Tukisema ligi ya EPL ndo kipimo Sahihi kwa Makocha na Wachezaji Tutakosea?

Tukisema ligi ya EPL ndo kipimo Sahihi kwa Makocha na Wachezaji Tutakosea?

Wewe wasema, haya twende EUROPA nazani Liverpool yako haina hamu na sitaki kuongelea UEFA maana huku ni majanga matupu
Football inamawanda mkuu, mbinu anazotumia mwenzako sio utakazotumia wewe, nakubaliana na wewe ligi ya uingereza haina ufundi na hata wakikutana na wababe wa ligi nyingine wanahangaika Ila napenda ushindani wake hakuna timu kubwa wala ndogo ukizubaa unaliwa
 
Ningesema Vilabu vya Uingereza ni bora kuliko Vingine sawa ila kwa leo nipo upande wa Wachezaji na Makocha.
Na kama ni hivyo, unamzungumziaje Antonio Conte wa Chelsea huu ni msimu wake wa kwanza ila anafanya vizuri pia, Kuna Jurgen Klopp pia.
 
Nadhani ni kwa kipindi hiki tangu msimu wa 2012 umalizike ndio timu za uingereza zimeanza kufanya vibaya kwenye mashindano ya ulaya.

Miaka ya 2005-2010 timu za uingereza zilisumbua sana ulaya. Ilikuwa ni jambo la kawaida nusu fainali UCL uingereza kuingiza timu 3, kama ilivyokuwa kwa italy miaka ya nyuma.

Nadhani huu ni muda wa spain kutamba kabla haijapokeza kijiti kwa nchi nyingine, na utaratibu huu utaendelea kwa miaka mingi.

Kila zama na nabii wake, iko wapi brazil ilokuwa ikisifika kwa kutandaza samba maridadi uwanjani?, vivyo hivyo kwa uingereza, nina imani msimu ujao UCL uingereza watarudi kwa kasi na kurudia makali yao ya zamani.
 
Yeah kuliko kuangalia katimu kanabahatisha kuchukua EPL alafu msimu unaofuata kapo kwenye hatihati ya kushuka daraja
Hiyo inaitwa second season syndrome, ila kwa leicester imechagizwa zaidi na udogo wa kikosi chao.
Ili kuendelea kupambana kwenye nafasi za juu leicester ilitakiwa isajili wachezaji wa kiwango cha juu zaidi ili waweze kusaidiana na wale waliopo kuendeleza ila bahati mbaya au nzuri hawakusajili majina makubwa mengi.
 
Kinachoifanya ligi ya uingereza kuwa inatamba ni uwekezaji mkubwa wa timu hasa kiuchumi yaani timu nyingi uchumi wake hautofautiani sana sasa angalia LA liga au bundersliga ukitoa Dortmund na munchen hakuna timu zenye uimara wa kushindana nazo. Angalia Felix magath alichukua ubingwa na werder Bremen alipoenda Fulham akashindwa kufanya chochote,hata pep ameshindwa kuendana na kasi ya ligi kuu
Umeanza vizuri ila conclusion yako imekinzana na main point yako, uwekezaji wa Manchester City na Leicester city unauzungumziaje?
 
kuna yule director wa Barcelona kafukuzwa kazi kisa kasema messi bila wenzake hawezi cheza mpira.

Akija pale akutane na watu kama kina Charlie Adam,Sharwcross,Cahil,Rojo anaweza kukaa nje mwaka mzima kwa ajili ya majeruhi.
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Kichaa tu ndiye anayeweza kuamini hayo mawazo yako "EPL ni kipimo tosha cha makocha na wachezaji"

Pep Gurdiola amezoea vya kunyonga na vyakuchinja haviwezi na kinachomkumba hapo Man City ni kipimo tosha kuwa yeye si kocha mzuri bali ni mtu aliyezoea kudandia mafanikio ya watangulizi wake ...
Man City wana uwezo wa kifedha na si uwezo wa timu kucheza mpira na hili ni tofauti na wakati Pep anaichukua Barcelona & Bayern Munchen uwezo wa kucheza mpira walikuwa nao vile vile uwezo wa kiuchumi wanao, hivyo basi tunasema hana jipya na ndicho kilichomtokea pale Bayern..
 
Mimi Kwajinsi nilivyofwatilia hizi ligi naona ligi bora ni laliga ikifwatiwa na bundesliga alafu ndo Epl.Epl ni ligi yenye uwekezaji mkubwa kibiashara na vyombo vya habari ila linapokuja kwenye swala la soka safi la kuvutia na lenye vionjo hakuna,wao nikukamiana basi.Ila laliga unapata soka safi na lenye vionjo na hakuna mbwembwe nyingi.Bundesliga nao wako nusu nusu,kuna soka safi na butua butua.Ila kama mtu ni mpenzi wa soka lakuvutia acheki ligi ya brazil,argentina na uholanzi.Sema kwa miaka ya karibun lile soka lavionjo lakuvutia limeshapita,nadhan okocha,zidane na gaucho ndo wamelimalizia sasa hivi imebaki kukimbiza tu.Ni wachezaj wachache sana wanaleta vionjo ila ule mshawasha kama enzi za hao jamaa kurud nyuma hakuna.
 
