Nomadix
JF-Expert Member
- Jan 5, 2025
- 2,411
- 6,646
Habari wakuu
Mara ya kwanza kujiunga na huduma za kibenki nilienda kwenye tawi la benki wakanisajili ikafika mda wa kufanya kadi iwe active.
Nimeenda kwenye ATM na yule mhudumu akaiweka kadi ndani ya ATM ananiambia chagua lugha, me hapo hata sijui wanabonyeza wapi, akanionesha zile button za pembeni nikachagua, akanambia bonyeza hapa nikabonyeza, akasema weka namba ya siri nikaanza kuijaza.
Sasa yeye akatoka nimemaliza akakawia kuja. Namsubiri mara nashangaa kadi inamezwa nikamuita nikamuuliza mbona kadi imedumbukia tena, akasema aisee ungeitoa dah, me nikamwambia sasa hukuniambia, nilikaa pale saa zima nasubiri wailete dah!
Mara ya pili, nimeenda ATM pekeangu kufika kumbe ile ATM ni ya touchscreen haina buttons za pembeni zipo za namba tu maandishi yale ya pembeni kumbe unatouch, duh nikadata nje kuna bonge la foleni wanasubiri nitoke, naweka kadi naweka PIN nasubiri hola! duh nikaona nitoke hapa nishatolewa ushamba, hata nikaona kuuliza watanicheka nikaenda kutoa kwa wakala, haha dah!
ushamba mzigo
Mara ya kwanza kujiunga na huduma za kibenki nilienda kwenye tawi la benki wakanisajili ikafika mda wa kufanya kadi iwe active.
Nimeenda kwenye ATM na yule mhudumu akaiweka kadi ndani ya ATM ananiambia chagua lugha, me hapo hata sijui wanabonyeza wapi, akanionesha zile button za pembeni nikachagua, akanambia bonyeza hapa nikabonyeza, akasema weka namba ya siri nikaanza kuijaza.
Sasa yeye akatoka nimemaliza akakawia kuja. Namsubiri mara nashangaa kadi inamezwa nikamuita nikamuuliza mbona kadi imedumbukia tena, akasema aisee ungeitoa dah, me nikamwambia sasa hukuniambia, nilikaa pale saa zima nasubiri wailete dah!
Mara ya pili, nimeenda ATM pekeangu kufika kumbe ile ATM ni ya touchscreen haina buttons za pembeni zipo za namba tu maandishi yale ya pembeni kumbe unatouch, duh nikadata nje kuna bonge la foleni wanasubiri nitoke, naweka kadi naweka PIN nasubiri hola! duh nikaona nitoke hapa nishatolewa ushamba, hata nikaona kuuliza watanicheka nikaenda kutoa kwa wakala, haha dah!
ushamba mzigo