Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

Tukio la kusisimua nililolishuhudia kwa macho yangu katika msitu wa Nairoto

hahahahahahaa et anafunua neti na yeye aingie sasa nmevuta picha jamaa alivyokuwa anapanda na ndevu zake....majini wana mikwara sana..
Yaani ninavyosimulia hapa, picha kamili inanijia kichwani kwasababu nakumbuka Kila kitu mpaka sura yake ingawa ilikuwa usiku. Mkuu acha kabisa kuonana na viumbe hivi
 
Zamani sana pale jirani na kwa bamkubwa Chamwino kuna kakijiji kanaitwa nzuguni,kuliibuka Chimbo dhahabu inatema mi dogo tu wa 12-14,
nilikua najichanganya sana na maanko wangu alafu walikua watu wa vagi na ubwiii ile mbaya,
sasa walinipenda kwasababu mlinzi wao huko wakipakaza,likianzishwa nzegembe mi nachukua wallet na mali zote zinazohamishika kisha nayeya home.
Machimbo yalipoanza Nzuguni tulienda hawakuniacha bodyguard wao.
Duh kufika kule nilichoka jamaa anachosimulia ni kweli kabisa.
uzinzi,pombe,bangi, kila aina ya uasi unaukuta .ushangae sasa machimbo hata mwezi hayana.
sisi tulikua na kagroup ketu mtu nne wote mayanki tu na tulikua tunachakata vumbi tu lile.
siku kadhaa tukapatapata vimawe viduuchu yani kwenda kuuza tukagawana kahela kadogodogo tu.
Ila mi niliridhika nikasepa nikawaacha maanko maana wao hata ndoto ya kurudi hawana ilikua km wamefika nyumbani,sio hata wachimbaji wao ilikua ni pary pary tu.bangi pombe mabibi na daily wana hela wale jamaa aisee
Ila walikua mafundi malori wazuri sana KAUDO pale na Madereva.
Ule mgodi ulikatika ghafla tu,upo hapo Chamwino pembeni kushoto ukiwa unaenda kwa baba mkubwa.
Daah Babu umeongea slang za kiswahili Cha zamani sana
 
Nisahihishe jambo moja, maranyingi huwa sipendi kuandika kutokana na kazi zangu.

Mimi sio muajiliwa, mimi ni mchimbaji, kwa hiyo maisha yangu ni yakushea na washkaji.

Some time naweza nikawa naandika jambo mala anatokea mtu (rafiki) anaanza kuniongelesha, kwa hiyo inanibidi niache kuandika nimalizane nae kwanza.

Kwahiyo munisameh kwa hilo.


************************************************************************,,*************

Kwenye safari ile nakumbuka niliongozana na mdogo wangu (Mtanzania mwenzangu pia kabila letu ni moja ) Dogo Chiko.

Tulitoka Nanhupo kuelekea nairoto kwenye dhahabu.

Tulifika Nairoto kijijini kisha pakesho yake tukaelekea polini (machimbo)

Kwanza pale kijijini tulikutana na umati wa watu usipime.

Kila mtu akiwa na shauku ya kufika polini.

Kesho yake palipo pambazuka kila mtu alikua tayari kwa safari ya kuelekea polini, me na chama langu (dogo Chiko ) tuliukanyaga kwa mguu kutokana na kutokua na nauli ya piki piki.

Nauli kwa mtu mmoja kutoka pale kijijini kwenda polini ilikua 500 quinhento miticais sawa na 25000 ishirini na tano shilling.

Tuliukanyaga mwendo wa masaa 12 kwa mguu, nakumbuka tuliingia matandani kama mida ya saa moja usiku hivi.

Lakini kwa mgodini (japo ni polini) tulikuta kama tuko mtaa wa kongo.

Watu ni wengi mno, vijana wa kiume na wakike, mabibi na mababu, mpaka watoto wa miaka 7.

Kila aina ya laana ilikua inapatikana huku, Vifo (kuuana) ubakaji, kutiana vilema yani ni kama kupakaa mafuta tu.

Pombe gani unayo itaka utaikosa, Heineken,Savana, breezer na mapombe kibao ya gharama.

Malaya kutoka kila pembe ya Africa.
Wamalawi, Watanzania, na wenyewe Mocambique.

Kiufupi huu ulikua uwanjani wa madhambi.

Nakumbuka nilifanya kazi kama week mbili tu, mala ghafla ukaibuka ugonjwa wa ajabu matandani pale.

Watu walikua wakibadilika rangi na kuharisha mwisho kifo.

Yani unaweza kukaa na mshikaji mala ghafla akaanza kubadika rangi ya macho yake, akienda kujisaidia akirudi (wengine walikua hawarudi) unamuona mwili wote ume badilika rangi kawa wanjanoo, hapo amalizi saa munamkimbia.

