Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

sasa hitimisho...


baada ya matibabu na kila kitu kukaa sawa ikawa sasa siyo siri kwamba mimi nimepata ulemavu na wale jamaa wamepotezwa na tamaa ya kutaka rupia za wajerumani,ile habari iliongeza sana hofu kuhusu ule msitu pia sikuwa napenda sana simulia lakini watu walikua wanasimuliana habari nyingi sana za uongo kuhusu lile tukio letu...

wengi walikua wanazipata kwa mangi,baada ya kuwa chizi ilikua wanamwita wanampa hata ubwabwa kama mzee rungwe anafunguka lakini vyote anasema ni uongo uongo sababu ya kuwa chizi

mimi bahati sana kazini sikufukuzwa na kibarua changu kilikua hakina uhusiano sana na matumizi ya huu mguu so nikaendelea kupata kipato ila sasa ikabidi nianze utafiti wangu usio rasmi kuhusu nyumbanitu na mambo ya hizo mali za wazungu

...kama niliyoyaona mule ndani ni ya kweli basi hizi mali zipo,kama hazipo basi kuna kitu na uchawi upo kabisa real

mambo yasiyo kawaida niliyoona mule

zile chain kushuka shimoni
beacon
michoro mbalimbali ya ajabu
ule mwanga mkali
sauti ya ajabu
kusisimka nywele

haya tu yanatosha kusema kwamba kuna activities zilishafanyika huko miaka ya zamani sana lakini kuna uchawi mkubwa ulifanyika kuzilinda,kwanini kuwe na zile chain zimeshuka chini na kwanini haya maeneo mengi ya aina hii huwa yanaambatana na miiko gulani na vitisho kuhusu kulifikia eneo hilo?!!

.....haya maeneo mengi yanaambatanaga na uwepo aidha wa hifadhi au makanisa au shule / hospitali hasa makongwe especially ROMAN CATHOLIC,lutheran na moravian,makanisa mengi yamejengwa juu ya hizo mali na maeneo ambayo hakukua na uwezekano wa kujenga makanisa basi ndio walifanya uzushi wa kufanya yaogopwe.

Kuna sekondari ya moravian zamani inaitwa rungwe iko tukuyu mbeya,iko mission ya makao makuu ya kanisa la moravian kanda ya kusini...kuna habari za kutisha sana na kuna mahandaki ya wazi kabisa kuanzia baadhi ya vyumba yametokomea huko chini gizani ambako hakuna anayejua ni wapi,kuna kipindi moja lilishawahi titia assembly

Pia makanisa mengi ya roman mkoa wa Njombe(ndio nina uzoefu nako zaidi) yanafanana ramani kwa yake ya zamani na kuna maeneo ambayo ni restricted kufika,kunakua aidha na misitu mikubwa au kitu tu kinaogopwa bila sababu...nilipokuepo kila mwaka wazungu walikua wanakuja kuanzisha project fulani ambazo ni za kijinga hivi na hazidumu na zote lazima zihusishe kuchimba na hapo hawataki wasaidizi kabisa weusi na wanafanya kazi usiku na mchana.

Pale Rungwe kila mwaka lazima mwanafunzi apotee na tukio la karibuni nililosikia na kuhakiki kuhusu pale ni kifo cha utata cha dogo wetu mmoja wa njombe iliripotiwa 2011/2012...mwaka huo huo alipotea mtoto wa kidato cha tano porini lakini huyu alifanikiwa kupatikana akiwa hai amechoka sana baada ya kufanywa mila na wazee wa kwao sumbawanga,baada ya siku kama saba hivi.

Kuna mahala kijijini Njombe huko alikuja mzungu akaanzisha project ya kulima kabichi,alikaa miaka mitatu hivi na aliwekeza vifaa vya gharama sana...siku ya siku usiku aliondoka yeye na briefcase zake kadhaa chini ya escort na aliacha kila kitu hapo watu walijiokotea tu vitu...hajawahi rudi hadi leo.

Nina mifano kadhaa...sababu baada ya ile nimekua mtu wa kudadisi sana kuhusu haya mambo ndio maana pia nilivutiwa kusoma uzi wa Kitoabu.

