Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Wala sio brother na mimi sikua mchimbaji nilianza kununua kidogo kidogo na kuwezesha wachimbaji.... Mbona mimi bd sana hata 40 sina[emoji16][emoji16][emoji16]...
Nashukuru niko mahali sijutii hii kazi kabisa pamoja na matatizo yake mengi ila imenitoa mbali na kunifikisha nisipopatarajia
Eti ni kweli hii kazi bila ushirikina hautoboi?
Naomba uwe mkweli...
 
Mzee Kitoabu nawe upo kwenye list ya waleta faraja humu jf japo Kuna wengine tunawadai mastori wa Kwanza

jerrybanks na stori yake ya Mambo ya giza mwingine yule msimuliaji wa Vita ya Rwanda

Bossless sema simu yake ilipasuka stori ikaanza kuwa na utata japo tunamdai aje mwingine mzee wa Swizz

Parabora huyu Mwamba naomba uje na ID nyingine alete vitu vya Europe na malysia, Singapore huko, mwingine n

digba sowey na stori ya kushuudia uchawi sema ule Uzi ulivamiwa na walolokole mbaya zaid n single mamaz waliaribu Uzi, yule

Habibu B. Anga aendelee kuwauzia tuu wasioelewa stori za kucopy na kutafsir japo kutafsir n Kaz Ila kuuza sio mzee.

Kwa ujumla mnatupa vitu ambacho vipo Ila kwa maana nyingine sie wengine hatujakutana navyo na vinatupa funzo zuri katka maisha hvyo msisite kuleta stori Kama hzo Kwan usisimua akili na funzo pia hvyo tunawaomba mrejee kwenye nyakati za dhama zetu
Struggle za mwanaume ni hatari,,, machimbo, kufanya mapenzi mara kwa mara,,kazi za ufundi ambazo ni hatari'umeme'kujenga'kuchomelea'uzinzi,, bodaboda,, uvuvi,, mabaharia
 
Mzee Kitoabu nawe upo kwenye list ya waleta faraja humu jf japo Kuna wengine tunawadai mastori wa Kwanza

jerrybanks na stori yake ya Mambo ya giza mwingine yule msimuliaji wa Vita ya Rwanda

Bossless sema simu yake ilipasuka stori ikaanza kuwa na utata japo tunamdai aje mwingine mzee wa Swizz

Parabora huyu Mwamba naomba uje na ID nyingine alete vitu vya Europe na malysia, Singapore huko, mwingine n

digba sowey na stori ya kushuudia uchawi sema ule Uzi ulivamiwa na walolokole mbaya zaid n single mamaz waliaribu Uzi, yule

Habibu B. Anga aendelee kuwauzia tuu wasioelewa stori za kucopy na kutafsir japo kutafsir n Kaz Ila kuuza sio mzee.

Kwa ujumla mnatupa vitu ambacho vipo Ila kwa maana nyingine sie wengine hatujakutana navyo na vinatupa funzo zuri katka maisha hvyo msisite kuleta stori Kama hzo Kwan usisimua akili na funzo pia hvyo tunawaomba mrejee kwenye nyakati za dhama zetu
Sana
 
Nisahihishe jambo moja, maranyingi huwa sipendi kuandika kutokana na kazi zangu.

Mimi sio muajiliwa, mimi ni mchimbaji, kwa hiyo maisha yangu ni yakushea na washkaji.

Some time naweza nikawa naandika jambo mala anatokea mtu (rafiki) anaanza kuniongelesha, kwa hiyo inanibidi niache kuandika nimalizane nae kwanza.

Kwahiyo munisameh kwa hilo.


************************************************************************,,*************

Kwenye safari ile nakumbuka niliongozana na mdogo wangu (Mtanzania mwenzangu pia kabila letu ni moja ) Dogo Chiko.

Tulitoka Nanhupo kuelekea nairoto kwenye dhahabu.

Tulifika Nairoto kijijini kisha pakesho yake tukaelekea polini (machimbo)

Kwanza pale kijijini tulikutana na umati wa watu usipime.

Kila mtu akiwa na shauku ya kufika polini.

Kesho yake palipo pambazuka kila mtu alikua tayari kwa safari ya kuelekea polini, me na chama langu (dogo Chiko ) tuliukanyaga kwa mguu kutokana na kutokua na nauli ya piki piki.

