Tukubali au tukatae kwenye hii sayari ya Dunia katika nyanja ya Soka hakuna kama Pele wa Brazil

Tukubali au tukatae kwenye hii sayari ya Dunia katika nyanja ya Soka hakuna kama Pele wa Brazil

Hat-trick 92 maisha yake yote
Mabao 4 mara 36 maisha yake yote
Mabao 5 mara 6 maisha yake yote
Mabao 8 mara 1 maisha yake yote

Miguu yake yote ilifunga magoli yasiyo na idadi
Kichwa chake kilifunga magoli yasiyo na idadi
Alikuwa na chenga ambazo aliemzidi ni garincha tu
Alikuwa na kasi ya sunami uwanjani
Ndiye mchezaji aliefunga bao bora kuwahi kitokea duniani santos vs juventus

Amecheza match 1385 katika maisha yake yote ya mpira kuliko mchezaji yeyote

Amefunga mabao 1280 katika maisha yake yote ya soka kuliko mchezaji yeyote

Bao lake la 1000 alifunga kwa penalty na mashabiki waliingia uwanjani kusherekea bao hilo kitu kilichopelekea mpira kusimama kwa nusu saa kuwaondoa watu uwanjani

Alianza soka la kulipwa akiwa na miaka 15 tu
Na hat-trick yake ya kwanza alifunga akiwa na miaka 15 mwaka 1956

Brazili haijawahi kupoteza match pele akiwa uwanjani

Takwimu ndio kila kitu zaidi ya hapo ni kudanganyana tu

Jamaa amechezea team 2 tu maisha yake yote huku akitumia muda wake mwingi santos

Fifa wanamtaja kama mchezaji bora kuwahi kuonekana duniani mpaka leo

Ni mchezaji pekee katika hii dunia alietwaa kombe la dunia mara tatu huku akiwa tegemeo kubwa kwa taifa lake la brazili
Mchezaji pekee aliekuwa akiumia mchezoni mashabiki wake wanamlilia mpaka arudi uwanjani

Na huyo ndiye mfalme wa kandanda duniani PELE
Hakuna siku alifunga mawili, moja na kutoka kapa?????[emoji36][emoji36][emoji36]
 
Nimecheki video nyingi sana za pele YouTube lakini nimeona ni mchezaji overrated tu hana lolote.

Hawezi gusa moto wa maradona na Messi.
 
Huyo Pele alitwaa vikombe gani vikubwa upande wa vilabu??
Kwako makombe makubwa ni yapi..

Campeoneto paulista 10
Seria a 6
Copa libertadores 2
International cup 2
Torneio rio sao paulo 4..

Hapo ni santos,

Akaenda kumalizia soka lake marekani baada ya kuombwa kwenda kulitangaza, soka la marekan sizungumzii alivyobeba huko
 
Ni waenga wenzio tu ndio watakuelewa hayo mapambio yako ila sio kizazi hiki cha King Messi.
 
Pele alifunga goli mbili ambazo kutokana na uhaba wa teknolojia hazikuwa kurekodiwa kuna hilo vs juve ambapo aliwapiga vidali mabeki 2/3 hiv na kipa nae akala kidali mwanaume akatupia kambani
na kuna jinginr linaitwa gol de la placa hilo hata maradona hakufunga lisake hilo, aliwala vyenga karibia timu pinzani yote.. Inasemekana ndio goli bora kufungwa katika nyasi za maracana.

Kutokana na uhaba wa teknolojia matukio ya pele yaliyowahi kirekodiwa ni 30% tu ya mabalaa yake yote uwanjani
Asante mkuu nimekukubali
 
Hawana akili
Hizi takwimu messi hana hata robo

Kuwa mstaarabu mkuu. Unavyosema hawana akili ndio mojawapo ya sifa!!!!! Naona umekuja na jazba sana baada ya kuona jana kile alichokifanya mfalme, hayo ni kawaida sana kwake ukizingatia anakutana na magreat teams, so ukaona uje umpambe babu yako na kumpigia mafumbo Mfalme sio? Tumia kauli nzuri mkuu, na hayo ni maoni yako tu, usilazimishe na wengine wakufuate unachoamini
 
Nonsense! Pele mwenyewe hajawahi kucheza soka ulaya. Kwa ubora wake alitakiwa angalao avae hata jezi za sporting lisbon au hata porto achilia mbali Barcelona na Real Madrid. Hajakutana na mabeki wenye roho mbaya kama Nigel de Jong au Frank Lebouf. Yeye alikuwa anapiga watu chenga wanamwachia tu.

