kwao madarakani kunategemea uamuzi wa wananchi katika chaguzi na michakato ya kibunge.

SIO kwa hawa wenye guarantee ya kuwa madarakani kwa utashi wao hata wafanye nini. Chawa wao tayari wameshajibu kwa kupuuza. Rais wa Tanzania ni mungu mtu. Ikidaiwa katiba mpya watu wanapuuza kuwa ni mahitaji ya kina Mbowe na Lissu. CCM ikikosolewa wanadai upinzani ndio ovyo kabisa bora tubaki na CCM. Wanafikiri upinzani daima ni Mbowe, Lissu, Zitto, Lema ….

Hawajui kuwa hata haya Malalamiko kuhusu tozo ndio upinzani wenyewe! Alichofanya Ndugai majuzi ndio upinzani wenyewe! Alifukuzwa kwa kuwa katiba ya sasa inampa nguvu zote Rais juu ya kila mhimili, taasisi na watanzania wote. - Haletewi vichokochoko - ni mhimili uliojichimbia chini zaidi! Deep state! All that sht! You can’t have your cake and eat it! Mbowe & co will fade away one day lakini sauti za upinzani zitaendelea kuwepo kwa kadiri maisha ya watanzania yanavyozidi kuathirika na maamuzi ya ovyo. Watanzania waache huu ujinga wa kukumbatia CCM kama ilivyo halafu wategemee maendeleo na kusikilizwa na watawala. Urais wa Tanzania ni mtamu sana. Bila kutikiswa tutaendelea na matukio yasivyo na tamati.
 
Vyanzo vya mapato... Mikopo ya nje, misaada na tozo ... Inafurikisha fuko la hazina... Hata hivyo halijai Lina matobo... Yasipozibwa hata uwe na vyanzo vingine lukuki ni Bure... Ipo shida kubwa ...!
 
Yaani uache tozo n.k uangaike na huu mlolongo unaohitaji akili thubutu. Haya yafanyie wewe kazi sisi tunalula nyuma ya ma great thinker kama mabenki, makampuni ya simu, makampuni ya mawasiliano n.k.
 
Weeee Nchii haiwezi kufanya hayo.

Uchumi wa nchi hii unategemea kuwanyonya wananchi tu kupitia tozo na kodi.

Ni TOZO TU ndicho wanachojua sio Miradi wala uwekezaji wowote. [emoji23]
 
Yapo mambo yanayotekelezeka na mengine ni imaginary zaidi na wala hayaongezi chochote zaidi sana yata deplete hata akiba yetu ya fedha za kigeni. Ungekuwa una taaluma ya uchumi tungefanya mjadala lkn kama huna taaluma hiyo tutakuwa tunabishana tu. Mfano kupunguza warsha usidhani kuna positive implications tu kwenye uchumi bali kuna negative implications pia ambazo impact inaenda athiri mambo mengi yanayomgusa mwananchi wa kawaida.
 
Back
Top Bottom