Kwahiyo hizi mali zipo ila sasa wazungu kama ambavyo walitutangulia kwenye kila kitu basi hata uchawi pia walitutangulia..wao uchawi wao ni mkali sana kuliko huu wetu na kwa sasa uchawi wao uko next level,huwa nawaza hivi inawezekana vipi eti nyimbo zinakaa kwenye simu jamani[emoji1][emoji1] eti picha unaweza print kwenye karatasi na kila rangi ikatoka hapo bila utata...na teknolojia zote hizi za ajabu,siku hizi wanaprint hadi nyumba[emoji1787][emoji1787][emoji1787](utani huu lakini unafikirisha)....wazungu wako mbali kwenye kila kitu,huu uchawi sisi tunafanya leo wao walifanya wakati wa biblia zinatungwa so ipo siku na sisi tutafika huko lakini watakua tayari mali zao wamebeba kitambo sana.

Hizi mali wamezifanyia ushirikina mkuu sana ambao hakuna huko bongo au kama wapo basi wachache,imagine mtu kuona tu hayo masanduku unaishia kuwa kichaa...hii kupata kichaa ni kukupumbaza usirudi tena huko kufanya tena ujinga uliojaribu kuufanya...ni kama wanakupa second chance kuishi lakini sasa na onyo kwamba tafuta mali zako acha kuvizia walizotafuta wenzio...kwangu ni mila zimenisaidia ila wameniacha na onyo pia,ndio maana nikiona hata watu wanazungumzia habari za kwenda kuiba rupia au madini ya wazungu wanasikiliza nawaacha hapo nahama kijiwe.

Kwenye mkoa wetu ni ndoto ya kila kijana,sasa ni sabBu kila tajiri kule inasemekana lakima awe ameingia kuzindikwa humo...Njombe huwezi kuwa na fedha ukaishi kama siyo mshirikina,kule ni kawaida kujua mtu kaua hata mzazi kwa panga na kila mtu anajua na kijana anakua na fedha mbaya...kule kukuta tajiri analala chini kawaida ,tajiri hazai ndio ilikua maarufu sana,unakua na mtoto mmoja tu kwenye huu ulimwengu wa nyama na wengine wote unazaa na majini ila mkeo akishika tu mimba lazima afe na hiyo mimba(nina ushahidi na hili,yuko tajiri mmoja huko ndio aliporogea)

Wazungu huwa wanakuja,nilisema wakati naanza moja ya masharti waliwapa watawala wetu ili waachie uhuru wa kujitawala ni kuwaachia mali zao na pindi watakuja kufata hakuna wa kuwabugudhi hata baada ya miaka milioni(haya mambo ya siri kubwa sana za nchi,ndio zile ambazo kiongozi mkuu anatakiwa kuijua yeye tu) na mengine mengi...hii ni sababu wao wakirudi wanazichukua kirahisi kabisa tena kwa ulinzi mahususi chini ya watu wa intelijensia.

Nilipoteza mguu kipande lakini nikapata maarifa na akili kwamba hakuna mali za shortcut,ili tufanikiwe lazima tupambane kupata vyetu kwa njia halali(kama unataka kula na kuvaa ili usife)

Ila ili uwe tajiri lazima uchague imani unasimamia

1.kama ni kwa Mungu(dini) basi shikana nayo haswaaa ,hili kundi matajiri wachache au hawapo kabisa,wengi wanajificha makanisani kujiosha ila ni wachawi wakubwa...walio pure na imani na ni matajiri kwa imani hizi haba ni kama hawapo kabisa.

2.kama ni kwa ushirikina basi shikana nao haswa na hapa ndio matajiri na utajiri uko nje nje,ngumu sana kutenganisha utajiri na uchawi..hela ni za shetani kwahiyo huwezi kukaa nazo kama huna ushetani,hapa ndio wale wauza viungo wanakuja.

Kuhusu Njombe watu walikua wanauliwa kwa imani ukienda mgodini lazima utatema...wavuvi wa ziwani ndio wanatumia sana vipande na miili ya binadamu kufanya uvuvi na wanatoboa.

Tutaendelea kupiga soga hapa hapa ila kwa ipande wangu nimemaliza.

Nilitaka mali nikaishia kupoteza kipande cha mguu na marafiki wapendwa wanne katika mazingira ya kutisha na kuogofya.

#tufanye kazi.