Unamzungumziaje Zlatan mliokuwa mkimbeza alipokuwa La liga, Serie A na Ligue 1 kwamba yupo ligi dhaifu, lakini ona anavyowapa shida mabeki wa EPL. Unazungumziaje wachezaji kama Sanchez na Ozil, walivyokuwa wakikalia bench kile la liga na sasa ndo mastaa hapo EPL. Kinachomuangusha Pep ni wachezaji alionao, umri umeenda sana lakini sio kocha dhaifu hata kidogo.
Ongeza Diego Costa, Pedro, Fabregas n.k
 
Inawezekana isiwe lig bora kwa maana ya mpira mnaoutaka
Ila Ni lig ambayo ina ushindan mkubwa kuanzia team ya kwanza mpka 20
Umemaliza mjadala, hata Ligi yetu bongo ina ushindani mkubwa saana lakini haimaanishi kwamba ni bora.

EPL hamna kitu zaidi ya matangazo tu.
 
Kichaa tu ndiye anayeweza kuamini hayo mawazo yako "EPL ni kipimo tosha cha makocha na wachezaji"

Pep Gurdiola amezoea vya kunyonga na vyakuchinja haviwezi na kinachomkumba hapo Man City ni kipimo tosha kuwa yeye si kocha mzuri bali ni mtu aliyezoea kudandia mafanikio ya watangulizi wake ...
Man City wana uwezo wa kifedha na si uwezo wa timu kucheza mpira na hili ni tofauti na wakati Pep anaichukua Barcelona & Bayern Munchen uwezo wa kucheza mpira walikuwa nao vile vile uwezo wa kiuchumi wanao, hivyo basi tunasema hana jipya na ndicho kilichomtokea pale Bayern..
Tangu siku Pep anaaga pale Barca, niliamini kuwa Pep sio kocha. Kiufupi ni kwamba jamaa alimkimbia Mourinho, Period! Mm ni shabiki wa Barca na najua ninachokiongea.

Timu ilianza kuyumba kutokana na ushindani mkubwa aliokuwa akiupata kwa Mourinho, na Pep alikuwa hana kabisa Plan B. Timu kubwa zilikuwa zinapark bus tu, kwisha habari yake. Now hatuoni Barca tukifanyiwa huo mchezo.

Pep kabeba Barca ikiwa tayari timu inacheza soka vyema na tayari timu ilikuwa ktk Good condition, kaenda Bayern kipindi ambacho ni mwaka wa 4 sasa kama sio wa 5 Bayern anafululiza yeye tu makombe Ujerumani. Hakika mimi nakwambia Bayern hata isipokuwa na kocha ujerumani kwa mwaka mzima, kombe la Ligi wanabeba. Kule Jukwaa la Barca zamani nilisemaga Pep HATOBEBA UEFA NA BAYERN! Kaondoka Bayern bila Uefa.

Kaenda EPL akitarajia atakuwa ni mungu mtu, amesahau kuwa EPL timu 5 za juu hazina tofauti kubwa sana ya kiwango na timu 5 za chini. Hii ni tofauti na German na Spain.
 
Kinachowashinda EPL ni team zenyewe. Uingereza haina team zenye wachezaji wenye nguvu kama tuchukulie La liga.
Mfano ukichukua team zinazorank duniani ni Chelsea inakuja ya tano. lakini La liga inaanza Real Madrid, inafuata Bayern Munchen, Barcelona, Juventus then Chelsea, then Atletical Madrid, Borrusia Dortmund, Arsenal, Benfica, PSG, kwa hiyo unaona katika kumi Spain ziko tatu. angalia First 11 wa fifa utaona majina mengi yanatoka Spain.
Christiano Ronaldo, Lionel Messi and Neymar (attack). Midfield Andres Iniesta, Paul Pogba (EPL), Luka Modric. Defence: Marcelo, Thiago Silva, Sergio Ramos and Dan Alves (all Spain) Keeper Manuel Neuer (Bundasliga)
Kwa hiyo utaona ni wachezaji wangapi wameunda frst eleven je ukiwa kocha utapata shida kuwafundisha?
Kwa Pogba ondoa hiyo EPL, ameingia hapo kutokana na Juhudi zake kule Juventus na sio EPL. EPL ni maiti.
 
yaani kocha bora ranieri lakin hakuna mchezaj wa timu yake aliyestahili kuingia kwenye kikosi cha dunia!?..inaingia akilin?..hivi kantelele hakufaa kuingia hapo,calwalker hakufaa,coutinho,sanchez,koscielny
Embu taja sehemu ambazo wangechukua hao wachezaji uliowaorodhesha. Mfano hao akina Sanchez, Ozil n.k
 
Jana nilikuwa naangalia game ya Man u vs liver ,sikuona ladha yeyote ile butua butua sana ,mipira mingi inarudishwa kwa kipa kisha kubutuliwa ,timu zote zilikuwa zinapoteza mipira sana ufundi hakuna

Usiku nilitizama game ya Sevilla vs real Madrid hakika nilitamani mpira usiishe ,mpira unachezea chini ,ufundi ,passing ,tactical nk

Pressing ,passing ,ufundi wa kila namna ulikuwepo ,huoni mpira ukipigwa juu hovyo au pass mbovu ,dribble za uhakika

Real Madrid ,Barca ,Atletico ,Sevilla watatawala sana ulaya kwa namna hii

Na hao leceister kazi wanayo kwa mpira wao wa kupaki basi dhahma itawapata kutoka kwa Sevilla

EPL bla bla halafu mguuni mpira mbovu butua butua. Ndio mechi za ulaya huwa wanaishia kupaki basi tu
ha ha ha ha wapasulie kaka!
 
Back
Top Bottom