Tukubali tu: Sisi wajinga... (I know, it hurts)

Tukubali tu: Sisi wajinga... (I know, it hurts)

Mzee Mwkjj, watanzania siyo wajinga, ni maskini na wasiojiamini! Lakini viongozi wetu ni wajinga wakubwa!

Mmmh, ya kweli hayo??? Umeona yaliyotokea kule kwetu Ntuzu kuhusu vijisenti??? Yaani unataka kuniambia umasikini na kutokujiamni ndio kuliko wasukuma wale wasukuma wenzangu kumpokea chenge. Kibaya zaidi wakasikiliza na hotuba yake!!!
 
Ukiwa na watu masikini na wasiojiamini halafu wakachagua watu wajinga, combination hiyo inatisha wangu!

Duh! ebwana leo unawapatia kishenzi watu humu ndani na vi-comebacks vyako. Yaani una-sound kaa mimi vile. Mega kudos!!
 
Kama aliyosema Prof. Ndulu ndio ukweli wenyewe, nini basi kifanyike?
1. Kampuni yoyote ya Kigeni inayofanya kazi Tanzania lazima isajiliwe kwa mujibu wa sheria za Tanzania.
2. Kampuni yoyote ya Kigeni inayosjiliwa kufanya fanya kazi Tanzania lazima iwe na account ya benki katika benki za Tanzania na
malipo yote kwa kampuni hiyo yafanywe kupitia accounti ya Tanzania.
3. Ikisha sajiliwa na kuwa na account ya Tanzania ni lazima ijisajili kama mlipa kodi TRA.
4. Itakuwa ni jukumu la TRA kufatilia makampuni yote yaliyosajiliwa kuhakikisha yanalipa kodi kulingana na mapato wayapatayo (Faida), kwa kazi za ujenzi wazifanyazo nchini kwetu.


Tatizo la mikataba mingi ya kimataifa kuna kipengele huwa kinawekwa kwamba kodi zote zitalipwa na client na siyo consultant. Matokeo yake mwenye kazi anamlipia kodi consultant/contractor. Kwa nini, sheria zetu za kodi zimekaaje?

kwamba kuna sheria inayoweza kumfanya mwekezaji aondoke na fedha zote alizochuma Tanzania na inaruhusu remittance iende huko ng'ambo.

kama asilimia 70 ya wakandarasi ni wageni... kuna ugumu gani wa kuhakikisha kuwa mapato wanayopata kiasi kikubwa nacho kinabakia Tanzania? Kwa mfano, tumepewa hizi bilioni 700 na US, sisi tukashangilia; na zimetolewa kwa ajili ya miundo mbinu nk sasa tutakapotaka kuleta mkandarasi na wamarekani wakatuambia tutafute mkandarasi wakwao ina maana when it is all said and done, kiasi kikubwa "tulichopewa" kinarudi Marekani!!

huu ni ujinga.

Ninavyoelewa mimi yote haya yapo kwenye statutes. Makandarasi wote wanatakiwa kuandikishwa na CRB. Hauwezi kuandikishwa kama hautambuliki kisheria kuwa una haki ya kufanya biashara Tanzania. Makandarasi wa kigeni ni wale ambao majority shareholders ni kutoka nje. Yako ya kutoka Kenya (Mugoya Construction and Engineering waliojenga Shoprite ya pale kamata na nasikia washakua mufilisi kutokana na tuhuma za rushwa n.k), ya wachina, ya wamisri, ulaya n.k. haya makampuni yanaajiri watanzania, yananunua saruji yetu, mchanga wetu, kokote yetu n.k. kama mkandarasi yeyote kuna vifaa ambavyo vinaagizwa kutoka nje lakini hivi mkandarasi hana maamuzi nazo bali ni konsaltant. Mengi ya haya makampuni ni miongoni wa walipa kodi wakubwa nchini. Makandarasi wa nje wanalipa ada kubwa kuliko local contractors. baadhi ya hawa makandarasi ni menejimenti kontraktors yaani wao wakipata kazi wanasub-contract, mara nyingi kwa specialised kontraktors wazawa na wageni! Mpaka sasa sijaona kinachogomba.

Tunaposema kuwa asilimia 70 ya miradi wanachukua makandarasi kutoka nje tunazungumzia value na sio quantities. Hawa wanafanya miradi ambayo ni lazima nikiri kuwa ni makandarasi wachache if any wazawa wana uwezo nazo. Quantity wise sehemu kubwa mno ya miradi, tukianzia ujenzi wa madarasa Rufiji mpaka hayo makasri ya Mbezi Beach na maofisi ya serkali n.k. inafanywa na makandarasi wazawa. Kwenye miradi mikubwa wengi hawana uwezo na hatuna luxury ya kuexperiment at that scale. Naamini iko siku yatachipuka makampuni yetu ambayo yataweza lakini wakati huo sio sasa.