[emoji1317]
Nyumba za kuprint mkuu zipo sio Jambo la kufikirika
 
Kweli nime elimika Sana hakuna shortcut kwenye maisha halali .

Nakumbuka mwaka 2013 nilipata mchongo mmoja wa magendo / haramu nikiwa ndio dogo nimeaza kazi,

Kwakweli nilipiga pesa Sana nikawa na kila kukicha na Jenga nakununua viwanja katikati ya mji, nakufungua vibiashara ndani ya mwaka mmoja ukweli nilifatwa na jamaaa zangu na kila Kona zikaenea habara nimejiunga na watoa kafara ndio utajiri una ninyoo keea .

Hivyo kwa story ya bwichibwich naamini nimatajiri wachache Sana chini ya Mungu.

kwani nilialikwa na watu wazito Sana nipeanenao mbinu za kufanya biashara nani niwatonye Ni mganga gani ananisaidia
Apo mwishoni sijakupata vizuri mkuu
 
Hii brother angu, Mtoto wa mama Mkubwa alinipa juu kwa juu hakutaka kwenda deep alishia kulia, Al maarufu Ras K, toka Mbeya CHUNYA, uroho wa dhaabu ulishia hapo na kwenda kulima Zabibu Dodoma kwa sasa ni marehem Ailfarikki miaka miwili baada ya kutoka Msumbuji, na mchizi wangu mwingine yupo geita kawa kama chizi hivi toka atoke msumbuji yeye alikuwa na duka huko alikimbia na kuliacha
 
Pale nilipo kaa (kuwangoja washkaji) usingizi ulinipitia nililalaa mpaka nilipo amshwa na makelele ya washkaji.

Sijui nilitumia muda gani kwenye usingizi ule ila nilipo angalia saa ilikua ni saa 6 mchana.

Nilipo amka nilikutana na kijua kikali utadhani niko Sudan, yani mpaka nguo nilizo vaa zilishaanza kunyauka.

Chakwanza niliwauliza kuhusu yule mmalawi, nikaambiwa bado wako camp wanaendelea kungoja mvua iishe waanze kazi.

Nilipo wauliza vipi kama mvua imeisha huko walikotoka, wakaniambia mvua imenyamaza sasa hivi baada ya kuvuka lile korongo.

Yani kumbe mvua inaanzia kwenye korongo kwenda matandani, ila kulimaliza korongo mvua hakuna.

Tulitembea mpaka kijijini, hakuna alie jua kua mimi nina dhahabu mbeleni.

Tuliingia kijijini saa 2 usiku, hapo tukalala.
Ila kwakua tulisha fika kijijini, kila mtu aliendelea kimpango wake.

Pale kijijini kila mtu anaham ya kujua kulikoni huko porini.
Nakumbuka nilitulia kwenye kiosk cha jamaa flani hivi, kila mtu alikua ananiuliza kuhusiana na porini.

Usiku kucha nilikesha kwenye kile kiosk cha jamaa nikila Royal gin (hii ni pombe kali sana) mpaka kuna kucha.

Kwakua nilikua na pesa ya kutosha niliyo chukua kwenye lile duka la marehem, hivyo ilikua mwendo wa kujimiminia pombe.

Kuna dem alinitamani nika lale kwake, lakini nilikataa kwa kuhofea asiniibie dhahabu yangu.

Migodini wanawake ndio wanaongoza kutuibia wachimbaji.

Kilicho fanyika nikumpa pombe mpaka dem akakimbia.

Asubuhi, sikutaka kulemba, na pombe zangu kichwani, nikakamata piki piki mpaka Montepuez.

Montepuez, hapa ndio kuna soko la madini yote.

Nikaingia kwa msirilanka nikapima dhahabu.

Dhahabu ilikua na uzito wa gram 112, kila gram kwa kipindi kile ilikua 2000 miticais sawa na laki moja shilingi kwa wakati huo.

Nikachukua 224,000 miticais, hapo akili yote inamuaza mama Abuu (Shemeji yenu)

Nakumbuka nilinunua piki piki na mazaga mengine kama nguo.

Nikatuma kama 60,000 miticais (sawa na Milioni tatu kipindi hicho) kwa mama yangu Tanzania, maisha yakaendelea.

MWISHO.