Halii hii ilitamba siku mbili tu, siku ya tatu matanda yote nyeupe.

Watu wote tulikimbia kurudi kijijini, sasa balaaa lilikua njiani.
Watu wengi walifia njiani, tulio tusua ni wachache sana.

Nakumbuka msafara wetu (wakurudi kijijini) ulikua na watu 8, kati ya hao wawili tuliwaacha njiani, (walifia njiani).

Moja kati ya watu hao ni Rafiki yangu kipenzi (mdogo wangu) Dogo Chiko, na mshikaji alieitwa Wamisunjo (Mateas)

Nakumbuka tulikiamsha kutoka matandani pale mida ya saa4 asbuh, tulitembea umbali mrefu, mdogo wangu Chiko akatuambia tumngoje anaenda kukata gogo (kunya)

Tulimngoja, tulikaa chini mwenye sigara aliwasha, mwenye bange lake alilipua, mwenye maji alikunywa.

Muda ulipita mara Chiko akarudi, na safari kuendelea.
Lakini kila tulipo muangalia usoni, macho yote yame badilika rangi nakua yanjano.

Tukampa maji na safari ikaendelea.

Hatukufika mbali sana, Chiko akaomba tumsubiri anakwenda tena kujisaidia.

Tilipu hii tulimngoja bila dogo kurudi, ikabidi mshikaji mmoja amfuate.
Alipo fika kule alimkuta chiko kesha kufa.
Jamaa akatuita tuje kumcheki, nikiwa mingoni mwao nilimkuta dogo amesha kauka pale alipo kaa.

Kwakua tangu tuna toka matandani tulishaambiana kua ugonjwa huu ni kipindu pindu, hivyo ukifa hakuna mtu alie thubutu kukushika.

Kwahiyo Dogo Chiko tulimuacha hapo na sisi kuendelea na safari.

Nitarudi muda si mrefu.
Ebola hio baba.
 
Kuna jamaa alianzisha stori ya jinsi alivyopata demu wake wa geita. Akaanza kuzingua analeta kipande kimoja kimoja kwa siku kadhaa tena kifupi. Aatokea jamaa akahadithia vilevile kama muanzisha stori na akaimaliza wadau tukaridhika na mwisho wa simulizi uliomaliziwa na stranger. Baada ya hapo uzi ulikufa.
Yule jamaa aliyemalizia anshitajika kwenye uzi huu asee..Arosto hatutaki🙄🙄
Hahaha.
 
Zamani sana pale jirani na kwa bamkubwa Chamwino kuna kakijiji kanaitwa nzuguni,kuliibuka Chimbo dhahabu inatema mi dogo tu wa 12-14,
nilikua najichanganya sana na maanko wangu alafu walikua watu wa vagi na ubwiii ile mbaya,
sasa walinipenda kwasababu mlinzi wao huko wakipakaza,likianzishwa nzegembe mi nachukua wallet na mali zote zinazohamishika kisha nayeya home.
Machimbo yalipoanza Nzuguni tulienda hawakuniacha bodyguard wao.
Duh kufika kule nilichoka jamaa anachosimulia ni kweli kabisa.
uzinzi,pombe,bangi, kila aina ya uasi unaukuta .ushangae sasa machimbo hata mwezi hayana.
sisi tulikua na kagroup ketu mtu nne wote mayanki tu na tulikua tunachakata vumbi tu lile.
siku kadhaa tukapatapata vimawe viduuchu yani kwenda kuuza tukagawana kahela kadogodogo tu.
Ila mi niliridhika nikasepa nikawaacha maanko maana wao hata ndoto ya kurudi hawana ilikua km wamefika nyumbani,sio hata wachimbaji wao ilikua ni pary pary tu.bangi pombe mabibi na daily wana hela wale jamaa aisee
Ila walikua mafundi malori wazuri sana KAUDO pale na Madereva.
Ule mgodi ulikatika ghafla tu,upo hapo Chamwino pembeni kushoto ukiwa unaenda kwa baba mkubwa.
Nzuguni gani hiyo ambayo iko chamwino
 
Baada ya heka heka ya kutwa mzima ya kuzikusanya kwa mafungu zile maiti, jioni iliingia na zoezi tukali simamisha.

Tukasogea pembeni na tukio, kama kawaida yetu, moto mkubwa ukalipuwa mwenye kulala ali lala, ila wengi hatukulala.

Tulibaki pale mpaka asubuhi, tukiwangoja wenzetu walio kwenda kijijini kununua petrol.

Kutokana na kijijini kua mbali ilikua ngumu kwa mtu kwenda leo kurudi leo leo.

Kwahiyo huku tukiwasubilia walio kwenda kijijini, tukaamua kuanza ujenzi wa Camp.