Ninavyoelewa ni kuwa kinachokuwa remitted ni faida ambayo nielewavyo mimi ni haki ya mfanyabiashara yeyote kupeleka faida yake kokote anakotaka ili mradi atimize vigezo vya benki kuu. Kama ni hivi kweli basi kwa nini basi tuwalaumu wenzetu kwa kufanya ambacho hata sisi tunaweza kufanya?

Hiyo ya mikataba ya kimataifa sijakuelewa. Ninachojua lakini I stand to be corrected kuna issue ya reciprocity kwamba kuna nchi tumekubaliana kuwa hakutakuwa na double taxation. Uwezekano mwingine ni kuwa katika hii misaada siku hizi huwa tunatakiwa kuchangia kwa imani kuwa kwa kufanya hivyo tutajisikia kama miradi hiyo ni yetu. Mchango wetu basi inawezekana ikawa ndiyo hiyo misamaha ya kodi maana mara nyingi uwezo wa kutoa fedha taslimu huwa hatuna!

Mkuu, Mzee Mwanakiji! Naona tumeanza kuwa masochists na wapenda self flagellation wakati wowote panapotokea matatizo. Kwa nini tunakimbilia kujihukumu wote kama jamii kwa matatizo ya watu wachache?
 
Fundi Mchundo, nimekusikia vizuri na pointi zako zinakubalika kabisa.

a. Je makampuni ya kigeni yanasimamiwa kwa kiasi gani katika kuendesha biashara zao Tanzania?

b. Je kuna sheria ya namna gani inayohakikisha kuwa menegiment ya kampuni ya kigeni nchini iwe?

c. Je faida wanayoipata Tanzania wanailipia kodi kwa kiasi gani?

d. Je mfumo tulionao sasa unaweza kwa namna yoyote kuboreshwa ili kuhakikisha kuwa mapato yanayopatikana nchini mengi yanabakia nchini pia?

Sidhani kama kuna nchi iliyoendelea ambayo inaacha kampuni ya kigeni kuchukua faida yote na kuipeleka kwao!
 
Fundi Mchundo, nimekusikia vizuri na pointi zako zinakubalika kabisa.

a. Je makampuni ya kigeni yanasimamiwa kwa kiasi gani katika kuendesha biashara zao Tanzania?

b. Je kuna sheria ya namna gani inayohakikisha kuwa menegiment ya kampuni ya kigeni nchini iwe?

c. Je faida wanayoipata Tanzania wanailipia kodi kwa kiasi gani?

d. Je mfumo tulionao sasa unaweza kwa namna yoyote kuboreshwa ili kuhakikisha kuwa mapato yanayopatikana nchini mengi yanabakia nchini pia?

Sidhani kama kuna nchi iliyoendelea ambayo inaacha kampuni ya kigeni kuchukua faida yote na kuipeleka kwao!

a.Sidhani kama kuna haja ya kuyasimamia nje ya mfumo uliokuwapo. Kama ni makandarasi watasimamiwa na makonsaltanti wao na bodi zao zilizowasajili. Kama kampuni nyingine yeyote. Dawa ni kuwa na level ground na kuwaona wote kama wafanya biashara ambao lengo lao ni kumaximize profits zao. Tatizo letu ni kutojiamini linapokuja suala la makampuni ya kigeni.

b.Hapa sijakuelewa mkubwa. Uamuzi wa aina ya menejimenti ni wa kampuni na sidhani kama itakuwa busara kuwa na sheria inayo'diktet' aina ya menejimenti inayotakiwa. Ni kwenye ownership ndiko kulikotungiwa sheria au bye-law ili kuweza kuainisha kampuni ya kigeni ni ipi. Kuwa kampuni ya kigeni au local kuna impact katika ada na kodi ambazo kampuni na wafanyakazi wake wanatakiwa kulipa. ninachojua mimi ni kuwa katika baadhi ya miradi imewekwa wazi kuwa kampuni local zitapewa upendeleo. Kutokana na ada hizo kuwa punitive (pamoja na kuongezeka kwa ushindani, vitendo vya rushwa n.k)kwa kampuni za kigeni ndiko kulikochangia wengine kufunga virago. Wengine wakaji'localise' kwa kutransfa kimpango majority shares kwa wazawa. Matokeo ni nchi yetu imekuwa wild east.

c. Faida niliyokuwa nazungumzia mimi ni baada ya malipo ya kodi zote.

d. Bila shaka! Ingawa inabidi tuwe makini tusimuue bata anayetutagia mayai ya dhahabu! Tuwe pragmatic na realistic katika expectations zetu.