Nauli kwa mtu mmoja kutoka pale kijijini kwenda polini ilikua 500 quinhento miticais sawa na 25000 ishirini na tano shilling.

Tuliukanyaga mwendo wa masaa 12 kwa mguu, nakumbuka tuliingia matandani kama mida ya saa moja usiku hivi.

Lakini kwa mgodini (japo ni polini) tulikuta kama tuko mtaa wa kongo.

Watu ni wengi mno, vijana wa kiume na wakike, mabibi na mababu, mpaka watoto wa miaka 7.

Kila aina ya laana ilikua inapatikana huku, Vifo (kuuana) ubakaji, kutiana vilema yani ni kama kupakaa mafuta tu.

Pombe gani unayo itaka utaikosa, Heineken,Savana, breezer na mapombe kibao ya gharama.

Malaya kutoka kila pembe ya Africa.
Wamalawi, Watanzania, na wenyewe Mocambique.

Kiufupi huu ulikua uwanjani wa madhambi.

Nakumbuka nilifanya kazi kama week mbili tu, mala ghafla ukaibuka ugonjwa wa ajabu matandani pale.

Watu walikua wakibadilika rangi na kuharisha mwisho kifo.

Yani unaweza kukaa na mshikaji mala ghafla akaanza kubadika rangi ya macho yake, akienda kujisaidia akirudi (wengine walikua hawarudi) unamuona mwili wote ume badilika rangi kawa wanjanoo, hapo amalizi saa munamkimbia.

Halii hii ilitamba siku mbili tu, siku ya tatu matanda yote nyeupe.

Watu wote tulikimbia kurudi kijijini, sasa balaaa lilikua njiani.
Watu wengi walifia njiani, tulio tusua ni wachache sana.

Nakumbuka msafara wetu (wakurudi kijijini) ulikua na watu 8, kati ya hao wawili tuliwaacha njiani, (walifia njiani).

Moja kati ya watu hao ni Rafiki yangu kipenzi (mdogo wangu) Dogo Chiko, na mshikaji alieitwa Wamisunjo (Mateas)

Nakumbuka tulikiamsha kutoka matandani pale mida ya saa4 asbuh, tulitembea umbali mrefu, mdogo wangu Chiko akatuambia tumngoje anaenda kukata gogo (kunya)

Tulimngoja, tulikaa chini mwenye sigara aliwasha, mwenye bange lake alilipua, mwenye maji alikunywa.

Muda ulipita mara Chiko akarudi, na safari kuendelea.
Lakini kila tulipo muangalia usoni, macho yote yame badilika rangi nakua yanjano.

Tukampa maji na safari ikaendelea.

Hatukufika mbali sana, Chiko akaomba tumsubiri anakwenda tena kujisaidia.

Tilipu hii tulimngoja bila dogo kurudi, ikabidi mshikaji mmoja amfuate.
Alipo fika kule alimkuta chiko kesha kufa.
Jamaa akatuita tuje kumcheki, nikiwa mingoni mwao nilimkuta dogo amesha kauka pale alipo kaa.

Kwakua tangu tuna toka matandani tulishaambiana kua ugonjwa huu ni kipindu pindu, hivyo ukifa hakuna mtu alie thubutu kukushika.

Kwahiyo Dogo Chiko tulimuacha hapo na sisi kuendelea na safari.

Nitarudi muda si mrefu.
Yani unavokaongea ni chinga ntupu!
 
Yaani yule jamaa alinidissapoint sana
Nilitegemea kujua mengi nikaishia kusoma malumbano ya mabaharia
Wajua ye aliweka heading ambayo iko nje ya uwezo wake[emoji28][emoji28][emoji28]

Na kama unavyojua JF wajuaji ni wengi, ndio pale mtifuano ukaanza wa kutunishiana misuli[emoji28][emoji28]

Hata hivyo yale maswali mliyokuwa mnamuuliza yalikuwa magumu, nimesoma nikacheka sanaa

Nilichompendea mhusika ni kuwa hakuwa anachukia wala kukata tamaa, ye aliendelea tu na yale aliyoweza mengine anayakaushia kama hayaoni na kudai amejibu maswali yote na simu yake mbovu haiwezi kuandika ujumbe mrefu
Ule ni moja kati ya uzi ambao ukiwa down na ukaupitia basi lazima mood itabadilika na furaha itarejea

