Jimena
JF-Expert Member
- Jun 10, 2015
- 25,935
- 96,056
HatareeJamaa hanaga hiyana aisee anashuka na Likes mwanzo mwisho[emoji38][emoji38][emoji38]
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
HatareeJamaa hanaga hiyana aisee anashuka na Likes mwanzo mwisho[emoji38][emoji38][emoji38]
Jitahidini kupunguza lugha za migodini kwa faida yetu wotedaaah......nilihudhuria mlio wa bulyanhulu kila siku alfajiri unaskia watu wamekufa maduara yalikuwa karibu 2000 pale....na yalichimbwa karibu karibu sana ardhi ya pale teketeke juu tu ndo kuna lukili ila chini mtihani kila mzamo au nusu mzamo timber boksi moja na miti ghali hatari..
dhahabu hii..
kuna mshkaji aligorogosha kwenye duara moja ambalo wamelitoa bomba shafti maana jamaa walistukia wanachimba gesi pale wakaacha lilikuwa limeenda kama mizamo 7 hivi....jamaa akagorogosha alikuwa amelewa akaingiza mguu imoo! cha ajabu kufika ndani anamkuta msela mwingine nae aligorogosha jana yake hahahaha kapiga kelele mpaka sauti imeisha..
kumbe huyu wa pili wakati anagorogosha kuna kamanda alimuona basi akawastua jamaa wakaja wakawatoa kwahyo yule aligorogosha jana yake akapata msaada kupitia yule aliyegorogosha siku iliyofuatia..
pole kwa majanga mkuu hilo tukio ni siku nyingi?!...umesema kuangukiwa kifusi.....hamkuwa mnafunga timber?!...
Haya mashimo huwa yana urefu gani?Mkuu tulifunga timber ila kama siku yako huwezi kukwepa.. mpaka leo sisahau sauti zao dah inauma sana.. nakumbuka nilivyo ona hapa nakufa nika wambia washikaji kwa herini jamaa waliongea kwa uchungu kwahiyo unatuacha tunakufa dah... kushika kamba nimevutwa kufika kati kamba ikakatika nikarudi chini hapo nikajisemea moyoni huu ndo mwisho wangu.. dah jamaa chini wanalalamika mi niko hoi damu tu.. kipindi icho nilikua na miaka 17 tu mkuu.. nisingeweza kufanya kitu..
Tunapima kwa koleo kuna mengine koleo 25+Haya mashimo huwa yana urefu gani?
Daaah kweli hatujiwez kwa wazungu[emoji23][emoji23]Baada ya kubembelezwa saaaana huko DM kwa kutumiwa hadi wadada kuniahidi tunu basi nimebadili mawazo sasa nitasimulia habari ya safari yetu ya kutafuta mali (RUPIA) humo msitu wa NYUMBANITU
(achaneni na utani wa hapo juu) sasa twende taratibu,matukio mengi nitafupisha tu kufanya story kueleweka
Kwa wasiojua...Nyumbanitu iko Njombe wilaya ya wanging’ombe kuna mahala panaitwa Mdandu huko,ni msitu wenye habari za kutisha sana wenyeji wa huko hakuna sehemu wanapaheshimu kama hapo
Huu msitu cha kwanza uko na wanyama wasio wa kawaida kabisa na wanapatikana huko tu,kuna kuku fulani weusi tiii na midomo myekundu,hawa wanaishi humo na hakuna anayewahudumia kwa chakula wala matunzo...pia kuna ng’ombe n.k wote hawa ni kwa ajili ya matambiko ya makabila mbalimbali ya mkoa wa Njombe,zamani ikiwa wilaya ya Iringa,,haswa wabena na wakinga.
Kuna ukoo kule unaitwa wa akina Mkongwa,hawa ndio wamiliki halisi wa huo msitu na inasemekana wao wakifa huwa wanageuka kuwa nyoka na wanaishi huko kwenye huo msitu...kwa waliofika kutalii kuna wazee wako nje huwa wanatoa maelekezo ya namna ya kuingia humo na mila za humo,kama una roho nyepesi unaweza ishia tu kufika mlangoni ukarudi zako ulikotoka...unapigwa mkwara mlangoni na moja kati ya issue unapaswa kujipanga ni kwamba kama mwanamke usiende ukiwa kwenye HEDHI sababu mizimu humo ikisikia tu harufu ya damu wote mlioongozana na huyo mnapotea na hamuwezi onekana hadi wazee wa mila wafanye yao...
achana na hayo...
