Tukio gani umewahi kufanya ukweni na hutokuja kulisahau?

Tukio gani umewahi kufanya ukweni na hutokuja kulisahau?

Judithkaunda

Member
Joined
Aug 21, 2022
Posts
90
Reaction score
231
Mwenzenu nimewahi kukaa ukweni zaidi ya miezi nane, nikiwa na ujauzito wa miezi mitatu mpaka nikajifungua, nilikuja kuondoka mtoto anamiezi mitatu. Katika muda wote huo niliwahi kufanya tukio ambalo najutia sana ingawa lilitokea kwa bahati mbaya tu.

Mume wangu alinikataza kitu fulani nikakubali tena nikamuahidi hakitajirudia tena. Basi siku hazikupita nyingi likajitokeza wakati nazuia si akanipinga, tena mbele ya wazazi wake! Aisee, nilijisikia vibaya na mbaya zaidi akaniita mbele nieleze.

Sasa wakati namlalamikia akumbuke yeye ndiye kanikataza, na hii sauti yangu mbaya sikujua kumbe nilikuwa namfokea mume wangu mbele ya wazazi na ndugu zake. Baadae nilijisikia aibu sana, niliomba radhi na kusamehewa lakini lilikuwa jambo baya sana kutokea. Nilitamani niondoke bila kuaga!

Umewahi kukaa muda mrefu kiasi gani ukweni, na tukio gani siyo rahisi kulisahau?
 
Huwa nashangaa sana watu, mwanaume unakaaje ukweni siku mbili tatu, unawasha na TV unataka nini? Ukweni naendaga kwenye misiba na matukio ya kijamii likiisha nasepa sitakagi shobo.

Mambo mengine ya aibu watu wanajitafutiaga wenyewe tuu.
 
Tatizo hata ukweni sina mda wa kwenda nikifika sikai hata saa 1 naondoka.
 
huwa nashangaa sana watu, mwanaume unakaaje ukweni siku mbili tatu, unawasha na TV unataka nini? Ukweni naendaga kwenye misiba na matukio ya kijamii likiisha nasepa sitakagi shobo.
Mambo mengine ya aibu watu wanajitafutiaga wenyewe tuu.
Yakobo alikaa ukweni kitambo sana...
 
Tulishakubaliana wanaume kuwa ukienda ukweni ni kwenye msiba au sherehe. Kama ni sherehe basi utafika siku ya tukio na kuondoka kesho yake, kama ni msiba utalala usiku mbili tu baada ya hapo unasepa. Kam itatokea umeenda kusalimia wakati wa likizo basi utakaa siku mbili pekee.
 
Tulishakubaliana wanaume kuwa ukienda ukweni ni kwenye msiba au sherehe. Kama ni sherehe basi utafika siku ya tukio na kuondoka kesho yake, kama ni msiba utalala usiku mbili tu baada ya hapo unasepa. Kam itatokea umeenda kusalimia wakati wa likizo basi utakaa siku mbili pekee.
Vp wamekusikia au tuongeze sauti!
 
huwa nashangaa sana watu, mwanaume unakaaje ukweni siku mbili tatu, unawasha na TV unataka nini? Ukweni naendaga kwenye misiba na matukio ya kijamii likiisha nasepa sitakagi shobo.
Mambo mengine ya aibu watu wanajitafutiaga wenyewe tuu.
Ukute wewe ndio umekaa ukweni sasa hivi umeweka na Miguu juu[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tulishakubaliana wanaume kuwa ukienda ukweni ni kwenye msiba au sherehe. Kama ni sherehe basi utafika siku ya tukio na kuondoka kesho yake, kama ni msiba utalala usiku mbili tu baada ya hapo unasepa. Kam itatokea umeenda kusalimia wakati wa likizo basi utakaa siku mbili pekee.
Na pia Kama wewe ni Mwanaume unaishi kwenu na Mkeo. Yani Mkeo umemfanya aishi kwenu(kwa wakwe zake). Basi jua hata wewe Mwanaume ni sawa na kuishi ukweni tu.
 
Kukaa ukweni kwa muda mrefu ni kutojitosheleza kiakili
Na pia usisahau ukiolewa na Mwanaume ambaye anaishi kwao na unaishi nae hapo. Ni upumbavu wa kiwango cha SGR.

Utakuja kumtamanisha Baba Mkwe akupige miti. Au utakuja kumtamanisha kaka/Mdogo wa Mumeo akuoige Miti.

Kwa kifupi Mwanaume kuishi ukweni ni janga na Mwanaume kuishi kwao na Binti ni janga part 2
 
Na pia usisahau ukiolewa na Mwanaume ambaye anaishi kwao na unaishi nae hapo. Ni upumbavu wa kiwango cha SGR.

Utakuja kumtamanisha Baba Mkwe akupige miti. Au utakuja kumtamanisha kaka/Mdogo wa Mumeo akuoige Miti.

Kwa kifupi Mwanaume kuishi ukweni ni janga na Mwanaume kuishi kwao na Binti ni janga part 2
Kabisa mkuu
 
Nilikaa mwezi 1 na nikawa nakula tunda kimasihara hapo hapo kwenye chumba nilichokabidhiwa aisee mie.
 
Mwenzenu nimewahi kukaa ukweni zaidi ya miezi nane, nikiwa na ujauzito wa miezi mitatu mpaka nikajifungua, nilikuja kuondoka mtoto anamiezi mitatu. Katika muda wote huo niliwahi kufanya tukio ambalo najutia sana ingawa lilitokea kwa bahati mbaya tu.

Mume wangu alinikataza kitu fulani nikakubali tena nikamuahidi hakitajirudia tena. Basi siku hazikupita nyingi likajitokeza wakati nazuia si akanipinga, tena mbele ya wazazi wake! Aisee, nilijisikia vibaya na mbaya zaidi akaniita mbele nieleze.

Sasa wakati namlalamikia akumbuke yeye ndiye kanikataza, na hii sauti yangu mbaya sikujua kumbe nilikuwa namfokea mume wangu mbele ya wazazi na ndugu zake. Baadae nilijisikia aibu sana, niliomba radhi na kusamehewa lakini lilikuwa jambo baya sana kutokea. Nilitamani niondoke bila kuaga!

Umewahi kukaa muda mrefu kiasi gani ukweni, na tukio gani siyo rahisi kulisahau?
Kama sijakuelewa hivi
 
Warombo hawata nisahau nilivyotembeza mkong'oto ukweni siku ya jubilee ya wakwe zangu nilipiga karibia ukoo wao wote kuanzia mke wangu, hawara yake, kaka zake, wajomba, mashangazi, baba wakubwa, baba wadogo, majirani n.k
 
Back
Top Bottom