Naahidi kuwahabarishine matukio mbali mbali yanayo / yatayo tokea hapa mgodini nilipo.

Kumbuka kwa sasa naishi Tete, Muatiz, ila kwa hizi mvua zilizo anza kunyesha, nategemea kurudi Cabo del Gado wilaya ya Montepuez, nikatafute Ruby.

Hapa nangoja hii kazi iishe, nione kama nitaokoa chochote kinisogeze kwenye Ruby.
Ahsanteni na kwaherini.
Dah story yako ni ya kwel. Mm naish Cabo del gado. Baada ya kumaliza chuo SAUT 2015 coz ya education nilipitia maisha magum sana kulingana na background yang so nkajiingiza kwenye biashara ndogo ndogo hatimae 2019 mwez wa 6 nkafika mozambique. Hapo nikiwa na ml 5 sawa na MT 160000 ya huku. Nkaanza kununua gold kwa wachimbaji nauza Jimbo la nampula ambako soko nizur, sometimes Pemba, Tz pia. Now na mshukuru Mung sana maake pamoja na degree yang hata ningepata ajira nisingekua na mtaji mkubwa huu nilio nao kwa sasa. Nauwezo wakuchagua niishi wapi na ni furahie vp na nmekua msaada kwa ndg hata na marafk zang. Ml 100 huku usipokua mlevi na mvivu ni suara la mwaka tu mambo yakikunyokea ukianza na mtaji tajwa hapo juu. So kwa story hii nikwel coz eneo hlo now watu wanaliita MOCHWARI coz mifupa ya watu kitu cha kawaida eneo hlo n hakuna anaejar. Mtu anajar kilichofikisha huku sio anachokutana nacho mtu mwingne. Mtoa maada ntakutafta tuonane. MAPAMBANO YA NAENDELEA
 
Dah story yako ni ya kwel. Mm naish Cabo del gado. Baada ya kumaliza chuo SAUT 2015 coz ya education nilipitia maisha magum sana kulingana na background yang so nkajiingiza kwenye biashara ndogo ndogo hatimae 2019 mwez wa 6 nkafika mozambique. Hapo nikiwa na ml 5 sawa na MT 160000 ya huku. Nkaanza kununua gold kwa wachimbaji nauza Jimbo la nampula ambako soko nizur, sometimes Pemba, Tz pia. Now na mshukuru Mung sana maake pamoja na degree yang hata ningepata ajira nisingekua na mtaji mkubwa huu nilio nao kwa sasa. Nauwezo wakuchagua niishi wapi na ni furahie vp na nmekua msaada kwa ndg hata na marafk zang. Ml 100 huku usipokua mlevi na mvivu ni suara la mwaka tu mambo yakikunyokea ukianza na mtaji tajwa hapo juu. So kwa story hii nikwel coz eneo hlo now watu wanaliita MOCHWARI coz mifupa ya watu kitu cha kawaida eneo hlo n hakuna anaejar. Mtu anajar kilichofikisha huku sio anachokutana nacho mtu mwingne. Mtoa maada ntakutafta tuonane. MAPAMBANO YA NAENDELEA
Ukifanikiwa kukutana na Kitoabu mpe salamu zangu,
Mniletee na dhahabu basi nichonge mnyororo kama ile wanayovaa wale madrug dealer maana huwa ni minene[emoji2][emoji2][emoji2]

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Yaaani...Pesa bhana...watu wanakufa Kama kuku wa mdondo...alafu mnawapekua wakati hamkutakiwa kuwashika Kwasababu ya Ugonjwa.

Duuuuh

Mimi namikasa Yangu yamaisha Yangu natamani kuhadithia....siku ntakuja na ID Feki
Duh uko vizuri bibie, we njoo tu bebilakeee
 
Sio kweli kabisa ushirikina ni tabia ya mtu binafsi na Imani zako ..
Mimi binafsi toka utoto wangu sijawahi yaona hayo kwetu na mimi sijawahi ya amini mpaka umri huu wa miaka 39...
Mimi ni mtu wa kuamini Imani yangu..ushirikina naona ni ujinga fulani hivi mtu rizki inaletwa na Mungu
Nilikuwa naamini kama wewe lakini yalinikuta, hadi nywele walinyoa usiku
 
Back
Top Bottom