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Story ya jamaa inanikumbusha 2005/2006 Nyakahura katikati ya msitu mzito Sana na 2016 October pale msitu wa council Ushirombo Bukombe...waliowahi kaa machimboni au miji ya machimbo tunamwelewa jamaa...ingawa anaweza kuwa ametunga story yake lakini inaakisi uhalisia wa maisha ya migodini
Umeanza vizuriii umemaliza vibaya!kutunga tena
 
Mzee Kitoabu nawe upo kwenye list ya waleta faraja humu jf japo Kuna wengine tunawadai mastori wa Kwanza

jerrybanks na stori yake ya Mambo ya giza mwingine yule msimuliaji wa Vita ya Rwanda

Bossless sema simu yake ilipasuka stori ikaanza kuwa na utata japo tunamdai aje mwingine mzee wa Swizz

Parabora huyu Mwamba naomba uje na ID nyingine alete vitu vya Europe na malysia, Singapore huko, mwingine n

digba sowey na stori ya kushuudia uchawi sema ule Uzi ulivamiwa na walolokole mbaya zaid n single mamaz waliaribu Uzi, yule

Habibu B. Anga aendelee kuwauzia tuu wasioelewa stori za kucopy na kutafsir japo kutafsir n Kaz Ila kuuza sio mzee.

Kwa ujumla mnatupa vitu ambacho vipo Ila kwa maana nyingine sie wengine hatujakutana navyo na vinatupa funzo zuri katka maisha hvyo msisite kuleta stori Kama hzo Kwan usisimua akili na funzo pia hvyo tunawaomba mrejee kwenye nyakati za dhama zetu
Mkuu umemsahau chongoe all the way from Mafia na mambo yake ya baharini



Cc travis 1 na fyddell

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Wajua ye aliweka heading ambayo iko nje ya uwezo wake[emoji28][emoji28][emoji28]

Na kama unavyojua JF wajuaji ni wengi, ndio pale mtifuano ukaanza wa kutunishiana misuli[emoji28][emoji28]

Hata hivyo yale maswali mliyokuwa mnamuuliza yalikuwa magumu, nimesoma nikacheka sanaa

Nilichompendea mhusika ni kuwa hakuwa anachukia wala kukata tamaa, ye aliendelea tu na yale aliyoweza mengine anayakaushia kama hayaoni na kudai amejibu maswali yote na simu yake mbovu haiwezi kuandika ujumbe mrefu
Ule ni moja kati ya uzi ambao ukiwa down na ukaupitia basi lazima mood itabadilika na furaha itarejea

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Baharini jinai nyingi ndio maana mengine kuyajibu nafiliria
 
Mida ilienda jamaa walirudi kutoka kuzichoma zile maiti na story zikaendelea mpaka asubuhi.

Chaajabu siku hiyo jua lilichelewa kutoka, tukicheki saa ni saa kumi na mbili asbuh (mida tuliyo panga tuanze kazi) lakini hakuna dalili ya kuchomoza jua yani ni kama wingu la alfajir, ila kwa porini kunakua kama kuna ukungu hivi.

Hali ile ya ukungu ilitamba kwa muda mrefu, mpaka mida ya saa 2 asubuhi bado hatujaenda kazini.

Ile hali kila mtu ilimshtua, yani ilikua kila tukitaka kwenda kuanza kazi lakini ile hali inatupa wasi wasi

Mala ghafla mvua ikaanza kunyesha, huwezi amini, mwezi wa nane, lakini mvua utadhani mwezi wa pili vile.

Mvua ilipiga mpaka basi, yani mpaka jioni halijatoka jua, ilikua inapungua tu, muda si mrefu inamwaga tena.

Nakumbuka mvua ilipo kua inapungua ndio muda tulio tumia kujisaidia, yani ikipungua tu utasikia "mwenye gogo akakate ".

Mvua ile tulishinda nayo, tuka kesha nayo mpaka asubuhi.

Mvua haikukata mpaka ikaanza kutujambisha.

