Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Safari iliendelea huku kila mmoja sasa anamuogopa mwenzie, kila mtu anaamini kile ni kipindu pindu.

Baada ya mwendo mrefu Wamisunjo akaanza kukosa nguvu ya kutembea.
Tumbo lilianza kumuuma na kila baada ya hatua kadhaa jamaa alikua akituomba tumngoje akajisaidie.
Baada ya mwendo mrefu Wamisunjo alishindwa kutembea nakutuambia ambia tumuache yeye hawezi kutembea.

Kwakua kila mtu alikua na uoga wa kuambukizwa, hakuna alie thubutu kumbeba, tulimuacha hapo na sisi kuendelea na safari.

Tulifika kijijini usiku kama saa 6 usiku.
Kijiji kulikua kumejaa huzuni tupu.
Nakumbuka kuna brother mmoja wa kinyakyusa (jina nimelisahau) nyumbani kwake kulikua na maiti kibao (kitu kama 19 hivi) zilikua zime tandazwa barazani.

Nyingi ya maiti hizo zilikua za watoto wa Mbeya.
Hawa walikua wanamiliki vingwendu (mashine za kusachia dhahabu)

Tulikaa pale kijijini kama week hivi, mwenye bahati ya kuwaona ndugu zao waliwaona wasio na bahati ndio basi tena

Kwa upande wangu nilipotezana na wengi, wengine walikufa, wengine ndio kama huyu mshikaji nilie kutana nae leo asbuh.

Yani ni miaka 5 ndio kwanza nakuta nae leo, mshikaji alikua kwenye misele hii hii yakwangu sema sehem nyingine.

Ndani ya week ile wengine walirudi walikotoka, wengine tuliendelea kubaki kwa kukosa nauli.

Mala zikaanza story za chini chini kutoka kwa wanakijiji wapale (nairoto)

****************************************************************************************
Wachimbaji wa mwanzoni kabisa baada ya kugundua dhahabu kwenye korongo lile, walienda mpaka kwa mwenye (chifu) wa kijiji kile na kumueleza azma yao ya kuchimba.

Chifu akawakubalia, ila kwa masharti ya kutovuta bange, sigara, pombe, wanawake wawapo polini.

Wachimbaji walikubali japo walijua kua masharti hayo kwa mchimbaji ni magumu na hayawezekani tu.

Jamaa wale walichimbaa na kila siku dhahabu ndio zilikua zikohowa tu.

Dhahabu zilitoka ile mbaya mpaka sisi wa mbali mlio ukatufikia.

Kama desturi ya mchimbaji, bila vileo (bombe, sigara, bange, wanawake) haendi.
Ikabidi washauriane kwenda kuomba kwa Mwenye, waruhusiwe kuishi maisha yao.

Walivyo fika kwa mwenye, Mwenye akakataa.
Akawaambia mizimu ya huko haitaki vitu hivyo, kwahiyo yeye haruhusu ila kama wanataka kutumia vitu hivyo ni hiari yao.

Wachimbaji walivyo rudi polini wakaanza kutumia vitu vyote.

Sigara, bange, gongo ndio vitu vya mwanzo kuingia.
Lakini kadili siku zilivyo kua zina songa ndio laana ikawa inaongeza polini.

Wanawake wakawa wengi, biashara ya ngono ikawa rasmi polini.

Polini kukawa mjini na kijijini kukageuka mstuni.
Ilifikia hatua mtu wa kijijini anakuja kutumia polini.

Baduka yakafunguliwa, bar zikawa zimezagaa.
Polini lakini mziki unagongwa utadhani uko lidas.
Mabanda ya video kama kawa.
Kiufupi poli liligeuka uwanja wa laana kwa muda mfupi tu.

Mpaka nafika mimi pale polini nilikuta kila kitu cha mjini kiko kule.

Nakuja kidogo.
 

Horror story
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…