Mkuu, nyingi tu maana hii ndiyo namna moja ya kuvutia wawekezaji kutoka nje. Wengine hata kodi hawataki ili mradi ufungue ofisi kwao maana wanajua watakupata sehemu nyingine!
 
Bila shaka Umaskini unatokana na Ujinga..
Hadi siku mtakapo kubali kuwa elimu ndio nguzo kuu ya maendeleo basi tutakesha na Umasikini wetu.
Na hili la kujifunza kiingereza kama ndio elimu dunia tutamezwa vibaya sana...
 
mzee kuna makampuni ambayo hayalipi kodi katika faida zao!!! kwa sababu ya ile capital gain clause aliyoipigia kelele Zitto Bungeni..
 
Bila shaka Umaskini unatokana na Ujinga..
Hadi siku mtakapo kubali kuwa elimu ndio nguzo kuu ya maendeleo basi tutakesha na Umasikini wetu.
Na hili la kujifunza kiingereza kama ndio elimu dunia tutamezwa vibaya sana...

na hapo ndipo ninakumbuka miaka ile tulipokuwa tunamaliza darasa la nne tunapewa karatasi ya kuchagua nafasi za kazi, hivyo tukawa hatuna mwanga zaidi wa kujiendeleza kielimu na haya sasa ndo matokeo yake taifa linawajinga wanaowaongoza wajinga.

nyerere hakutaka watu wasome coz alikuwa amejiandalia maisha ya ikulu milele, so alijua kama watanzania wangesoma na kufunguka wangekuja kumsumbua siku moja juu ya madaraka. sasa matokeo yake laana lile ndo linatusumbua mpaka sasa watanzania ni masikini wa fikra, mawazo na kipato.
 
Naomba nifahamishwe, katika hili suala ni kipi kinachothibitisha ujinga wetu? Kuwa makampuni ya kigeni ndiyo yanayoshikilia sehemu kubwa ya miradi ya ujenzi ambayo mara nyingi inafadhiliwa na kodi za wananchi wao? Au kuwa wanaremit faida wanayoipata? Au kuna jambo ambalo mimi sijalielewa!

Fundi,

The fact that we are allowing all these foreign companies to come and operate in Tanzania and provide them with "healthy" accomodations such as 5-10 years Income and Tax Break, in addition to other "incentives" to plush the red carpet fibre so they can walk like emperors to rescue Tanzania from its own failures, is enough to acknowledge that Ndivyo Tulivyo na ni Wajinga waliwao!

It does not matter that the payment of projects is repayment of their own Tax payers money, it is still a problem that we can not promote local industries and production and completely depend on imports of goods and services.

Mliokuwa mnalipinga Azimio, you have to ask yourselves now, if it was worth it to have strict policies that ensured every penny earned on our soil was accounted for and taxed.

Kuna mawili Fundi Mchundo, ukiangalia mkao wa kula aliofanya "Macheni" na Halibatoni, kupewa mikataba yote ya kujenga mitaa ya Uajemi, na misaada yote inayopewa serikali ya Ali Maliki, ni mchezo ule ule, ufisadi in crafty way!

La pili, ni sisi kuwa vibaraka wa hawa mabwana. Hizi safari za kujitangaza kila siku ni za kwenda kupokea amri na maagizo ya nini kifanyike. Tunadumaza wazawa kwa kuona bora wazungu na wawekezaji.

Ndio maana nimetoa hoja, Lets Privatize Ikulu, Bunge and.....
 
Akili zetu zimedumazwana sera za ukiritimba,tukaingia katika soko huria kama wajinga na tunaendelea kuwa wajinga hadi siku akili zitakapozinduka.Si katika siasa tu bali hata katika uchumi wetu.

Ksumaba ile ileee....haimaliziki hadi generation hii iondoke au atokezee Mkombozi atakayefanya kama Jerry Rawlings kule Ghana.Halafu kipite kipindi cha miaka kama kumi tukiwa chini ya mtu kama Jerry....na ten tuanze kuingia katika enzi za Kufour.hapo tutaweza kuwa Watanzania wenye akili hasa baada ya kupiga deki hizi akili zetu na kusafisha kabisa uoza uliomo ndani yake.