Siku ya tatu mvu inakamua tu, kumbuka tuna kalibia kumaliza week polini, lakini hakuna alievuta bange, sigara wala pombe.
Hivyo hali zetu zikaanza kuwa mbaya kutokana na alosto, ukizingatia baridi lake, sio poa.

Nathubutu sema sijawahi kuona mvua iliyo dumu kwa muda mwingi kama hii.

Nakumbuka kuna jamaa aliungua mkono kwa kuukumbatia moto kutokana na baridi.

Siku kama ya tano hivi, ubongo ukanisogea, akili ina niambia nimtoroke mrundi na ile dhahabu, tatizo mvua inayo piga ni kubwa, yani hata mbele uoni.

Tushukuru wengi tulikua na simu wengine saa hiyo ilitusaidia kujua muda, vinginevyo tusingekua tunajua kua huu ni usiku ama mchana?

Tukaanza mashauriano ya kurudi nyumbani, maana hali ishakua sio poa.

Hakuna mwenye uthubutu wakwenda kuchukua sururu na kwenda kuanzisha sonda.

Mashauriano yalidumu siku mzima, kuna watu tunaka turudi (mimi mmoja wapo) na kuna wengine wana fosi tubaki.

Tunao taka turudi tuko wachache, wengi wanataka tubaki, na yule mrundi nae anataka tubaki.

Lakini kati ya tunaodai turudi kuna wengine hata dhahabu hawana, hivyo wengine ilikua wako mguu ndani mguu nje.
Watu wanajiuliza tukirudi na mvua ikaishia na wenzetu wakafanya kazi wakarudi na dhahabu itakuaje?

Pale watu kama saba nane hivi niliona wako serious, na safari ya kurudi kijijini.

Mvua inaendelea kupiga, chaajabu hakuna radi wala umeta, yani ni mwendo wa kulowesha tu.

Akili ikaniambia, mimi ni mwanamme, nime zaliwa siku moja nitakufa siku moja, kufa kulala kaburi tuta.

Nilijipa moyo, kama liwalo na liwe, ila lazima nitoroke na ile dhahabu, kwanza mshikaji anazingua, namuambia tuondoke, yeye ananiambia tukomae, ukizingatia tumejuana kule kule polini.

Mimi na yule mrundi tunaishi camp moja kati ya zile mbili tulizo zijenga hapa karibuni.

Moto mkubwa (porini mvua hata inyeshe vipi, lakini kuni zitawaka tu ) mbele yangu nimenyoosha mikono kuota, huku mawazo yakinirudisha nyumbani, kitambo sijarudi home (Tanzania) muda mrefu sijamuona mkewangu na watoto wangu (hawa wanaishi Nampula).

Moyoni najua kua nilicho nacho (dhahabu) ni cha thamani, uchawi kutoka hapa nilipo tu, nikiingia mjini mimi ni mzungu.

Hapo sijui ni uzito gani, lkn nilisha kadiria kua pesa ya kutamba kwa mama Abuu ninayo.

Nilicheki kisimu changu cha tochi nikagundua ni saa 8 usiku, nikaona huu ni usiku sana, ila ikifika saa 10 alfajir nitoroke.

Kichwani nilijua kua lile kundi lililo apa kuondoka asbuh lazima litanikuta mbele nawasubiri.

Saa kumi alfajir, camp mzima ime lala, mvua kubwa nje inapiga, nikaona hapa sasa mchizi boti wacha nipotelee kizani.

Nikachukua moko yangu (moko ni kifaa cha kazi) tochi yangu, kama naenda kukojoa vile, mbele.

Nitarudi muda si mrefu.
Mkuu mbona hueleweki, Post za zamani ulisema mwenzio huyo ni mmalawi saizi tena mrundi
 
Nilichomoka camp kwa tahadhari, sikutaka mtu ajue tena zaidi yule mmalawi (huyu ni mmalawi sio mrundi )

Mdogo mdogo huku mvua ikinichapa, nilipo hakikisha nime ziacha hatua kadhaa zile camp nikawasha tochi yangu ya kichwani moko yangu begani taratibu nasonga na njia.

Nilitembea mwendo wa masaa kama mawili hivi, mvua ikinyesha, uoga ukaanza kuniingia, japo tuchi yangu ilikua ikiwaka vizuri tu, lakini nilipata tabu kuona mbele.