kilichotutia tamaa sisi kuhusu humo ndani ni story za uwepo wa RUPIA za mjerumani bwanaaa...na hakika zipo na zilikuepo,tulichogundua wale wazungu washenzi sana,hii ya kujenga hofu watu wasiende humo kwa kujiamini ndio imefanikiwa kuziacha mali zao salama mule msituni...wazungu akili nyingi sana,humo wamepandikiza uchawi mkali sana na unalindwa na hao wazee wa mila bila wao kujua wanalinda mali za watu....
ilikua 2001 mwezi wa 12 sasa tukiwa na jamaa zangu tukapanga mkakati wa kuingia mule bila kufata sheria zao za kichawi...maana ukifata protocal kuna maeneo huruhusiwi kufika na ndio inasemekana yana mali
kuna mapango makubwa inasemekana yakitumika wakati wa vita...kwa story tulizopata ni kwamba hizi mali zimefichwa kwenye masanduku makubwa yananing’inia kwenye mapango/mahandaki yaliyoko ndani kabisaaaa wanakosemaga ndio anakaa mzee mwenye msitu,ingawa kikweli huko sababu ya giza na kutisha basi kumekua makazi salama ya nyoka wakubwa wa kila aina na hao kuku wa kichawi ndio chakula chao...
tukiwa tumejipanga,plan ilikua ni kazi ya usiku mmoja tu tunamaliza tunarudi na mali na utajiri wetu...kulikua na habari kwamba soko ya rupia ni uhakika...
nikirudi naanzia sasa kwenye safari yenyewe kuingia msituni nyumbanitu
..........
Kwann hao majini wanaosimuliwa wengi wao wakijigeuza kuwa binadamu huwa wanakuwa na asili ya kiarabu na isiwe mzungu, mchina, mjapani au muhindi?Kuna uhusiano gani kati ya waarabu na majini?
Kuna mkuu alisema huko juu kwmba inasaidia hata Kwa wanaume piasiku amemaliza period anaoga vizuri halafu anapaka juu juu tu.....then baadae akioga athari inapotea..
usiwe muoga sana......wewe kama binadamu kuna jini unatembea nae muda wote kama umejilea kufanya mema anakuwa dhaifu na nguvu za kukushawishi zinakuwa kwa kiwango kidogo sana.....na kama ni muovu anakuwa na nguvu sana na ushawishi wake unatawala maisha yako.....anapenyeza wasiwasi na ushawishi direct kwenye moyo wako na unafanya .....so usiogope sana..
usiwe muoga sana......wewe kama binadamu kuna jini unatembea nae muda wote kama umejilea kufanya mema anakuwa dhaifu na nguvu za kukushawishi zinakuwa kwa kiwango kidogo sana.....na kama ni muovu anakuwa na nguvu sana na ushawishi wake unatawala maisha yako.....anapenyeza wasiwasi na ushawishi direct kwenye moyo wako na unafanya .....so usiogope sana..
ahahaahahaha allah amridhie.....na wewe ndo uko hivyo!?..
daah na matatizo yametokea kimgodi mgodi mkuu na hivyo vitu vingi kiswahili chake ndo hicho.....sasa kitu kama bomba shafti nitakutafsiriaje?!..Jitahidini kupunguza lugha za migodini kwa faida yetu wote
Unaweza kuandika kitu kizuri ukaishia kuelewana na wenzio wawili tu
okay kwa ufupi sana bila kuchosha watu.....jini ni kiumbe kama mimi na wewe na aliyekuumba wewe ndio alomuumba jini....na malengo yalomleta jini duniani ndio yaleyale yaliyokufanya wewe uwe hapa duniani pia.....tofauti yenu kubwa wewe unaonekana yeye haonekani lakini anakuona wewe....na wewe umeumbwa kwa udongo yeye ameumbwa kwa ndimi za moto yeye akiwa muovu na akimuasi aliyemuumba anaitwa shetani na wewe ukimuasi aliyekuumba unaitwa muovu na unakuwa na daraja ndogo sana mbele za muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo kiongozi wao ni ibliys yeye ni wa zamani sana na yuko duniani kutafuta kundi na wafuasi watakaoingia nae motoni siku ya mwisho kwani tayari anajua hukmu yake .....mwisho yeye ana uwezo fulani wa ziada na wewe huna....lakini hana mamlaka yeyote zaidi ya kuwa mja wa muumba kama ulivyo wewe.....kumtumia kwenye kukusaidia mambo yako kama kurudisha kitu kilichopotea....kukuletea mali....chakula....kukupa mafanikio ni ushirikina..Jini ni nani na anapatikana ulimwengu gani kwa mujibu wako. Mimi ni wa Yesu alie hai....yule aliekufa kwaajili yetu na kufufuka....Nipo ktk ukimwengu wa nuru sio wa giza.
