Hii ya juzi ya Serengeti boys, nilikuwa na hamu sana iende Madagascar yaan nilikuwa na hisia kweli kweli!
Kilichotokea Kongo Brazzaville ndo kilinitoa jasho jumapili iliyopita.
Nilikuwa nimekaa tu nasubiri kusikia Serengeti wamepita, mida ya saa moja jioni nasikiliza E- sport Kitenge akasema bado kidogo mpira uishe na matokeo ni 0-0.
Nikaanza kuzunguka zunguka ili muda uishe, baadae Kitenge akasema mpira umeisha na matokeo yamebaki vile vile.
Nikafurah sana, nikaingia kwenye mtandao nikakuta hivyo hivyo nikafurah sana.
Sasa, ilipofika saa mbili nikiwa nasikiliza redio moja ya huku mkoani, mtangazaji wa michezo akasema tumeshindwa kufuzu.
Nikampotezea nikajua amejikoroga, lakini akazidi kusema, nikasema ngoja nirudi tena kwenye mtandao, looh!
Nikawa bado siamini amini, saa tatu clauz wakaongea na Bakari Shime, jasho lilinitoka.
Tangu siku hiyo sina hamu na mpira sina kabisa. Sitaki tena mambo ya mpira.