Kuna muda nilikua natoka nje ya barabara, yani napotea njia, mara nimeingia kwenye mashimo, uoga ukanizidi.

Nimelowa mpaka boxa ya ndani, meno yana tetema mpaka yanauma, hapo natamani atokee mtu na bange lake anitembezee.

Nilizidi kutembea huku nikitetema, mkono nilio shika moko vidole vyote vimekufa ganzi, Kiufupi nilijiihisi naota.

Mbele kidogo kuna korongo limezunguka, kikawaida makorongo haya hupitishaga maji, natangu naiwaza hii safar akili yangu ilikua hapa kwenye korongo, sababu kwa mvua ile ni lazima ningeyakuta maji yame jaa, na hakuna njia nyingine.

Chaajabu nililikaribia korongo nakulikuta korongo kavu, yani kuna vimaji tu vya ugoko, yani hata suruali hukunji.

Hapa nili shangaa sana, maana si rahisi kwa mvua ile, sehem ile isijae maji.

Nilitambuka mpaka ng'ambo ya korongo, hapo nikaendelea na safari.

Kadri nilivyo kua natembea ndivyo sasa mvu ikawa inapungua na hata ka mwanga nikawa nakaona kwa mbaali.

Hapa nikaona ngoja sasa nitwete niwasubiri wale jamaa waolikusudia kurudi kijijini.

Nilipo kaa pale, usingizi ukanipitia (kati ya vitu ambavyo hatuwezi kuviamrisha sisi wenyewe ni usingizi na haja kubwa, binaadam anaweza kulala hata kwenye dimbwi la maji ) nililalaaaaaaaaaaaa

Nitarudi muda si mrefu
Ndugu zangu sifanyi kusudi sema ndio vivyo tusamehane.
 
Aisee mwamba umenikumbusha chimbo moja huko Katoro.

Kuna mzee alikua na eneo lake afu lina mali (dhahabu). Tumeenda kwa mtaalamu (mganga), akatupa masharti tusivute sigara, bange, kulala na mwanamke na mzee mwenye eneo alikatazwa asiguse chochote kitokacho ndani ya duara (shimo) .

Lile duara lilikua na miujiza sana ukizingatia haya mambo ya madini yanaendana sana na mambo ya kishirikina,,kuna watangulizi wetu waliwahi kuchimba hapo wakakosea masharti duara likaanza kutetemeka kila mtu akakimbia hakuna aliyerudi.

Tulipiga piga pale, aliyekuja kuharibu ni yule mzee mwenye eneo yaani....

Huu uchimbaji hasa wa dhahabu unamambo sana.

*Hapo kwenye masharti waliyokua wamepewa huko kwenu wasivute sigara, bange na wanawake ndo yamefanya nikumbuke hili jambo.
 
Yaaani...Pesa bhana...watu wanakufa Kama kuku wa mdondo...alafu mnawapekua wakati hamkutakiwa kuwashika Kwasababu ya Ugonjwa.

Duuuuh

Mimi namikasa Yangu yamaisha Yangu natamani kuhadithia....siku ntakuja na ID Feki
Tunasubir
 
Aisee mwamba umenikumbusha chimbo moja huko Katoro.

Kuna mzee alikua na eneo lake afu lina mali (dhahabu). Tumeenda kwa mtaalamu (mganga), akatupa masharti tusivute sigara, bange, kulala na mwanamke na mzee mwenye eneo alikatazwa asiguse chochote kitakacho ndani ya duara (shimo) .

Lile duara lilikua na miujiza sana ukizingatia haya mambo ya madini yanaendana sana na mambo ya kishirikina,,kuna watangulizi wetu waliwahi kuchimba hapo wakakosea masharti duara likaanza kutetemeka kila mtu akakimbia hakuna aliyerudi.

Tulipiga piga pale, aliyekuja kuharibu ni yule mzee mwenye eneo yaani....

Huu uchimbaji hasa wa dhahabu unamambo sana.

*Hapo kwenye masharti waliyokua wamepewa huko kwenu wasivute sigara, bange na wanawake ndo yamefanya nikumbuke hili jambo.
Hivyo vitu vitatu hata ktk Maisha ya kawaida ukiachilia Mbali Machimboni.. havifai kbs.. hasahasa Pombe na wanawake.. Laana.
 
Back
Top Bottom