Nilidhani ndugu yangu JK angeweza kuwa smart na kuleta kitu kipya lakini mpaka sasa naona hana will ya kufanya hivyo.
Hali inakuwa ngumu kila kukicha na ahadi za Mheshimiwa hazionekani kutekelezeka.
Kwa nini Kikwete asiwe kama Jerry? Kwa nini Kikwete asiwe kama Nelson Mandela?

Ni kwa sababu ya kasumba ya tangu awali kabisa ambayo inashindikana kuondoka kichwani mwake?Mbona ni mtu ambaye ametembea nchi nyingi tu duniani?

Waliotuingiza katika Soko huria ambao ni viongozi wetu, hawakuwa wajinga au vipofu walipofanya maamuzi hayo. Ni sisi wananchi ambao tulikubali kiimla kuingia katika mfumo mpya wa kiuchumi bila kushirikishwa na kuandaliwa kikamilifu.

Leo ukipiga kura ya maoni, kutaka kujua kama wananchi wanataka mfumo gani wa kiuchumi, 85% watakuwambia mfumo wa Ujamaa na kufuata siasa za Ujamaa na Kujitegemea (Azimio la Arusha).

Viongozi walitumia mwanya wa ukosefu wa bidhaa na kuzorota kwa uzalishaji kama kigezo makini kuwa Umasikini umetukolea na njia pekee ya kujinasua kutoka umasikini ni kuwa na mfumo mpya wa kuchumi ambao utalenga katika kufungua milango ya uwekezaji wa wageni wenye mtaji mkubwa, sheria laini na nyepesi za maadili ya uongozi, na kusukuma jukumu na mzigo wa wananchi kuchangia huduma kwa mwendokasi wa roketi, na si kwa taratibu.

Watanzania tumepigwa limbwata na ramli na viongozi wetu, wametuingiza mkenge kwa makusudi, wamepindisha sheria na hata katiba kukidhi mahitaji yao na familia zao na za "marafiki" zao wawekezaji!

Yes, sisi ni WAJINGA!
 
Mifano iliyotumika kuonyesha kwamba "sisi ni wajinga" si mizuri. Fundi Mchundo katoa somo tosha sana.

Chukulia mfano uliotolewa wa msaada wa bilioni 700 toka Marekani. Sawa, watajenga barabara makandarasi wa Kimarekani. Sehemu kubwa ya fedha itarudi huko, lakini sisi tutabaki na barabara! Kuna ujinga gani hapo?

Kuna kushangilia maoni kama mpira. Kumpa tenda ya ujenzi mzawa ambaye hana uwezo wa kufanya hiyo kazi ndio kungekuwa ujinga kweli kweli.

It is defeatist to think that we are stupid. We are not. Ukiamini kwamba wewe ni mjinga, basi unaanza kuzorota tu.

Ushabiki wa mawazo hapa, bila kuangalia ukweli, unaweza kuwa dalili ya kuingia kwa ujinga hapa JF (sio nchi nzima).
 
BoT: We`ve no control over earnings by foreign firms

2008-05-09 09:20:15
By Patrick Kisembo

........He cited lack of funding from financial institutions as one of the biggest challenges facing local contractors.
``This is due to the fact that most of the local contractors are small with no tract record and lack collateral to enable them access loans from financial institutions,`` he said..

Je wakipata hizo funds si ndio hapo wanamwaga hovyo kwa vimwana au kwenda kupeleka offshore accounts....sisi si wajinga bali hatuna ile sense of PATRIOTISM



CRB Registrar Boniface Muhegi admitted that foreign contractors benefited a lot owing to the fact that they were able to access finance, plant and machinery, as well as support, from their home countries or institutions.

Lakini tujue nchi zao zinawapa vifaa kwanza wanajua kuwa haya makampuni yana create job ambayo ni kitu muhimu sana kwa hawa wazungu na pili hizi kampuni zinarejesha hizo mikopo tofauti na sisi wangapi tumechukuwa mikopo na tukaingia mitini? wengi sana
 
Mifano iliyotumika kuonyesha kwamba "sisi ni wajinga" si mizuri. Fundi Mchundo katoa somo tosha sana.

Chukulia mfano uliotolewa wa msaada wa bilioni 700 toka Marekani. Sawa, watajenga barabara makandarasi wa Kimarekani. Sehemu kubwa ya fedha itarudi huko, lakini sisi tutabaki na barabara! Kuna ujinga gani hapo?

Kuna kushangilia maoni kama mpira. Kumpa tenda ya ujenzi mzawa ambaye hana uwezo wa kufanya hiyo kazi ndio kungekuwa ujinga kweli kweli.

