ANKO JEI
JF-Expert Member
- Jul 21, 2018
- 1,302
- 2,462
Maisha yana matukio mengi ambayo yana muunganiko wa moja kwa moja kwenye hisia zetu, hivyo unapoyakumbuka unaweza patwa na hisia ya huzuni au furaha.
Hivyo leo tukumbuke matukio ambayo tuliwahi yashuhudia yakatuchekesha,lakini hata baada ya siku, wiki, miezi au miaka kupita bado matukio hayo hutuchekesha tunapoyakumbuka hata tunapokuwa peke yetu chumbani, njiani au chooni.
Binafsi kuna matukio mawili huwa yananichekesha sana kila ninapoyakumbuka.
TUKIO LA KWANZA
Mwaka 2018 nilikua katika harakati zangu za kununua matisheti ya buku jero, pale karume, nilipomaliza nikavuka upande wa pili, pale wanapouza mabegi begi nikawa nasubiri gari ya Mabibo niirukie nirudi home.
Sasa kuna shehe mmoja alikua amekula kanzu nyeupe safi inayong'ara kama umetoka dukani jana. Sasa kuna ile mitaro mikubwa sana ya kupitisha maji taka, na shehe akawa anataka avuke bara bara kwa haraka, bahati mbaya akasahau kuwa mavaa kanzu na inabidi aikunjie kwa juu ili aweze kukimbia vema na kuruka ile mitaro. Hivyo shehe akajaribu kuruka ule mtaro, aisee ndugu msomaji kanzu ilimchota ngwara, shehe mzima mzima kaingia mtaroni mpaka akapotelea, nilishtuka sana lakini shehe alivyotoka ndani ya mtaro akiwa mzima wa afya aisee nilijikuta nacheka kila nikikumbuka hahahhah aisee shehe alikimbilia karume sokoni kutafuta hifadhi.
TUKIO LA PILI
kipindi nipo sekondari shule ya bweni, nilikua na tabia ya kudoji bwenini tukiwa na wana kibao wenye tabia kama zangu, kikubwa tulikua tukicheza karata na kupiga soga.
Sasa ilikua lazima awepo anaepiga chabo kuangalia kama kuna mwalimu anakuja,sasa siku hiyo kumbe walimu kama wanne hivi wamezunguka njia nyingine wakitaka kutuwinda.Tumekuja kushtuka wapo karibu sana na bweni, hivyo mpiga chabo alivyotushtua, ilikua pata shika.
Kila mmoja alikimbilia alikojua, sasa mimi nikakimbilia chooni nijifanye nilikuja kujisaidia haja kubwa,mwalimu akausoma mchezo akaja hadi vyooni akawa anafungua mlango mmoja baada ya mwingine, me nikawa nishavua suruali nimekaa mkao kabisa kama najisaidia, sasa mwamba choo cha pili alisahau kuvua suruali so akawa amechuchumaa huku amechomekea.
Me nasikia tu mwalimu anafungua milango ya karibu, mara akafungua mlango ambao niko mimi akanambia "dogo maliza fasta kimbia darasani"
Nikajua tu nimepona, sasa wakati namwaga nazuga kujisafisha ticha akaenda mlango alipo jamaa, akafungua akamkuta mwana kachuchumaa. Nikawa nasikia maongezi
Ticha akamuuliza jamaa, unafanya nini? Jamaa kwa woga akajibu "najisaidia" ticha akacheka sana akauliza "dogo unajinyea au? Unajisaidiaje umechomekea?" jamaa akakosa jibu akatolewa nje akila kichapo me nikapita kama siwajui huku kicheko kimenibana sana.
Tafadhali share nawe ni tukio gani lilikuchekesha na linakuchekesha mpaka leo.
Hivyo leo tukumbuke matukio ambayo tuliwahi yashuhudia yakatuchekesha,lakini hata baada ya siku, wiki, miezi au miaka kupita bado matukio hayo hutuchekesha tunapoyakumbuka hata tunapokuwa peke yetu chumbani, njiani au chooni.
Binafsi kuna matukio mawili huwa yananichekesha sana kila ninapoyakumbuka.
TUKIO LA KWANZA
Mwaka 2018 nilikua katika harakati zangu za kununua matisheti ya buku jero, pale karume, nilipomaliza nikavuka upande wa pili, pale wanapouza mabegi begi nikawa nasubiri gari ya Mabibo niirukie nirudi home.
Sasa kuna shehe mmoja alikua amekula kanzu nyeupe safi inayong'ara kama umetoka dukani jana. Sasa kuna ile mitaro mikubwa sana ya kupitisha maji taka, na shehe akawa anataka avuke bara bara kwa haraka, bahati mbaya akasahau kuwa mavaa kanzu na inabidi aikunjie kwa juu ili aweze kukimbia vema na kuruka ile mitaro. Hivyo shehe akajaribu kuruka ule mtaro, aisee ndugu msomaji kanzu ilimchota ngwara, shehe mzima mzima kaingia mtaroni mpaka akapotelea, nilishtuka sana lakini shehe alivyotoka ndani ya mtaro akiwa mzima wa afya aisee nilijikuta nacheka kila nikikumbuka hahahhah aisee shehe alikimbilia karume sokoni kutafuta hifadhi.
TUKIO LA PILI
kipindi nipo sekondari shule ya bweni, nilikua na tabia ya kudoji bwenini tukiwa na wana kibao wenye tabia kama zangu, kikubwa tulikua tukicheza karata na kupiga soga.
Sasa ilikua lazima awepo anaepiga chabo kuangalia kama kuna mwalimu anakuja,sasa siku hiyo kumbe walimu kama wanne hivi wamezunguka njia nyingine wakitaka kutuwinda.Tumekuja kushtuka wapo karibu sana na bweni, hivyo mpiga chabo alivyotushtua, ilikua pata shika.
Kila mmoja alikimbilia alikojua, sasa mimi nikakimbilia chooni nijifanye nilikuja kujisaidia haja kubwa,mwalimu akausoma mchezo akaja hadi vyooni akawa anafungua mlango mmoja baada ya mwingine, me nikawa nishavua suruali nimekaa mkao kabisa kama najisaidia, sasa mwamba choo cha pili alisahau kuvua suruali so akawa amechuchumaa huku amechomekea.
Me nasikia tu mwalimu anafungua milango ya karibu, mara akafungua mlango ambao niko mimi akanambia "dogo maliza fasta kimbia darasani"
Nikajua tu nimepona, sasa wakati namwaga nazuga kujisafisha ticha akaenda mlango alipo jamaa, akafungua akamkuta mwana kachuchumaa. Nikawa nasikia maongezi
Ticha akamuuliza jamaa, unafanya nini? Jamaa kwa woga akajibu "najisaidia" ticha akacheka sana akauliza "dogo unajinyea au? Unajisaidiaje umechomekea?" jamaa akakosa jibu akatolewa nje akila kichapo me nikapita kama siwajui huku kicheko kimenibana sana.
Tafadhali share nawe ni tukio gani lilikuchekesha na linakuchekesha mpaka leo.