Btw kwa mujibu wa matokeo ya kumtafuta mchezaji bora wa karne aliyeibuka mshindi sio pele. Hapa aliibuka Diego Armando Maradona. Fifa kwa fitna zao wakasema tuzo wapewe wote Maradona na Pele. Kwa madai kwamba Maradona ndani ya uwanja kwwli alikuwa nyoko ila nje ya uwanja alikuwa ni mtovu wa nidhamu mla madawa nk

Wakati wakikabidhiwa tuzo Maradona alisema NIPO HAPA KUPOKEA TUZO HII NILIOPEWA NA WAPENDA SOKA KOTE ULIMWENGUNI, NA SIPO TAYARI KUSHEA NA MTU MWINGINE. HII NI YANGU PELE MTAFUTIENI YA KWAKE.

Upo sahihi kabisa Mkuu. Na evidence ipo na wakibisha nitaileta hapa
 
Messi ni zaidi ya Pele. Sidhani kama Pele angekatiza mbele ya Rio Ferdinand ktk ubora wake.
Pele hamna kitu, alicheza na MIZEE enzi hizo alafu mpira wake hata kwa kuuangalia haina mvuto wowote. Anabebwa sana huyu jamaa. Maradona pia kamuacha mbali sana Pele.

Upo sahihi kwa %100. Watu mnaoujuwa mpira....
 
Nonsense! Pele mwenyewe hajawahi kucheza soka ulaya. Kwa ubora wake alitakiwa angalao avae hata jezi za sporting lisbon au hata porto achilia mbali Barcelona na Real Madrid. Hajakutana na mabeki wenye roho mbaya kama Nigel de Jong au Frank Lebouf. Yeye alikuwa anapiga watu chenga wanamwachia tu.

Btw kwa mujibu wa matokeo ya kumtafuta mchezaji bora wa karne aliyeibuka mshindi sio pele. Hapa aliibuka Diego Armando Maradona. Fifa kwa fitna zao wakasema tuzo wapewe wote Maradona na Pele. Kwa madai kwamba Maradona ndani ya uwanja kwwli alikuwa nyoko ila nje ya uwanja alikuwa ni mtovu wa nidhamu mla madawa nk

Wakati wakikabidhiwa tuzo Maradona alisema NIPO HAPA KUPOKEA TUZO HII NILIOPEWA NA WAPENDA SOKA KOTE ULIMWENGUNI, NA SIPO TAYARI KUSHEA NA MTU MWINGINE. HII NI YANGU PELE MTAFUTIENI YA KWAKE.
Umesahau kipindi Pele anacheza Mpira, faulo ilikua kuanzia kiunoni kuja juu, marefa hawakua wakiwalinda Wachezaji Masuper star kama Leo!
 
Ndiye mchezaji aliefunga bao bora kuwahi kitokea duniani santos vs juventus

Hapo red goal of century alifunga Diego Maradona. Nusu fainal kombe la dunia 1986 kule mexico dhidi ya chamdomo England. Alipiga chenga mabeki wa5 kabla ya kumrudia beki mwingine na kumfunga Peter Shilton


Fifa wanamtaja kama mchezaji bora kuwahi kuonekana duniani mpaka leo
Sio kweli. Tuzo ya mchezaji bora wa karne alipewa na wapenzi wa soka duniani na kukabidhiwa na fifa wakimshirikisha Pele ambaye alishindanishwa na kubwagwa na Maradona.

Mkuu upo vizuri sana katika kuchambua. Na umeongea true kabisa.

  1. Maradona alipata 53.6%
  2. Pele 18.53%
  3. Roberto bagio wa italy 5.42%
  4. Romario wa brazil 1.69
 
Mkuu upo vizuri sana katika kuchambua. Na umeongea true kabisa.

  1. Maradona alipata 53.6%
  2. Pele 18.53%
  3. Roberto bagio wa italy 5.42%
  4. Romario wa brazil 1.69
Hizo ni za mashabiki vilaza kwa sisi tunaoujua mpira maradona ni namba 3
1 pele
2 messi
 
Wewe na akina nani mnaojuwa mpira??? Sikiliza hayo ni maono yako tu na usiwajumlishe na wengine mkuu.

Messi
Maradona
Pele
De stefano
Zidane n.k
Unaonyesha jinsi usivyoujua mpira ndugu
Mpira ni takwimu kama unazo toa za messi
Toa za maradona
Ili tuone kama wamemzidi Pele au laa
Sasa unaongea bila takwimu hapa nani mwenye akili atakuelewa?
Kwa sisi tunaoujua mpira duniani kwa upande wa soka Pele ni namba 1 mpaka sasa labda tumsubiri mwingine lakini sio messi wala maradona wala yeyote kwa sasa
 
Back
Top Bottom