It is defeatist to think that we are stupid. We are not. Ukiamini kwamba wewe ni mjinga, basi unaanza kuzorota tu.

Ushabiki wa mawazo hapa, bila kuangalia ukweli, unaweza kuwa dalili ya kuingia kwa ujinga hapa JF (sio nchi nzima).

Mwalimu nadhani neno Ujinga hulielewi maana yake. Ujinga si upumbavu. Upumbavu ni tusi na ujinga ni hali ya kutojua. Ujinga huondolewa kwa mtu kuerevuka au kuelimika. Kila mtu ni mjinga (ignorant) kwa jambo fulani. Sasa mtu ambaye anafanya mambo kana kwamba anajua na wakati anajua kuwa hajui ujinga wake umejificha katika kujifanya anajua.

Sisi ni wajinga kwa sababu hatujui nini kinapaswa, nini kinastahili, na nini tunaweza; na hapa nazungumzia kama Taifa na si mtu mmoja mmoja. Kama tungekuwa tunajua kuna mambo ambayo kamwe tusingeyafanya kwani mtu anayejua hafanyi mambo ya kijinga.

Mjinga is as mjinga does..
 
Mwalimu nadhani neno Ujinga hulielewi maana yake. Ujinga si upumbavu. Upumbavu ni tusi na ujinga ni hali ya kutojua. Ujinga huondolewa kwa mtu kuerevuka au kuelimika. Kila mtu ni mjinga (ignorant) kwa jambo fulani. Sasa mtu ambaye anafanya mambo kana kwamba anajua na wakati anajua kuwa hajui ujinga wake umejificha katika kujifanya anajua.

Sisi ni wajinga kwa sababu hatujui nini kinapaswa, nini kinastahili, na nini tunaweza; na hapa nazungumzia kama Taifa na si mtu mmoja mmoja. Kama tungekuwa tunajua kuna mambo ambayo kamwe tusingeyafanya kwani mtu anayejua hafanyi mambo ya kijinga.

Mjinga is as mjinga does..

Man, you are on point with this one! Hata mimi baada ya kusoma bandiko la Prof. moja kwa moja nikaona anachanganya maana ya ignoramus (mjinga) na stupid (mpumbavu, zuzu). Ujinga hauhusiani hata kidogo na akili ya mtu lakini upumbavu au uzuzu unahusiana.

Hayo/ hilo ya/ la ujinga "wetu" sitalitolea maoni. Nawaachia nyie...
 
Jamani maneno yanaweza kuwa na maana zaidi ya moja.

Hivi kweli ukimwambia mtu mjinga atakuacha kweli? Sio tusi neno mjinga katika jamii yetu?
 
Jamani maneno yanaweza kuwa na maana zaidi ya moja.

Hivi kweli ukimwambia mtu mjinga atakuacha kweli? Sio tusi neno mjinga katika jamii yetu?

Anaweza akakukasirikia lakini kwa vile hajui maana yake sahihi. Kuna wakati niliwahi kumsikia Nyerere akijiita mjinga wa baadhi ya mambo. Kwa kujiita hivyo alikuwa hajitukani bali alikuwa anamaanisha hajui kila kitu....

Na ni kweli maneno yanaweza yakawa na maana zaidi ya moja lakini sidhani kama hili la mjinga, ukiangalia muktadha wa jinsi alivyolitumia Mwanakijiji linakuwa ni tusi au neno linalokasirisha.
 
Naomba nifahamishwe, katika hili suala ni kipi kinachothibitisha ujinga wetu? Kuwa makampuni ya kigeni ndiyo yanayoshikilia sehemu kubwa ya miradi ya ujenzi ambayo mara nyingi inafadhiliwa na kodi za wananchi wao? Au kuwa wanaremit faida wanayoipata? Au kuna jambo ambalo mimi sijalielewa!

..fundi,

..kwani best practice katika masuala kama haya ni ipi? huko kwao au nchi nyingine mambo yako vipi?

..what about kutengeneza sheria[au kuirekebisha]itakayowataka hawa wa kutoka nje kuwa na ubia na local ones,say 40/60[local 40/foreign 60]au vinginevyo.

..nawasilisha.
 
naangalia mjadala unavyokwenda, ila mwisho wa siku tutakuja kufika kwenye point "je nani katufanya tuwe wajinga hivi?" na hapo sasa ndo nitainuka bila hata kuchaguliwa na nitapiga kelele kwa nguvu zangu zooote "NYERERE"
 
Back
Top Bottom