Tukimbilie wapi? Mtetezi wetu CHADEMA amekaa kimya!

Tukimbilie wapi? Mtetezi wetu CHADEMA amekaa kimya!

Chadema wako walikokuwa wanataka kufika so no need to blame them. Wako kwenye kilele cha buyu la asali ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚

Ni muda wako wewe na wenzio mnaaona hali sio nzuri upande wenu muingie mstari wa mbele kupinga udhalimu na kupaza sauti. Tuko nyuma yenu mkuu.
Wakiitwa kwenye maandamano hawatoki wanataka CHADEMA wafanyaje?
 
Huu utegemezi uliopitiliza kwa Chadema sasa ndio umezidi kunifungua macho, tuliwaegemea viongozi wa Chadema kwa kiasi kikubwa sana wawe wasemaji wetu, huku sisi tukibaki nyuma na kuwaacha wao mstari wa mbele.

Matokeo yake tumedumaa, Chadema wakiwa kimya hatujui cha kufanya, na bahati mbaya wakati mwingine hata Chadema wakituambia nini tufanye, bado hatufanyi, tuliwaacha wakazoeleka wazungumzaji wa kila siku kwa press zao.

Muhimu tu tutambue, press bila vitendo ni bure, sasa ni wakati wa kila mmoja wetu kutimiza jukumu lake, kama kweli mnawapenda Chadema wasiachwe peke yao kufanya kila kitu, mabadiliko yanaanzia hapo ulipo.
Exactly, watanzania tumekuwa dormant mno. Wote tu wajinga, I am sorry to say so! Chadema wamejitoa mhanga Sana kuitetea Umma wetu, lkn tupo tupo tu
 
Mkuu kuwa neutral tu kama mimi.

Wenzako wako field wewe unataka matamko ili upate cha kuandika huku mitandaoni.

Yani ni kama Chadema wanafurahi sisi wananchi tunavyopata shida ya hayo yote uliyoyataja maana shida zetu zinawasaidia wao kujijenga.
Huu ndio ukweli mchungu Ni Bora kubaki njia kuu kuwa neutral...

Upinzani umeshindwa kutuletea mageuzi kabisa ..Ni Kama vile wanapiga mahesabu ya 2025...

Kipindi ilisemwa jiwe amebana Kila Kona haya Sasa kimewakwamisha Nini...

Kuiachia Ccm itufanye wananchi inachotaka Ni dhulma kubwa Sana....

Mimi kwa hesabu zangu mbovu naona Top leaders washapenyezewa Asali...
 
Hata yule CHIZI WA UBELGIJI siku hizi kaufyata.

Hatetei wanyonge tena.
 
Bro kuwa makini na propaganda,CCM Wanajitahidi sana siku hizi kuonesha kuwa CHADEMA imekaa kimya kwasababu wanafaidi urais wa Samia.
Sasa ni wakati wa kudai katiba mpya kwa nguvu zote ili asije kichaa mwingine akavuruga sheria kama jiwe.
Kutokuoanda mishahara ni matokeo ya udikteta wa jiwe kwa kutokufuata sheria ya ongezeko la mshahara na kuamua kadri ya anavyoona.
Tuache CHADEMA ipambanie mambo makubwa kama KATIBA MPYA na MARIDHIANO YA KITAIFA.
Mambo ya wafanyakazi viachiwe vyama vyao sasa vifanye kazi yake na wafanyakazi wenyewe waamue kuamka.
Umenena Jambo kubwa Sana.
 
Nani mfanyakazi?

..Ccm kinajitambulisha kama chama cha wakulima na wafanyakazi.

..Kwa bahati mbaya kimekuwa mnyanyasaji mkubwa wa makundi hayo mawili.

..Jambo mnalopaswa kufanya ni kujiunga kwa wingi ktk vyama vya upinzani.

..Hiyo itasaidia hoja zenu kusikika ndani ya vyama hivyo. Vilevile mtavipa nguvu na uhalali wa kupigania maslahi yenu.
 
SIDHANI, SIDHANI SIDHANI... NADHANI WANATOA NAFASI KWA HAYA MAJADILIANO... i THINK SO!
Hoja yako Retired Ni dhaifu Sana....Taifa hili haliwezi kuwa na upinzani wa bargain na wanyonyaji...Ccm naturally Ni kupe.
 
Hakika Kauli ya Mbowe itatikisa Dunia , Vuta Subra .
Hizi hoja mkuu@Erythrocyte Ni za kisiasa Sana unachosahau Ni kuwa Mwamba kabakisha mwaka mmoja kuretire ...Hoja ya mkuu@Retired inamashiko huwezi kukaa kimyaa wakati Taifa linazamishwa...Ccm bila kushtuliwa kwa critism haiendi ng'o!!!
 
Bado nina Imani kubwa na Chadema. Toa neno Mh. Mbowe katika hizi vurugu za "kudanganywa "mishahara, Kingai (mbambikaji wa kesi kupanda cheo) and many other hot issues!
Mungu ibariki CHADEMA [emoji1545]
 
Kelele zote zile ni kwasababu bwana Yule alikata mirija. Sasa hivi mirija yote inatema asali! Kafieni mbele hakuna mtetezi

Kuua na kuwafunga ndio kukata mirija? CHADEMA wamepitia mengi waacheni wakae kimya. Kuna kipindi kuwa CHADEMA lilikuwa kosa la jinai.
 
Bado nina Imani kubwa na Chadema. Toa neno Mh. Mbowe katika hizi vurugu za "kudanganywa "mishahara, Kingai (mbambikaji wa kesi kupanda cheo) and many other hot issues!
Mkuu 'Retired', umeuliza swali muhimu kweli kweli ambalo linahitaji mjadala wa maana sana kupata jibu/majibu yanayoeleweka.

Mimi nitachangia hapa kwa kuwa upande wa 'devil's advocate', kuwateyea CHADEMA; lakini kiuhalisia hapo baadae nitageuka na kuonyesha kukosa ukomavu upande wao.

CHADEMA na viongozi wake wote wamepitia katika hali ngumu sana katika miaka hii ya karibuni iliyopita. Wamefanya kila juhudi kutetea maslahi ya wananchi huku mapigo yakielekezwa kwao.

Badala ya wananchi (nina maana ya umma wa waTanzania) kuunga juhudi hizo na kuleta mabadiliko, ikawa kama CHADEMA na viongozi wao ndio wanaojitafutia maumivu bila ya sababu. Ni kama juhudi za CHADEMA zilipuuzwa na wananchi wengi. Au hawakuona maana ya kazi iliyokuwa ikifanywa na CHADEMA kwa niaba ya wananchi.

Viongozi wanapigwa risasi, wananchi kwa wingi wao kimya!

Viongozi wanawekwa ndani hovyohovyo tu, wananchi wanapuuza, hawanyooshi hata kidole!

Hebu niambie ukweli wako, ingekuwa ni wewe usingejiuliza maswali juu ya mambo kama haya? Mtu unajitoa juu maslahi ya watu wasiotambua maana ya kujitoa kwako, huwezi hata ukastuka kuna nini?

Hapa nimetiririka tu, kama kuna mahali hapakunyooka vizuri, tafadhari naomba uelewe maana yangu kuu.

Viongozi wanazushiwa kesi za ugaidi, wananchi wanacheka tu
 
Back
Top Bottom