Na wewe mwenye kusema shake na si shaka ni kabila gani?
kwa mwanaume niliskia inasababisha achelewe ila sina ushahidi kwenye hili mkuu wangu..Kuna mkuu alisema huko juu kwmba inasaidia hata Kwa wanaume pia
hahahaa nimecheka sana.....mkuu mchawi hakutishi odds zikienda upande wake anakunyoosha vizuri tu....uchawi unaleta maradhi, ulemavu, utasa na hata kifo..DADECK. ..
Nilikua nauchukulia poa huu Uzi, maana nilisomaga post ya kwanza post ya pili nikaitafuta wee nikaikosa so nikaamua kuachana nao, Leo nimesoma wooote. MAZEE hii dunia ni zaidi ya ujuavyo nimesoma hapo mikasa ya majini n.k daaaah moyo umeingia baridi sana.
Sisi watoto wa maskani tunaona kama movie vile lakini kiukweli watu mmepitia msoto. Binafsi sijawai kuona mchawi wala jini.
scenario ya kichawi ninayo kumbuka labda kukututana na vitu njia panda vimepasuliwa, picha linaanza nimeamka nawai shule Mimi na dogo flani mida ya asubui tayari jua limechomoza tumefika njia panda tukakuta mayai, Nazi na vitu vingine vimepasuliwa pia kulikua na shilingi kama 20 zilikua nyingi nyingi, so watu walikua wanapita wanaogopa nilipofika na yule dogo tukachukua zile chenchi zilizokuepo (zile shillingi 20)....Siku hiyo ilikua murua tulikula mandazi na barafu za kutosha pale Pamba primary......kila Siku tulikua tunapita hiyo njia tuone nani mwingine ataweka hela hapo.
Scenario ya pili nilipokua Chuo na mshikaji wangu tumetoka club, pikipiki ikaogopa kuendelea so tukaamua tutembee kwa mguu mida ya saa 9 kasoro usiku, kwa mbele njia panda tukamuona mtu hivi so kwasababu kulikua kuna vichaka tukapitia vichakani huku tunanyata. Dah kumbe alikua ni mwanamke anaoga alikua anapasua na nazi kitu kama hicho, mshikaji wangu akanambia hapa tusiondoke tuangalie mpaka mwisho (nadhani lile umbo la Yule mama lilichanganya). Daah kwa upande wangu nilitamani nimuibukie yule mwanamke pale sema uoga pia ulichangia, alimaliza mambo yake akasepa na sisi tukasepa nikaenda kupiga nyeto kwa kupitia taswira ya yule mwanamke.
Scenario ya tatu nimemaliza kucheck movie Nipo geto nataka kulala (nilipokua Chuo ) Mara nasikia juu ya bati kishindo Mara paka wanalia nje nikaona huu ni udwanzi, nilikua na Panga langu nikatoka nalo nje nikaanza kujiongelesha huku nikiwa nimejaa uoga ""oyaa acheni ungese kama mnajiweza jitokezeni tukutane" nikarudi ndani huku uoga umejaa nikasali nikalala sikuwai kusikia tena mpaka nimegraduate.
Kitu ambacho Baba alinambia katika maisha kuna nguvu mbili zina operate ni Nuru pamoja na Giza it depend na wewe huko wapi lakini vyote vinanguvu na vinafanya kazi.
Kuna kipindi mzee wangu alinihadhitia tulipokua wadogo aliamka asubui akakuta mtu kapasua Nazi mlangoni pamoja na karatasi ina maandishi ya kiarabu hakuwaza wala hakujipa time kufatilia tafsiri yake, alichoma hicho kikaratasi then akapiga ombi na mpaka leo anadunda na anao uwezo wa kufanya mambo yake ya maendeleo.
Mwisho, nitaogopa usiku nikikutana na mwizi au jambazi maana nitatumia akili nyingi kumzuia physically na sijui amebeba nini, ila siwezi muogopa mchawi maana yeye awezi kukupiga anafanya kunitisha . Ikitokea siku endapo nikipigwa kofi na mchawi na nisione kofi limetokea wapi hapo ndipo nitatoka barutiiiiiiii....