Tulijenga camps mbili, kwa haraka, ukizingatia miti imelewa, maturubai tuliyo yakimbia, ilikua ni kwenda kuamisha tu kwenye ma camp ya zamani.

Mpaka mida ya saa 8 mchana kazi ya kujenga camps ilikua ime kwisha, mavyakula yalikua ni yakusaza.

Maana ulikua unaingia tu ndani ya maduka yaliyo kimbiwa na wenyewe na kujichukulia unachotaka.

Kumbuka mpaka muda huu hakuna alie vuta bange, sigara wala pombe, japo tulivikuta.

Jioni ilipo ingia wale walio kwenda kijijini walirudi, na mungu ali saidia, jamaa walipata petrol.

Jamaa walirudi na kundi lingine la watu kutoka kijijini.
Hakuna alie thubutu kuwaeleza kua jana walivyo tuwacha tulizisachi zile maiti.
Siunajua mambo ya pesa.
Ukiwaambia lazima watataka mugawane.

Tukakubaliana usiku tukisha kula tuje tuzichome zile maiti.

Usiku ulipo fika watu wakaelea kuzichoma moto zile maiti.

Nakumbuka mimi nilibaki Camp, sikwenda kuzichoma moto.

Sikwenda kwa sababu mbili, kwanza kuchoka ukizingatia kuna mida kinyaa kinanijia.

Pili, muda mwingi nilikua nakaa peke yangu nikiangalia lile donge la dhahabu, akili ikiniambia, " nasubili nini hapa na ninacho kitafuta ninacho mfukoni"
(japo nilijipigilia mbeleni)

Wazo likaja kichwani, akija jamaa (Wamalawi) nilie sachi nae yule malehemu, nimshauri twende kijijini tukagawane ile dhahabu, kwakua pale polini hakukua na skeli (mzani wa madini).

Kuna kipindi akili inaniambia nimkimbie jamaa.
Yani pakikucha nimtoroke nirudi kijijini.
Kumbuka kazi zetu kudobana (kudhulumiana) ni kitu cha kawaida, ndio maana tulivyo fanikiwa kutoka na ile dhahabu nilijitahidi nibaki nayo mimi.

Kwanza huyu mwamba mwenyewe ni mtu na nusu.
Simuwezi kimapambano, labda nishike panga.

Nitarudi muda si mrefu.
Ila naapa kuimaliza leo.

Nilichomoka camp kwa tahadhari, sikutaka mtu ajue tena zaidi yule mmalawi (huyu ni mmalawi sio mrundi )

Mdogo mdogo huku mvua ikinichapa, nilipo hakikisha nime ziacha hatua kadhaa zile camp nikawasha tochi yangu ya kichwani moko yangu begani taratibu nasonga na njia.

Nilitembea mwendo wa masaa kama mawili hivi, mvua ikinyesha, uoga ukaanza kuniingia, japo tuchi yangu ilikua ikiwaka vizuri tu, lakini nilipata tabu kuona mbele.

Kuna muda nilikua natoka nje ya barabara, yani napotea njia, mara nimeingia kwenye mashimo, uoga ukanizidi.

Nimelowa mpaka boxa ya ndani, meno yana tetema mpaka yanauma, hapo natamani atokee mtu na bange lake anitembezee.

Nilizidi kutembea huku nikitetema, mkono nilio shika moko vidole vyote vimekufa ganzi, Kiufupi nilijiihisi naota.

Mbele kidogo kuna korongo limezunguka, kikawaida makorongo haya hupitishaga maji, natangu naiwaza hii safar akili yangu ilikua hapa kwenye korongo, sababu kwa mvua ile ni lazima ningeyakuta maji yame jaa, na hakuna njia nyingine.

Chaajabu nililikaribia korongo nakulikuta korongo kavu, yani kuna vimaji tu vya ugoko, yani hata suruali hukunji.

Hapa nili shangaa sana, maana si rahisi kwa mvua ile, sehem ile isijae maji.

Nilitambuka mpaka ng'ambo ya korongo, hapo nikaendelea na safari.

Kadri nilivyo kua natembea ndivyo sasa mvu ikawa inapungua na hata ka mwanga nikawa nakaona kwa mbaali.

Hapa nikaona ngoja sasa nitwete niwasubiri wale jamaa waolikusudia kurudi kijijini.

Nilipo kaa pale, usingizi ukanipitia (kati ya vitu ambavyo hatuwezi kuviamrisha sisi wenyewe ni usingizi na haja kubwa, binaadam anaweza kulala hata kwenye dimbwi la maji ) nililalaaaaaaaaaaaa

Nitarudi muda si mrefu
Ndugu zangu sifanyi kusudi sema ndio vivyo tusamehane.
Nimehangaika kulipata hili jina😬

Cc: Chumchang Changchum
 
Back
Top Bottom